Iringa: Kanisa Katoliki lawazuia waumini walioshiriki kongamano la Mwamposa kutopokea Sakramenti ya Ekaristi Takatifu mpaka watakapoungama

Na Wewe una akili ya kuku, summarization ya waraka ni kwamba kama umeamua kuabudu maji na mafuta basi huku hapakufai (RC) labda utimize masharti tajwa kwenye waraka.
Sasa hapo nani amenyimwa uhuru wake?
Ni sawa na kuwa mwanachama wa CCM Halafu ukataka viti maalum kupitia CHADEMA.
una uhuru ndio, tumia uhuru wako kuchagua, usituvuruge
 

Si wameshachagua pa kwenda sasa, mnawawekea matangazo ya nnni?

Waacheni wawe huru na wanachotaka, endeleeni, hata zamani mafarisayo walikuwa wanatisha watu pia kwamba watawafukuza kwemye masinagogi yao kwa sababu tu waliamini alichokuwa anafanya bwana yesu!!
 
Waoh hawajazuia ww kwenda, Ila wametoa masharti Yao, mbona jamaa wameweka na facts kabsa.
Jaribuni kuwa waelewa. Wala hamna wanaotishwa, ni hivi ukienda huko Sisi tunaamin umepotea hakuna utajiri bila kazi,
Hivi na wewe unaaminj hiyo nadharia, kwamba: "hakuna utajiri bila kazi"?
 
Nafkr kanisa katoliki Lina taratibu zao, endapo ukienda kinyume na Imani pamoja na taratibu zao kuna namna wanakuajibisha ili urudi kundini , kama wanahitaji kurudi kundini wafate hzo taratibu ili warudishwe kundini, kama hawaafiki basi wahamie Kwa Mwamposa, kuchanganya Imani mbili Kwa pamoja ni kuleta machafuko....Katoliki wamesimama Imani Yao isichafuliwe na propaganda ya mtu mwingine


.
 
Nyakati hizi waumini wanabembelezwa sana maana makanisa ni mengi unaweza ukaenda kusali kanisa lolote tu ila katoliki mapato yatapungua
 
Hii ikifanywa na waislam ingechukuliwa tofauti, bora wamefanya hao
 
Hata waislamu ukiwa mpumbavu hawakuziki, Kuna kijana Muislam hapo Dar alikuwa mchicha Mwiba alipofariki hakuzikwa na watu,
Nakumbuka walishamwambia Lundenga mzee wa miss tz enzi zile kuwa akidedi hawatahangaika nae ingawa kidini walikosea maana Allah ameagiza yeyote atakayefariki aswaliwe
 
Naam, ndivyo ilivyo.Ni juu yao kuchagua kusuka au kunyoa hakuna anayewalazimisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…