SI KWELI Iwapo tunda la nyanya linaonesha dalili kama hizi, linaweza kuwa na sumu kwa kung'atwa na nyoka

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kwa uelewa wangu mdogo..kuhusu hilinyoka ni hapana....
Nyoka hutumia sumu yake katika madhumuni makuu mawili,1..kuwinda na 2.ni kumdhuru adui....
Sasa hili la nyanya ni ukakasi kwa sababu...nyoka pia sio vegetarian.
Nimekupata mkuu... πŸ‘
 
Hapa umeshindwa, kutuelewesha sisi tunao soma coment.
Kwanza mimi nilivyoelewa hiyo picha ya nyoka imetumika kama mfano, maana siyo lazima awe aina hiyo.
Ila kwakua unaamini swila anaweza kuigonga nyanya, basi kuna haja ya kutilia shaka nyanya za namna hiyo, maana isije kuwa imetobolewa na swila.
 
Ukinywa sumu ya nyoka haufi labda uwe na vidonda mdomoni au tumboni kwasababa sumu ya nyoka ni venom na sio poison
Ni sawa ukinywa mtori haufi ila tukichukua mtori tukauweka direct kwenye blood stream hauchukui sekunde
 
Sumu ya nyoka ikishaingia kwenye tunda hilo tunda lazima liharibike mkuu. haliwezi kubaki kama lilivyo na hadi kupona
Hapo hata waje na majibu vipi ni ngumu kuwa elewa. mfano koboko akikung'ata muda sio mrefu utakufa na kuanza kuharibika haraka. vilevile aking'ata hata lile bapa la mkonge{katani} hukauka ama kunyauka kwa muda ule ule.

Kwa maelezo mengine naweza kusema kwamba hiyo picha kwa sisi wakulima huwa ni funza fln {caterpilar} huwa wanaingia kwenye tunda ukiwahi kumthibiti kwa sumu atakufa na tunda litapona na kuonyesha hali hiyo mkuu
 
Sumu ya nyoka au nge au tandu (venom) ina madhara ikiingizwa kwenye mfumo wa damu. Vinginevyo, haina madhara.
 
Inategemea na aina nyoka, kuna baadhi wana sumu kali wakikatiza juu ya kitu ukashika kuna namna unadhurika.
 
Kimtazamo huwa nafikiria kuwa meno ya nyoka ndo yana sumu, kumbe ipo ndani ya mwili wake... Au hii imekaaje mkuu??
 
Ukinywa sumu ya nyoka haufi labda uwe na vidonda mdomoni au tumboni kwasababa sumu ya nyoka ni venom na sio poison
Ni sawa ukinywa mtori haufi ila tukichukua mtori tukauweka direct kwenye blood stream hauchukui sekunde
Duh hapo kwenye mtori sasa ni mpya hii.. Kwamba mtori unaweza kusababisha blood clot??
 
Sumu ya nyoka au nge au tandu (venom) ina madhara ikiingizwa kwenye mfumo wa damu. Vinginevyo, haina madhara.
Tumekupata kiongozi πŸ‘πŸ‘
 
Kimtazamo huwa nafikiria kuwa meno ya nyoka ndo yana sumu, kumbe ipo ndani ya mwili wake... Au hii imekaaje mkuu??
Sumu haipo kwenye meno. Sijui inakuwaje hapo lkn Sumu Huwa ni option ya mwisho kabisa ya kujirinda ama kuwinda. Haitumii ovyo tu. Ndio maana ukutanapo na nyoka lazima atajitahidi akimbie iwapo ataona Bado una mfuata basi lazima ajihami kutumia siraha yake hiyo kama swila atatema mate kwanza Ili usione akimbie au vyote viwili
 
Umeeleweka mkuu πŸ‘πŸ‘πŸ‘
 
Kazi kuu ya jamiicheck ni kupembua maada tatanishi au zile zinazosambaza taarifa za uongo ili kuhakikisha kuwa taarifa au jambo limetolewa majibu kwa ufasaha , sasa nashangaa kwa nini hii thread imefutwa " katika pita pita zangu, nimekutana na maada inayosema kwamba matunda kama nyanya (pichani) yanaweza kushambuliwa na popo, au yoka, endapo binadamu atalitumia likiwa mbichi, afya yake inaweza kuathirika na sumu ya viumbe hao"

Sasa najiuliza:-
1. Je mmekosa majibu sahihi ya swali hili ??

2. Au moderator umeamua tu kufuta hii thread bila sababu maalum ??

3. Na je Kama majibu yamekosekana kwa nini msiache hii thread kama NADHARIA??
 
Wamefuta sababu wenyewe wamechoka kutafuta majibu au wamekutana na majibu wasiyokubariana nayo
 
Habari Nyafwili,

Mada hii inafanyiwa kazi, utapatiwa majibu hivi punde.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…