Unasema Hakuwa mke ila biblia Inasema alikuwa Mke sasa Tumuamni nani weeewe Au biblia unayoifuata au ulipotoa kisa...?
Bilha na zilpa wana status tofauti na Hajiri na ndo maana Umeona anadiskasiwa kwa mapana..
Nakurudisha tena kusoma Mwanzo 16:3 ambayo huchangii chochote kuihusu..
Mwanzo 16:3
"Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe."
And Sarai Abram's wife took Hagar her maid the Egyptian, after Abram had dwelt ten years in the land of Canaan, and gave her to her husband Abram to be his wife.
Hakuna Kijakazi yoyote Aliwahi kupewa Hii status Kwenye Biblia kama ulimpata Nionyeshe Andiko nijifunze kitu kipya ambaye alikuwa kijakazi halafu akaitwa mke
Nimekujibu kwamba Sheria Za kiyahudi au sheria za kiebrania zimepitia Mapito mengi sana Na zimekuwa zikibadilisha na kutiliwa mkazo...
Sheria za Musa na torah na Sheria za Halakha (Sheria za sasa za kiyahudi) ni tofauti na sheria kipindi cha Ibrahimu na kina Yakobo..
Ni sawa ufananishe Sheria ya Kipindi cha Kinjikitile ngwale na kipindi hiki cha sasa Eti kwa sbabu tu zote ni Tanganyika ....Hapana..