Japan yaitangaza Tanzania kuwa Kitovu cha Uwekezaji, viwanda. Honda kujengwa nchini

sasa nchi inauzwa kwa 10% mikataba mibovu, tunawatoa wanachi kwenye maeneo yao tunawapa wawekezaji, nchi yetu tunakuwa wakimbizi.
Acheni mawazo potofu!, we kama una shamba unahisi utanyang'anywa tumia akili vizuri. Shamba umekua nalo tangu babu wa babu yako hujawahi kulima chochote humo! Unafurahia tu kuwa pori na umeridhika na kijumba chako cha majani. Mpaka lini?

Kwa kukusaidia mawazo: Nenda andikisha kampuni ya kilimo (itakugharimu si zaidi ya laki 5 kuandika nyaraka na kulipa ada), mashamba yako yamilikishe kampuni hiyo, halafu kaa chonjo kuuliza na kusikilizia hao wajapani wanaotaka kuja kulima pamba uwaambie walete mashine na utaalamu mshirikiane!

"Usipokubali kuliwa, kidogo huli"...JK
 

Mi nasubiri mageuzi hapo Bandarini tu
 
katika viwanda vitakavyojengwa na Japan tanzania tuwekee mchanganuo wajapani wanachukua pasenti ngapi na sisi tunabaki na pasenti ngapi? VINGINEVYO NI KUUZIWA MBUSI KWENYE GUNIA
 


Yeap! YOU NAIL IT Kiongozi! Hata mawaziri kutoka Ujerumani walikuja na kutoa ahadi kutengeneza upya reli ya kati, hatujaona hata taruma moja lililo letwa kuimarisha hiyo reli.

Inachekesha kuona kwamba IKULU inaendeleza siasa za AHADI wakati uchaguzi ulishaisha miaka mitatu iliyo pita. BURE kabisa hii serikali.
 
Hii thread imebeba ujumbe muhimu na mzito kwetu lakini kwa sababu haina chadema wala sheikh ponda ndani inaonekana ya hovyo

nimefurah sana mtazamo wako kaka-vijana hawajitambui, wao ni kupinga kila kitu. Upinzan unawanyima akili ya kufikir na sasa wanadhan ili uwe mpinzani unatakiwa kupinga killa kitu-wataathirika
ki akili na wataanza kujipinga hata wao wenyewe kwa yale wanayokubaliana-
 
Karibu sana Wajapani, Tanzania ni nchi ya amani, tushirikiane kwa faida ya wote.
TANZANIA MBELE, AFRIKA MASHARIKI INAFUATA.
tatizo si wageni njoo! tatizo mtanzania ananufaikaje, tuache mizaa kwenye maisha
 

Mkuu umenena ,CCM hawana mpango wowte wa kuhandle hizo issue, hawajui kuwa wajapanai wanapanua empire yao kushindana na wachina kwani mauzo ya toyo si unayaona?Hii ni nafasi ya Serikali kutumia hiyo fursa kuwashindanisha hawa mataifa, na kuweka mipango ili japani wakianza tengeneza reli basi wasituibie madini hadi wajilipe hapo hapo, na baada ya kujilipa waje igeuza kuwa miundo mbinu yao y akupanua soko, watanzania wajiandae kuwa na share, wajiandae kubana level ya uzalishaji, na kuiba hizo technologia, pia waje wengine tena wa nchi zingine zenye technologia nyingine.

Serikali isipojiandaa, hivi viwanda vitaajiri wageni wengi sana kwa kiasi cha kuleta matatizo mengine makubwa ya uhamiaji.
 
Mojawapo katika sera hii ya Wajapan ni upanuzi na uboreshaji wa bandari ya Dar es Salaam.

Katika mkataba wa Wachina wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo nasikia kuna kipengele ambacho kinazuia uendelezaji wa bandari za Dar es Salaam, Tanga na Mtwara.

Hili limekaaje? Serikali itakuwa haijakiuka masharti ya mkataba wa Wachina?
 
Wakubwa wanainyemelea Tz kama SIMBA akiwa lindoni
 
Bila kujali itikadi ya chama katika hili mh kikwete anastahili pongezi Kama hawa jamaa watajenga viwanda itatusaidia sana hii mipango ya kuinua kilimo bila viwanda ni kudanganyana tu again I hope wajapan watatekeleza a hadi zao wakati mwingine ni vizuri tuweke tofauti za kisiasa pembeni tuangalie mambo mazuri ya nchi yetu
 
Hii thread imebeba ujumbe muhimu na mzito kwetu lakini kwa sababu haina chadema wala sheikh ponda ndani inaonekana ya hovyo
Naniyahovyo kwelikweli, nashangaa sana watanzani kufurahia jambo la hovyo kama hili. Sasa watanzania tusahau kabisa kuja kuwa na viwanda vyetu wenyewe! tutaendelea kuwatajirisha wenzetu huku sisi tukiimba wimbo wa umaskini milele na milele, amina.
 
Kwasasa pikipiki tuna import kutoka nje lakini matokeo ya SUNLG ya kuua kila siku kwa ajali na BOXER kwa kupora,kuua na kumwagia watu tindikali yanatumaliza sasa wakituletea hapa hapa basi tutegemee kiama.
 
Ndo michoro ya kushinda uchaguzi 2015, subiri mtaniambia!!! Magamba nouma, it will sound good kama hiki kiwanda kitajengwa pale Tabora au Simuyi na siyo kila kitu Dar.
 
Hili jambo ni jema sana kwa nchi ila nasikitika tuna viongozi wa ajabu nchini. Mwezi uliopita alikuja makamu Rais wa Samsung akitokea South Africa alikuja kwa lengo la kuangalia eneo zuri la kujenga kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za samsung nchini. Alipokelewa na afisa wa wizara wakaenda kumtupa bagamoyo bila ya maelezo yeyote yenye umuhimu kuhusu uwekezaji. Kisa ni tu hakuelewana na wakubwa wetu basi wakubwa wetu wakampotezea. Matokeo yake akapanda ndege na kwenda zake Kenya na kuishia zake South Korea. Hawa wawekezaji wanaweza kuwa na nia nzuri ya kuwekeza nchi ila na sisi tunalazimika kubadilika kifikra na kiakili na tuwe na uzalendo zaidi kwenye mambo yenye maslahi ya nchi.

Nashauri wahusika wafanye maandalizi kabambe kuwezesha wawekeze nchini ili tupate kutoa ajira kwa vijana wetu na taifa liende mbele. Tuache ubinafsi na tuwe wazalendo.
 
HAWA JAMAA TUKIWA NA SERA NZURI ZA UWEKEZAJI TUTAFAIDIKA SANA NAKUMBUKA MWAKA 2011 NILITEMBELEA TOYOTA PALE JAPANI NA PIA NIKAFANIKIWA KUTEMBELEA NEMC TOKYO JAMAA WANA TEKNLOJIA YA HALI YA JUU SANA !Big up President japo wengine wanasema eti unaenda kula bata!KEEP IT UP.
 
Wafungue na Kiwanda cha Tindikali pia
 
Hii thread imebeba ujumbe muhimu na mzito kwetu lakini kwa sababu haina chadema wala sheikh ponda ndani inaonekana ya hovyo

Haya ni mawazo yako. Nani kakuambia yaonekana hovyo? Watu wanasema kile wanachofikiri na kuona.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…