Jamani, tuwe wakweli: Hali ni mbaya siyo kwenye Ndoa pekee bali hata Mahusiano mengine

Jamani, tuwe wakweli: Hali ni mbaya siyo kwenye Ndoa pekee bali hata Mahusiano mengine

Ipo hivi sasa niwachane;

1. Kama hauna akili kuwa singo ni mbaya, kuoa pia ni majanga.

2. Kama kichwani hapaeleweki kuwa katika ajira ni tatizo na hata kujiajiri ni taabu tupu.

3. Ukiwa waruwaru kuwa na njaa ni tabu tupu na kushiba vizuri ni shida pia.

Kwa upande mwingine sasa kama una akili utafaidi vyote tu hapa duniani kuanzia usingo, mahusiano hadi ndoa. Akili tu watu wangu. Mtu mpumbavu hata tu mpenzi wake akinuna yeye anachukulia kama personal attack kwake anaishia kusema ndoa chungu😏
 
Mifumo imeshindwa kutoa majibu ya maswali yanayokikabili kizazi hiki, mifumo ya dini, siasa, elimu, fedha, familia na sayansi na teknolojia! Ukinielewa utakua umejua jambo kubwa sana!
na jibu linakosekana sababu mifumo inachuana kuonyesha yupi bora ili kuchaguliwa, mwishoni wanaumia wachaguzi

"wakipigana tembo nyasi zinaumia"
 
Kuishi na mtu uliemloga ili awe kondoo Kuna maana gani!!?zaidi ya kuishi na roboti lililosetiwa na rimoti!!
Haya endelea kuishi na ndoa zako za miez 6..... Huku wenzako waliish miaka 50 mpk kuzikana!!
Anyway endeleen na 50/50 tunawasubiri kweny jukwaa la mapenz mje kutueleza jins ndoa zilivyowachakata
 
katika Kanuni alizoziweka mungu ukiaribu moja itaathiri na nyingine pia... nimemaliza
Mimi huwa najiuliza kwanini wanaopewa wadhamani Tanzania, huwa wanaahirisha kufikiri kizalendo a.k.a kujizima data halafu jamii inakaa kimya, (jamii ya kanyaga twende)
 
Wazee wa zaman walikuwa wakishaoa wanamlaza mke akili kabla ya lolote.... Hii code nilipewa na faza kwenye story za hapa na pale 🤔

Au basi🚶
comment bingwa sana hii mkuu nipe hiyo code vitu vya kufanya wanawake wa sasa wajifanya wajuaji sana bora kumlaza akili
 
Kizazi Cha kiume Cha kujitoa mhanga kwa wanawake na watoto kinageukwa na kusalitiwa sana !!

Kataa ndoa wanaendelea kupata point tatu!

Kwasasa mtoto anatumika kama chambo Cha kutumaliza me kiakili,kiuchumi Hadi uhai!

Elungata!
Sure
 
Ipo hivi sasa niwachane;

1. Kama hauna akili kuwa singo ni mbaya, kuoa pia ni majanga.

2. Kama kichwani hapaeleweki kuwa katika ajira ni tatizo na hata kujiajiri ni taabu tupu.

3. Ukiwa waruwaru kuwa na njaa ni tabu tupu na kushiba vizuri ni shida pia.

Kwa upande mwingine sasa kama una akili utafaidi vyote tu hapa duniani kuanzia usingo, mahusiano hadi ndoa. Akili tu watu wangu. Mtu mpumbavu hata tu mpenzi wake akinuna yeye anachukulia kama personal attack kwake anaishia kusema ndoa chungu😏
Mmasemaga ivyo ivyo mkishapigwa nyundo ya utosi ndo mnapata somo. Wanawake washavulugwa hawajali chochote. Kanuni pekee ya kuishi nao iliyobaki ni kuepuka kusaini ule mkataba wa ndoa na kujipa kipaumbele mwenyewe tu
 
Mmasemaga ivyo ivyo mkishapigwa nyundo ya utosi ndo mnapata somo. Wanawake washavulugwa hawajali chochote. Kanuni pekee ya kuishi nao iliyobaki ni kuepuka kusaini ule mkataba wa ndoa na kujipa kipaumbele mwenyewe tu
Kwan na ww unaamini kuwa wasiwasi ndo akili?

Sie wengine tunajua kuwa udadisi ndo akili so tunaingia, tunasaini na tukipata somo inakuwa ni kwa fulllu experience of it. Udadisi kamilifu..... akili mtu wangu, akili tu nakuambia
 
  • Thanks
Reactions: 2v1
Kwan na ww unaamini kuwa wasiwasi ndo akili?

Sie wengine tunajua kuwa udadisi ndo akili so tunaingia, tunasaini na tukipata somo inakuwa ni kwa fulllu experience of it. Udadisi kamilifu..... akili mtu wangu, akili tu nakuambia
Kuna tofauti kati ya kuogopa na kufanya maamuzi sahihi. Udadisi unaotaka kuufanya wewe, sisi ambao tupo mbele ya wakati tulishaufanya kitambo kirefu ndio maana tukaja na maamuzi sahihi.
 
1)MAADILI KUSHUKA KATIKA JAMII
Hofu ya Mungu kushuka
Uzinzi michepuko fasheni
Dhambi imekuwa kitu cha kujisifia

2)NAFASI YA MWANAMKE IMEPANDA
Wanawake wamepanda ki ELIMU kujua haki zao na wanazitetea wanatetewa,nafasi za usawa katika sekta zote uongozi pia ,pia wapambanaji wanatafuta pesa,wanafanya baadhi ya shughuli/kazi zinavyofanywa na wanaume .

3)NDOA HAIHESHIMIWI
Kuachana imekuwa ni rahisi tu,kuwa single mother single father ni kitu cha kawaida,uvumilivu umepungua au haupo.

4)KUTOJITAMBUA KUKOSA AKILI/BUSARA/ULIMBUKENI
Kuna wanaotema bigi ji kwa karanga za kuonjeshwa.
Kuna wanaopata bahati au neema ya kuwapata wenza sahihi ila wanawaacha na kuamua kwenda kwa wanaume masharobaro au wanawake wenye muonekano mzuri au makali makubwa lakini wasio na akili.Mpumbavu huibomoa ndoa yake kwa mikono yake mwwnyewe badala ya kuijenga.
Mwisho wa siku wakitendwa huko walikokimbilia ndio hukumbuka shuka na kutaka kuyarudia matapishi.

5)KUKOSA UNYENYEKEVU
EGO kuwa juu kuna wakati inabidi kwenye baadhi ya vitu ujishushe uwe mjinga na yeye kuna baadhi ya vitu awe mjinga ili mfike kati kati mwende sawa.Yani kuna vitu kila mmoja havipendi kitoka kwa mwwnzake kila mmoja awe tayari ku compromise ili mfike kati.KUSIKILIZANA ,KUVUMILIANA ,KUHESHIMIANA.

6)UPENDO ndio cha mwanzo unatakiwa ujue kwanini mwenza wako ameamua kuwa na wewe na wewe kwa nini umeamua kuwa na yeye.Kupata muda wa kuchunguzana na kujua kuna upendo .Kama ni mwenzako anakuhitaji kama wewe unavyomuhitaji yeye.Yani mapenzi ya upande mmoja.
Mi naamini kama una akili timamu inteligence ndogo ya kumsoma au kumchunguza mtu,ni rahisi kujua huyu mwenza niliyenaye ana sifa za kuingia naye kwwnye agano la ndoa au hapana.Kusoma dalili ya mvua ni mawingu.Mana anayejipiga mwwnyewe halii.Yani kuna sehemu unajichomeka unaona kabisa hapa ni kwenye hamna unategemea atakuja kubadilika ndani ya ndoa sio rahisi.
Kama kulikuwa na uzi kuna mtu alikuwa anasema anataka aoe baa medi sasa ina maana huyu anataka kubadilisha daladala iwe gari binafsi,au sumu kwa kuionja
Ipo njia ionekanayo njema machoni pa mwanadamu ila mwisho wake ni mauti
NI VIZURI TUONGOZWE NA AKILI SIO HISIA ZA MAPENZI
Pia tuongozwe na Mungu katika kupata mwenza sahihi.
NI BORA KUZIBA UFA KULIKO KUJENGA UKUTA.
Ni bora kuachana katika hatua ya uchumba kabla ya ndoa kama utapata muda wa kutosha wa kuchunguzana katika hatua ya uchumba kabla ya ndoa.,kuvunja uchumba ni bora kuliko kuvunja ndoa.
 
1)MAADILI KUSHUKA KATIKA JAMII
Hofu ya Mungu kushuka
Uzinzi michepuko fasheni
Dhambi imekuwa kitu cha kujisifia

2)NAFASI YA MWANAMKE IMEPANDA
Wanawake wamepanda ki ELIMU kujua haki zao na wanazitetea wanatetewa,nafasi za usawa katika sekta zote uongozi pia ,pia wapambanaji wanatafuta pesa,wanafanya baadhi ya shughuli/kazi zinavyofanywa na wanaume .

3)NDOA HAIHESHIMIWI
Kuachana imekuwa ni rahisi tu,kuwa single mother single father ni kitu cha kawaida,uvumilivu umepungua au haupo.

4)KUTOJITAMBUA KUKOSA AKILI/BUSARA/ULIMBUKENI
Kuna wanaotema bigi ji kwa karanga za kuonjeshwa.
Kuna wanaopata bahati au neema ya kuwapata wenza sahihi ila wanawaacha na kuamua kwenda kwa wanaume masharobaro au wanawake wenye muonekano mzuri au makali makubwa lakini wasio na akili.Mpumbavu huibomoa ndoa yake kwa mikono yake mwwnyewe badala ya kuijenga.
Mwisho wa siku wakitendwa huko walikokimbilia ndio hukumbuka shuka na kutaka kuyarudia matapishi.

5)KUKOSA UNYENYEKEVU
EGO kuwa juu kuna wakati inabidi kwenye baadhi ya vitu ujishushe uwe mjinga na yeye kuna baadhi ya vitu awe mjinga ili mfike kati kati mwende sawa.Yani kuna vitu kila mmoja havipendi kitoka kwa mwwnzake kila mmoja awe tayari ku compromise ili mfike kati.KUSIKILIZANA ,KUVUMILIANA ,KUHESHIMIANA.

6)UPENDO ndio cha mwanzo unatakiwa ujue kwanini mwenza wako ameamua kuwa na wewe na wewe kwa nini umeamua kuwa na yeye.Kupata muda wa kuchunguzana na kujua kuna upendo .Kama ni mwenzako anakuhitaji kama wewe unavyomuhitaji yeye.Yani mapenzi ya upande mmoja.
Mi naamini kama una akili timamu inteligence ndogo ya kumsoma au kumchunguza mtu,ni rahisi kujua huyu mwenza niliyenaye ana sifa za kuingia naye kwwnye agano la ndoa au hapana.Kusoma dalili ya mvua ni mawingu.Mana anayejipiga mwwnyewe halii.Yani kuna sehemu unajichomeka unaona kabisa hapa ni kwenye hamna unategemea atakuja kubadilika ndani ya ndoa sio rahisi.
Kama kulikuwa na uzi kuna mtu alikuwa anasema anataka aoe baa medi sasa ina maana huyu anataka kubadilisha daladala iwe gari binafsi,au sumu kwa kuionja
Ipo njia ionekanayo njema machoni pa mwanadamu ila mwisho wake ni mauti
NI VIZURI TUONGOZWE NA AKILI SIO HISIA ZA MAPENZI
Pia tuongozwe na Mungu katika kupata mwenza sahihi.
NI BORA KUZIBA UFA KULIKO KUJENGA UKUTA.
Ni bora kuachana katika hatua ya uchumba kabla ya ndoa kama utapata muda wa kutosha wa kuchunguzana katika hatua ya uchumba kabla ya ndoa.,kuvunja uchumba ni bora kuliko kuvunja ndoa.
picha chini inaelezea point namba 5
TV ya chogo na stendi ya tv ya flat screen.
Ndo hii inawezekana kati ya MR.TV CHOGO na miss stend ya flat tv
Kama tv chogo ata kuwa mnyenyekevu aji adjust kuendana na stend iliyopo,na stend atakuwa mvumilivu na kujishusha kunyenyekea na kuvumilia kumbeba tv chogo na kumchukulia madhaifu yake na mapungufu yake.
UVUMILIVU,KUJISHUSHA UNYENYEKEVU,KUBEBANA,KUHESIMIANA,UPENDO,KUSAMEHEANA,KUFANYA VITU KWA PAMOJA KUSHIRIKIANAKUAHIRIKISHANA,HOFU YA MUNGU NA UPENDO
 

Attachments

  • Screenshot_20241031-223912.jpg
    Screenshot_20241031-223912.jpg
    271.4 KB · Views: 2
Mifumo imeshindwa kutoa majibu ya maswali yanayokikabili kizazi hiki, mifumo ya dini, siasa, elimu, fedha, familia na sayansi na teknolojia! Ukinielewa utakua umejua jambo kubwa sana!
Kiriba kipya, mfumo mpya
 
Ndoa ni tatizo kubwa sio dogo na tatizo kubwa ni Mwanaume kurudisha mpira kwa kipa hasa akiteteleka kipato Wanawake wengi wa mjini sio wavumilivu wanataka kila siku uwe na pesa na ndio maana unaona sehemu wanazouza vilevi zinajaa sana mtu anaona bora arudi nyumbani mwenza wake akiwa amelala kupunguza zogo.
 
Tukubaliane na mabadiliko tuliyoyapokea kwa jina la utandawazi, kwa waliotuletea utandawazi tayari wana solution za vitu ambavyo kwetu Leo hii vinaonekana ni changamoto, kuendelea na mbinu za kuvumiliana kwenye shida na raha hadi kifo kiwatenganishe hakuendani na Hali halisi ya mfumo wa maisha ya sasa ingawaje inaweza kuwa relevant kwa Jamii ndogo sana
 
Hapa napokea ujumbe toka kwa jirani yangu amepanda mbegu kwa shemeji wa jirani yake anaomba kusindikizwa kwenda kurekebisha hali ya hewa
😄😄😄 Usiende mnaeza uliwa wote.
 
Back
Top Bottom