Jamii na mtazamo hasi kuhusu kuoa/kuolewa

Jamii na mtazamo hasi kuhusu kuoa/kuolewa

ASIWAJU

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2022
Posts
1,938
Reaction score
1,632
Ningependa kuwakaribisha wadau wote wa Jamii Forums mtakaopendezwa kushiriki katika huu mjadala wenye maswali/changamoto kadhaa zenye kuhitaji majawabu kutoka kwenu.

Awali ya yote ningependa kufahamu haya kuhusu mtazamo wa jamii kuhusu kuoa au kuolewa kwa vijana wa kuanzia miaka 30 mpaka 40 na kuendelea:

1. Kwanini jamii inajenga tafsiri mbaya kwa vijana wa kiume na wa kike wenye umri kuanzia miaka 30 mpaka 40 na kuendelea ambao hawajaoa ua kuolewa, mfano wa tafasiri hizo ni malaya, mzinzi, mhuni n.k?

2. Kwanini jamii huamini kijana mwenye umri huo lazima awe ameoa au kuolewa?

3. Kwanini jamii za hutafsiri ndoa kama kasumba na siyo maamuzi binafsi?

4. Kwanini jamii haijawa tayari kupokea mabadiliko katika jamii inayotambua uwepo wa useja na maseja?

5. Kwanini jamii hutoa shinikizo kubwa kwa vijana wa rika hilo kuwaridhisha wao kuhusu swala zima la kuoa au kuolewa?

6. Kwanini jamii/familia hutafsiri kutokuolewa au kuoa ni kama laana, mkosi au aibu kwa familia?

7. Kwanini jamii hutafsiri vijana wa rika hilo ambao hawaja oa au kuolewa ni kuwa wana chembechembe za kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja [ ushoga au usagaji ] au wana mapungufu katika mfumo wao mzima wa uzazi?

Mwisho: Ningependa kufahamu zaidi je, suala zima la kuoa au kuolewa ni suala la maamuzi binafsi ya mwanaume/mwanamke au ni maamuzi ya jamii?

Karibuni nyote kushiriki, pia ningeomba tujikite kwenye maswali tajwa.
 
Ishi utakavyo, jamii haiwezi kuja na pingu kukufunga kisa tu hujaoa/olewa. Ilimradi tu usitumie hiyo nafasi ya kutooa/olewa kufanya uzinzi (hata hapa jamii haitokufanya chochote zaidi ya kuongea tu). Besides, siku hizi mambo ya kufuatiliana yamepungua sana, labda kama bado mnaishi kwenye familia zenye mshikamano sana. Watu wanatafuta ugali, hawahangaiki sana na status zetu za mahusiano
 
Kuoa au kuolewa ni maamuzi binafsi ikizingatiwa hata ukilala njaa, ukakosa kodi ya nyumba hakuna jamii itakayokuja kukunyanyua. Kikubwa ishi utakavyo na si watakavyo.
 
Wewe endelea kuwafata wana jamii, utapelekeshwa mpaka akili ikae sawa. Ishi maisha yako jipangie
Bora hata umuambie wee, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Vijana wakiume oeni na mabinti oleweni hakuna kutaf sababu sjui nin sjui una umri wa miaka 35 afu unaleta sababu zisizo na kichwa.
Kwani ni sababu zipi unazo hitaji kukidhi haja yako? Kwani swala la kijana wakiume kuoa na wakike kuolewa ni maamuzi ya mtu binafsi au ni maamuzi ya jamii ?
 
Unaishi kwa kuiridhisha jamii? Poleeeee sanaaaaaa.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Dunia ilishatoka huko. Lol
 
Wewe endelea kuwafata wana jamii, utapelekeshwa mpaka akili ikae sawa. Ishi maisha yako jipangie
Asante kwa mchango wako wa swali la mwisho, vipi kuhusu maswali mengine hapo juu ?
 
Kama unaishi kwa kuiridhisha Jamii hapo lazima iwe hoja kwako
Kwa hiyo mchango wako wa swali la mwisho ni maamuzi binafsi ya vijana warengwa wa rika hilo kuzingatiwa, vipi mchango wako kwa maswali mengine upoje ?
 
Back
Top Bottom