LGE2024 Jaji Warioba: Wapinzani Waliniambia Wangeweza Kupata Ushindi Kwa 25% tu

LGE2024 Jaji Warioba: Wapinzani Waliniambia Wangeweza Kupata Ushindi Kwa 25% tu

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

The Sunk Cost Fallacy 2

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2022
Posts
9,436
Reaction score
10,944
Swali.
Kama hivi ndivyo,Kwa nini CCM mnakuwa wadogo wa madaraka wakati kiuhalisia Wapinzani hawana uwezo wa kushindana na kushinda?

My Take
Ni vyema CCM ikajifunza Namibia sio lazima ushinde Kila pointi ndio uhasabiwe umeshinda.

Wapinzani wakishinda watangazwe Ili kuepusha chuki na sintofahamu kwenye jamii.

=====

"Mimi ninazungumza na vyama vyote na viongozi wao, si muda mrefu umepita, ilikuwa kama miezi sita hivi, nilimuuliza kiongozi mmoja wa upinzani, je, kweli mnategemea nini?

Akaniambia walikuwa wamefanya utafiti waone hali itakavyokuwa, alisema matokeo yaliyotoka kwamba tukijitahidi sana upinzani kwenye uchaguzi wowote unaokuja hatutazidi 25% wakijua kwamba wao kwa wakati huu hawana uwezo wa kuweza kutoa ushindani mkubwa, nikawauliza kwanini?

Wakasema ‘kwa miaka 6 shughuli za siasa zilikuwa zimesimamishwa, sisi hatukufanya kazi, sasa ndiyo tunaanza kufanya kazi, hatujasambaa hata kwenda chini, kwahiyo ukija uchaguzi kuna mahali hata hatutaweza kusimamisha wagombea’, na ndilo hilo ambalo limetokea.

Walikuwa wanasema asilimia 25, lakini hawakufika hata 1 kwasababu walijua hawana uwezo wa kuweka wagombea kila mahali, lakini hata walipokuwa na uwezo wa kuweka wagombea, wameenguliwa"- Jaji Warioba.

Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania Jaji Joseph Sinde Warioba akizungumza na wanahabari siku ya Jumatano Desemba 04, 2024 mkoani Dar es Salaam kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Novemba 27, 2024.
1733313418524.png
 
Swali.
Kama hivi ndivyo,Kwa nini CCM mnakuwa wadogo wa madaraka wakati kiuhalisia Wapinzani hawana uwezo wa kushindana na kushinda?

My Take
Ni vyema CCM ikajifunza Namibia sio lazima ushinde Kila pointi ndio uhasabiwe umeshinda.

View: https://x.com/Jambotv_/status/1864266399222210818?t=9_tJuEphhVqgXG2TcaRefA&s=19

Wapinzani wakishinda watangazwe Ili kuepusha chuki na sintofahamu kwenye jamii.

Kabisa mkuu..najua hawawez kushinda kwa asilimia zote kutokana na mizizi ambayo ccm imejiwekea. Lakini angalau waachiwe hata hicho kidogo wanacho pata.
 
Swali.
Kama hivi ndivyo,Kwa nini CCM mnakuwa wadogo wa madaraka wakati kiuhalisia Wapinzani hawana uwezo wa kushindana na kushinda?

My Take
Ni vyema CCM ikajifunza Namibia sio lazima ushinde Kila pointi ndio uhasabiwe umeshinda.

Wapinzani wakishinda watangazwe Ili kuepusha chuki na sintofahamu kwenye jamii.

=====

"Mimi ninazungumza na vyama vyote na viongozi wao, si muda mrefu umepita, ilikuwa kama miezi sita hivi, nilimuuliza kiongozi mmoja wa upinzani, je, kweli mnategemea nini?

Akaniambia walikuwa wamefanya utafiti waone hali itakavyokuwa, alisema matokeo yaliyotoka kwamba tukijitahidi sana upinzani kwenye uchaguzi wowote unaokuja hatutazidi 25% wakijua kwamba wao kwa wakati huu hawana uwezo wa kuweza kutoa ushindani mkubwa, nikawauliza kwanini?

Wakasema ‘kwa miaka 6 shughuli za siasa zilikuwa zimesimamishwa, sisi hatukufanya kazi, sasa ndiyo tunaanza kufanya kazi, hatujasambaa hata kwenda chini, kwahiyo ukija uchaguzi kuna mahali hata hatutaweza kusimamisha wagombea’, na ndilo hilo ambalo limetokea.

Walikuwa wanasema asilimia 25, lakini hawakufika hata 1 kwasababu walijua hawana uwezo wa kuweka wagombea kila mahali, lakini hata walipokuwa na uwezo wa kuweka wagombea, wameenguliwa"- Jaji Warioba.

Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania Jaji Joseph Sinde Warioba akizungumza na wanahabari siku ya Jumatano Desemba 04, 2024 mkoani Dar es Salaam kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Novemba 27, 2024.
Hii dhambi aliyofanya Mchengerwa malipo yake yatakuwa 2025, Mungu atawapiga kofi kubwa hawataamini macho yao.
 
Kabisa mkuu..najua hawawez kushinda kwa asilimia zote kutokana na mizizi ambayo ccm imejiwekea. Lakini angalau waachiwe hata hicho kidogo wanacho pata.
Hata hiyo 25% ilikuwa ni makisio ya Juu,wasingeweza pata labda 20%.

So hakuna sababu za msingi za kutumia Nguvu Kupitia kiasi.

Kuna Wilaya Fulani niliko yaani Wapinzani walikuwa wanaweza kushinda Mitaa na Vijiji sio zaidi ya kumi kati ya 132 ,Sasa shida zote za kulazimisha ushindi za nini?
 
Pascal Mayalla Sasa thibitisha yale nilivyosema juu ya uchawa wa kutisha wa radio ya Bakhressa Ufm kama kwenye
taarifa zao habari hii wataitoa .
Habari ya vyama vya upinzani wanavyotoa ni zile za DP, Demokrasia Makini, Ford, Labour Party na vyama kumi na nne vinavyo shonewa suti za kwenye press ya kuishutumu CHADEMA.
 
Hata hiyo 25% ilikuwa ni makisio ya Juu,wasingeweza pata labda 20%.

So hakuna sababu za msingi za kutumia Nguvu Kupitia kiasi.

Kuna Wilaya Fulani niliko yaani Wapinzani walikuwa wanaweza kushinda Mitaa na Vijiji sio zaidi ya kumi kati ya 132 ,Sasa shida zote za kulazimisha ushindi za nini?
Mwalimu Nyerere kwenye moja ya hotuba zake anasema "aliyezoea kula nyama ya mtu, haachi. Akiiona atakula tena." Na ndicho kilichotokea.
 
Mzee wetu, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Jaji Joseph Sinde Warioba, Nampenda na kumkumbali sana sana,

Maelezo, maoni, tahadhari nk nk alizozitoa mzee wangu je Jukwaa alilotumia ni sahihi kiasi gani?

Je Mzee wangu kwani si member wa Baraza la usalama wa taifa?

Je kama ni member wa Baraza la usalama wa taifa wao kama wazee wastaafu waliolitumikia hili taifa kwa jasho damu na kwa nguvu zao zote na baadaye kutengeneza viongozi hata hawa wa sasa Wameshindwa je kukaa wao kwanza wastaafu wa hilo Baraza, kisha yale ambayo wanaona watawala hawako sawa wakutane ana kwa ana na Rais, Waziri mkuu, Mkurugenzi mkuu wa usalama wa taifa, CDF na IGP waambie ukweli na hali halisi anavyoona wao,
Je hii ya kutoka hadharani tena mstaafu mmoja tu rais na watu wake watafanyia kazi maneno ya mzee wetu?
 
Pascal Mayalla Sasa thibitisha yale nilivyosema juu ya uchawa wa kutisha wa radio ya Bakhressa Ufm kama kwenye
taarifa zao habari hii wataitoa .
Habari ya vyama vya upinzani wanavyotoa ni zile za DP, Demokrasia Makini, Ford, Labour Party na vyama kumi na nne vinavyo shonewa suti za kwenye press ya kuishutumu CHADEMA.
Nilikuwepo kwenye press conference ya JSW, Azam media sikuwaona, hivyo wssipotoa ni kuwaonea bure!. Editorial policy na editorial independence ➕ pressures shaping the news, zinaamua news gani wa cover na news gani waache!。
P
 
Hata hiyo 25% ilikuwa ni makisio ya Juu,wasingeweza pata labda 20%.

So hakuna sababu za msingi za kutumia Nguvu Kupitia kiasi.

Kuna Wilaya Fulani niliko yaani Wapinzani walikuwa wanaweza kushinda Mitaa na Vijiji sio zaidi ya kumi kati ya 132 ,Sasa shida zote za kulazimisha ushindi za nini?
Hicho ni makisio ya chama kimoja. Tuseme hao ni Chadema ambao wangeweza kupata 20%. ACT Wazalendo nao wana ngome zao kwa hiyo labda wangeshinda 10% na CUF 5%, hivyo jumla ingekuwa 35% na CCM 65%. Hiyo inatosha kabisa kwa kujiweka kwa uchaguzi wa 2025.

Amandla....
 
Kabisa mkuu..najua hawawez kushinda kwa asilimia zote kutokana na mizizi ambayo ccm imejiwekea. Lakini angalau waachiwe hata hicho kidogo wanacho pata.

..wapinzani walimwambia Mzee Warioba wataweka wagombea 25%.

..kwa kumbukumbu zangu Chadema walikuwa wamejipangia lengo la kuweka wagombea 85%.

..Sasa tunapaswa kwenda kwenye uhalisia wapinzani waliweka wagombea asilimia ngapi na wakaenguliwa.

..Pia tuangalie Mchengerwa alibakisha wagombea wangapi baada ya kuengua?
 
Hiyo 25% ni kwasababu kwanza watu wengi walikuwa wamekata tamaa. Watu wengi walikuwa wanakataa kugombea kwasababu ya yale ya 2019.

Pili upinzani hawakuwa na resource watu na resource pesa. Vitu hivi viwili vinahitaji Hamasa kwanza.

Uchaguzi huu ungefanikiwa kwenda vizuri na upinzani wakashinda hata hiyo 25%. Uchaguzi wa 2025 ungelikuwa balaa maana Hamasa ingeongezeka mno. Hicho ndicho wanakiogopa CCM.
 
Hii dhambi aliyofanya Mchengerwa malipo yake yatakuwa 2025, Mungu atawapiga kofi kubwa hawataamini macho yao.

Nshengwerwa anajipanga kupokea kijiti kwa mkw3 wakw3.

Atawamaliza wote mpaka ndani ya Frelimo ili iwe rahisi kupita bila kutumia kifua .
Vijana ndani ya Frelimo ndio watakaoshughulikiwa mission ya kutokomeza na kukata mikia ikiisha . Watakaofuatia ni ndani ya Frelimo.

Binafsi namkubali Februa kuliko Nchengerema.
Februari hana mambo ya kishamba shamba na ya Udini Udini kama yule gaidi mbaobevu wa kule kanda ya ugaidi uliotikisa awamu ya 555.
 
Hicho ni makisio ya chama kimoja. Tuseme hao ni Chadema ambao wangeweza kupata 20%. ACT Wazalendo nao wana ngome zao kwa hiyo labda wangeshinda 10% na CUF 5%, hivyo jumla ingekuwa 35% na CCM 65%. Hiyo inatosha kabisa kwa kujiweka kwa uchaguzi wa 2025.

Amandla....
Aisee una akili balaa.Tungekuwa na Watanzania hamsini wanaofikiria kama wewe basi tungekuwa mbali sana.
 
Kabisa mkuu..najua hawawez kushinda kwa asilimia zote kutokana na mizizi ambayo ccm imejiwekea. Lakini angalau waachiwe hata hicho kidogo wanacho pata.
Huu uchaguzi wa serikali za mitaa unahitaji chama kiwe na mtandao mpana na fedha nyingi. Ila uchaguzi wa bunge upinzani wana uwezo wa kuweka mgombea kila jimbo. UKWELI ni huu: CCM kwa kusaidiwa na TISS hufanya survey ya namna serikali inavyokubalika kwa kutumia kura ya maoni na wanatumia wataalam wazuri sana. Hivyo ukiona wanapora kura ujue wameshajulishwa kuwa kiwango cha kukubalika ni kidogo sana. Hivi mnadhani CCM ingekuwa na uhakika wa kukubalika hata kwa asilimia 80 wangeiba kura?
 
Back
Top Bottom