Jamhuri yakata rufaa dhidi ya Masheikh Uamusho

Jamhuri yakata rufaa dhidi ya Masheikh Uamusho

Me zamani nilikuwa ninadhani kuwa kupata haki mahakamani ni kule kuachiwa huru, nilikuwa najidanganya.

Kumbe hata kupatikana na hatia na kufungwa ni haki pia!
haki ni haki iwe kwa yeyote.
 
Kama kweli walifanya vitendo ya kigaidi wanastahili vifungo kwa mujibu wa sheria.

Ogopa ugaidi ni hatari ,just imagine WTC ilivyoshuka na kuua watu 3000+ ,kama kweli walifanya vitendo vya ugaidi waendelee kusota tu mahabusu ila kama si kweli watatoka tu maana ushahidi utakuwa hakuna.
Kwanini wasifungwe? Hivi kwanini wakae mahabusu bila sababu ya msingi? Mahakama iwahukumu kwa makosa yao sio kuwaweka watakaa miaka mingapi? Mahabusu
 
2021 bado unaamini WTC ni shambulia la kigaidi? Like seriously???
kuna mzee mmoja kaishi USA miaka 21...na kipindi tukio la 9/11 alikuwepo kule anakwambia lile tukio limetabiriwa kutokea toka zamani sana sio eti ni ugaidi kama tunavyo karirishwa huku,ile ni mipango ya wazungu kuuhadaa ulimwengu tu.
 
Nikikumbuka mtiti wa hawa jamaa wa uamsho nasikitika sana, wali mobilize vikundi vya wahuni waliokata tamaa wakawajaza maujinga ya dini kwenye bongo zao ili wakawadhuru watu kutoka bara na wasio waislam pia, sema nashukuru maeneo niliyokuwa naishi( MBWENI) wabongo wengi na hata waislamu waishiyo maeneo hayo ni wastarabu na wenye kujitambua ila huko uswahilini kama D/bovu, Aman, Bububu, Mtoni nk yaani ilikuwa kujitambulisha kwamba wewe ni mkristo unaogopa kuhofia usalama wako.

Dhambi ya ubaguz ni mbaya sana, walipomaliza kuwabagua wabongo wakaja kwenye uunguja na upemba, ilifikia stage kupata kitambulisho cha mzanzibar mkaaz ukiwa unatoka Pemba ni shida na huwez kuajiriwa SMZ kama huna hicho kitambulisho, ila tunamshukuru sana Mh Hussein Mwinyi amekuja kuondoa huu upumbavu watu sasa hivi wanaishi kwa amani kabisa.

Sent from my TECNO-W5 using JamiiForums mobile app
 
kuna mambo ya kuyaangalia sana kwa ustawi wa Taifa.......kuna watu watasema watashangilia wakiachiwa, na wenginge wakiendelea kusota mahabusu.....tujiulize amani ya Tanzania iko mikononi mwa wakina nani?..nna hakika ni mikononi mwetu kwa umoja wetu......tunajua madhara yaliyotokana na misimamo ya hao ndugu zetu???sawa wao familia zao zinateseka,,,, na waliodhurika na chokochoko zao kuna ambao ni walemavu milelel.....hapa haki itendeke....ila kwa weledi wa hali ya juu...sio kwa mihemko......ila ninachojua itachukua miaka mingi sana......hakuna mtawala anaetaka machafuko yaanzie kwenye kipindi chake........kila mmoja anasema ngoja nimalize muda wangu...danadana mpaka kitenesi kipasuke.....tuzidi kuwaombea....najua wamejifunza....sitaki kuamini kama wale ni waislamu......Waislamu wa Kweli wana Hekima na Busara.....ila wametumia kivuli cha uislamu.....ni ndugu zetu wale....
 
kuna mzee mmoja kaishi USA miaka 21...na kipindi tukio la 9/11 alikuwepo kule anakwambia lile tukio limetabiriwa kutokea toka zamani sana sio eti ni ugaidi kama tunavyo karirishwa huku,ile ni mipango ya wazungu kuuhadaa ulimwengu tu.
Hahaha, hizi akili hizi
 
Wana wamekata Rufaa

Na nyie mlizidi...mlishangilia ushindi wa yale mashitaka yaliyotolewa mapema.....

Angalia sasa wanakatia rufaa ngoma ianze upyaa....
Heee!!kwa hiyo wasingeshangilia serikali isingekata rufaa?!!daaa, mawazo mufu
 
Hiyo ni danganya toto tu ili isionekane mwendazake alikuwa na mkono.

Mbona hiyo case ishakwisha tangu ujasiri wa kukiri mapungufu Mar 17 ulipopatikana?

Ni suala la muda tu.
Wewe utakuwa namatatizo ya akili,mwendazake kawakuta hao mashehe walishakamatwa siku nyingi,leo unamsingizia kitu ambacho yeye amemkuta ?,kwa kweli upumbavu ni mzigo
 
Kabla ya mashekh kukamatwa kulikuwa na vitendo vya uhalifu kama mapadri kumwagiwa tindikali na makanisa kuchomwa moto. Ila walipokamatwa mpaka leo hii ni amani, hakuna padri au kiongozi yoyote kamwagiwa tindikali na makanisa hayajachomwa moto mpaka leo.
Kinachoogopesha zaidi, hawa watu wakiachiwa huru huenda kitaibuka kikundi cha Islamic State km Msumbiji, Nigeria na Somalia .

Ila wee jamaa unawachukia sana waislamu, mada kama hizi huwa hukosekani na kutoa maneno makali. Mungu akuongoze
 
SHIDA KUNA WATU WANASAHAU KUWA HII NI TANZANIA HIZO HAKI MNAZOSEMA MNAPATA MAHAKAMANI NI MPAKA SERIKALI IAMUE WALIKAMATWA HENZI ZA JK MPAKA LEO DANADANA WAMEWAACHA MFUNGE GOLI MOJA WA WANAENDA KUPIGA 3
 
Huyo wakili mwenye mawazo ya kukata rufaa dhidi ya watu waliokaa miaka 9 ndani bila hukumu sidhani kama ana akili.Kukaa mahabusu tu ni hukumu tosha
 
Bismillahir Rahmaanir Rahiim

SHURA YA MAIMAMU TANZANIA

LEO TAREHE 28.04.2021, SERIKALI IMEKATA RUFAA MAHAKAMA YA RUFAANI DHIDI YA MASHEIKH

Tarehe 23.04.2021, Mahakama Kuu ilitoa hukumu ya ushindi kwa Masheikh wa kesi 14, Kati ya 25, zilizokuwa zinawakabili Masheikh.

Baada ya uamuzi huo shauri lilipangwa liendelea leo kwa kusikilizwa kesi 11, zilizobaki.

Katika hali ya kuonesha nia ya Serikali ya kuendelea na msimamo wake dhidi ya Masheikh hao leo hawakufika Mahakamani kama ilivuotarajiwa na badala yake wametuma hati ya kukata rufaa dhidi ya hukumu iliyowapa ushindi wa kesi 14, Masheikh.

Kufuati hatua hiyo shauri hilo litasitishwa kuendelea Mahakama Kuu mpaka litakaposajiliwa Mahakama ya Rufani na kukapangiwa Majaji wa kusikiliza na hatimaye kutolewa uamuzi.

Wito wa Shura ya Maimamu Tanzania kwa wananchi ni ule ule wa kuwa karibu na kesi hizi kubwa ili kuona na kupata fursa ya kutafakari mgumo wetu wa sheria, uongozi na mustakbali wa Taifa letu .

Ibrahim Z. Mkondo
Msemaji wa Shura ya Maimamu Tanzania.
0713118812

Hahaa huyo hakimu wa mashitaka, na wenzie wenye nia mbaya kwa masheikh wasio na hatia, wanachokitafuta watakipata, Mungu hachezelewi hata kidogo.
 
Ila wee jamaa unawachukia sana waislamu, mada kama hizi huwa hukosekani na kutoa maneno makali. Mungu akuongoze
Sina chuki nao ila nachukia vitendo vyao. Wakiwa wengi tu wanapitisha sharia zao. Ushawahi kuhudhuria kwenye mahubiri ya kiislam ya mijadala? Wameweka mjadala kabisa kuhusu uchambuzi wa Biblia na Quran.
 
Kwanini wasifungwe? Hivi kwanini wakae mahabusu bila sababu ya msingi? Mahakama iwahukumu kwa makosa yao sio kuwaweka watakaa miaka mingapi? Mahabusu

Kiukweli sisupport ugaidi hata kidogo,kama jamhuri imekata rufaa it means labda wana ushahidi wa kutosha,ngoja tuone referral wataamua kitu gani,kwasasa waendelee kusota rumande wakati wakisubiri hukumu.
 
kwa nini wasihukumiwe kufungwa hata maisha kuliko kuwekwa mahabusu miaka 9,hauoni kama kuna walakini mkuu?
Sheria za Tanzania zina walakini mwingi. Anza kupambania sheria kwanza, maana raia wengine ni zaidi ya miaka 15 bado hukumu zao hajizotoka.
 
Back
Top Bottom