Itapendeza zaidi kuomba radhi, kulinda hadhi ya kuendelea kuitwa mama

Itapendeza zaidi kuomba radhi, kulinda hadhi ya kuendelea kuitwa mama

Wanasiasa wanapotosha wananchi kwamba katiba ndio Suluhu la matatizo yote ya nchi hii na kwamba Rais awaze katiba mpya na kuharakisha mchakato wake.

Lakini kiuhalisia wanasiasa hao wanaona katiba mpya itaongeza nafasi ya wao kushinda uchaguzi. Huu ni ubinafsi wa hali ya juu.

Tumeona na kushuhudia hata mnapopewa nafasi majimbon au kuongoza halmashaur kadhaa hakuna unique features mnazoonyesha.

Binafsi naona Katiba mpya isiwe Kipaumbele ktk hali hii ya changamoto za kiuchumi duniani.

Na mkumbuke kwamba Rais Samia akiamua kuwajibu mnapokosa adabu za Kiafrika hataingia yeye front Bali atatumia vyombo vile vile alivyotumia JPM.

Muache Kudemka.
 
Bora aseme Katiba itakuja baada ya kuweka baadhi ya mambo sawa ila Ili kupooza joto la siasa yeye awaruhusu wapinzani wafanye siasa zao za mikutano ila maandamano iwe marufuku.

Afu nchi hii bado ccm ina nafasi kubwa ya kushinda hakuna sababu ya kuwa na hofu maana shida za nchi ni ndogo ndogo kama maji, barabara,afya,haki,elimu,umeme na biashara ambapo kwenye hili ameanza vizuri.

Lakini kubwa zaidi anaungwa mkono kwa sehemu kubwa na wanawake ambao ndio wapigakura wa kuaminika kuliko vijana wa mihemko.Aruhusu tuu demokrasia ila watakaotukana kama kina Mdude awatie adabu hakuna demokrasia na uhuru usio na wajibu na mipaka kwa mujibu wa sheria.
 
Ur acting as if Mama katawala miaka 2

mbona kwa Hayati hamkumpa hii pressure?.
Wanafki sana nyie..
mmekaa bila hio Katiba miaka 6 leo fyuu fyuu
Muacheni Mama
Mngekua mnaitaka kweli mngekomaa na Hayati
Inawezekana kupitia matendo mabovu kipindi cha hayati ndo watu wameona kuna hitaji la haraka kupata katiba bora.kwasababu mabadiliko toka kwenye kibovu kwenda kwenye kizuri hayana mwisho.kwahiyo kama ukuliona hitaji jana haimaanishi hautaliona hitaji leo.Ata sasa hakuna anayempa rais wa sasa pressure bali watu wanatoa mawazo yao.
 
Dawa yao inachemka.

Hatuyumbishwi na hatutetereshwi, Sisi wananchi tutaendelea kumuunga mkono Mheshimiwa rais ili tupate maendeleo aliyotuahidi.

Atakae jaribu kumkwamisha rais tutashuka nae jumla jumla
Walioshuka na watu wako wapi sasa ?!
 
Mama omba radhi watanzania kauri yako ya kusubiri kwanza kufufua uchumi ndiyo turuhusu marekebisho ya katiba na mikutano UA kisiasa hii umechemka.
1. Utachukiwa kuliko hata JPM
2. Utapoteza heshima ya kuitwa mama.
3. Utazalisha akina Sabaya na Makonda wengi kuliko JPM
4. Unaweza kuwa Rais wa mwisho kutoka Z'bar.
5. Mataia ya nje walioanza kukuunga mkono watakugeuka ndani ya muda mfupi.
6. Wanufaika wa utawala wa JPM wataungana na wapinzani kukushambulia.
7......
Nitaendelea nachaji simu kwanza.
Huo uchuro wala hautatokea,ni dua la mwewe,maza hatazalusha sabaya wala makonda hakuna mtu atakayekamatwa hovyo wala kupigwa
 
Rais Samia alikiri kwamba kasi ya ukuaji wa uchumi imedondoka kutoka 7% mpaka 4.7% kipindi ambacho JPM “alisimimamisha” matumizi ya Katiba huku akiomba apewe muda

Did it work? Nop. Sasa huyu Rais Samia anataka kutuambia nini? Anadhani issue ya kukuza uchumi ina deadline?

Huyu asiitwe tena Mama. Aitwe Rais Samia tu
Mbona kipundi cha jpm mlikua hamdai katiba , mwacheni mama achape kazi katiba tulionayo iko vizuri tu
 
Mama kweli akizingua kwenye matakwa ya wananchi anaweza kuchukiwa mara mbili ya alivyochukiwa Magufuli.

Maana calculations anazozifanya Samia ni kudhani kuwa anaweza kuituliza nchi hii kwa kurekebisha makosa ya Magufuli na kujenga uchumi imara peke yake na kwamba suala la katiba mpya linaweza kusubiri tu.

Kwenye kurekebisha makosa ya Magufuli yuko sahihi, kwenye kujenga uchumi yuko sahihi ila kwenye ishu ya katiba mpya amekosea tena amekosea kwelikweli.
Tatizo ninaloliona ni kuwa

1. Anaweza kujikuta anafikia hatua serikali yake ni unpopular sana na sasa ili kudhibiti sauti za wananchi basi naye akajikuta anarudi kulekule kwenye kufanya mambo yaleyale ambayo wananchi waliyoyachukia sana kwenye utawala wa Magufuli ya ubabe, ukatili, uongo mkubwa, propaganda kubwa, kununua wanasiasa kwa kuwahonga pesa na vyeo ili wamuunge mkono, na kuzidisha uonevu ili kunyamazisha sauti za wananchi wanaotaka mabadiliko nchini. Sasa akianza kufanya hayo atachukiwa mara kumi na kwa kuwa yeye siyo Bandidu kihulka kumfikia Magufuli, hatoweza kudhibiti hiyo hali, kimsingi anaweza kusababisha machafuko nchini.

2. Uchumi ni suala endelevu, halina mwisho wa ujenzi wake, Iwapo Atashindwa kumeet expectations za wananchi kwenye maisha mazuri na uchumi mzuri atakutana na hasira mbili, hasira za wananchi kunyimwa katiba yao wanayoitaka na hasira ya uchumi mbaya. Ilifikia hatua hii atakosa kitu cha kuwatuliza wananchi nacho!. kutegemea economic reform ukaachana na political reform, unakuwa unakuwa unacheza kamari, maana huo uchumi ukibuma basi unakuwa huna kadi ya kisiasa ya kutuliza joto hapo ni hatari.
Hili bandiko liwekewe pin, haya uliyosema yatatokea yote. Mwaka 2025 mama atakuwa unpopular at both sides ( wapinzani na CCM) kiasi kwamba atakuwa hana wa kumuunga mkono zaidi ya wazanzibar wenzake. Maana watu wengi waliokuwa wanamuunga mkono sasaiv walikuwa ni wapinzani, na sasa ameshaanza kuwapoteza
 
Mama kawatuliza hadi mmeanza mkosea adabu sio?

Hv mngeweza kumuambia Hayati maneno ya hivi?.

Msisahau na yeye ana madaraka yaleyale
Tumemtukana sana Magufuli humu jamii forum mpaka akamkamata Maxence Melo atoe true id za watu humu. Tumemtukana Magu na hajafanya chochote
 
Nafikiri unapaswa ujiulize swali moja, hivi hill neno mama mwanzilishi ni nani mpaka akaitwa mama? Kwa nini umama wake ushuke hadhi? Unafikiri wewe na wenzako mutampa thamani kwa sababu ya kupewa katiba mpya?
Kwa hiyo mlitaka mama baada ya JPM kufa aanze mchakato wa katiba mpya, are you sure kwa akili yenu mungemuona wa maana? Leo tunashuhudia vitu ambavyo vikitokea ambavyo havikutokea ndani ya miaka sita iliyopita, wafungwa wanatoka magerezani, vyombo vya habari vinaanza kuwa huru, wafanyabisha wanaanza kutabasamu, safari ya matumaini imeanza, lakini nyinyi bado mnatafuta namna ya kumkera na kumtafuta kama huyu mwanamke anaweza kuwa mkali?
Hata Yohana alipokuwa gerezani aliuliza maswali kama yenu, Yesu ndiye au asubiriwe mwingine, Yesu akamwmbia, sasa vipofu wanaona na viwete wameanza kutembea heri mwenye kuamini. Yohana pia alikuwa na haraka ya kutoka gerezani. Kumbuka watanzania wengi tupi kwenye hili gerezani la katiba, na katika ni jambo nyeti sana.
Iweni na subira kama mama alivyosema, kwani tupo wengi pia tuliopata tumaini kwa Huyu mama na hatuko tayari kuona akiyumbishwa, kwa sabaabu tumeiona nia njema aliyonayo. Narudia iweni na subira, iweni na subira, mama ameinjika chungu kiko jikoni ni dalili kwamba kila mtu atakula lakini unataka kutumbukiza mkono kushinikiza chakula kupakuliwe kabla hakijaiva. Tutakuunguza mdomo tena mtaunguzwa midomo tena sana ili hata chakula kikipoa kwenu kibaki kuwa chamoto ili musiwe na hamu hata ya kula, endeleeni kuwa na tabia kama ya watoto waliokataliwa tangu matumboni mwa mama zao.
Kipindi cha Jpm kuna watu tulisema kua kama kweli Jpm ni kiongozi mzuri basi ajitahidi atengeneze mifumo thabiti ya uendeshaji nchi ili ata siku akiondoka nchi iende kwenye misingi aliyoiweka,sasa kwasababu hakufanya hivyo ndo maana umetaja baadhi ya mambo ya ovyo yaliyofanyika kipindi chake sasa leo hayupo kwahiyo kuna uwezekano pia hiyu aliyepo akafanya aidha mazur au mabaya kabisa kwa sababu nchi bado haina mifumo na miongozo thabiti.Sasa tunakua ni nchi ya leo hivi kesho vile kutegemea tu rais kaamkaje.kwahiyo kama kweli ana nia njema na hili taifa basi ni vyema akaweka mambo mazuri kwa ajili ya nchi ili ata atakapoondoka nchi iendelee vyema.Na muda mzuri wakufanya jambo ni kipindi watu wanalizungumzia kwasababu hakuna aijuaye kesho.
 
Hili bandiko liwekewe pin, haya uliyosema yatatokea yote. Mwaka 2025 mama atakuwa unpopular at both sides ( wapinzani na CCM) kiasi kwamba atakuwa hana wa kumuunga mkono zaidi ya wazanzibar wenzake. Maana watu wengi waliokuwa wanamuunga mkono sasaiv walikuwa ni wapinzani, na sasa ameshaanza kuwapoteza
Mkuu mbona unaongea nadharia sana?
Yaani mwenyekiti wa chama tena mwenye kofia mbili akose ushawishi? Et sababu top oppositional leaders demands katiba mpya ndo akose ushawishi? Naamini wewe sio mgeni ni mzawa hapa bongo. Regime iliyopita ilikuwa na makosa kibao lakini ikapita kwa KISHINDO Asilimia zaidi ya 95%.

Au unafikiri mamlaka aliyokuwa nayo hayati, mama yetu hana? Msijifariji bhana. Tafteni namna ya kuongea na Mama sio kujidai mnaijua katiba sana. Huku wengine mkijidanganya mtaingia barabarani kwa maneno nyuma ya keyboard hahahaha. Wale jamaa wenye kofia nyekundu hawana kazi za kufanya mtajua hamjui.

Hata ningekuwa mimi nisingekubali yaani niwawekee mazingira ya kuingia kwenye uongozi kiulaini tu et sababu ya wapiga kelele. iiihiiiiii aaaaaahaaaaa.
 
Pumbavu sana hawa ndezi.

Wanataka twende nao hivi hivi kindezi ndezi.

Yaani jambo limekubaliwa, mnaambiwa Nipeni muda nishughulikie wao wameng'ang'ania tu ujinga ujinga.
Mambo mengine yamekuzidi uwezo wa kufikiri.uwezo wako kuvaa dera .kwanza nenda kabadili nguo ya ndani uku sio sehemu yako.
 
Back
Top Bottom