Iringa: Wakala wa malipo anaswa akidaiwa kuiba TSh Bilioni 2.1, Polisi wafanikiwa kuokoa TSh Milioni 956

Na hizo Benki nazo tatizo.
Kijana umeajiriwa juzijuzi tu leo uko kwenye kesi ya kutakatisha fedha!
Vijana acheni tamaa. Angalia mbele kwanza na ujiulize: "Hivi dili hii ikigalambuka itakuwaje?"
Show-off mbaya sana na ndiyo inayoponza vijana!
 
Ilula sokoni, ilula mtua, ilula mwaya, ilula itunda, ilula masukazi wanalima nyanya hawa jamaa utakutaga mafuso yamepakia nyanya hasa kipind Cha mwenz wa nne hadi wa Saba
 
Kumbe harrier zimepanda bei. Milioni 72 sio mchezo
 
Acha uongo!

Utahamishaje pesa zote hizo kwenda e-wallet bila kupitia mfumo rasmi wa kifedha (bank/mobile money transfer).

Fedha yoyote kwenda account ya nje lazima ipite BoT.

Pale ukipita mzigo mrefu lazima wapate red alarm. Wanazuia
 
Acha uongo!

Utahamishaje pesa zote hizo kwenda e-wallet bila kupitia mfumo rasmi wa kifedha (bank/mobile money transfer).

Fedha yoyote kwenda account ya nje lazima ipite BoT.

Pale ukipita mzigo mrefu lazima wapate red alarm. Wanazuia
Haha sio uongo mzeee, Means utakua na line fake kama zotee, Ukishajihamishia mzigo, unaingia kwenye simu yako alafu unanunua local bitcoins Hapo inakua imeisha
 
Kama puto, hiyo bei ya 72m kwa Harrier, hiyo bei imepigwa juu kwajuu!
Utakua unaishi kijijini na huna elimu, thamani ya gari huendana na mwaka uliotengenezwa(model)
Harrier zipo za mil 15, 25, 40, 70, 80 , 120, 150, 170
Ni wewe tu unataka ipi.
Bei ya harrier ya 2020 unataka ifanane na harrier ya 2006 mnayoiita tako la nyani?
Hiyo harrier ipo hapo chini unahisi ni sh.ngap?
 
Kuna shehe mmoja kwenye kijiwe cha gahwa alipata kusema, "matanzania yote ni majizi bila kujali kabila zao".
 
Huenda hao polisi lile la ntwara limewashtua ndio maana wakaamua kuwa wazi bila hivyo............
Naomba niishie hapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…