Jana ulikuwa ni mkutano wa CCM uliovalishwa vazi la CHADEMA

Jana ulikuwa ni mkutano wa CCM uliovalishwa vazi la CHADEMA

CHADEMA limebaki jina tu. Ila imechoka chakaliii.

Unapandisha jukwaani mianasiasa iliyokula IMESHIBA inaongea ikihema JUU JUU.

Sura zile zile kwa miaka 15 Sasa.

Stori zile zile.

Siasa zile zile.

Hakuna JIPYA.

Wewe una jipya gani?. Baki na CCM yako hujalazimishwa.
 
Yani jana wamechemka hasa watu hawakuamini kama ni mbowe yule anaongea au mzimu wake

Hakika mwenyekiti kalambishwa asali si bure,sasa kama hautakuwa na nguvu ya kuisema CCM na mwenyekiti wake kuna upinzani hapo?

Mkutano wao wa jana umedhihirisha upinzani bongo hakuna wamejaa wachumia tumbo tu

Kazi ipo.

Mbowe kaboronga Jana, lakini ujinga wa mbowe usiulete CHADEMA. Lissu akichemka Basi itabidi niachane na siasa.
 
Uko sahihi kabisa. Na maana yake ni kwamba hana sifa za kuwapigania wananchi anaowaaminisha kwamba atawaletea ukombozi. Musa wa nchi hii kwa kipindi hiki alikuwa JPM. Wao wakamuona adui. Sasa wamepoteza dira. 😀😀 na badoooo

JPM alikuwa Mussa gani?. Mussa hakuwa mbaguzi na muuaji dhidi ya raia wake. Kapamabana na CHADEMA mpaka kafa.
 
Uko sahihi kabisa. Na maana yake ni kwamba hana sifa za kuwapigania wananchi anaowaaminisha kwamba atawaletea ukombozi. Musa wa nchi hii kwa kipindi hiki alikuwa JPM. Wao wakamuona adui. Sasa wamepoteza dira. 😀😀 na badoooo

Sifa unazo wewe muoga uliyejificha ukisubiria Mbowe akusemee.
 
Kama kweli ccm wamempongeza Mbowe, basi kazi imeisha. Hatuna upinzani tena, tuna waungaji mkono juhudi za Samia
 
Aliekwambia mimi ni mpinzani nani?tena mwambie mbowe hata huo uwenyekitii sasa basi maana hafai kuwa kiongozi wa upinzani na kwenda kusifia chama anachopinzana nacho,naona CHAWA wake umepanic hatari Ila habari ndio hiyo Jana kachemka na leo musoma hapati watu

Punguza kelele Kama sio mpinzani. Mbowe Mbowe, wakati upo CCM juzi mlimwita gaidi, leo mnajifanya kukasirika kwanini hajaisema CCM.
 
"Hakukuwa na sababu za kumtaja Rais, achilia mbali kumsifia"

Hiyo kauli mara nyingi inatoka kwa cowards, wanaoendekeza siasa za kuvizia, wakidhani mwenyekiti wa Chadema kumtaja na kumsifia Samia, basi Chadema itapoteza umaarufu wake.

Hayo kwangu ni mawazo mgando yaliyopitwa na wakati, kama hamuwezi kurekebishana wenyewe kati yenu, au kutoa shukrani kwa mpinzani wenu, hizo ni siasa mfu zilizopitwa na wakati, hamjui hata kwenye siasa kuna fair play.
 
JPM alikuwa Mussa gani?. Mussa hakuwa mbaguzi na muuaji dhidi ya raia wake. Kapamabana na CHADEMA mpaka kafa.
Una ushahidi wa mauaji aliyoyafanya?
Hata hivyo ni kweli musa hakuua lakini waliokengeuka walikufa jangwani na wengine ardhi ilifunguka ikawameza!

Na maadui waliokuwa kikwazo cha safari yao, walizamishwa baharini. Sio wote ni waisrael wanaohitaji kuvushwa, wengine walikuwa wafilisti wanaozuia safari...hakuna budi wauwawe ili safari iendelee
 
Una ushahidi wa mauaji aliyoyafanya?
Hata hivyo ni kweli musa hakuua lakini waliokengeuka walikufa jangwani na wengine ardhi ilifunguka ikawameza!

Na maadui waliokuwa kikwazo cha safari yao, walizamishwa baharini. Sio wote ni waisrael wanaohitaji kuvushwa, wengine walikuwa wafilisti wanaozuia safari...hakuna budi wauwawe ili safari iendelee

Yeye ndio alizamishwa ndio maana kafa kwa aibu. Leo watu wanafanya mikutano kwa amani Tena kwa kusindikizwa na Polisi.
 
Na, Robert Heriel

Jana agenda kuu ya mkutano ilikuwa kumshukuru na kumpongeza Rais, na ukimpongeza Rais tafsiri yake umeipongeza CCM. Ninaweza kusema Ulikuwa Mkutano wa CCM katika Vazi la CHADEMA. Na Hii ndio inaweza kutoa picha ni aina gani ya Siasa katika nchi hii tulizonazo.

Hakukuwa na sababu hata moja ya kumtaja Rais achilia mbali kumsifia kama kweli ule ungekuwa Mkutano wa CHADEMA.

Mwenyekiti Mbowe na viongozi wengine waliomsifia mwenyekiti wa CCM, Rais, Dr Samia Suluhu, wamefanya kosa kubwa kisiasa, kiushawishi.

Kimantiki, Kilichokuwa kinafanyika Jana ni kuushawishi umma wa watanzania waikubali CCM na kumuamini Rais Samia katika kuongoza Dola.

Sio ajabu Mbowe alizomewa, na walikuwa na haki ya kumzomea wafuasi wa Chadema. Jambo ambalo kama ingekuwa ni Mkutano wa CHADEMA lisingetokea.

Kama ungekuwa Mkutano wa Chadema, basi wazungumzaji wote waliopewa nafasi ya kusimama kuzungumza wangewashawishi watu kwa hoja namna CCM na Mwenyeketi wake walivyokosa sifa na vigezo vya kuongoza taifa hili.

Mkutano wa Jana Mwanza wa CCM, umejaribu kuonyesha watu wa nchi hii picha halisi ya wapinzani tulionao.

Hakuna anayetaka siasa za matusi, Mbowe kusema kuwa ati hatamtukana Mwenyekiti wa CCM, inashangaza, hakuna aliyemuambia amtukane. Wanachokataa ni Mbowe kuwa upande wa Samia, kuwa CCM. Tafsiri yake ni kuwa Wanachadema hawataki kuongozwa na MTU aliyeupande wa CCM.

Wanachadema wanaposema Mbowe analamba Asali, bila Shaka wanarejelea maana ya kuwa Mbowe yupo upande wa watawala wa CCM. Indirect way wanajaribu kusema Mbowe ni CCM. Na kama Mbowe yupo upande wa CCM automatically Mkutano wa Jana ulikuwa wa CCM.

Kulikuwa na hoja nyingi za msingi za kuzizungumzia,

1. Mbowe alipaswa aanzie alipoishia, kuwekwa ndani na baadaye kesi yake kufutwa. Ingawaje ni Jambo gumu 😀 lakini angeanzia hapo. Mfano Lissu yeye huanziaga pale alipopigwa Risasi. Wanasema ukitaka kumuua nyoka anzia miguuni.

2. Hoja ya Katiba Mpya, hii wameijadili lakini katika kiwango cha Chini.

3. Hoja ya Hali ngumu ya Maisha. Mkutano wa Jana ungepaswa utoe muhtasari wa jinsi serikali iliyopo madarakani ilivyoshindwa kuwapa unafuu Wananchi. Bei za bidhaa zipo juu. Wananchi wanataabika. Badala yake wanasifia CCM. Mpaka unajiuliza ulikuwa Mkutano wa chama cha upinzani kweli au Laa.

4. Hoja za Haki na Uhuru wa kujieleza.
Katika uwasilishaji wangejaribu kuwashawishi watu namna gani walivyofanikiwa kupigania hilo eneo. Hoja zao zijikite kuwa kila mafanikio na Maendeleo ya haki na Uhuru ndani ya nchi hii yamechangiwa Kwa kiasi kikubwa na Chadema.

Wangetakiwa wasema hata kuruhusiwa kwa mikutano ya kisiasa ni Kutokana na juhudi zao. Na watahakikisha kuwa Haki na Uhuru watavipigania Kwa gharama yoyote.

Hivi MTU akisema hivyo ametukana popote, amevunja sheria yoyote, jibu ni Hapana. Sasa unapomsifia hasimu wako kuwa bila yeye mikutano isingeruhusiwa unajaribu kuwaambia nini Wananchi?

Yaani ni sawasawa unaenda mtongoza Demu, alafu badala ujisifie wewe ATI unamsifia Mshindani wako. Unategemea Demu atakuonaje, si atakuona hamnazo!

5. Hoja ya UMOJA na USHIRIKIANO.
Katika Mkutano, Chadema ingeeleza kwa namna gani CCM ilivyoshindwa kuleta UMOJA na USHIRIKIANO ndani ya nchi. Kwa Hoja ZENYE mashiko na mifano dhahiri Wananchi wangeelewa.

Kisha iseme, Chadema Ipo kwaajili ya kuijenga nchi hii katika UMOJA na USHIRIKIANO. Sio kama CCM walivyofanya(unataja mifano).

Binafsi nimesikitishwa na chama ambacho ni kikubwa chenye miaka 30 Kwa Makusudi kabisa kikashindwa kuifanya siku ya Jana kuwa siku kweli ya uzinduzi. Badala yake wamezindua UCCM.

Kama tutaweka unafiki pembeni, nataka kusema, viongozi wa Chadema wamewaangusha wanachadema,
CCM inawazidije ujanja, Sasa si Bora hata msingefanya Mkutano kuliko kupoteza Muda na Pesa.

CCM wenzenu watapitia humohumo kwenye mapungufu yenu.

CCM ninavyowajua watakuja na kuwapaka Mavi mnuke,

Mimi ngoja nipumzike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es

Maneno mengi bila maana. Mbowe ukimfuata kichwa kichwa hautamuelewa. Wewe jifanye mchambuzi wa kila kitu utakula za uso. Mkutano mmoja eti ulikuwa mkutano wa ccm. Una akili kweli?. Kama Kuna jambo hulijui kaa kimya, usioneshe ujinga wako.
 
Watu wanamsikiliza Kiongozi.
Atakachoongea Kiongozi Mkuu ndio kinasikilizwa.
Hao wengine hatuwazingatii sana

Kiongozi gani? Mbowe kaongea kwa nafasi yake lakini msimamo wa CHADEMA unajulikan. CHADEMA itawasumbua Sana Kama mtaingia kichwa kichwa bila kutafakari.
 
Watetezi wa wananchi kwa sasa ni team magu tu, wapinzani washalambishwa asali.😀😀
Hawaoni hata haja ya kuzungumzia mfumuko wa bei, mikopo isiyo na tija, safari na ziara za viongozi ndani na nje ya nchi. Wao ni kupongeza tu!

Wewe ulikuwepo Jana?. Tatizo umesikiliza hotuba ya Mbowe pekee. Mbona Viongozi wengine wameongelea issue za wananchi?. Msitumie kauli ya Mbowe. Jana mlisema mkutano hata kuja mtu wamekuja watu mnadai mkutano wa CCM .
 
Na, Robert Heriel

Jana agenda kuu ya mkutano ilikuwa kumshukuru na kumpongeza Rais, na ukimpongeza Rais tafsiri yake umeipongeza CCM. Ninaweza kusema Ulikuwa Mkutano wa CCM katika Vazi la CHADEMA. Na Hii ndio inaweza kutoa picha ni aina gani ya Siasa katika nchi hii tulizonazo.

Hakukuwa na sababu hata moja ya kumtaja Rais achilia mbali kumsifia kama kweli ule ungekuwa Mkutano wa CHADEMA.

Mwenyekiti Mbowe na viongozi wengine waliomsifia mwenyekiti wa CCM, Rais, Dr Samia Suluhu, wamefanya kosa kubwa kisiasa, kiushawishi.

Kimantiki, Kilichokuwa kinafanyika Jana ni kuushawishi umma wa watanzania waikubali CCM na kumuamini Rais Samia katika kuongoza Dola.

Sio ajabu Mbowe alizomewa, na walikuwa na haki ya kumzomea wafuasi wa Chadema. Jambo ambalo kama ingekuwa ni Mkutano wa CHADEMA lisingetokea.

Kama ungekuwa Mkutano wa Chadema, basi wazungumzaji wote waliopewa nafasi ya kusimama kuzungumza wangewashawishi watu kwa hoja namna CCM na Mwenyeketi wake walivyokosa sifa na vigezo vya kuongoza taifa hili.

Mkutano wa Jana Mwanza wa CCM, umejaribu kuonyesha watu wa nchi hii picha halisi ya wapinzani tulionao.

Hakuna anayetaka siasa za matusi, Mbowe kusema kuwa ati hatamtukana Mwenyekiti wa CCM, inashangaza, hakuna aliyemuambia amtukane. Wanachokataa ni Mbowe kuwa upande wa Samia, kuwa CCM. Tafsiri yake ni kuwa Wanachadema hawataki kuongozwa na MTU aliyeupande wa CCM.

Wanachadema wanaposema Mbowe analamba Asali, bila Shaka wanarejelea maana ya kuwa Mbowe yupo upande wa watawala wa CCM. Indirect way wanajaribu kusema Mbowe ni CCM. Na kama Mbowe yupo upande wa CCM automatically Mkutano wa Jana ulikuwa wa CCM.

Kulikuwa na hoja nyingi za msingi za kuzizungumzia,

1. Mbowe alipaswa aanzie alipoishia, kuwekwa ndani na baadaye kesi yake kufutwa. Ingawaje ni Jambo gumu 😀 lakini angeanzia hapo. Mfano Lissu yeye huanziaga pale alipopigwa Risasi. Wanasema ukitaka kumuua nyoka anzia miguuni.

2. Hoja ya Katiba Mpya, hii wameijadili lakini katika kiwango cha Chini.

3. Hoja ya Hali ngumu ya Maisha. Mkutano wa Jana ungepaswa utoe muhtasari wa jinsi serikali iliyopo madarakani ilivyoshindwa kuwapa unafuu Wananchi. Bei za bidhaa zipo juu. Wananchi wanataabika. Badala yake wanasifia CCM. Mpaka unajiuliza ulikuwa Mkutano wa chama cha upinzani kweli au Laa.

4. Hoja za Haki na Uhuru wa kujieleza.
Katika uwasilishaji wangejaribu kuwashawishi watu namna gani walivyofanikiwa kupigania hilo eneo. Hoja zao zijikite kuwa kila mafanikio na Maendeleo ya haki na Uhuru ndani ya nchi hii yamechangiwa Kwa kiasi kikubwa na Chadema.

Wangetakiwa wasema hata kuruhusiwa kwa mikutano ya kisiasa ni Kutokana na juhudi zao. Na watahakikisha kuwa Haki na Uhuru watavipigania Kwa gharama yoyote.

Hivi MTU akisema hivyo ametukana popote, amevunja sheria yoyote, jibu ni Hapana. Sasa unapomsifia hasimu wako kuwa bila yeye mikutano isingeruhusiwa unajaribu kuwaambia nini Wananchi?

Yaani ni sawasawa unaenda mtongoza Demu, alafu badala ujisifie wewe ATI unamsifia Mshindani wako. Unategemea Demu atakuonaje, si atakuona hamnazo!

5. Hoja ya UMOJA na USHIRIKIANO.
Katika Mkutano, Chadema ingeeleza kwa namna gani CCM ilivyoshindwa kuleta UMOJA na USHIRIKIANO ndani ya nchi. Kwa Hoja ZENYE mashiko na mifano dhahiri Wananchi wangeelewa.

Kisha iseme, Chadema Ipo kwaajili ya kuijenga nchi hii katika UMOJA na USHIRIKIANO. Sio kama CCM walivyofanya(unataja mifano).

Binafsi nimesikitishwa na chama ambacho ni kikubwa chenye miaka 30 Kwa Makusudi kabisa kikashindwa kuifanya siku ya Jana kuwa siku kweli ya uzinduzi. Badala yake wamezindua UCCM.

Kama tutaweka unafiki pembeni, nataka kusema, viongozi wa Chadema wamewaangusha wanachadema,
CCM inawazidije ujanja, Sasa si Bora hata msingefanya Mkutano kuliko kupoteza Muda na Pesa.

CCM wenzenu watapitia humohumo kwenye mapungufu yenu.

CCM ninavyowajua watakuja na kuwapaka Mavi mnuke,

Mimi ngoja nipumzike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es
Aisee Taikon ktk mabandiko yako yote hili umesema mambo ya maana sana

Sasa na wewe anzia hapa usirudi tena kule kwenye laana za wazazi
 
Mtoa hoja jipiganie mwenyewe kwa hayo unayoyaamini uliyoyaandika humu, usijifanye shujaa kwa kujificha kwa ID fake hizi,Mh.Mbowe amekaa jela zaidi ya 150days bila ya kuwa na wapendwa wake, wewe ulifanya nini?maana muda wote ulikuwa na familia yako, Mh.Mbowe he done his bit sasa ni wakati wa ninyi middle class kujitokeza na kufanya mabadiliko ya kuisukuma nchi yetu mbele, it's craze mtu unatumia muda mwingi kumlaumu mtu mwingine eti akupiganie haki zako, uoga na uzuzu wa middle class ni cancer ndani ya nchi hii
Mbowe ule ni wajibu wake cheo na hadhi aliyonayo inakwenda sambamba na maswahibu anayopitia

Kuwekwa jela sio sababu eti asitimize uamuzi wake

Yeye anapaswa kuendelea kutimiza kama anadhani kafanya part yake na akae kando Taikon akachukue gurudumu
 
Back
Top Bottom