Janet Yellen: Washington yatatokea madhara makubwa Marekani ikijitoa China

Janet Yellen: Washington yatatokea madhara makubwa Marekani ikijitoa China

Hukumsikiliza vizuri yule Mbunge wa Hong Kong kwenye video aliyokuwa anaongea na mtangazaji Mhindi. Ameeleza vizuri jinsi jinsi ambavyo IMF na World Bank wanakuwa misled na serikali ya China kwa kupewa data feki.
Kwa hiyo tuache taarifa za IMF na WB tuchukue maneno ya Mhindi na huyo mbunge wa HK? 🤭🤣🤣🤣
 
Win win siyo kwamba utishie usalama wa majirani zako halafu wote tushangilie; kila mara kunapokuwa na matatizo ya wakimbizi huwa hawakimbilii China au Urusi, wote hukimbilia europe, US, Canada na Australia. Win win siyo kwamba urushe bumuda lako ndani ya mipaka yangu wazi wazi kupiga picha halafu mimi nishangilie kuwa hiyo ni wini wini. Ni failure kubwa sana ya diplomacy ambayo haikuwa miaka ya tisni na elfu mbili. Waziri wa ulizni wa marekani anasema tukutane na waziri wa ulizni wa china tuongee ili kupunguza tension baina yetu, lakini waziri wa china anasema kwa kiburi kuwa hana interest; mambo ya kijinga sana hayo. Kama waziri wa ulinzi hana interest ya kuondoa Tension na marekani, unaona kuwa ni unafiki kwa viongozi wa China kuitisha mikutano na viongozi wa biashara wa marekani, ingawa wao hawakujibu rudely kuwa hawana interest lakini walihudhuria mikutano hiyo ingawa wengine bado wanaendelea kuhamisha biashara zao kutoka China kwenda nchi za jirani.




Kati ya US na China nani mchokozi? uyo US anafanya chokochoko kule TAIWAN, punguza mahaba kwa hao west na punguza chuki kwa China. China anachokozwa na US unataka aendelee kumwabudu??
 
Nikukuambia ukweli wewe unaukataa. Sasa nadhani ukiwasikia hao wachina wenyewe ambao siyo wapiga propaganda nadhani utawaamnini kuliko mimi mmatumbi. Mwingine ni huyu mwanamke ambaye nilikuwa sijamaliza kumsikiliza




Unapodai China walikuwa ni viwanda tangu zamani na kufanya kuwa hiyo ndiyo criterion yako, unasahahu kuwa hata North Korea walikuwa na viwanda, Czechoslovakia (kabla ya kuvunjika) walikuwa na Viwanda, na hata Argentina walikuwa na viwanda tangu zamani lakini uchumi wao haujakuwa. Ukiangalia kwa nini utagundua kuwa hawajawahi kupata investments kutoka West. Ila ukiambiwa ukweli unashindwa kuumeza na kujaribu kuendeleza propaganda. Nchi za kiimra kama china na Urusi ni wazuri sana kwa propaganda kwa vile wanachuja sana habari na wewe ni victim wa hizo propaganda.


Mkuu tuambie indicators za GDP ni zipi? Tuanzie hapa, Hizo video nyingi ni Propaganda.
 
  • Thanks
Reactions: TPP
Hapo Yellen kasema vizuri kuwa itakuwa mbaya endapo Marekani atajiondoa China kiuwekezaji.

Kumbe uwekezaji mkubwa ni wa Marekani na wala haringi
Hilo mbona linafahamika, wakiondoka watakuja wengine kwenye production line ile ile, swali ni je hao watakaoondoka(wamarekani) wataenda kuwekeza wap bila kuathiri production line I.e. price of raw material, energy na supply route!
 
Uchumi wa China uliitegemea sana Marekani na ulijengwa wakati wa Hu Jintao. Huyu jamaa yeye amekuja na zile fikra za kizamani za anti-US zinafofuatwa na Putin na ameanza kuharibu nchi yake. Usitukane wakunga wakati uzazi ungalipo.
Mchina uchumi umeyumba sababu ya athari za corona, kipindi cha lockdown uzalishaji Ulishuka sana,, kwa sasa anarudi no maana hata serikali imeandaa stimulus package kwa makampuni yaliyopigika kipindi cha lockdown
 
Hapo Yellen kasema vizuri kuwa itakuwa mbaya endapo Marekani atajiondoa China kiuwekezaji.

Kumbe uwekezaji mkubwa ni wa Marekani na wala haringi
Na tukusaidie tu viwanda vingi vya marekani vipo china kwa sababu ya cheap energy, easy supply routes na sheria ngumu za mazingira ambazo zipo marekani, wamarekani wenyewe hawawezi kukubali hii kitu watamuondoq huyo babu kulinda uchumi wao!
 
Kati ya US na China nani mchokozi? uyo US anafanya chokochoko kule TAIWAN, punguza mahaba kwa hao west na punguza chuki kwa China. China anachokozwa na US unataka aendelee kumwabudu??
US iko Taiwan, Japan, Phillipnines, na Korea kwa tangu mwaka 1949. Kwa hiyo haijachoikoza, na hayo yalikuwa makubaliano baina ya Merakani na nchi hizo na ilikuwa ni kitu normal tu kabla ya chokochoko zilizoanza kufanywa na Rais wa Maisha.
 
US iko Taiwan, Japan, Phillipnines, na Korea kwa tangu mwaka 1949. Kwa hiyo haijachoikoza, na hayo yalikuwa makubaliano baina ya Merakani na nchi hizo na ilikuwa ni kitu normal tu kabla ya chokochoko zilizoanza kufanywa na Rais wa Maisha.

Unazingua sana uelewa wako ni mdogo sana kwenye haya mambo. Mmelishwa sana Propaganda na US.
 
Mchina uchumi umeyumba sababu ya athari za corona, kipindi cha lockdown uzalishaji Ulishuka sana,, kwa sasa anarudi no maana hata serikali imeandaa stimulus package kwa makampuni yaliyopigika kipindi cha lockdown
Nimeshangaa kuna mwingine anashangaa China kuja na stimulus package. Kwenye uchumi hii ni kitu ya kawaida sana
 
Mkuu tuambie indicators za GDP ni zipi? Tuanzie hapa, Hizo video nyingi ni Propaganda.
Huyo mama ni mchina, na yeye mwenyewe ni mchumi. Ameweka takwimu za kutosha kukonyesha GDP halisi ya china ni ipi. Amefikia hata kusema kwa nini China bado ina njia ndefu kiuchumi kwa sababu ya kutokuwa na national brand yoyote inayotambulika duniani na kwamba viwanda vyote vya china vingi ni vya kuassemble parts zilzonunuliwa nje au kutoka kwenye viwanda vya nchi za nje na hata kueleza kuwa Huawei bado siyo national brand ya China. Mwishoni ametumia muda kujibu maswali kadhaa aliyokuwa anaulizwa na watazamaji wake na kayajibu vizuri sana.
 
Huyo mama ni mchina, na yeye mwenyewe ni mchumi. Ameweka takwimu za kutosha kukonyesha GDP halisi ya china ni ipi. Amefikia hata kusema kwa nini China bado ina njia ndefu kiuchumi kwa sababu ya kutokuwa na national brand yoyote inayotambulika duniani na kwamba viwanda vyote vya china vingi ni vya kuassemble parts zilzonunuliwa nje au kutoka kwenye viwanda vya nchi za nje na hata kueleza kuwa Huawei bado siyo national brand ya China. Mwishoni ametumia muda kujibu maswali kadhaa aliyokuwa anaulizwa na watazamaji wake na kayajibu vizuri sana.

Hujajibu SWALI nitajie indicators za GDP.
 
Huyo mama ni mchina, na yeye mwenyewe ni mchumi. Ameweka takwimu za kutosha kukonyesha GDP halisi ya china ni ipi. Amefikia hata kusema kwa nini China bado ina njia ndefu kiuchumi kwa sababu ya kutokuwa na national brand yoyote inayotambulika duniani na kwamba viwanda vyote vya china vingi ni vya kuassemble parts zilzonunuliwa nje au kutoka kwenye viwanda vya nchi za nje na hata kueleza kuwa Huawei bado siyo national brand ya China. Mwishoni ametumia muda kujibu maswali kadhaa aliyokuwa anaulizwa na watazamaji wake na kayajibu vizuri sana.

Achana na hizo video mdogo wangu zinakupoteza, China hawana National Brand inayotambulika duniani.? Kwaheri ndugu ntakua napoteza muda kubishana na wewe.
 
Waziri wa ulizni wa marekani anasema tukutane na waziri wa ulizni wa china tuongee ili kupunguza tension baina yetu, lakini waziri wa china anasema kwa kiburi kuwa hana interest; mambo ya kijinga sana hayo. Kama waziri wa ulinzi hana interest ya kuondoa Tension na marekani, unaona kuwa ni unafiki kwa viongozi wa China kuitisha mikutano na viongozi wa biashara wa marekani, ingawa wao hawakujibu rudely kuwa hawana interest lakini walihudhuria mikutano hiyo ingawa wengine bado wanaendelea kuhamisha biashara zao kutoka China kwenda nchi za jirani.
General Li Shangfu yupo chini ya vikwazo toka U.S toka 2018 kivipi anaweza zungumza na mwenzie wakati amewekewa vikwazo na US wenyewe ?
 
Unazingua sana uelewa wako ni mdogo sana kwenye haya mambo. Mmelishwa sana Propaganda na US.
Mimi nimewahi kuishi Hongkong, Japan, Korea na Marekani ingawa sijawahi kuishi Taiwan.

Historia ya kwa nini jeshi la Marekani liko kwenye maeneo iko wazi na hayakuaza leo. Kuwa US wana mktaba wa kulinda Japan baada ya kuiangusha mabomu ya atomiki mwaka 1948 na bado wanaheshimu mktaba huo. Baada ya Korea kugawanyika kati ya North na South na kupigana vita mwaka 1952 ahdi 1953, Urusi iliamua kuisidia sehemu ya North ambayo ilikuwa na viwanda Sana kusudi wajenge nchi ya kikomunist chini ya Kim Il Sung, Marekani ikailinda sehemu ya kusini ambayo ilikuwa maskini sana wakati huo ikiwa chini ya Syngman Rhee ikiahidi kujenga uchumi wa Capitalism. Vile vile baada ya vita ya China ya mwaka 1949, Chiang Kaishrk alipohamia Taiwani alisaidiwa na Marekani kujenga uchumi wa kicaptalist na kumwachia Mao kujenga uchumi wa kikomunist huko China bara. Kuanzia mwaka huo 1949 Marekani imekuwa inalinda visiwa vile vya Taiwan, ndiyo maana kwenye population ya wachina walioko marekani leo wengi ni wa kutokea Taiwan.

Kwa kufuata historia hiyo utaona wazi kuwa Marekani imeshakuwapo pale kijeshi kwa miaka zaidi ya 70 na maisha yalikuwa yanaenda vizuri tu sehemu zote bila msuguano. Tatizo lilianza wakato Rais wa Maisha alipoanza kunyang'anya maeneo ya bahari ya China sea kutoka kwa majirani zake akijenga visiwa artificial. Hii tabia ya kunyanganya maeneo ya majirani (conquests) ni tabia ya kizamani sana (barbaric) ambayo naona inafanywa na viongozi wa China na Urusi tu
 
Back
Top Bottom