Israel yasema shambulio la Yemen ni onyo kwa maadui zake wote wa mashariki ya kati

Saudia si alikua na ugomvi na houthi juzi tu,houthi wakapiga miundombinu yake ya mafuta kwa drone, saudia akaomba majadiliano na ugomvi ukaisha,shida ya houthi hawana Cha kupoteza,fikiria washushe makombora Cairo
Nimemaanisha kupigana vita rasmi, sio mashambulizi ya drone ambayo ni ya kushtukiza, yoyote akiwahiwa anapigwa. Kuwe na taarifa rasmi kuwa sasa tunapambana. Anaweza yapiga hayo mataifa?
 
Kwa hiyo houthi wana nguvu kuliko Egypt?
Houthi jumba la miti, Egypt la vioo,vigae, unadhani houthi akirusha mawe Egypt nani ataumia
Nimemaanisha kupigana vita rasmi, sio mashambulizi ya drone ambayo ni ya kushtukiza, yoyote akiwahiwa anapigwa. Kuwe na taarifa rasmi kuwa sasa tunapambana. Anaweza yapiga hayo mataifa?
Wakati saudia anapigana na houthi Vita kamili hukuwa mfuatiliaji wa mambo eeh!?..si juzi tu hapa,Hadi ulinzi wa marekani saudia ukaonekana wa kidwanzi, patriot sijui zile, Putin akajisigeza kwa mbs
 
Kwamba ww una technical knowledge kuliko israel airforce ? Dude pls
kwanza F-35 wanazotumia F-35 ni modified kwa matumizi yao tu, wamechuku airframes waka install mifumo yao according to their needs. And hawana tu F-35 wana fleet kubwa ya ndege nyingine, so kwenye flight sortie hawa fly ndege aina moja.

Sisem israel is the best, but dont under estimate them na experience waliyo gain of all years
 
Mkuu unakosea sana.
Kwanza hayo makundi ni non-state actors.
Tofauti na USA na UK serikali zao ndizo zinazoisapoti Israel directly.
Usifananishe sovereign government na non-state actors armed groups kaka.
Pia Iran hatoi tu msaada wa fedha na silaha na mafunzo,bali pia hata wanajeshi anatoa.
Umeshasahau kama Qassem Soleiman kamanda wa jeshi la Iran aliuawa Syria?
Je alikua anafanya nini kule!?
Usisahau juwa Syria kuna jeshi la Iran tena Iran pale Syria kapoteza wanajeshi wengi sana akimsaidia Bashar Assad asitolewe madarakani ni vikundi vya kiasi ambavyo vingi vina muunganiko na Israel.
-Bila Iran basi Lebanon ilikua inapoteza eneo lake lote la Kusini pamoja na mpaka wa bahari wenye utajiri wa gesi na mafuta.
-Bila Iran Syria ilikua ishapotea nje ya mikono ya Assad.
-Bila Iran Yemeni ingekuwa haina msimamo mmoja na ingekuwa ina vikundi vya kiasi kila eneo kama Iraq.

Iran haijapoteza tu pesa na silaha bali imezika wanajeshi wake wa IRGC maeneo mengi tu hususan Syria,Yemeni na Lebanon.
Na mind you,hayo makundi vita pia zimekua nyepesi kwao kwasababu ya nguvu ya wanajeshi wa Iran kupigana nao pamoja.
Nadhani unajua historia ya Iran kivita ni kubwa kuliko ya Israel.
Iran ambayo ilimudu vita ya miaka 8 ikiwa na jeshi la mapinduzi tu ambalo bado halikutengemaa.
 
Unaamini Houthi ana uwezo wa kumpiga Misri au Saudia?
Anao kwasababu alishafanya kwa Saudi Arabia na alifanikiwa kumpiga Saudi Arabia miaka ya 2017-2020.
Unapopigana na Houthi jua tu unapigana na Iran revolutionary guards corps.
 
Israel huwa hawamtishi mtu awaye yote.Huwa wanatuma taarifa tu.Kwamba,nitakupiga huku tayari kakukung'unta unalialia.
 
Nimemaanisha kupigana vita rasmi, sio mashambulizi ya drone ambayo ni ya kushtukiza, yoyote akiwahiwa anapigwa. Kuwe na taarifa rasmi kuwa sasa tunapambana. Anaweza yapiga hayo mataifa?
Kwani ulikua hujui kama Houthi na Yemeni walipigana vita rasmi!?
Tokea 2017 mpaka 2020 Saudi Arabia ilituma jeshi kamili ikiwa na vifaa vyote hitajika.
Nia yao wakomboe miji yote iliyoshikiliwa na Houthi ili wairudishe kwenye utawala wa Mansour ambaye hakutakiwa na raia wa Yemeni.
Ila cha ajabu Saudi alipoteza askari na hata mji mkuu aliosema wa Sana'a ataulinda akapokonywa vile vile.
Msichokijua ninyi Houthi akipigana jua kuna askari wa Iran wapo mule ndani.
 
Siyo kweli hakuna sehemu yoyote ndani Eilat iliuoshambuliwa na hata idf walikataa.
IDF kukataa kawaida yao.
Hata hilo tukio la Tel Aviv kama isingekuwa media kuwahi kulirekodi basi wangekataa.
Eilat imeshambuliwa ila vyombo vingi vya habari vilikosa coverage.
IDF hao hao walikataa kama jeshi lao limepata walemavu wa kudumu 12000 kutokana na vita ya Gaza.
Mpaka gazeti la Haaretz likawaumbua.
 
Houthi ni chama cha kisiasa kihistoria unasemaje wanahifadhiwa hapo Yemeni!?
Ni sawa useme ACT wazalendo wanahifadhiwa hapa Tanzania mkuu utakua uko serious kweli!?
Houthi wote ni asili ya Yemeni na wana historia katika kila siasa za Yemeni toka 1990s.
Unasema mtu anahifadhiwa nchini kwake!?
 
Anao kwasababu alishafanya kwa Saudi Arabia na alifanikiwa kumpiga Saudi Arabia miaka ya 2017-2020.
Unapopigana na Houthi jua tu unapigana na Iran revolutionary guards corps.
Ok. Vipi kwa Misri?
 
Ok. Vipi kwa Misri?
Kwa Misri hawakuwahi kupigana.
Ila kama watapigana vita itakua ngumu maana tabu kuu ilipo ni kuwa IRAN iko nyuma ya Houthi.
We hujiulizi nguvu ya makombora ya masafa marefu,vifaru na APC vehicles na bunduki zenye nguvu Houthi wanatoa wapi!?
Yani ili Houthi wafeli basi Iran isiingilie kati.
 
Yote hayo nayafahamu, swali langu lililenga kupata maoni ya huyo niliemuuliza. Asante mawazo yako pia.
Tusichokijua wangapi au kina nani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…