Israeli yatangaza rasmi kuingiza majeshi nchini Lebanon upande ya kusini. Nini kitajiri baada ya hatua hii ngumu ya Israeli?

Israel inaripotiwa kuingiza jeshi ndani ya mipaka ya kusini mwa Lebanon ikiwa na lengo la kupambana na Hizbollah.
Uvamizi huo ulianza jana tarehe 30 September 2024.
Leo ni Oktoba mosi.
Je,ya 2006 yatajirudia ama Lebanon inaenda kuwa Gaza mpya!?
 
Ulikuwa umelala bado habari hii imetoka tarahe 1 iliposoma tu Israel ilipanga iwe recorded Tarehe moja October 2024

Mod unganisha hii thread
 
Maisraeli yanapenda vita kuliko hata ngono. YAMELAANIWA
Si kwamba Israeli yapenda vita bali ni client state kwa niaba ya Marekani katika kulinda maslahi na kihakikisha usalama wa eneo la Mashariki ya kati wa ajili ya ustawi na ukuaji wake. Ni kama ilivyo kwa Ukraine itumiwavyo na NATO na Marekani dhidi ya Russia.

Lengo kuu la Marekani ni kuliunda upya eneo hilo la mashariki ya kati kikwazo akiwa ni Iran hivyo Iran akijichanganya atakuwa kitoweo.

Ukipata muda msikilize tena Benjamini Netanyahu katika hotuba aloitoa juzi UN akielezea mikakati ya Mashariki ya kati mpya na huku aliilenga Iran kuwa ni kikwazo.

Mara tu baada ya hotuba ile akanyanyua simu na baadae Nasrallah akamalizwa.
 
Updates:Hezbollah yakanusha kwamba majeshi ya Israeli yamevuka mpaka kuingia kusini mwa Lebanon.

Hapa ni vita ya propaganda na kisaikolojia.

Wakti huohuo Uturuki imesema jaribio la Israeli kuingiza majeshi ya ardhini kusini mwa Lebanon ni kinyume cha sheria za kimataifa na yakiuka maslahi na heshima ya mipaka ya Lebanon.

Jeshi la kulinda amani la umoja wa mataifa limesema limetaarifiwa na Israeli juu ya operesheni yake kusini mwa Lebanon.

Operesheni hii ya Israeli yaitwa Operation Arrow.

Russia imesema yafuatilia kwa makini operesheni ya Israeli katika nchi za Lebanon na Syria.
 
🇱🇧🇮🇱 | Hezbollah’s Media Relations Officer Mohammad Afif to Reuters: 'No Israeli troops have entered Lebanese territory. The strikes on Tel Aviv earlier were only the beginning'

@MilitaryPOV
 
🇱🇧🇮🇱 | Hezbollah’s Media Relations Officer Mohammad Afif to Reuters: 'No Israeli troops have entered Lebanese territory. The strikes on Tel Aviv earlier were only the beginning'

@MilitaryPOV
 
Ok. Very simple. Wanalebanon; 1. Wakataeni Hezbollah kwani hao sio wenzenu kabisa-ona walipowafikisha sasa.
2. Muwe watiifu na Wepesi wa kuzingatia na utekelezaji kikamilifu maelekezo yatolewayo na IDF.
3. Acheni ushabiki wa Kidini. Hiyo vita asilani sio ya kidini.
4. Beba bendera nyeupe (ishara ya AMANI) esp. mnapokuwa wengi/Kikundi kwa pamoja.
 
Lebanon iko hoi, si taifa imara tena.

Itachukua miaka mingi kwa Lebanon kuja kusimama kama taifa huru.
 
Hezbollah kuanzia jana wamevua magwanda yao wanavaa Kiraia wanaogopa kifo.
AaaH! Mambo ya kuweka mpira kwapani waturudishie viingilio vyetu. Eti wanavaa kiraia? yani wao sio wapiganaji tena?? Kwa hiyo wamerejelea uvaaji wa vipedo, kobazi, hijabu na kujificha nyuma ya makalio ya akina mama na watoto?
 
Nchi ama vikundi vingine vya magaidi inatakiwa wajifunze sasa kuwa Iran anawatumia kwenye maslahi yake tuu wakati wa kipigo yeye anakaa pembeni.
Lakini mkuu, Marekani awatumia Israeli na Ukraine kwa kazi zake kujitengenezea himaya zaidi duniani.

Marekani ataka Ukraine, ataka eneo la Pasific akimtumia taiwan na pia ataka eneo la mashariki ya kati akimtumia Israeli.

Kikwazo Mashariki ya kati ni Iran, Ukraine ni Russia na Kusini mwa Asia ni China.
 
Rabin alikuwa na tatizo gani au unakurupuka tuu.
Yitzhak Rabin aliuawa kwa baada ya kusaini mkataba wa Oslo mwaka 1994 na kiongozi wa wapalestina Yaser Arafat maarufu kama Oslo Accord.

Kwa kusaini mkataba huo Rabin akauawa (assassinated) na muisraeli mwenye msimamo mkali Yigar Amir mwaka 1995.

Leo hii waisraeli wenye msimamo mkali wameapa kwamba wataiangusha serikali ya Israeli endapo Benjamin Netanyahu atasaini mkataba wowote wa makubaliano na wapalestina.

Ndo maana suala la "two state solution" bado lachungulia dirishani na hii vita aloianzisha Netanyahu ni katika pia kujitengeneza na kujiimarisha kisiasa baada ya rekodi yake kuvurugwa na shambulizi la Hamas mwaka jana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…