James Rugemalira aachiwa huru, DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka

James Rugemalira aachiwa huru, DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka

Huyu jamaa anastahili kuwa tajili, ana roho ngumu na kauzu kisawasawa.

Yule marehemu dhulumati kamchimba mikwara yote mzee kakaza bora afie jela kuliko kutishwa na mwehu.
Duh! Mwhehu tena. Hapo upipo uko chini ya ulinzi!!!
 
Mtu kauza kampuni yake, kalipa na Kodi kwa Kayafa, hapo kosa lake nini?
Shida ilikuja pale tulipotaka waliohusika wawajibishwe, nadhani unakumbuka mkutano ule wa bunge ulienda hadi saa 4 usiku, huku mbowe akitahadharisha kuwa tutaenda kuwa failed state.
Baada ya muda kikwete alimuwajibisha mama tibaijuka.
Ikiwa hakukuwa na shida basi tuseme tulikosea kuomba waliohusika na escrow kuwajibishwa, na mama tibaijuka aombwe msamaha kwa kufutwa uwaziri
 
Mimi nimemkubali, mzee ameona potelea Kwa mbali afie gerezani watoto wabaki na utajiri, hiyo ndio Tafsiri ya Kufa kiume
vijana tijifunze kupata hela ni jambo moja na kuilinda ni jambo jingine linahitaji uwe kauzu na roho ngumu
"it takes talent to make money,but it takes brain to keep it"

Rugemealira msimamo Kama che Guevara
 
Kama jamaa yako alikuwa mkweli. Mbona hakuwakamata Simba trust ?!. Yule alikuwa mnafiki tu.

Jamaa yangu gani? Ukweli hauna ujamaa wala kupepesa macho, hata hivyo amejifunza kuwa malipo ni hapa hapa kwa ubaya wake.

Kuna mtu anaitwa Simba Trust? Au sijakuelewa. Kampuni ni watu na washirika wake ni watu.
 
Hii kesi alie loose ni singa singa[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Ndio alikuwa mlengwa ...
Ruge tatizo lake ni kuchanganya pesa zake safi kuchanganywa na chafu ......

Ni dhahiri kuwa kuna raia wengi wapo nyuma ya nondo kwa mizengwe mama endelea kufungua milango yao.....
 
Kama kweli Mungu amsimamie na wadhalimu wooote waendelee kupatwa na yale ambayo yalimpata mwendazake. Huwezi kuonea watu ukaishi Mungu sio binadamu. Mungu amtetee huyu mzee aendelee kuona watesi wake wanavyopakatika
Kwa nchi hii ilivyo hasa wakati ule wa awamu ya 4, ni vigumu kwangu kuamini kuwa hawa majamaa walibambikiwa kesi. Kapuku kama mimi nawewe kushangilia kuachiwa kwao ni mapema sana, ngoja Lissu aje atupe za ndani ndani. Tumezoea kupigwa na tuendelee kupigwa. Upinzani una ajenda nzuri za kampeni 2025. Na kwa speed hii mgombea yeyote wa CCM akipata 50% aende kwa mganga!

DPP mpya kasimikwa, mwanasheria mkuu mpya kasimikwa leo kesi iliyokuwa ngumu kama chuma inalainishwa kama keki...Mmmmmmmm. Watanzania ndio waliwao.
 
Acha wapige.

Mtu yeyote mwenye nafasi kama hatapiga hela atakuwa ni mpumbavu wa hali ya juu sana.

Namshangaa sana Mbowe ana kila kitu sasa anapata tabu yote kisa kumpigania mtz? Mtz yupi?

Ukirejea hoja za wanachadema enzi za Jk juu ya Rugamalila na sasa aisee..

Narudi! Mtu mwenye nafasi hapa nchini kama hatapiga hela atakuwa mpumbavu sana.
Mawazo finyu sn
 
Kwa nchi hii ilivyo hasa wakati ule wa awamu ya 4, ni vigumu kwangu kuamini kuwa hawa majamaa walibambikiwa kesi. Kapuku kama mimi nawewe kushangilia kuachiwa kwao ni mapema sana, ngoja Lissu aje atupe za ndani ndani. Tumezoea kupigwa na tuendelee kupigwa. Upinzani una ajenda nzuri za kampeni 2025. Na kwa speed hii mgombea yeyote wa CCM akipata 50% aende kwa mganga!

DPP mpya kasimikwa, mwanasheria mkuu mpya kasimikwa leo kesi iliyokuwa ngumu kama chuma inalainishwa kama keki...Mmmmmmmm. Watanzania ndio waliwao.
Akifungwa wew utapata nn!?
 
View attachment 1940085
Salaam Wakuu,

Leo nimepita maeneo ya Mahakama ya Kisutu, Nikakuta Mkurugenzi wa kampuni ya VIP na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL, James Rugemalira anatabasamu akiwa na ndugu zake wakipeana hugs na kuchumiana. Inaashilia kuna dalili nzuri leo Mzee wa Henken akaliona jua. Langu Dua.

_MG_0435.JPG

James Rugemalila(Kulia) na mmiliki wa Kampuni ya IPTL, Harbinder Seth Sigh(Kushoto), wakiwa chini ya ulinzi wa Polisi kabla ya kupanda kizimbani Mahakamani Kisutu Jijini Dar.

Tarehe 19 Jun, 2017 TAKUKURU wawafikisha mahakamani Seth Na Rugemalila kwa uhujumi uchumi. walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu wakishtakiwa kwa makosa sita ya uhujumu uchumi, likiwamo la kuisababisha Serikali hasara ya jumla ya takriban Sh358 bilioni.

Wakili wa Serikali, Paul Kadushi aliyataja mashtaka mengine yanayowakabili wawili hao kuwa ni kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu na kuisababishia hasara Serikali.

Zaidi Soma:

1). TAKUKURU yawafikisha mahakamani Harbinder Sethi na James Rugemalira kwa kosa la Uhujumu uchumi

UPDATE:

Rugemalila yupo huru!

Mashtaka yake yameondolewa chini ya kifungu cha 91(1) cha Mwanendo wa Makosa ya Jinai

View attachment 1940204

View attachment 1940227
Huyu ndio mwanaume... Unakufa na siri gerezani. Ukitoka unakula nchiii.... Nimempenda kiukweli.
 
Ukijifunza akili na miemko ya watanzania wala hupati shida.

Yaani unaweza kufanya lolote mpaka kuwaumiza watakuchukia kwa muda mfupi then wanageuka kukuonea huruma yaani.

👉🏾Chukua maisha ya maasai yaani yeye kila mtu ni rafiki, ndivyo ilivyo kwa mtanzania 🤓!.
 
Back
Top Bottom