Jana ulikuwa ni mkutano wa CCM uliovalishwa vazi la CHADEMA

Jana ulikuwa ni mkutano wa CCM uliovalishwa vazi la CHADEMA

Lakini kumsifia hasimu wako Mbele ya Mkeo na wanao Huko sio kuanza taratibu Mkuu.

Haikupaswa kivyovyote Chadema kuisifia CCM.
Tactic ya kumsifia mtu ni kubwa sana wengi wameangamizwa kwa ujanja huu. Hizo ndio busara za siasa za Tanzania na hata Samia mwenyewe anaelewa nini maana ya “kusifiwa” na Mbowe. Mbowe asingekuwa na busara za kisiasa kwa hakika Magufuli angelisha mmaliza siku nyingi! Ujue Magufuli alimchukia Lissu lakini alimwogopa Mbowe.
 
Hizo ndio busara za siasa za Tanzania na hata Samia mwenyewe anaelewa nini maana ya “kusifiwa” na Mbowe. Mbowe asingekuwa na busara za kisiasa kwa hakika Magufuli angelisha mmaliza siku nyingi!

Sasa hapo ndio ataiua Chadema mioyoni mwa Watu.
Wanachadema wa Chini wanaamini CCM ni adui Yao. Sasa unaposhirikiana na adui yao, lazima wakuone Msaliti. Rejea 2015 Wakati WA Lowasa.

CCM inachokifanya sasa ni kumpa mtoto mchawi. Watakuwa wamejipunguzia mzigo.

Chadema ambacho wangefanya Kwa sasa ni kubali na agenda Yao ileile ya kupigana na mafisadi, kisha kuwashawishi team magufuli wawe upande wao.

Sasa wakiungana na ccm, watapoteza uungwaji mkono na watu.
Alafu CCM wao kazi Yao itakuwa kuwabembeleza kirahisi wananchi
 
Sina hakika kama ndio aliyeimaliza, bali nina uhakika aliharibu sana haiba ya CDM. Lile lilikuwa ni kosa la karne.

Aliiharibu Kwa sababu Wananchi wengi walishaanza kuiamini Chadema.
2015 wangemuacha Slaa hata kama asingepata Kura nyingi lakini ingezidisha Imani ya Watu ndani ya chama.
 
Siasa za nchi hii ukihangaika kuzifuatilia utaumia kichwa, wanasiasa ni wafanya biashara kama wafanya biashara wengine. Masilahi ya tumbo yapo mbele.

Kama unasubiri wanasiasa wakutatulie shida zako, basi utasubiri sana... huu ni wakati wa mwenyekiti kurudisha biashara zake na utajiri wake. Umri alionao saizi anahitaji kupata assurance ya miaka 20 ijayo, akipiga hesabu vizuri huu ndio muda wa kuweka pride pembeni na kuumega mkate.
 
Aliyeidhuru CDM sio Lowassa ni Magufuli akitumia ukabila na dola.

Magufuli hakuidhuru Chadema Kwa kiasi kikubwa, labda katika umbo la nje.
Lakini Kwa umbo la ndani Chadema walijidhuru wenyewe pale walipoanza kutetereka kwenye msimamo. Hasa walipomkaribisha Lowasa
 
Siasa za nchi hii ukihangaika kuzifuatilia utaumia kichwa, wanasiasa ni wafanya biashara kama wafanya biashara wengine. Masilahi ya tumbo yapo mbele.

Kama unasubiri wanasiasa wakutatulie shida zako, basi utasubiri sana... huu ni wakati wa mwenyekiti kurudisha biashara zake na utajiri wake. Umri alionao saizi anahitaji kupata assurance ya miaka 20 ijayo, akipiga hesabu vizuri huu ndio muda wa kuweka pride pembeni na kuumega mkate.

😂😂😂😂
Usiseme hivyo mkuu
 
Mbowe ni mwanasiasa makini. Hata CCM tutaanza kutumia ile hashtag ya #mwambatuvushe. Jana Mbowe alifanya kitu kikubwa sana kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ninaomba Mbowe ataeuliwe hata kuwa mwenyekiti wa bodi ya parole kama itampendeza Mama Samia.
 
Mbowe ni mwanasiasa makini. Hata CCM tutaanza kutumia ile hashtag ya #mwambatuvushe. Jana Mbowe alifanya kitu kikubwa sana kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ninaomba Mbowe ataeuliwe hata kuwa mwenyekiti wa bodi ya parole kama itampendeza Mama Samia.

Aiseeeh!
 
Makada wa CCM wamepongeza sana hotuba ya Mbowe wanasema Mbowe sasa amekua mwanasiasa makini.

CCM ya sasa wanamchukia Lisu wanajua yule bwana mkubwa Lisu huwa anapiga kwenye mfupa mwanzo mwisho,ana point na data za kutosha kuhusu mambo yanayowagusa wananchi moja kwa moja.
Ni kweli Ana data za kutosha namna wale Wana madini wawekezaji watakavyoipeleka mahakamani Serikali sababu ya makinikia..sure..!!
 
Sasa hapo ndio ataiua Chadema mioyoni mwa Watu.
Wanachadema wa Chini wanaamini CCM ni adui Yao. Sasa unaposhirikiana na adui yao, lazima wakuone Msaliti. Rejea 2015 Wakati WA Lowasa.

CCM inachokifanya sasa ni kumpa mtoto mchawi. Watakuwa wamejipunguzia mzigo.

Chadema ambacho wangefanya Kwa sasa ni kubali na agenda Yao ileile ya kupigana na mafisadi, kisha kuwashawishi team magufuli wawe upande wao.

Sasa wakiungana na ccm, watapoteza uungwaji mkono na watu.
Alafu CCM wao kazi Yao itakuwa kuwabembeleza kirahisi wananchi
Sawa Robert kumbuka CDM imepitia magumu mengi mno hata mimi nashangaa kwamba CDM bado ipo. Pia kwanini watu wanai-judge CDM kwa mkutano mmoja tu wa jana ilhali ipo mikutano kibao inafuata? Mambo CDM wanataka kuyafanya ni process na sio tukio moja. Naogopa atakapokuja Lissu tutamwomba apoe kidogo kwani kama alimpa za uso Magufuli sijui itakuwaje kwa mama. Na Lissu ana machungu mengi, itabidi busara kubwa itumike. Ni hatari kweli kuwa mpinzani Africa especially of the kind of Lissu.
 
Sawa Robert kumbuka CDM imepitia magumu mengi mno hata mimi nashangaa kwamba CDM bado ipo. Pia kwanini watu wanai-judge CDM kwa mkutano mmoja tu wa jana ilhali ipo mikutano kibao inafuata? Mambo CDM wanataka kuyafanya ni process na sio tukio. Naogopa atakapokuja Lissu tutamwomba apoe kidogo kwani kama alimpa za uso Magufuli sijui itakuwaje kwa mama. Na Lissu ana machungu mengi, itabidi busara kubwa itumike. Ni hatari kweli kuwa mpinzani Africa.

Umesema vizuri Kabisa.
Hofu yangu ni Ile ya kutaka kuibomoa katika umbo la ndani Kabisa.
Chadema isingekufa kivyovyote Kwa mbinu alizokuwa anatumia Magufuli, kwani yeye alijikita kupasua Kwa nje Kwa Kutumia nguvu kubwa.
Ilhali ukitaka kukiharibu kitu totally unatakiwa kukiangamiza Kwa ndani.

Watu wakishapoteza Imani na Chadema kurudi ni kipengele.
 
Sawa Robert kumbuka CDM imepitia magumu mengi mno hata mimi nashangaa kwamba CDM bado ipo. Pia kwanini watu wanai-judge CDM kwa mkutano mmoja tu wa jana ilhali ipo mikutano kibao inafuata? Mambo CDM wanataka kuyafanya ni process na sio tukio moja. Naogopa atakapokuja Lissu tutamwomba apoe kidogo kwani kama alimpa za uso Magufuli sijui itakuwaje kwa mama. Na Lissu ana machungu mengi, itabidi busara kubwa itumike. Ni hatari kweli kuwa mpinzani Africa especially of the kind of Lissu.

Siasa za Lisu ni zahatari lakini zinaeleweka zaidi kuliko Siasa za kina Mbowe na zitto.

Wakitokea kina Lisu kama 10 hivi ndani wanawawe kuleta matokeo yanayotarajiwa ndani ya muda mfupi.

Ila Kwa Afrika ni ngumu Sana
 
Makada wa CCM wamepongeza sana hotuba ya Mbowe wanasema Mbowe sasa amekua mwanasiasa makini.

CCM ya sasa wanamchukia Lisu wanajua yule bwana mkubwa Lisu huwa anapiga kwenye mfupa mwanzo mwisho,ana point na data za kutosha kuhusu mambo yanayowagusa wananchi moja kwa moja.
Lissu na yeye tunamsubiri akija atapita mle mle amsifie mama samia na hapo sjui ntamsubir nan tena , ukweli ni kuwa chadema ushawishi hamna
 
Na, Robert Heriel

Jana agenda kuu ya mkutano ilikuwa kumshukuru na kumpongeza Rais, na ukimpongeza Rais tafsiri yake umeipongeza CCM. Ninaweza kusema Ulikuwa Mkutano wa CCM katika Vazi la CHADEMA. Na Hii ndio inaweza kutoa picha ni aina gani ya Siasa katika nchi hii tulizonazo.

Hakukuwa na sababu hata moja ya kumtaja Rais achilia mbali kumsifia kama kweli ule ungekuwa Mkutano wa CHADEMA.

Mwenyekiti Mbowe na viongozi wengine waliomsifia mwenyekiti wa CCM, Rais, Dr Samia Suluhu, wamefanya kosa kubwa kisiasa, kiushawishi.

Kimantiki, Kilichokuwa kinafanyika Jana ni kuushawishi umma wa watanzania waikubali CCM na kumuamini Rais Samia katika kuongoza Dola.

Sio ajabu Mbowe alizomewa, na walikuwa na haki ya kumzomea wafuasi wa Chadema. Jambo ambalo kama ingekuwa ni Mkutano wa CHADEMA lisingetokea.

Kama ungekuwa Mkutano wa Chadema, basi wazungumzaji wote waliopewa nafasi ya kusimama kuzungumza wangewashawishi watu kwa hoja namna CCM na Mwenyeketi wake walivyokosa sifa na vigezo vya kuongoza taifa hili.

Mkutano wa Jana Mwanza wa CCM, umejaribu kuonyesha watu wa nchi hii picha halisi ya wapinzani tulionao.

Hakuna anayetaka siasa za matusi, Mbowe kusema kuwa ati hatamtukana Mwenyekiti wa CCM, inashangaza, hakuna aliyemuambia amtukane. Wanachokataa ni Mbowe kuwa upande wa Samia, kuwa CCM. Tafsiri yake ni kuwa Wanachadema hawataki kuongozwa na MTU aliyeupande wa CCM.

Wanachadema wanaposema Mbowe analamba Asali, bila Shaka wanarejelea maana ya kuwa Mbowe yupo upande wa watawala wa CCM. Indirect way wanajaribu kusema Mbowe ni CCM. Na kama Mbowe yupo upande wa CCM automatically Mkutano wa Jana ulikuwa wa CCM.

Kulikuwa na hoja nyingi za msingi za kuzizungumzia,

1. Mbowe alipaswa aanzie alipoishia, kuwekwa ndani na baadaye kesi yake kufutwa. Ingawaje ni Jambo gumu [emoji3] lakini angeanzia hapo. Mfano Lissu yeye huanziaga pale alipopigwa Risasi. Wanasema ukitaka kumuua nyoka anzia miguuni.

2. Hoja ya Katiba Mpya, hii wameijadili lakini katika kiwango cha Chini.

3. Hoja ya Hali ngumu ya Maisha. Mkutano wa Jana ungepaswa utoe muhtasari wa jinsi serikali iliyopo madarakani ilivyoshindwa kuwapa unafuu Wananchi. Bei za bidhaa zipo juu. Wananchi wanataabika. Badala yake wanasifia CCM. Mpaka unajiuliza ulikuwa Mkutano wa chama cha upinzani kweli au Laa.

4. Hoja za Haki na Uhuru wa kujieleza.
Katika uwasilishaji wangejaribu kuwashawishi watu namna gani walivyofanikiwa kupigania hilo eneo. Hoja zao zijikite kuwa kila mafanikio na Maendeleo ya haki na Uhuru ndani ya nchi hii yamechangiwa Kwa kiasi kikubwa na Chadema.

Wangetakiwa wasema hata kuruhusiwa kwa mikutano ya kisiasa ni Kutokana na juhudi zao. Na watahakikisha kuwa Haki na Uhuru watavipigania Kwa gharama yoyote.

Hivi MTU akisema hivyo ametukana popote, amevunja sheria yoyote, jibu ni Hapana. Sasa unapomsifia hasimu wako kuwa bila yeye mikutano isingeruhusiwa unajaribu kuwaambia nini Wananchi?

Yaani ni sawasawa unaenda mtongoza Demu, alafu badala ujisifie wewe ATI unamsifia Mshindani wako. Unategemea Demu atakuonaje, si atakuona hamnazo!

5. Hoja ya UMOJA na USHIRIKIANO.
Katika Mkutano, Chadema ingeeleza kwa namna gani CCM ilivyoshindwa kuleta UMOJA na USHIRIKIANO ndani ya nchi. Kwa Hoja ZENYE mashiko na mifano dhahiri Wananchi wangeelewa.

Kisha iseme, Chadema Ipo kwaajili ya kuijenga nchi hii katika UMOJA na USHIRIKIANO. Sio kama CCM walivyofanya(unataja mifano).

Binafsi nimesikitishwa na chama ambacho ni kikubwa chenye miaka 30 Kwa Makusudi kabisa kikashindwa kuifanya siku ya Jana kuwa siku kweli ya uzinduzi. Badala yake wamezindua UCCM.

Kama tutaweka unafiki pembeni, nataka kusema, viongozi wa Chadema wamewaangusha wanachadema,
CCM inawazidije ujanja, Sasa si Bora hata msingefanya Mkutano kuliko kupoteza Muda na Pesa.

CCM wenzenu watapitia humohumo kwenye mapungufu yenu.

CCM ninavyowajua watakuja na kuwapaka Mavi mnuke,

Mimi ngoja nipumzike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es
Kuandika hivi umeona fahari, lakini wakati Mbowe mali zake zinaharibiwa na yeye kuwekwa ndani kwa miezi mingi, je, hao Wana CHADEMA walifanya nini kupinga? Mikutano ilivyozuiwa Wana CHADEMA walifanya nini kupinga? Baada ya Rais Samia angalao kurudisha Uhuru wa kisiasa, ni hoja ya msingi kwa Mhe. Mbowe kushukuru kwa kilichofanyika Kama utangulizi. Hatupaswi kurusha lawama Kama hizi wakati wana Chadema hawakuweza hata Kutoka barabarani kupinga ukiwemo wewe mtoa mada. Je mapambano ya kudai haki ni ya mtu mmoja?
 
Magufuli hakuidhuru Chadema Kwa kiasi kikubwa, labda katika umbo la nje.
Lakini Kwa umbo la ndani Chadema walijidhuru wenyewe pale walipoanza kutetereka kwenye msimamo. Hasa walipomkaribisha Lowasa
Hakuna boost kubwa kwa CDM kama tukio la Lowassa kugombea kupitia CDM! Ukweli ni kwamba CCM walitetemeka kwa hofu kwani Lowassa alikuja na timu yake na kwa mara ya kwanza ushindani mkubwa kwenye kampeni ulionekana, watu hawakuona tofauti kubwa ya “mafuriko” ya watu kati ya vyama hivi. Ila CCM hawakuwa tayari kuachia madaraka. Unajua yote yaliyotokea wakati wa Magufuli vs Lissu, CCM ilikuwa idondoke ila Magufuli alifanya yote aliyofanya bila chembe ya aibu.
 
Basi sawa, lakini mleta hoja nadhani anayo hoja ya msingi.

Yesterday it was a "missed opportunity." Kila mmoja akikaa akatafakari moyoni analithibitisha hilo.

..mimi nadhani vyama vingine vya upinzani vifanyie kazi mapungufu yaliyoonyeshwa na Chadema.

..Mikutano ya hadhara imefunguliwa sasa ni muda wa kila chama kutumia fursa hiyo kujitambulisha kwa wananchi na kuelezea sera zao.

..Mwisho wa siku tuelewe kwamba hakuna chama ambacho hakina mapungufu. Na kila mwanasiasa ana mazuri yake, na mapungufu vilevile.
 
Umesema vizuri Kabisa.
Hofu yangu ni Ile ya kutaka kuibomoa katika umbo la ndani Kabisa.
Chadema isingekufa kivyovyote Kwa mbinu alizokuwa anatumia Magufuli, kwani yeye alijikita kupasua Kwa nje Kwa Kutumia nguvu kubwa.
Ilhali ukitaka kukiharibu kitu totally unatakiwa kukiangamiza Kwa ndani.

Watu wakishapoteza Imani na Chadema kurudi ni kipengele.
Robert Magufuli alifanya mauaji ya CDM nje na ndani. Nje: kwa kuuwa mfumo wa siasa za upinzani e.g. kuzuia mikutano na hata ruzuku za vyama. Ndani: alitargeti watu binafsi kama kina Mbowe kwa kuwafilisi na Pia wafanyabiashara waliodhaniwa kuisapoti CDM walikiona. Lililokusudiwa kwa Lissu lengo lake linajulikana ni kuwamaliza CDM kisaikolojia kwa hofu. Ni viongozi wangapi CDM walurubuniwa kwa fedha na vyeo? Alijitahidi kuua ndani na nje kwa nguvu zote.
 
Kuandika hivi umeona fahari, lakini wakati Mbowe mali zake zinaharibiwa na yeye kuwekwa ndani kwa miezi mingi, je, hao Wana CHADEMA walifanya nini kupinga? Mikutano ilivyozuiwa Wana CHADEMA walifanya nini kupinga? Baada ya Rais Samia angalao kurudisha Uhuru wa kisiasa, ni hoja ya msingi kwa Mhe. Mbowe kushukuru kwa kilichofanyika Kama utangulizi. Hatupaswi kurusha lawama Kama hizi wakati wana Chadema hawakuweza hata Kutoka barabarani kupinga ukiwemo wewe mtoa mada. Je mapambano ya kudai haki ni ya mtu mmoja?

..nadhani kauli yako ni ya kuwakandamiza wanaChadema.

..kuna wanachama na wafuasi zaidi ya 400 waliotiwa magerezani na mahabusu wakati wa Jpm kwasababu ya kuitetea Chadema na kusimamia haki.

..Ni kweli hakuna mwana Chadema aliyeingia barabarani, lakini wapo wengi waliotumia njia za AMANI kudai na kutetea haki na utawala wa sheria.
 
Back
Top Bottom