Chipsi yaipembeni
Senior Member
- Jan 8, 2015
- 128
- 92
KAMPUNI ya Jamii Media, ambao ni wamiliki wa mitandao maarufu ya mijadala kwa jamii kupitia mitandao ya jamii,JamiiForums na FikraPevu nchini Tanzania, imelaani kitendo cha baadhi ya kundi/watu walioishambulia miundombinu ya kampuni hiyo na kuzuia kupatikana kwa huduma zake kwa siku kadhaa.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni hiyo ndg Maxence Melo, tangu katikati ya mwezi Oktoba, 2015 mtandao wao pendwa wa JamiiForums ulianza kupata mashambulizi yaliyojulikana kama "DDOS Attack" mfululizo bila kikomo.
Amesema kwa kawaida yapo madaraja matatu tofauti ya mashambuzili (daraja la 3, la nne na la 7), na hivyo walipambana na mashambulizi kuanzia la daraja la tatu na la nne lakini waliokuwa wanataka kuhujumu miundombinu hiyo waligundua kuwa mashambulizi yao yamedhibitiwa, wakaamua kushambulia hadi daraja la 7 ambalo ndilo kubwa na la mwisho.
Muonekano wa picha unavyoonyesha jinsi miundombinu ya mtando huo ilivyoshambuliwa hadi kufikia Novemba mosi mwaka huu
Aidha, amesema mashambulizi ya DDOS Attack yanalenga kuzuia upatikanaji wa huduma na kufanya tovuti yoyote husuani ya mtandao wa JamiiForums kuzidiwa (kuchelewa kufunguka) na kutoa huduma kwa watumiaji.
''Walipoona tumeweza kudhibiti daraja la nne, walishambulia daraja la saba, sasa makampuni mengi yanayotoa huduma za kusimamia mtandao 'Server Hosting Providers' yanapoona unashambuliwa sana yanakufukuza kwa kuwa wewe unashambuliwa na kuvuruga miundombinu yao'' alieleza Maxence.
Amesema licha ya kampuni nyingi za kutoa huduma ya vihifadhi mtandao (Web Servers) kuogopa daraja la 7, yapo baadhi ya makampuni yanayoweza kukabiliana na hali hiyo.
"Hakuna mtoa huduma ambaye anakubali kuendelea kutoa huduma ya kuendelea kushikilia seva yako kama unaendelea kupata mashambulizi ya aina hii.
Picha hizi zinazoonyesha jinsi miundombinu ya mtando huo ilivyoshambuliwa hadi kufikia Oktoba 31, 2015
Mtandao wa JamiiForums unatajwa kuwa miongoni mwa mitandao ya kijamii inayosimamia uhuru wa habari, kuhabarisha na kushirikisha wananchi kwa habari na matukio katika kila nyanja.
Ni hivi majuzi, JamiiForums imetunukiwa tuzo ya Chombo Huru (Free Media) na taasisi ya Tanzania Media Foundation (TMF) kufuatia utendaji kazi wake unaoonekana kutoa fursa sawa kwa wote.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni hiyo ndg Maxence Melo, tangu katikati ya mwezi Oktoba, 2015 mtandao wao pendwa wa JamiiForums ulianza kupata mashambulizi yaliyojulikana kama "DDOS Attack" mfululizo bila kikomo.
Amesema kwa kawaida yapo madaraja matatu tofauti ya mashambuzili (daraja la 3, la nne na la 7), na hivyo walipambana na mashambulizi kuanzia la daraja la tatu na la nne lakini waliokuwa wanataka kuhujumu miundombinu hiyo waligundua kuwa mashambulizi yao yamedhibitiwa, wakaamua kushambulia hadi daraja la 7 ambalo ndilo kubwa na la mwisho.
Muonekano wa picha unavyoonyesha jinsi miundombinu ya mtando huo ilivyoshambuliwa hadi kufikia Novemba mosi mwaka huu
Aidha, amesema mashambulizi ya DDOS Attack yanalenga kuzuia upatikanaji wa huduma na kufanya tovuti yoyote husuani ya mtandao wa JamiiForums kuzidiwa (kuchelewa kufunguka) na kutoa huduma kwa watumiaji.
''Walipoona tumeweza kudhibiti daraja la nne, walishambulia daraja la saba, sasa makampuni mengi yanayotoa huduma za kusimamia mtandao 'Server Hosting Providers' yanapoona unashambuliwa sana yanakufukuza kwa kuwa wewe unashambuliwa na kuvuruga miundombinu yao'' alieleza Maxence.
Amesema licha ya kampuni nyingi za kutoa huduma ya vihifadhi mtandao (Web Servers) kuogopa daraja la 7, yapo baadhi ya makampuni yanayoweza kukabiliana na hali hiyo.
"Hakuna mtoa huduma ambaye anakubali kuendelea kutoa huduma ya kuendelea kushikilia seva yako kama unaendelea kupata mashambulizi ya aina hii.
Picha hizi zinazoonyesha jinsi miundombinu ya mtando huo ilivyoshambuliwa hadi kufikia Oktoba 31, 2015
Mtandao wa JamiiForums unatajwa kuwa miongoni mwa mitandao ya kijamii inayosimamia uhuru wa habari, kuhabarisha na kushirikisha wananchi kwa habari na matukio katika kila nyanja.
Ni hivi majuzi, JamiiForums imetunukiwa tuzo ya Chombo Huru (Free Media) na taasisi ya Tanzania Media Foundation (TMF) kufuatia utendaji kazi wake unaoonekana kutoa fursa sawa kwa wote.