Jaji Mkuu achukizwa na wapelelezi wanaokamata mtuhumiwa kabla ya kukamilisha upelelezi

Jaji Mkuu achukizwa na wapelelezi wanaokamata mtuhumiwa kabla ya kukamilisha upelelezi

Kama Mh. Jaji Mkuu anaweza kukemea sisi wananchi basi atumie mamlaka yake kukemea wapelelezi, wanasiasa, wakuu wa serikali kuwarundika watuhumiwa mahabusu na ikiwezekana atoe maelekezo maafisa hao wa Polisi wanaokiuka haki za watuhumiwa watiwe rumande kwa kukaidi maelekezo ya mahakimu na majaji walio chini yake Jaji Mkuu ili kulinda heshima ya Mhimili wa Mahakama na kubwa ni haki kutendeka
 
Mfano muafaka kabisa wa kuonesha unyonge wa Mhimili wa Mahakama. Jaji Mkuu wa Tanzania aache kuomba hisani au kulalama bali awachukulie hatua maafisa wanaokiuka haki za msingi za watuhumiwa kwa kuwafunga maafisa wakaidi wa idara ya polisi.

Yap, hiyo ndio hatua ambazo anapaswa kuchukua na sio kuongea lugha za kubembeleza kwakuwa sio yeye anayeteseka kwa uzembe, na hila za watawala na vyombo vya upelelezi. Kwa ujumla hiyo hali ya vyombo vya upelelezi kufanya kazi kwa kukomoa na kutokujali yeye ni sehemu ya hiyo dhuluma. Kama kungekuwa na mahakama binafsi kisha watu kupeleka kesi huko kwa kulipia, tungeona weledi wa hali ya juu na sio huo ugoigoi wa mahakama.
 
Huyu jaji hautendei haki mhimili Wa mahakama, yeye lazima alaumiwe.mhimili wake umekubali kutumika kisiasa, kesi ya maded Ni mfano halisia.badala ya kulinda katiba mahakama inatetea uvunjifu Wa katiba.
 
Tatizo wa Tanzania wengi hawajui haki zao zakiraia

Sent using Jamii Forums mobile app
Kaka ukishakuwa kwenye kundi la mwananchi huna haki yeyote dhidi ya wenye nchi. Hao kina Magoti ni wana sheria, wana harakati na wanafanya kazi katika kituo cha sheria na haki za binadamu na bado yanawakuta yanayowakuta.

Hao wanasiasa ambao wana mawakili na wengine wakiwa mawakili wanatendewa wanayotendewa itakuwa sisi? "kama mti mbichi unatendewa hivi itakuwaje kwa mti mkavu" Ili uwe na haki jitahidi uwe upande wa wenye nchi mkuu na si huku kwa wananchi
 
Jaji mkuu wa Tanzania ameshauri wapelezi wa kesi kuharakisha upelelezi wa kesi ndipo mtu akamatwe "Mahakama hazipaswi kulaumiwa kwa msongamano wa watu magerezani bali wapelelezi wa kesi, wapelelezi huchukua muda mrefu kukamilisha upelelezi na sababu wao kuchukua muda mrefu wakati mwingine hazina mashiko" Jaji Mkuu
Huyo nae ni team jiwe ndio amenajisi mahakama zetu kesi za utakatishaji anawape wakosoaji wa ccm,yeye ndio No.1 kuvuruga mahakama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaji mkuu wa Tanzania ameshauri wapelezi wa kesi kuharakisha upelelezi wa kesi ndipo mtu akamatwe "Mahakama hazipaswi kulaumiwa kwa msongamano wa watu magerezani bali wapelelezi wa kesi, wapelelezi huchukua muda mrefu kukamilisha upelelezi na sababu wao kuchukua muda mrefu wakati mwingine hazina mashiko" Jaji Mkuu
Ila Mh.CJ,the problem is faked allegations are very difficult and not easy to prove beyond doubts. I'm pretty sure that you know the route course, you have to do your home works.
Justice must be observed for all the Tanzanians.
 
Ngonjera tumesikia mno. Action speaks louder than words. Your Honor!!Hebu fanza hivii; Amuru wewe kama chief kuwa kesi yeyote itakayofika mahakamani na Dpp aseme, uchunguzi bado, hakimu atakayetoa sharti lolote la dhamana ufe naye. Mtu apewe dhamana ya kujidhamini mwenyewe aende kwao hadi siku polisi watakapo maliza upelelezi wamkamate na kumleta mahakamani si zaidi ya masaa 24 tangu kumkamata. Uone ka mahabusu zitajaa. Watatafuta mbuzi za kufungia humo au mbwa koko
 
Acha tu.
Sikukuu hizi kulala kituo cha polisi ni kawaida sanaa . kama kule mapinga bagamoyo.wanaishi kama wapo Somalia usiku wakikukuta wanakukamata unaenda kulala kituoni.yaani ni kamata kamata zisizokuwa na kichwa wala miguu.
Kifupi ni uonevu.
Tatizo wa Tanzania wengi hawajui haki zao zakiraia

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upelelezi utakamilikaje wakati wengi ni kesi zakusingiziwa?
Jaji mkuu wa Tanzania ameshauri wapelezi wa kesi kuharakisha upelelezi wa kesi ndipo mtu akamatwe "Mahakama hazipaswi kulaumiwa kwa msongamano wa watu magerezani bali wapelelezi wa kesi, wapelelezi huchukua muda mrefu kukamilisha upelelezi na sababu wao kuchukua muda mrefu wakati mwingine hazina mashiko" Jaji Mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiwekwa utaratibu ya kwamba ukimshikilia mtu pasipo hatia yapaswa alipwe fidia ambayo itakatwa kwenye mishahara ya waliosababisha uwe ndani,hii ingesaidia kupunguza idadi ya mahabusu pia tukapunguza gharam
Waambie jeshi la polisi wanaotupeleka lockup week nzima na kutuachia bila kosa.
Je? Huo muda tulioupoteza wataufidia vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
U
 
Jaji mkuu wa Tanzania ameshauri wapelezi wa kesi kuharakisha upelelezi wa kesi ndipo mtu akamatwe "Mahakama hazipaswi kulaumiwa kwa msongamano wa watu magerezani bali wapelelezi wa kesi, wapelelezi huchukua muda mrefu kukamilisha upelelezi na sababu wao kuchukua muda mrefu wakati mwingine hazina mashiko" Jaji Mkuu
tatizo ni ule muhimili unaotoa pesa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaji mkuu wa Tanzania ameshauri wapelezi wa kesi kuharakisha upelelezi wa kesi ndipo mtu akamatwe "Mahakama hazipaswi kulaumiwa kwa msongamano wa watu magerezani bali wapelelezi wa kesi, wapelelezi huchukua muda mrefu kukamilisha upelelezi na sababu wao kuchukua muda mrefu wakati mwingine hazina mashiko" Jaji Mkuu
Hivi ile kesi ya seifu vs lipumba huyu jaji kibaraka, kilaza alikuwa wapi?

Kesi ya wakurugenzi kusima.ia uchaguzi, Nayo ilitegemea upelelezi?

Wanasubiri watu wameishaumia ndo wanakuja kongea upumbavu

Kama ushaidi unacheleweshwa kuwe na limit ya muda, watuhumowa waachiwe, kusema tu haisadii bila kuja na suluhu ya tatizo
 
Huyohuyo wa Kenya aliyepigwa mkwara na Uhuru Kenyatta ktk uchaguzi wa marudio na akafuata mkia?
Tatizo mhimili huu wa Mahakama umepotezwa na mhimili wa dola.

Nchi zilizo na mihimili huru, Mahakama ikitoa dhamana kwa mtuhumiwa inatakiwa vyombo kama Polisi, TAKUKURU kuheshimu uamuzi wa Mahakama. Sana sana Polisi wanaweza kumtaka mtuhumiwa kuripoti Polisi kila mara kusaidia upelelezi ukamilike na siyo kumrundika mahabusu mtuhumiwa.

Mahakama kupitia kwa Jaji Mkuu watakuwa watu wa kulalamika mpaka lini juu ya suala hili la kikatiba?

Jaji Mkuu wa Tanzania aige wenziwe wa nchi za Jumuiya ya Madola kukataa kuburuzwa au kuomba Hisani na kusimama kidete kama Prof. Assad Mussa GAG au Jaji Mkuu wa Kenya Mh. David Maraga kuonesha kwa Vivendi kusimamia utawala wa sheria na Katiba

Jamhuri Day 12. December 2019
Jaji Mkuu Kenya akataa unyonge

Jaji Mkuu David Maraga asusia hafla kuonesha kuchoshwa na vitendo vya dola / serikali kubinya bajeti za Mahakama na uingiliaji wa shughuli za mhimili huu unaofanywa na watendaji wa serikali.




November 4, 2019

Ati mwasema Kumbe Kenya ina wenyewe ?
- Jaji David Maraga aidindia serikali na Bunge





Oktoba 28, 2019
Mahakama nchini Kenya zachechemea kwa kubinywa bajeti yake, huku idara zingine za serikali hazipitiwi na panga la kupunguza bajeti. Hii ni jinsi msuguano kati ya mhimili wa Mahakama na mhimili wa dola ilivyo, ila kuna nchi mhimili wa Mahakama haukubali kuwa nyonge mbele ya mhimili wa dola au Bunge.





August 20, 2019
Mahakama yaitaka mihimili ya Bunge na Dola kuongeza pesa za Mahakama


Mahakama yaitaka serikali kuongeza bajeti ya Idara hiyo muhimu ya kuamua haki nchini Kenya




July 30, 2019
Chama cha Mahakimu na Majaji nchini Kenya chaja juu kutokana na mwenendo wa mhimili wa dola / serikali kuu kuiburuza Idara hiyo nyeti inayounda Mihimili muhimu ya uendeshaji nchi. Hii ni kufuatia mihimili ya Bunge na Dola / Serikali kushutumiwa vikali na Jaji Mkuu wa Kenya Mh. David Maraga kutokana na 'njama' zao kutaka kudhoofisha mhimili wa Mahakama


Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwani ofc ya dpp iko chini ya nani?kama iko chini ya mahakama basi aiagize ibadilishe taratibu na kanuni za kizamani iende kisasa kama alivyoshauri
 
Back
Top Bottom