Jaji Mgeta: Niliumizwa na Waziri Mkuu kuchana Hukumu ya kesi niliyotoa kuwa kashindwa

Jaji Mgeta: Niliumizwa na Waziri Mkuu kuchana Hukumu ya kesi niliyotoa kuwa kashindwa

Magumu yake hayatuhusu, hakuna binadamu dunia hii hapitii magumu, hii ni lugha dhaifu na mtu dhaifu ndio hutaja taja magumu yake to public, hata Yesu kapitia magumu kuliko mwanadamu yeyote.

Magumu ni kwa kila binadamu, hatutaki mtu atutangazie magumu yake, akae nayo sbb kila mmoja ana magumu yake, tukianza kutangaziana hatutamaliza.
Umeshapanic 😂😂
 
KATIBA TU. MHIMILI MMOJA UMEJICHIMBIA ZAIDI UFUKULIWE NA KUNG'OLEWA NDIPO MAMBO YATAKUWA SAWIA. HAPA MAMBO YOTE LAZIMA YASUJUDU MHIMILI ULIOJICHIMBIA. Mfano: Ni dharau kubwa kujipanga msululu kumchagua mgombea na mnauhakika ameshinda halafu anapinduliwa na kuwekwa ambaye MHIMILI uliojichimbia unamtaka sio wananchi. Maneno ya Jaji yanatoa ushahidi WA umuhimu WA mfumo/katiba kuundwa Upya ili mihimili iheshimiane na kudhibitiana.
 
halafu umri wa kustaafu majaji ni miaka mingapi? inaonekana majaji wanao staafu wamezeeka sana!!! Kwa Nini umri wa kustaafu majaji usipunguzwe?!!! maana wamechoka sana!!!
Inaonekana wengi wao umri umesonga sana.

Wanadanganyaga umri
 
Alimchongea kwa prezdaa amle kichwa ili wamwonyeshe kazi, au kama vipi angemchongea kwa mheshimiwa chupika walale naye mbele kule mjengoni......wakishamwondolea cheo basi kwishaaa...
 
Huyu jaji mstaafu kaishi na nyongo kali muda mrefu, amepata nafasi ya kuitema ndio kaitema kwa kumsema huyo waziri mkuua akijua hayupo madarakani na hataweza kumjibu
 
Jaji aliyemaliza muda wake wa kuitumikia Mahakama, Jaji John Mgeta amesema katika kazi yake ya utumishi kama Jaji hatasahau namna ambavyo kigogo wa Serikali alichana hukumu mbele yake.

Jaji Mgeta ameyasema hayo leo Mei 4, 2023 muda mfupi baada ya hafla ya kuagwa yeye na majaji wengine wawili iliyofanyika Mahakama Kuu Kanda Masjala ya Dar es Salaam.

Jaji Mgeta amelitaja tukio hilo kama moja ya changamoto kubwa aliyowahi kukutana nayo katika utendaji wake.

“Miongoni mwa changamoto nilizokutana nazo ni kusimamia kesi ya aliyekuwa kigogo wa Serikali na kushindwa kesi kwa kigogo huyo. Katika shauri hilo kigogo wa serikali alishindwa kesi lakini nilipopeleka maamuzi ya mahakama aliyadharau na kuamua kuchana karatasi ya hukumu, kitendo hiki kiliniumiza sana na nilikosa furaha, lakini nashukuru baadae serikali ilisimama na kutekeleza kile kilichoagizwa na mahakama,”amesema Jaji Mgeta.

Awali, akizungumza katika hafla ya kuwaaga majaji hao, Jaji Kiongozi Mustapha Siyani amesema wananchi hawapaswi kuwa na wasiwasi na mahakama kwani ni huru na inatoa haki.

Jaji Siyani amewataja majaji hao waliomaliza muda wao wa utumishi kuwa ni Jaji Sekela Moshi, Jaji Beatrice Mtungi na Jaji John Mgeta ambapo amesema kuwa kipindi chote cha kazi kwa majaji hao walikuwa wanafanya kazi kwa weledi.

Amesema mbali na kuchapa kazi pia waliomaliza muda wao na wenye utii kwa kila mtu na kwamba kuondoka kwao ni pengo.

“Wananchi wakikosa imani na mahakama kila mtu atachukua sheria mkononi, na nchi yoyote duniani lazima iwe na mahakama, hivyo tuna mahakama nchi nzima zipo kwa ajili ya kuwasikiliza wananchi,” amesema Jaji Siyani.

Amesema kitendo cha kumaliza muda wao wa kazi kisheria ni alama tosha ya kuweza kuigwa kwa watumishi ili kuleta ufanisi katika kazi yao.

“Tunawakumbuka kwa bidii yenu ya kazi lakini na namna bora ya uongozi kwa kutatua kesi mbalimbali bila kujali ukubwa wake,” ameongeza Jaji Siyani.

Aidha, amesoma wasifu wa viongozi hao ambapo amesema wote walikuwa wamejaaliwa ujuzi katika kuandika hukumu pamoja hekima wanapokuwa na watu.

Chanzo: Mtanzania
Kwa nini kichwa ni waziri mkuu huku habari inasema ni kigogo aliyechana hukumu. Kama ni waziri mkuu mbona habari haimtaji jina. Tutajie alikua nani?
 
Kumbuka aliyefanya hivyo alikuwa kigogo wa serikali[emoji848]aliwaza mafao yake na penshen yake ya uzeen akaamua kutumia busara kuliacha lipite[emoji1787]he knows the court system is somehow fu.ck.e.d up[emoji1733]
Inasikitisha sana
 
Nauliza, Je Jaji mstaafu Mugeta kumtuhumu Waziri Mkuu mstaafu kwa kuchana hukumu mbele yake Je maneno hayo dhidi ya kiongozi Mkuu ni ukosefu wa maadili au Nini hiki?

Tuangalie vizuri mienendo ya Majaji kwa maoni yangu sio busara kumtuhumu kiongozi wa juu kama waziri Mkuu!!!

Tukiachia tabia hii kesho utasikia anatuhumiwa Makamu wa Rais siku nyingine Rais, huu ni utovu wa nidhamu ulio jificha kwenye mwamvuli wa kustaafu.

Unafiki na uzandiki ndio umewatawala vichwani mwao.
Naomba kutofautiana na wewe..

Kwa maoni yangu naona ni vyema kwanza ingejulikana kama ni kweli kuna huyo kigogo( Waziri mkuu) alichana hukumu ya mahakama? au jaji amejitungia stori?

Jambo la pili tujiulize,kama ni kweli alichana hiyo hukumu,ni jambo sahihi kwa kiongozi yoyote wa serikali kuchana hukumu kama hizo?

Jambo la tatu ni tujiulize,kuchana hiyo hukumu,kiongozi huyo aliidharau Mahakama kama mhimili au alimdharau Jaji husika? ( Maana tunaona aliyeumia ni jaji binafsi na wala siyo mahakama)

Kama hayo yote hapo juu ni kweli,je viongozi uliowaorodhesha hapo juu ukiwa na hofu kuwa iko siku nao watatuhumiwa, je wanayo haki ya kuchana hukumu iliyotolewa na viongozi wa mhimili mwingine?

La mwisho ni kuwa,maoni yako japo nayaheshimu, bali yamejaa ukale wa kuwatukuza viongozi uliowaita wa juu hata kama wakifanya makosa ya wazi,watu wakae kimya tu
 
Tuache kumlaumu jaji mstaafu kutotaja jina la waziri mkuu mstaafu.

Waandishi wa habari za kiuchunguzi wa magazeti na mitandao na raia wenye uchungu Mahakama kutishwa na wanasiasa wa chama tawala CCM waingie mtandaoni ili waweze kupata maamuzi ya kesi husika : Home | Tanzlii

Home
Image

Karibu kwenye Tanzania Legal Information Institute​

TanzLII ni tovuti ya Mahakama ya Tanzania inayochapisha maamuzi, Sheria na Kanuni kwa ufikiaji bure Mtandaoni. TanzLII provides free access to the law of Tanzania and is a member of the African LII community

Judgement database:

Judgment Databases​

Court of Appeal Arusha Registry
Court of Appeal Bukoba Registry
Court of Appeal Chake Chake Pemba Registry
Court of Appeal Dar es Salaam Registry
Court of Appeal Dodoma Registry
Court of Appeal Iringa Registry
Court of Appeal Kigoma Registry
Court of Appeal Mbeya Registry
Court of Appeal Morogoro Registry
Court of Appeal Moshi Registry
Court of Appeal Mtwara Registry
Court of Appeal Musoma Registry
Court of Appeal Mwanza Registry
Court of Appeal Shinyanga Registry
Court of Appeal Songea Main Registry
Court of Appeal Songea Registry
Court of Appeal Sumbawanga Registry
Court of Appeal Tabora Registry
Court of Appeal Tanga Registry
Court of Appeal Tanga Registry
Court of Appeal Vuga Registry
Court of Appeal Zanzibar Registry
High Court Arusha Registry
High Court Bukoba Registry
High Court Chake Chake Pemba Registry
High Court Commercial Division Arusha
High Court Commercial Division Dar es Salaam
High Court Commercial Division Mwanza
High Court Dar es Salaam Main Registry
High Court Dar es Salaam Zone Registry
High Court Dodoma Registry
High Court Iringa Registry
High Court Kigoma Registry
High Court Manyara Registry
High Court Mbeya Registry
High Court Mediation Center
High Court Morogoro Registry
High Court Moshi Registry
High Court Mtwara Registry
High Court Musoma Registry
High Court Mwanza Registry
High Court of Zanzibar
High Court Shinyanga Registry
High Court Songea Main Registry
High Court Songea Registry
High Court Sumbawanga Registry
High Court Tabora Registry
High Court Tanga Registry
High Court Vuga Registry
Labour Court of Tanzania
One Stop Judicial Center Temeke
High Court Commercial Division
High Court Corruption and Economic Crimes Division
High Court Labour Division
High Court Land Division
Source : Judgments | Tanzlii
 
Naomba kutofautiana na wewe..

Kwa maoni yangu naona ni vyema kwanza ingejulikana kama ni kweli kuna huyo kigogo( Waziri mkuu) alichana hukumu ya mahakama? au jaji amejitungia stori?

Jambo la pili tujiulize,kama ni kweli alichana hiyo hukumu,ni jambo sahihi kwa kiongozi yoyote wa serikali kuchana hukumu kama hizo?

Jambo la tatu ni tujiulize,kuchana hiyo hukumu,kiongozi huyo aliidharau Mahakama kama mhimili au alimdharau Jaji husika? ( Maana tunaona aliyeumia ni jaji binafsi na wala siyo mahakama)

Kama hayo yote hapo juu ni kweli,je viongozi uliowaorodhesha hapo juu ukiwa na hofu kuwa iko siku nao watatuhumiwa, je wanayo haki ya kuchana hukumu iliyotolewa na viongozi wa mhimili mwingine?

La mwisho ni kuwa,maoni yako japo nayaheshimu, bali yamejaa ukale wa kuwatukuza viongozi uliowaita wa juu hata kama wakifanya makosa ya wazi,watu wakae kimya tu
Hayo maswali yote uliyo yauliza hayana maana kwa wakati huu.

Yalikuwa maswali ya msingi wakati tukio lilipo tokea tu sio sasa.

Jaji alikuwa na malaka ya kisheria ya kuchukua hatua lkn akashindwa kuyatumia!! na kuachilia uhuru wake kuingiliwa na kudharauliwa kama ni kweli!!!! Hii ni stori ya kipuuzi kabisa na inalengo la kumdhalilisha kiongozi aliye tuhumiwa.

Kama alishindwa kuchukua hatua kipindi kile basi ni Bora angeendelea kukaa kimya kuliko alivyo onyesha udhaifu wake leo hii!!!!
 
Itasaidia Nini kwa sasa?!
alitakiwa asema jambo hilo wakati uleule angeonekana jasiri na mwenye msimamo madhubuti kuliko kusema sasa.

alionyesha udhaifu mkubwa sana kwa kutokuchukua hatua kipindi like na akabaki na maumivu Hadi Leo!!!!!!

anawafumdisha nidhamu ya uoga, kwamba ukifanyiwa jambo baya usiseme usubirie Hadi siku ya kustaafu ndipo uelezee kama stori!!!!!!!
Hapana. Jata sasa ina msaada. Kama ni Majaliwa, basi hii ni kashfa kubwa kwake, hastahili hata kuwa Waziri Mkuu.
 
Mahakama inahitaji utulivu wa kichwa.

Watu wazima akili zao ziko settled kuliko vijana wenye matamanio ya mambo mengi.

Mgeta alikua poa sana.

Sasa hivi Kuna mahakimu na majaji wadogo ila bado hawajaiva vizuri
Wale walioteuluwa na marehemu, wengi wao hawafai kwa sababu waliteuliwa kwa lengo maalum la kwenda kuua uhuru wa mahakama. Karibia wote walikuwa maafisa wa TISS.

Hata simba, siyo jaji yule. Fikiria afisa wa TISSS anapokuwa msajili.wa mahakama. Yeye ndiye anayepanga kesi gani isikilizwe na jaji gani.
 
Back
Top Bottom