TANZIA Iringa: Katibu wa CCM Kilolo avamiwa na kuuawa na Watu wasiojulikana

TANZIA Iringa: Katibu wa CCM Kilolo avamiwa na kuuawa na Watu wasiojulikana

Kama ambavyo tunapiga kelele haya kutokea kwa viongozi wa CDM, vivyo hivyo kwa CCM.

Haya hayapaswi kutokea katika jamii yetu, tuungane kuupinga unyama huu.
Futa ile kauli ya kifo ni kifo tu, chanzo cha yote ni hio kauli means umetoa amri watu wauane umeshasahau mara hii unaona huruma wakati ulitamka mbele ya kadamnasi kwamba kifo ni kifo tu hukuona madhara ya hio kauli?

Kauli yako yoyote ni amri sio ombi sasa unapotoa kauli next time jiulize mara 3 what is next nikishasema haya ninayoyasema? Watu wataingia kwenye machafuko ya kuuana huku na huko kwa kauli yako moja tu yenye utata
 
Haya matukio yakitokea opposition tunasingizia CCM, serikali yake na Green Guard... Je na Kwa hili tulalamike Moja Kwa moja kuwa ni CDM na Redbrigade Yao???
Nafikiri tuliache kuwa halina majibu hadi uchunguzi wa pasipo na shaka yoyote utakapotoa majawabu
Wanamalizana wenyewe kwa wenyewe rejea hotuba za Babu, dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana hawa ni CDM hawa ni CCM mkishawamaliza CDM mtaanza kumalizana wenyewe ndani ya CCM ndicho kinachoendelea wameanza kutafunana wenyewe kwa wenyewe
 
Kuna kafeeling flani amazing.... Haya kazi iendelee ..... Kifo ni kifo tu alisikika.
 
Watu Wasiojulikana Wanadaiwa wamemvamia aliyekuwa Katibu wa Chama Cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa, Christina Kibiki na kumuua kwa kumpiga risasi.

Taarifa ambayo Matukio Daima Media tumeipata inadai kuwa watu hao Wasiojulikana wamefanya uvamizi huo usiku wa kuamkia leo Novemba 13, 2024 katika Kijiji cha Njia Panda ya Tosa, Wilaya ya Iringa Vijijini nje kidogo na Mji wa Iringa ambako alikuwa akiishi.
Kuwa baada ya kumshambulia kwa risasi alikimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa ya Tosamaganga ambako amefariki Dunia.

Matukio Daima Media imezungumza kwa njia ya simu na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kilolo, John Kiteve amesema tukio hilo limemgusa sana na amesikitishwa na tukio hilo.

Huku Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Allan Bukumbi hajapatikana ili kuthibitisha tukio hilo, bado Matukio Daima Media inaendelea kufuatilia zaidi.

Chanzo: Matukio Daima Media

==============================

JamiiForums imemtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Allan Bukumbi, simu imepokelewa na msaidizi wake ambaye baada ya kuelezwa kuhusu tukio hilo akasema “Kamanda yupo kikaoni, tukio hilo bado hajalizungumzia.”


Pia, Soma:
Mdude Nyagali! Mdude Nnyagali, pamoja na yule Askofu anayetembea kila kona na Lissu, wachunguzwe, wametishia kutoa watu roho mara kadhaa
 
Ungempa huo ushauri mapema asingepigwa risasi.
mimi sina haja kumpa mtu moja au wawili ushauri,

mawadha yangu mujarabu na maridhawa huwa ni ya jumla kwa wadau wote muhimu wa JF.

ukipuuza yatakayokukuta ni juu yako gentleman 🐒
 
mimi sina haja kumpa mtu moja au wawili ushauri,

mawadha yangu mujarabu na maridhawa huwa ni ya jumla kwa wadau wote muhimu wa JF.

ukipuuza yatakayokukuta ni juu yako gentleman 🐒
Kwahiyo yeye alipuuza ushauri wako.
 
Back
Top Bottom