Iran yaishambulia Israel kwa makombora
Mimi ninaona wote wanaogopana. Iran Karusha drones na Ballistic missiles ambazo anajua zitatumai almost za tisa kufika Israel ambayo iko 700 miles away from Iran ikiwa ina maana alijua watajiandaa kuzidungua. Angekuwa ana lengo la kusababisha hasara kwa Israel angempiga shambulizi la ghafla. Sasa wewe unarusha kitu kinifikie masaa tisa, Israel na wapambe wake wakasema wanatrack kila drone na kila missile kabla ya kuingia kwenye anga ya Israel.
Upande wa pili ngoja tuone ila sidhani kama Israel naye atajibu kwa kurusha makombora au ndege kwenye anga ya Iran labda kama atapiga proxy wa Iran.
Ila la msingi naombea hawa watuw asiingie vitani maana dunia naona inaanza kuchanganyikiwa. Nikisoma comments za raia wa Marekani, wanaomba serikali yao iache Israel apambane na matatizo yake maana wanadai serikali iko busy na Israel wakati mambo yao ndani yanaharibika uchumi unayumba china anasonga kwa sababu ya kujifanya wanatia mkono kwenye mambo yasiyo wahusu.
Sasa najuilizaga Marekani anabenefit nini kwa israel mbaka anasahu mambo yake ya ndani
 
Wanaangalia na aina ya retaliation na damage iliyofanywa na adui kulinganisha na damage walio fanya wao Israel kwa Iran.

Kama Iran hawajafanya madhara yoyote makubwa kwa Israel then hawanahaja ya ku retaliate.

Makombora ya Irani hayaja fanikiwa kusababisha maumivu sawasawa na waliyoyapata kwenye ubalozi wao kule Syria.
Israeli wanapima kiwango cha maumivu walicho mpa Irani nakuona kinamtosha kwamuda huu na bila shaka ndio maana hawana araka ya kulipiza.


Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app
 
Tunashabikia Vita halafu maisha yakipanda tunaanza kulaumu chama Cha mapinduzi mnajua kabisa kule middle East ndio kunatoka wese lote tunaloendeshea maisha huku bongo.
 
Yamepiga na kuharibu kambi kubwa ya jeshi la anga ,pia matokeo ya shambulizi hili yatadumu kwa muda mrefu kati ya hizo nchi mbili.

Na pia shambulizi hili litaifaidisha Iran kimkakati.

Kwa hili shambulizi litaifanya Israel ianze kujifikiria mara 2 kabla ya kushambulia masilahi ya Iran tofauti na mwanzo.
Kiufupi hili shambulizi litaifaidisha Iran kwa muda mrefu.
Muda mwingi Israel ilipiga na kutamba maslahi ya Iran ndani ya Syria na hata Iran kwenyewe.Ilizoea kupiga na kuchukulia Iran ni waoga sana hawawezi kujibu.
Kitendo cha kujibu tena kupiga miji mikuu na kambi za jeshi hata kama hawajaweka wazi madhara kwa sasa.Israel itaiheshimu Iran daima kuanzia sasa.
 
Ujasiri wa kurusha makombora hewa!! Wangetuma wanajeshi tuone huo ujasiri! Hatushabikii vita ila hawa waarabu na waajemi waliokuzwa ktk imani ya chuki ya kidini dhidi ya wanaowaita makafiri wanadekezwa sana na wayahudi na wazungu, dawa yao ingekuwa kuwajibu wanachokifanya kutofuata sheria za kivita ndiyo wataacha ujinga wa kubagua dini za wenzao na kuwaona wenye imani tofauti hawapaswi kuishi duniani au wakiishi wawe watumwa wao tu.
Unaongea ujinga tu ,unajua Iran au Persia imehost mamilioni mangapi ya hao wayahudi feki tangia enzi za dola ijulikanayo kama ya waajemi mpaka leo hii kujulikana kama Iran ?
 
Mkuu kambi kubwa moja wapo ya anga Israel imeharibiwa na mashambulizi ya jana imeharibiwa hivyo kuna makombora yalipenya na kushambulia.

..Good.

..ndio maana nasema kila upande umepata kujua nguvu na mapungufu ya silaha zao.

..kabla ya hili tukio mambo mengi yalikuwa ya kupiga ramli tu.
 
Waongo huwezi tuma drone zinazotumia masaa 9 hadi 10 ukasema eti hyo ni mashambulizi.
Vita gani inapiganwa hivyo?

Yani kwa ulinzi uliopo Israrl unatuma drones, hao wanatafuta covarage ya habari na kudanganya,wananchi wao.

Au nao wanaupiga mwingi ksma sisi, sikutegemea kwa Iran kutuma drone Israel.
 
Waongo huwezi tuma drone zinazotumia masaa 9 hadi 10 ukasema eti hyo ni mashambulizi.
Vita gani inapiganwa hivyo?

Yani kwa ulinzi uliopo Israrl unatuma drones, hao wanatafuta covarage ya habari na kudanganya,wananchi wao.

Au nao wanaupiga mwingi ksma sisi, sikutegemea kwa Iran kutuma drone Israel.
Sisi zana zetu zitatumia siku ngapi kufika huko?

Kumbuka kwenye vituo vya mafuta harufu ya kukosekana mafuta imesha anza kunukia.
 
Back
Top Bottom