LGE2024 Jaji Warioba: Wapinzani Waliniambia Wangeweza Kupata Ushindi Kwa 25% tu

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Ni kweli wapinzani wasingeweza kuweka wagombea sehemu zote lakini asilimia kubwa mijinini wangeza kupata viti vingi sana na mijini kuna watu wengi sana kuliko vijijini, asimia w5 ya mitaa ya mijini kwa mfano Dsm, Mwanza, mbeya, Arusha ni watu wengi sana ukicopare na vijijini. Yote kwa yote wanyang'anyi wamelamba vyote.
 
Hata mjini hawana jeuri ya kushinda kuzidi CCM.

Kuna maeneo mengi ya mjini Wabunge ni Wapinzani ila Halmashauri ni CCM so sio kweli
 

..tuchukulie kauli ya Mzee Warioba ni kweli.

..kama wapinzani walilenga 25% basi tuseme kiuhalisia wangepata 15%.

..kwa msingi huo CCM walikuwa wanakwenda kushinda kwa 85% ya kura.

..katika mazingira mazuri namna hiyo kwanini CCM hawakutuandalia uchaguzi mzuri na wa mfano duniani?

..CCM ni kama wamepatwa na wendawazimu. Niambie ni chama au mgombea gani wa uchaguzi hataridhika na ushindi wa 75%, 80%, au 85%.

..kuna ulazima gani wa kumwaga damu, na kuharibu uchaguzi, wakati uhakika wa ushindi wa halali upo?
 
Ulishawahi kufanya utafiti wowote katika maisha yako. Tell us about ur methodologies. Kwann huwa una hukumu kabla ya ku analyse ???
 
CCM ingeshinda tu. Shida ni kuiba kura ili washinde kama walivyojipangia bila kujua kuwa wanajiharibia kabisa kwa kuaminika kwa wananchi.
 
sidhani hata walistahili walichokipata,
nadhani hawakusatahili kupata chochote kwasababu hawakujiandaa kabisa.

hata hivyo,
walivyokwambia wangepata walau 25% kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, wewe uliwasaidiaje wapate zaidi ya hiyo? maana inaonekana wazi wewe ndio kama mpiga ramli chonganishi wao au mganga wao wa kishirikina kwenye chaguzi
 

ACT inaweza kuwa hata chama kikuu cha upinzani kama Chadema kitaendelea na siasa za kisanii na kumtegemea mbowe ambaye analamika muda wote kuwa anapata hasara za mali zake na fedha zake kuendesha chama .
Chama chenye wanachama mil. 6 hakina uwezo wa kujiendesha halafu kinataka kuingia madarakani . Ni chama cha kis3ng3 kabisa kuliko hata chama cha mashoga . Yaani hata Admini wa group la watu elfu moja anaweza kuliongoza na kujitatua matatizo ya group na sio kumtegemea mtu mmoja. Siku hizi hata harusi zinawezeshwa na watu na sio mtu .
Ina maana kwa bahati mbaya Mbowe akaanguka na kuparalize au kufa basi na Chadema kitakufa.


ACT hata namna wanavyojipanga kwa hoja na kwa sera wanaonyesha ni chama chenye dira inayoendana na watanzania . Ubapari wa chadema na Mbowe hauna mvuto kwa watanzania na hawajui kabisa dira ya chadema kwenye nchi ya kijamaa .

ACT kwa uchaguzi huru na haki wanapata 18 %+ Chadema 40% CCM 38%, Cuf 2% na vyama vingine vilivyobaki 2%.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba CCM haikubaliki kwa kizazi cha miaka ya kuanzia 2000 ambao ndio wengi sana . Kizazi hiki hakipigi kura kabisa kutokana na kutoamini zoezi zima la uchaguzi. Hawa siku akipatikana mtu wa mwenye ushawishi na mvuto kama alivyo Makonda basi Chadema wataingia ikulu Chamwino asubuhi na ACT kule Zanzibar saa sana mchana.

Hajapatikana Mpinzani anayepigania maslahi ya wananchi zaidi ya upinzani kutaka wananchi wapiganie maslahi ya chama kwa falsafa ya nguvu ya umma.
Umma kwenye ubepari haina nafasi ya kiuchumi zaidi ya siasa. Sasa Tanzania umma ni maskini unatakiwa kwanza ukombolewe kutoka kwenye umaskini . Dr.Slaa ,Mrema ,Makonda na Magufuli walifanikiwa kuteka mioyo ya umma kwa sababu wanazungumzia maslahi ya umma mkubwa kuliko maslahi ya vyama .
 
Lakini kuna namna wangeweza kuiba kwa kutumia akili mkuu.siyo unaiba kwa asilimia 99.9
 
Kabisa mkuu..najua hawawez kushinda kwa asilimia zote kutokana na mizizi ambayo ccm imejiwekea. Lakini angalau waachiwe hata hicho kidogo wanacho pata.
Siasa ni Biashara inalipa vizuri !
Ni nani yupo tayari kumuachia mwingine biashara yake ??!
Tuwe wakweli tu ! Ili tuwe Huru !
Au nasema uongo ???!
 
"Nilimuuliza kiongozi mmoja wa upinzani. Je, kweli mnategemea nini? Akaniambia walikuwa wamefanya utafiti. Matokeo yake tuliyoonyeshwa tukijitahidi sana upinzani kwenye uchaguzi wowote unaokuja hatutazidi asilimia 25"

Waziri Mkuu mstaafu Jaji Sinde Warioba.
 

Attachments

  • VID-20241205-WA0016.mp4
    4.1 MB
"Nilimuuliza kiongozi mmoja wa upinzani. Je, kweli mnategemea nini? Akaniambia walikuwa wamefanya utafiti. Matokeo yake tuliyoonyeshwa tukijitahidi sana upinzani kwenye uchaguzi wowote unaokuja hatutazidi asilimia 25"

Waziri Mkuu mstaafu Jaji Sinde Warioba.

Your browser is not able to display this video.
 
Sijawahi kumsikia Mbowe "akilalamika" kuwa anapata hasara za mali zake. Ni ukweli ulio wazi kuwa amepoteza mali zake kama Clubs, mashamba n.k. Ni kweli usiofichika kuwa ni Mwenyekiti pekee wa chama cha siasa ambae amewahi kufungwa, kupigwa, kuwekwa rumande n.k. bila kutetereka. Hao ambao wewe unaona ni mfano wa kuigwa hawajapitia theluthi moja ya aliyopitia na anayopitia Mbowe. Sio Slaa, sio Makonda, sio Mrema, sio Zitto.

Hatujasahau Slaa na Mrema walivyoimba nyimbo tofauti walipotikiswa kidogo. Slaa aliunga mkono juhudi kwa sauti kubwa na alikuwa mpiga debe mkubwa wa serikali ya awamu ya tano. Alikaa kimya hata pale waliokuwa wenzake walipokuwa wanashikishwa adabu. Mrema hivyo hivyo.

Hivi unataka wapinzani wapiganie vipi hayo unayoita maslahi ya umma? Juzi juzi Chadema wameita maandamano ya kukemea utekaji, upoteaji na hata kuuawa kwa wananchi. Wangapi wa hao wananchi walitokeza? Wangapi wa viongozi wa vyama vya upinzani waliojitokeza na kuwaunga mkono? Waliojitokeza ni Mbowe, binti yake ( baada ya watu kama nyinyi kudai kuwa ana wachuuza wananchi wa kawaida wakati watoto wake wanakula bata) na mashujaa wa Bawacha ambao kwa kusema kweli wako msitari wa mbele kwenye masuala kama haya. Wewe mwenyewe ulikuwa wapi? Hata wale waliopotelewa na ndugu zao hawakuonekana! ACT-Wazalendo walikuwa wapi?

Linganisha jinsi Chadema walivyokuwa wakipiga kelele wakati ACT-Wazalendo wanabanwa Zanzibar!

Vyama vya upinzani vitakabiliana vipi na umasikini unaozungumzia vikiwa nje ya serikali? Vyama hivyo vitakomboaje fikra za hao wananchi kutoka dhana ya utegemezi ( kutegemea sponsor kila wakati atayewatatulia matatizo yao) kwenda kwenye ya kujitambua bila vyama hivyo kuwa imara?

Ni rahisi mno kukebehi na kutukana wale ambao wanajitahidi kwa kiasi chao kukupigania kuliko kuingia mtaani na kuungana nao katika kutafuta haki yako.

Mbowe sio malaika lakini hastahili hii vilification mnayo mfanyia. Yeye, wanachama na wafuasi wa chama chake kwa kweli wanastahili pongezi.

Amandla...
 
Mimi sio mwanasiasa na sijui sana siasa wala sjui ni viti vingap vilikua vinagombewa ila kwa akili ndogo nafasi za wenyeviti wa mtaa zilikua zaid ya elf3+ na vyama vya upinzani ni zaidi ya 12+ na vyama ivyo vinataka 25% tu ya viti vyote huo ni upuuzi na ujinga wa kiwango cha kimataifa

Vyama vya upinzani vyenye zaidi ya miaka 30+ tangu vianzishwe vinawaza 25% afu tunasema tz kuna upinzani hapana tuna CCM A,B,C,D,E&+
 
Nakubaliana na Jaji Warioba. Kwa sababu kama walijipa makadirio ya kupata kura asilimia 25 hizo walizopata ni sahihi kabisa kutokana na maandalizi mabovu.

Nilizunguka vituo karibu 50 Dar hawakuwa na mawakala. Wamethibitishaje kura? CCM na serikali tunawapa mzigo badala kueleza ukweli upinzani wajipange.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…