Januari Makamba: Wanaohoji kuchelewa Mradi wa JNHPP ni upuuzi tu

Januari Makamba: Wanaohoji kuchelewa Mradi wa JNHPP ni upuuzi tu

IMG_20211228_160309.jpg
 
Waziri Makamba namkubali sana kwa utendaji, sina mashaka nae, ni waziri mbunifu, makini na mchapa kazi.

Sasa Jambo la msingi ni kwa watendaji wote wa Tanesco, vhapeni kazi kwa masilahi ya watanzania, acheni majungu.
 
Kama ni kuuawa basi atauawa kama wezi wengine huko mitaani. Vibaka wanauawa kila kukicha, na yeye atauawa kama vibaka.
 
Leo Waziri wa Nishati, Januari Makamba amewajibu wanaohoji kuchelewa kwa Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere JNHPP ni upuuzi tu na kama hawaamini majibu yake basi wamuue.

"Ukisema Bwawa litachelewa kwa sababu hii na hii wanasema muongo huyo, mshenzi huyo basi njooni mniue basi kama hamuamini, wote ni upuuzi tu" amesema Makamba

Source: Wasafi Media


Watoto wa kiswahili. Ndimi hazina stop. . tuna lamba asali ya mama.
Shenzi kabisa.
 
Leo Waziri wa Nishati, Januari Makamba amewajibu wanaohoji kuchelewa kwa Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere JNHPP ni upuuzi tu na kama hawaamini majibu yake basi wamuue.

"Ukisema Bwawa litachelewa kwa sababu hii na hii wanasema muongo huyo, mshenzi huyo basi njooni mniue basi kama hamuamini, wote ni upuuzi tu" amesema Makamba

Source: Wasafi Media



Sasa naungana na wale wote wanaohitaji katiba mpya.
 
Kwa hiyo bwawa limeisha??
Yeye alianza kwa uongo uongo wa lengo la kuhujumu bwawa ambalo ni hazina ya nchi.
Hilo halikubaliki asilani. Tutamkimbiza kama paka mwizi.
Mtakimbia nyinyi mkalinde kaburi kinguvu!
 
Huyo ndo January Halisi, Mediocre at his highest level.Jibu vitu objectively na siyo ku_ seek public sympathy!
Huwezi kufeli mitihani au kuiba papers halafu ukubwani ujifanye wewe genius!
Huyo ndo genius wa akina Mwijaku na li media house lao.
 
Kweli Waziri jasiri sana anaiita Kamati ya Bunge ya Nishati iliyosema hairidhishwi na sababu za kuchelewa kwa mradi kuwa ni Wapuuzi?
Ni muhimu kufahamu kuwa watu wapuuzi ni wengi sana kulinganisha na wenye akili, hivyo siyo ajabu.
Ikitokea hao wapuuzi wakiungana, huwa na nguvu kubwa ya uelekeo kama wa nyumbu wa Serengeti wanaohama.
 
Huyu ndio maana JPM alimtia kapuni analazimisha tu siasa ila sio mwanasiasa
 
tunamtaka waziri aachane na wapika majungu na fitina,

Ukiwa kiongozi makini na mchapa kazi kamwe huwezi kupendwa na kila mtu, wala huwezi kumfurahisha kila mtu, ila jambo la msingi ni kutatua kero za wananchi kwa masilahi ya wananchi.
 
Kwani ni lazima awe waziri.

Si akalime tu huko bumbuli kupitia ile saccos yake?
 
Back
Top Bottom