TUSHIRIKISHANE JamiiForums yazindua rasmi mradi wa "Tushirikishane"

TUSHIRIKISHANE JamiiForums yazindua rasmi mradi wa "Tushirikishane"

Tupo Nzega tayari mkuu. Tutamaliza baada ya siku 3 zijazo.

Tunafanya upembuzi kwanza kubaini kama wananchi wanatambua majukumu ya Mbunge na kama wanakumbuka ahadi zake. Aidha, tunafuatilia kama wanafahamu wajibu wa Halmashauri kwao na wajibu wa madiwani kwao.

Tuna mengi tumeona na tumewahamasisha wananchi katika kuyapata maendeleo katika maeneo yao. Bahati wananchi wanatuelewa na viongozi wao wanauona mwitikio wa wananchi katika maeneo tunakopita.

Mradi huu upo katika hali ya majaribio (pilot project) na lengo la awali lilikuwa ni kuufanya katika majimbo matatu kwanza lakini mwitikio wa waheshimiwa wabunge ulipelekea nasi kujisogeza na kujikuta idadi inaongezeka zaidi.

Nafasi za ajira ya Afisa Mawasiliano ambaye atakuwa anatuwakilisha katika kila jimbo zilitangazwa hapa JamiiForums katika jukwaa la Nafasi za Kazi.

Kukiwa na ufanisi katika hatua hii ya awali, tutajisogeza zaidi (scale-up) na kufanya katika majimbo zaidi na tutajitahidi tukatafuta wahisani ili mradi uweze kuwafikia wengi na kuongeza tija zaidi.

Mbunge, Halmashauri na wananchi watakaofanya vema watatuzwa mwishoni mwa mradi (top 3).
Hongereni sana Mkuu, Mungu awatangulie katika kazi yenu hii. Mimi na Watanzania wenzangu tunazidi kuwaombea. Mwisho kabisa, Misahau kulifikia jimbo kubwa la Rais Magufuli Yaani Tanzania. Muwaulize Wananchi kama ahadi za Rais Magufuli zimetekelezwa kwa kiasi gani. Kama wananchi inabidi tujue mpango uliopo foreplan kuhusu Tanzania ya Viwanda.

Tunapaswa kujua ahadi za Rais Magufuli zimetekelezwa kiasi gani? Rais hata akiwa busy itabidi atoe maelezo hata kwa maandishi tuyaone.
 
Hongera mkuu Max, na crew mzima ya JF, Mungu awatie nguvu.

Kazi yenu itasaidia kufumbua wananchi kujua majukumu ya viongozi wao.

Maana kuna watu walikuwa wakienda nyumbani kwa wabunge ili kutaka misaada binafsi, kwa kujua nalo ni jukumu la mbunge.
 
Hii safi sana ...

Wazo langu hapa haina haja ya kuongeza wingi... Nyinyi wachache mlioanza muendelee kwanza mpaka matunda yaliyopangwa kufikiwa kwa asilimia za kutosha... Kisha kwenye mchakato mwingine ujao waheshimiwa watajileta wenyewe na hapa hawapiti hadi mchujo kwa wenye nia ya kweli ya maendeleo
 
Safi kabisaaaa! Mabadiliko siyo tunayoyaombea bali tunayojiletea!..
Hongera saana Maxence ingawa hukushirikisha wilaya zingine, polepole ndio mwendo!

Mbunge wetu Jackson Lweikiza kuna miradi ya maji Kata Ibwera kijiji cha Itongo. Kitongoji Bwagula
World Bank funded since 2015 or 2014, hakuna maji na majibu sahihi kwa wananchi hakuna.

Miradi ifuatiliwe phyisical ili kuwa na majibu sahihi.

Ubarikiwe!!
 
ni vizuri na wasiishie na majimbo hayo tu waendelee zaidi
 
Max mmetoka Bukoba hadi Nzega, mbona hamkupita hapa Rock City.

Hongereni sana kwa ubunifu huu, nauombea mradi udumu na kuleta matunda yaliyokusudiwa
 
Asanteni sana wana JF, hakika hiki ndicho kitu tunachokihitaji na kutegemea, vyombo vya habari vinawajibu wa kuzifikia pande zote, viongozi, wananchi huku wakiwagusa wote katika tofauti zilizopo.

Hii imedhihirisha kuwafikia wananchi ka wingi hata kama mnaongea na wachache wao lakini naamini wanatuwakilisha. Viongozi kuulizwa maswali ana kwa ana na wapigakura wao. HII NI MAENDELEO TOSHA {Atakachokijibu atakitekeleza}

ASANTE SANA JAMII FORUMS
 
Back
Top Bottom