Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Mkuu hakuna kitu kama hicho mkiristu anaweza kufanya kama wewe, kwamba kusherehekea kukombolewa kwa huyo jamaa, inshort haina ishara kwa mkristo maana huyo jamaa hakuwa na ishara iliyotolewa na mwenyeezi Mungu kwamba apewe nafasi yoyote kwa ukumbusho.

Sikia kijana kisa cha Ibrahim na mwanae kile kilikuwa ni kwa ajili ya kuonyesha Imani, unyenyekevu na kujitoa katika hali ya maumivu kwa kitu unachokipenda hasa.

Kama hujui (soma Mwanzo 20:1... hadi mwisho na 21 yote kuna kisa hapo why Ibrahimu alipewa JARIBIO lile na ingia hapo Mwanzo 22 fungu la 1 na 2 kisha chop to verse 13, utaona badala ya kutoa yule jamaa Isaac Mungu akamletea mwana kondoo.

Verse 12.b inasema "kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee"

Mwenyeezi Mungu alikuwa anampima mzee Ibrahim pamoja na bibi Sarah kama wana imani kwake kwa mtoto wao wa uzee, sababu walikaa muda mrefu bila mtoto *Mwanzo 17:17.
Sawa, mi sikatai kuwa hiyo ilikuwa ni kipimo cha imani kwa Ibrahim na familia yake, hata Quran imeelezea hivo
 
1000017884.png


Kwa Waislam au Watu ambao wanataka kupotosha kuhusu Wapi Mlima Moria ulipo na kutaka kuhusisha na Mecca.

Moria ni Eneo lilikuwa Jerusalem, Wakati wa Ibrahim anakaa Kaanani Jerusalem ilikuwa ni Nchi ya Jebusites.

Hili Eneo kwenye hii Ramani lilioandika Haram El Sharif ndipo kuna ile inaitwa Dome of the Rock, ndani yake kuna Jiwe linalosemekana Ibrahim alimlaza Isaka, Ndio maana inaitwa Dome of the Rock, this is proof kuwa Quran in most cases ni fabricated document
 
Hayo ni maoni yako,...lakini Biblia haijasema kwamba Isihaka ndiyo mtoto wa pekee wa Ibrahim......so kwa akili ya kawaida tu utajua kwamba Ismail ndiyo amewahi kuwa mtoto wa pekee wa Ibrahim kabla ya kuzaliwa wadogo zake.....
Bible imetawataja watoto wote wa kiume wa Ibrahim
 
Hapo kuna ukweli fulani lakini siyo kwa Qur'an, itakuwa ni wafasiri / washereheshaji (commentators) wa Qur'an.

Binfsi sifahamu kwanini walikihusisha kisa cha Ibrahim cha kwenye Qur'an na vitabu vilivyotiwa mikono ya watu.

Uzuri ni kuwa Qur'an orijino ipo kwa lugha ileile orijino iliyoletwa nayo, mtu akiongeza lake kwenye tafsiri tunamstukia tuliojaaliwa kuijuwa kwa lugha yake oroijino na si kwa kufata washereheshaji wanaopotosha.
Waandishi wa Quran waliifanyia editing BIBLIA.

Nadhani tupo pamoja.
 
Wanabodi,
Leo ni sikukuu ya Eid El Haji, Iddi ya Kuchinja.

Leo ni siku ya Sikukuu ya Idd El Haj, ni iddi ya kuchinja, asubuhi nilikuwa naangalia matangazo ya mubashara ya Baraza la Iddi kupitia TBC, kutoka Msikiti wa Mfalme Mohammed VI wa Morroco, Bwakwata, Kinondoni jijini Dar es Salaam, kumbe Msikiti Mkuu wa Bakwata, sasa umebadilishwa jina!, na kupewa jina la Mfalme wa Morroco!.

Mgeni rasmi kwenye Baraza la Iddi ni Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, ambaye ameandamana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye amesilimishwa na kupewa jina la Aboubakar Chalamila!, na mawaziri akiwemo Waziri Mhe. Mohamed Mchengerwa. Baadhi ya watu maarufu niliowaona ni pamoja na Alhaj Sheikh Ali Nguruko, Alhaj Chande, Idda Azan, Shaweji Abdalah, Salum Mwalimu, Juma Simba Gadafi, Salum Abladaha "TRY Again", Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Mruma, Kadhi wa Dar es Salaam, Shamin Khan, mwenyekiti wa JUAKITA, pia kulikuwa na mabalozi wa Balozi wa Moroko, na wa Comoro.

Katika salam zake, Sheikh Aboubakar Chalamila alisema utulivu wa jiji la Dar es Salaam, unawategemea sana viongozi wa Dini.

Salaam za Waislamu, zimetolewa na Alhaj Sheikh Nuru Mruma, Katibu Mkuu wa Bakwata ambaye amewasisitiza Waislamu kudumisha amani na kuilinda amani. Wazazi watakiwa kulea watoto wao kwa tabia njema, kujenga taifa la kizazi cha watu wema ambao hawatapokea rushwa wala kufanya ufisadi.

Amesema kupanda miti na utunzaji wa mazingira ni ibada muhimu kwa Waismamu wote.

Pia amewataka Waislamu kujitokeza kwa wingi, kujiandikisha kwenye uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura.
na wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya kidemokrasia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Salaam za Mufti, zimetolewa na Kaimu Mufti Sheikh Ali Muhidin Mporogore, Mjumbe wa Baraza la Maulamaa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania, Bwakwata. Aamezungumzia Watanzania tutafakari, sadaka ya kuchinja siku ya Iddi El Haj, ni iddi ya kuchinja. Zamani ilikuwa sio kuchinja tuu wanyama, bali walichinja hata binadamu ana akatolea mfano Sadaka ya Nabii Ibrahim kutaka kumtoa mwanae Ismail, kwa sadaka ya kuchinja.

Hakuna ubishi kuhusu Wakristo na Waislamu, kuwa ni watoto wa Baba mmoja, Nabii Ibrahim hivyo huu ni uthibitisho wa Mungu wa Wakristo na Waislamu ni Mungu Mmoja, ila kuna watu wanafundishwa ukweli na kuna watu wanadanganywa!.

Hakuna ubishi kuwa mtoto wa kwanza wa Ibrahim ni Ismail aliyezaa na mjakazi wa Kimisri, Hagir, na Isaka ni mtoto wa pili wa Ibrahim, aliyemzaa na mkewe Sarah.

Hakuna ubishi Ibrahim alitaka kumtoa mtoto wake Sadaka ya kuchinja.

Waislamu na Kitabu chao Kitukufu cha Quran Tukufu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Ismail.
Wakristo na Kitabu chao Kitakatifu cha Biblia Takatifu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Isaka.

Jee ukweli halisi ni upi?.
Hii maana yake
Kama tukio la Ibrahim kutaka kumchinja mwanae kumtoa sadaka ni tukio moja, then
1. Hii maana yake ni kuna watu wanadanganywa, haiwezekani kwa Waislamu mtoto huyo awe ni Ismail na kwa Wakristu mtoto huyo awe ni Isaka, hii maana yake kuna kitabu hapo kinasema kweli na kuna kitabu kinasema uongo!, jee ukweli ni upi?.

Umuhimu wa kuujua ukweli huu, unakupa fursa ya kujua ukweli ni upi, hivyo ufuate mafundisho yapi ambayo ndio mafundisho ya kweli!.

Bandiko hili linakutaka kwanza uwe open minded, kama wewe ni mfia dini, unaamini dini yako ni ya ukweli mtupu, bandiko hili halikufai.

Pili unatakiwa uwe na ngozi ngumu ya kuukubali ukweli halisi hata uwe mchungu vipi!, ikitokea ni dini yako unayoiamini kuwa ni dini ya kweli, kumbe ni dini ya uongo, uwe na uwezo wa kustahimili maana...

Nawatakia Waislamu wote,
Iddi Mubarak njema ya kuchinja.

Paskal
Hakuna umoja kati ya waislam na wakristo tunatofautiana hata kimaandiko sisi biblia haitufundishi kulipa kisasi wala kuua
 
Katika watoto hao wote,..yupi amewahi kuwa mtoto wa pekee wa Ibrahim?

Namaanisha Mtoto yupi aliishi kipindi ambacho Ibrahim hakua na mtoto mwingine isipokua yeye?
Upekee wa huyo mtoto ni hilo agano Mungu alilofunga na Ibrahim. Agano lilitaka Baraka ziende kwa mzao na sio wazao kana kwamba ni wengi. Mungu hakukosea kwenye kutamka. Kwani siku amemleta Adam duniani akishindwa kuleta wanadamu wengi. Sote tuliumbwa siku Moja kule mbinguni ila tumeletwa duniani Nyakati tofauti tofauti. Roho yako ilikwisha kuumbwa toka Mungu alipomuumba mwanadamu.
Alifunga agano na mtu mmoja ili baraka zipitie kwake kwenda Kwa alio wapenda.
 
Upekee wa huyo mtoto ni hilo agano Mungu alilofunga na Ibrahim. Agano lilitaka Baraka ziende kwa mzao na sio wazao kana kwamba ni wengi. Mungu hakukosea kwenye kutamka. Kwani siku amemleta Adam duniani akishindwa kuleta wanadamu wengi. Sote tuliumbwa siku Moja kule mbinguni ila tumeletwa duniani Nyakati tofauti tofauti. Roho yako ilikwisha kuumbwa toka Mungu alipomuumba mwanadamu.
Alifunga agano na mtu mmoja ili baraka zipitie kwake kwenda Kwa alio wapenda.
Hujajibu swali nililouliza.....

Katika watoto hao wote,..yupi amewahi kuwa mtoto wa pekee wa Ibrahim?

Namaanisha Mtoto yupi aliishi kipindi ambacho Ibrahim hakua na mtoto mwingine isipokua yeye?
 
Kabla ya kujibu hilo swali tumjue kwanza. Kati ya ismail na isihaka nani mtoto wa kwanza kuzaliwa kwa ibrahim
Wa Kwanza Kuzaliwa ni Ishmael, according to Muslims scholars Ishmael alitaka kutolewa Sadaka Mecca.

At the same time wanakubali kuwa Ibrahim na familia yake waliishi Kaanani Israel ya Leo na hata Ishmael alizaaliwa na kukulia Kaanani na hata alipofukuzwa yeye na mama yake walifukuzwa kutoka Kaanani kwenda Edom ambayo ni Jordan ya Leo..

Wanazuoni wa Kiislam wanakubaliana kabisa Kaburi la Ibrahim liko Hebron katika Israel ya Leo.

Ni lini Ibrahim na Ishamel walifika Mecca, huoni Quran au watafsiri wake hawakuwa na story Sahihi?
 
Kwa nini Ibrahim alimfukuza Hajiri na Ishmael huku akijua mtoto wa kwanza ndiye mrithi?
Si kweli kwamba mtoto wa kwanza ndio mrithi, rejea historia ya Yusuf alikuwa ni mtoto wa kumi na mbili kama sijakosea, ila si ndo yeye aliyefuatia katika utume baada ya baba yake wakati anao kaka 11 juu yake.

Pili, narration ya kwamba Ibrahim aliwafukuza Hajra na mwanawe hii ni narration ya biblia sio Quran. Ibrahim alienda pamoja nao akawaacha pale alipoamrishwa na mwenyezimungu akawaache (jangwani), hii ilikuwa ni trial kwake kama ile trial ya kumchinja mwanawe.

Naendelea kutafuta ecidence ya ayah ila kama yupo anayeijua atuwekee hapa
 
Hakuna umoja kati ya waislam na wakristo tunatofautiana hata kimaandiko sisi biblia haitufundishi kulipa kisasi wala kuua
Wakristo na Waislamu ni watoto wa Baba mmoja Ibrahim na Mungu wao ni mmoja, Waislamu ni watoto wa mtoto wa kwanza wa Ibrahim aitwae Ismail na Wakristo ni watoto wa mtoto wa pili Isaka, hata sheria ya Mungu ni sheria ya Musa.

P
 
Upekee wa huyo mtoto ni hilo agano Mungu alilofunga na Ibrahim. Agano lilitaka Baraka ziende kwa mzao na sio wazao kana kwamba ni wengi. Mungu hakukosea kwenye kutamka. Kwani siku amemleta Adam duniani akishindwa kuleta wanadamu wengi. Sote tuliumbwa siku Moja kule mbinguni ila tumeletwa duniani Nyakati tofauti tofauti. Roho yako ilikwisha kuumbwa toka Mungu alipomuumba mwanadamu.
Alifunga agano na mtu mmoja ili baraka zipitie kwake kwenda Kwa alio wapenda.
Lakini pia unapozungumzia baraka,... mbona inaonyesha Ismail na Isihaka wote wamepewa baraka nyingi tu... hii imekaaje
 
Huu si ugwadu tu,Wana wa Mungu!!?..Mungu Hana watoto,Wala Aya haisemi mission ya nuhu ni kujenga safina tu,nabii wa kujenga safina tu!!?..be serious babu

Aya ipi Haisemi wito wa Núhu
Mimi nilikuwekea aya hiyo kujibu swali lako ilipouliza Núhu alikuwa mpagani.

Jibu la biblia ni kuwa hiyo Núhu mwenyewe alipata tuu neema sio kwamba alikuwa mtakatifu kihivyo

Ukisoma stori yoyote lazima ujue na kuzingatia yafuatayo;
1. Dhamira kuu ya stori.
2. Mbebaji wa dhamira hiyo ni nani? Huyu huwa mhusika Mkuu


3. Ujumbe wa stori ni upi.
4. Mtazamo na falsafa ya stori

Sasa nje ya Safina Núhu anajambo lipi linalomfanya aandikwe kwenye Biblia au Quran?

Au unafikiri watunzi na waandishi wanaandikaga tuu?

Mungu ni Baba.
Kasome Semantic ya Lugha kisha soma Falsafa ya dini (Theolojia) utaelewa mambo haya

Lakini kwa akili ndogo ndogo huwezi kuchambua mambo ya kitaalamu na kifalsafa au Kifasihi au Isimu. Yaliyopo kwenye maandishi
 
Kwanza mimi sijasoma theology. Nasoma biblia kujifunza tu.

Documentary Hypothesis
nimeiosoma ila ni mawazo ya wanadamu tu hasa wanatheology wanaotumia hekima za kibidamu yenye kikomo, ndio maana kuna mambo mengi watu wameyatambua mpaka kwenye ujio wa Yesu alipokuja. D hypothesis kama ni kwel basi biblia yote haina maana ni story za kusadikika.

Ukiangalia matukio ya Mwanzo 12;12-20, 20:1-8, 26:6-10 ni tofauti kabisa japo yanafanani. Ila ni Mungu ndio aliyefanya kwasabab hawezi kuchanganya uzao wake na wanadamu ndio maana kila wakati alikua anazui hichi kitu. Soma Mwanzo 6.

Twende kwenye maswali yako.

Beersheba inaanza kuonekana kwenye Mwanzo 21:14 kuwa palikua na jangwa la Beersheba Ibrahimu na Ismael walipita tu kwenye jangwa hili. Mwanzo 21: 21 inaonesha Ibrahimu na Ismael alilipita jangwa la Beersheba akenda mpaka jangwa la parani ambapo Ismael aliishi parani.

Kwaio hapa tuna miji mitatu Hebron, Beersheba na parani utasoma hizi sehem tatu vizur.

Mwanzo 21;22 Abimeleki baada ya kuona Ibrahimu amemsogelea kwa kuogopa yaliomtokea miaka ya nyuma kwenye Mwanzo 20. Ndio maan alikuja kutafta mapatano na Ibrahimu. Ibrahimu alikua anashuka kusini kwasabb ya njaa kali na kusini palikua kuna hauweni ya malisho kwa ajiri ya mifugo yake. Mwanzo 26:1.

Mwanzo 22:19 baada ya jaribu la kumtoa isaka kafara. Ibrahimu alirudi mpaka Beersheba, inaonesha makazi ya Ibrahimu na Isaka ilikua ni Beersheba kama Mwanzo 21:34. Inayosema Ibrahim alikaa na wafilisti miaka mingi kabla ya jaribu la kumtoa kafara Isaka.

Hata ukisoma Mwanzo 28:10 na Mwanzo 46:5 yote yanaonesha Beersheba waliishi Ibrahimu na Isaka. Maana ibrahim, isaka na yakobo wote waliishi hapo kama Mungu anavyojitambulisha.

Hapa nakujibu swali la umri wa isaka wakati wa kutolewa kafara hakuwa mchanga. Kama unabisa lete ushaidi wa maandiko. Kama utatumia Qur'an pia itakua vizur
Umeandika Mengi ila Kitu nachosikitika Umetunga Hoja zako na Umezijibu yaani Umefanya Self Implication..
Hakuna Hoja yangu hata moja Uliyojibu..
 
Si kweli kwamba mtoto wa kwanza ndio mrithi, rejea historia ya Yusuf alikuwa ni mtoto wa kumi na mbili kama sijakosea, ila si ndo yeye aliyefuatia katika utume baada ya baba yake wakati anao kaka 11 juu yake.

Pili, narration ya kwamba Ibrahim aliwafukuza Hajra na mwanawe hii ni narration ya biblia sio Quran. Ibrahim alienda pamoja nao akawaacha pale alipoamrishwa na mwenyezimungu akawaache (jangwani), hii ilikuwa ni trial kwake kama ile trial ya kumchinja mwanawe.

Naendelea kutafuta ecidence ya ayah ila kama yupo anayeijua atuwekee hapa

Tunaomba hiyo simulizi ya Quran inayoonyesha mahali aliporithishwa, achiwa huyo Ishmael
 
Wakati Mungu anmtembelea Ibrahim kwenye mialo ya Mamre alikua tayari ana Ismael lakini alimwambiaje Sara? Utakua mama wa mataifa. Hakuambiwa Hajiri Mmisri wala uzao wake. Pia angalia singularity ya neno mzao na sio wazao. Unatrace uzao kwenye ndoa na ndio maana hata Leo mtoto wa ndoa anatambulika mpaka na mamlaka.
Alitahiriwa maana maagizo yalikua ni watu wote wa nyumbani kwake. Pia kama amemrithi baba yake kwa nini mama amtafutie mke? Kwa Nini mama ndo angolee mahari ya mwanae na baba alikua hai? Mbona Isaka Mzee alimtafutia mke? Unajua Kwa Nini hakumchukulia mke huko Kanaani alikoishi Hali ya ugeni?
Habari Ammoshi!
Ibrahimu alimuoa Hajiri na alikuwa Mke wake wa Ndoa (Mwanzo 16:3)..

Ibrahimu Alimbariki na Kuomba Baraka kwa Mungu Naye Mungu akamsikia na kumbariki Ishamael soma Mwanzo 21..

Maagano kipindi Yanatoka Ibrahimu alikuwa na Miaka 99 na Ishmael alikuwa na miaka 13 Hivyo alitahiriwa na familia yake yote na hilo ndilo agano la.kwanza..

Kuhusu kutafutiwa Mke Unajisahau kabisa kwamba Isaka alikuwa Uzao wa Nadhiri Na Ishmael alikuwa uzao wa Mwili???

Wagalatia 4:28-29

"Basi, ndugu zangu, kama Isaka sisi tu watoto wa ahadi.
Lakini kama vile siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo na sasa."

Wazao wa Nadhiri wote Hutafutiwa Mke ndani ya Ukoo Na ulinzi wa Baba zao..(Fuatilia Kisa Cha Esau (Edomu) na Yakobo)

Kuhusu Urithi na kuwa Pamoja Je Hukusoma Kuwa Isaka na Ishmaeli walimzika Baba Yao alipofariki akiwa na Miaka 175??
 
Wa Kwanza Kuzaliwa ni Ishmael, according to Muslims scholars Ishmael alitaka kutolewa Sadaka Mecca.

At the same time wanakubali kuwa Ibrahim na familia yake waliishi Kaanani Israel ya Leo na hata Ishmael alizaaliwa na kukulia Kaanani na hata alipofukuzwa yeye na mama yake walifukuzwa kutoka Kaanani kwenda Edom ambayo ni Jordan ya Leo..

Wanazuoni wa Kiislam wanakubaliana kabisa Kaburi la Ibrahim liko Hebron katika Israel ya Leo.

Ni lini Ibrahim na Ishamel walifika Mecca, huoni Quran au watafsiri wake hawakuwa na story Sahihi?
Soma hapo.kama una swali lingine uliza.pia baada ya hajr kijakazi wa bibi sara kumzalia Ibrahim mtoto wake wa kwanza Ishmael. Mama Sara akaanza kuona wivu akamchukia hajr na mwanae.ndipo Ibrahim akaamua kuwatorosha na kwenda kuishi makka. Na usisahau kisima cha zam zam.kilichimbwa kwa ajili ya hajr na ismail walipofika makka. Hakukuwa na mji
 

Attachments

  • Screenshot_20240621_103908_Chrome.jpg
    Screenshot_20240621_103908_Chrome.jpg
    572.9 KB · Views: 4
Sarah kumpa Ibrahim Hajiri amfanye mkewe haibadili status ya Hajiri kuwa ni mke wa Ibrahim

Ndoa ni suala la kisheria na kimila. Sarah hana mamlaka wala uwezo wa kumuozesha Mwanamke yeyote kwa Ibrahim ilhali yeye ni Mke.

Huko mbeleni tunaona Ibrahim akimwambia Sarah kuwa huyo Hajiri ni kijakazi wake(wa Sarah) hivyo yeye ndiye mwenye mamlaka ya kuamua uwepo au kutokuwepo kwa huyo kijakazi.

Pili, ishu ya wake za Yakobo ni walewale wawili. Recho na Leah. Hao vijakazi hawahesabiki kama wake Yakobo.

Watoto wa kina Bilha na zilpa walihesabika kwa sababu walikubali mfumo wa familia ha Yakobo. Hawakuwa wasumbufu kwa Mabosi zao.
Hahahaaaa Una Uhakika Mkuu Unajua Sheria Za Ndoa za kiyahudi kama Inavyosema Gimera au Halakha au Torati??

Unafahamu Mwanamke alikuwa na Mamlaka gani kwa mume??

Bhasi nikupeleke Mbele kwa Hao Wake za Yakobo..
Unajua kuwa hata Yakobo hakuwahi Kumregard Lea kama mkewe??

Na unafahamu Kuwa hakuna Mahali imeandikwa kuwa Yakobo alimuoa Lea bali alidanganyika kulala na Lea tu..

So mke wa Yakobo alikuwa Rahel na hao wengine watatu hawakuwa wake wa Yakobo..

Unaweza ukadouble check..Biblia inamtaja Rahel kama ndiye Mke wa Yakobo..ila haimtaji Lea kuwa ni mke wa Yakobo..

TItle ya Mke kwenye Biblia ni title Kubwa Sana Ambayo Kama hakuwa Mke Basi Hajiri angeitwa Suria (Ambayo Ni upgrade ya Kijakazi anapolala na Bwana..

Tatizo letu hatuelewi maandiko ila tunataka Tumeze tulivyoaminishwa bila kureason vitu... nilitoka huko zaman nilipoacha Uchungaji...

Kwanini Mke wa Kwanza alikuwa na Nguvu ya Kumrisha na hata Nguvu ya Kuomba kuolewa mwingine..(Ngoja nakuja na Halakha(Sheria za kiyahudi))
 
Hajiri hajawahi kuwa Mke wa Ibrahim
Alikuwa kijakazi wa Sarah mkewe Ibrahim.

Aliyemfukuza Hajiri ni Boss wake ambaye ni Sarah.

Hiyo simulizi unaijua vizuri?
Kwani Nyie huwa hamsomi Biblia au Mnaongozwa na Chuki..
Hebu someni Mwanzo 16:3 halafu Ichambue bila chuki Au mnataka mpaka tulete Hebrew Version of it tuichambue
 
Back
Top Bottom