JB: Mganda huyu ni nani na anafanya nini Tanzania?

JB: Mganda huyu ni nani na anafanya nini Tanzania?

Mwanakijiji akamwambia; Bwana mkubwa tuliona mtu anawekeza Tanzania kwa jina la la JB; tukakerekwa moyoni, kwa sababu 1, 2, 3, 4,........................ PConsultant akawaambia akamwambia, usikerekwe/usichukie/ wala usishtuke, kwa kuwa yeye ambaye si kinyume chenu yu upande wenu. (Mathew 9:50 KJV)
 
shida yako ni kasi ya kumiliki ama uhalali wa umiliki?Inaonekana umeathiriwa na snail-pace attitude ya Kitanzania,ile ya mtanzania kununua kiwanja then anakaa miaka kumi ndio anaweka msingi.Waganda wanafanya kazi na wame-embrace ujasiriamali kwa moyo wa ujasiri na bidii.

Ujinga kama huu wako ndio janga halisi la kitaifa-watu kupenda uzushi au ku-conclude mambo bila hoja au ushahidi wowote!JB(ingawa simjui) ni janga la taifa kivipi?Halipi kodi?Yeye ndie anayefanya sisi tusifanye kazi na kuishia kuimba nyimbo za ufisadi na freemason?Kuna mtanzania amezuiliwa kufanya biashara Uganda?Tatizo letu ni elimu ya kukariri na kujibu mitihani ya darasani tu.Huu ndio utandawazi uliokariri darasani,watu wanazunguka dunia nzima kutafuta business opportunities.Acha JB afanye kazi huku sisi tukiendeleza porojo zetu za kuogopa kujiunga na EAC kwa sababu ya uvivu wetu.Unamwita JB malaya na kusahau kuwa kama ni umalaya si anaufanya na Watanzania wenzetu,kwa nini tusiwalaume hao watanzania wenzetu,let's deal with our own failures first.


Unaposoma comments za wachangiaji wa hii Thread unazidi kupata picha halisi ya elimu yetu na uwezo wa kufikiri.Mtu anaandika kuwa JB ni janga la taifa(huu nao umekuwa msemo ambao kila asiye na hoja anautumia kuficha utupu wake) bila kutoa sababu yoyote.Wengine wanadai Kasi ya JB inatisha,haya ni madhara ya watu kuzoea kasi ya kobe,kila kitu foleni,mipango kuchukua miaka mingi kuliko utendaji.Uvivu wetu unazidi kukua kwa kasi kwa hio wakija wageni wakaona nafasi za kukua kwa biashara zao hapa Tanzania tunaishia kwenye porojo zetu za kila siku ilhali ripoti zote za kimataifa zinaonesha kuwa tunaongoza kwa uzembe kwenye EAC.


I find your statement to be too subjective...ni kama umesha-form an opinion about this 'JB character'.Ni sawa na mtu kukuuliza ' You look so nervous,how do you feel?'

Lonestriker Mbona umetoka sana povu kwenye hii thread ndugu? What are you not telling us about this JB?
 
Last edited by a moderator:
Kwanini kuna jitihada kubwa ya kutotaka kumwangalia au kumsogelea huyu ndugu kihivyo. Wanaojaribu kudivert attention ndio wanavyoweza kumuuza mwenzao. Ndivyo ObL alivyoweza kuuzwa na jamaa kule Guantanamo, Cuba. Walipoulizwa kuhusu x,y courier wa Osama kila mtu aliruka kuwa hamjui kabisa na wale ambao walikiri kumjua walisema ni a non-player... kumbe ndiyo walikuwa wanathibitisha how important he was.
 
pia huyu bwana amepamgisha godown pale mlimani city la vitu vya electronics used toka UK, possible hiyo biashara pia imempatia faida kubwa, hilo la kuajiri watu wenye elimu ndogo na kuwa train nakubaliana nalo coz kuna jamaa mmoja wa kipare anaitwa Luka yeye ndo kama Manager wake na ni std 7 tu.

Hata mimi nilikuwa na kasumba hiyo hiyo kwamba watu wenye elimu za Chuo Kikuu ndiyo kila kitu - raia walio maliza darasa la saba nilikuwa siwa wachukulii seriously mpaka nilipo kwenda TAZARA karakana for the first time, mambo niliyo yashuhudia humo yalibadirisha kabisa perception zangu totally - toka siku hiyo nilikoma kabisa ku-under rate watu ambao hawajasoma sana. Nilikuta wanaweza kusoma very complex michoro ya spare parts na kuzichonga, mambo ya umeme, forge and foundary na kutengeneza patterns za spare, mahabara za chemicals: organic/inorganic,instrumentation, metrology, metallugy si hilo tu hata mambo ya internal Combustion Engines, kilicho kuja kunitoa jasho ni pale jamaa alipo nilieza kwa ufasaha kuhusu hydraulic transmission na torgue converter zake nakamuuliza mwezangu haya mambo umejifunza chuo gani, akasema nilifundishwa na Wachina humu humu kwenye karakana!!!

Nilichokuja gundua baadae ni kwamba watu wa namna hiyo wako na shahuku kubwa ya kujuwa mambo na kujifunza, hawana kiburi wala dhalau; kwa hiyo mimi simushagai Buguma ku-recruit watu kama hao, watakuwa royal kwake at all times.
 
Umechangia lakini!
Si ndio hapo, jamaa ananikumbusha mshikaji wangu mmoja long time katika stori za kijiweni akawa anawaponda wenzake kwa kula maharage kila siku huku yeye ganda la harage limegandia kwenye jino..basi akawa anakaza mshipa wa shingo kuyaponda maharage watu wanacheka kuliona lile ganda la harage..alipokuja kujua alitaka kubadilisha stori ghafla ikawa ngumu akakimbia kijiwe kwa muda.ikabaki masela wanamtania maharage,ila jina hali kudumu maana alimanusura atoe uhai wa mtu na chupa..Hajui kusema tu sitochangia tayari ameshaingiia kwenye rekodi ya wachangiaji wa thread,sema amechangia negatively maana ajaendana na mada
 
Fitna zinaanza, wacha nitazame sinema ya majungu!

JB = Juma Bhalo.
 
Kwani ni lazima mimi niulize; kwanini na wewe usiulize?

Wewe si ndio mwenye ile sifa humu JF "Ufataani".

Ulisema sana humu kuhusu Richmond na Dowans ilipogeuzwa na kuwa Symbion ukakaa kimya na kuufyata, kwanini?
 
Huyu jamaa anavyodai aliwahi kuwa waziri kule Uganda na baada yakuingia Museveni ikabidi akimbilie Uingereza.JB aliingia hapa tanzania mwaka 2004 hakiwa kama muwekezaji bila mtaji kwa mara ya kwanza alimtapeli mzungu mmoja aliyekuwa akimiliki kampuni ya Reclaimed Tanzania Appliances Ltd iliyokuwa ikijihusisha na huingizaji wa vyombo vya electronics-used na baadaye kumfilisi na yeye kuanzisha duka lililojulika kama PT&Electronics appliances pale mitaa ya msimbazi jirani na BIG BON kisha huyu bwana akafilisiwa kutokana na kesi zilizokuwa zikimkabili za utapeli,huyu jamaa aliingia ana kitu ila ni TAPELI mzuri sana ana sound nzuri na anajisifu kuwa yupo jirani mno na wakuu wa nchi.ni kweli yupo nao jirani kwa sound.
 
Mzee Mwanakijiji,

Mr Justus Baguma, a Ugandan entrepreneur in Tanzania, owns the JB Belmont, Savannah and some shops at Quality Centre and has also been elected the chairman of the Ugandan Community in Tanzania.

He is a self-proclaimed self made man and attributes his success to hard work... Whether "hard work" means "trouble for Tanzania" I don't know....

Naona hoja ya who is JB imejibiwa ila sijaona mchangiajia aliyeainisha tatizo la mtu huyu lakini kama ni enterpneur sioni ubaya. Mleta mada funguka
 
Last edited by a moderator:
Unaposoma comments za wachangiaji wa hii Thread unazidi kupata picha halisi ya elimu yetu na uwezo wa kufikiri.Mtu anaandika kuwa JB ni janga la taifa(huu nao umekuwa msemo ambao kila asiye na hoja anautumia kuficha utupu wake) bila kutoa sababu yoyote.Wengine wanadai Kasi ya JB inatisha,haya ni madhara ya watu kuzoea kasi ya kobe,kila kitu foleni,mipango kuchukua miaka mingi kuliko utendaji.Uvivu wetu unazidi kukua kwa kasi kwa hio wakija wageni wakaona nafasi za kukua kwa biashara zao hapa Tanzania tunaishia kwenye porojo zetu za kila siku ilhali ripoti zote za kimataifa zinaonesha kuwa tunaongoza kwa uzembe kwenye EAC.

Hii ya porojo na kutokuwa serious NDIYO JANGA LA KITAIFA!!!!! Maana huu msemo umekuwa misused kama KUATHIRIKA!!!!!! Ni heri kwanza tukubali kwamba tunalo tatizo kama NCHI (kutokuwa makini; wenye kujituma na mara zote kuwa walalamikaji bila ya kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu) kabla hatujaanza KUBWABWAJA maneno ya kutafuta mchawi (ambaye ni foreginer) hali sisi hapa TUMEBWETEKA na kulialia tuu !!

Hivi kwani hata hawa FOREIGNER WEVI waliruhusiwa na wanaendelea kuruhusiwa na nani KUIBA??? KAMA SIYO WALE WALIOPEWA MAJUKUMU YA KUHAKIKISHA WEVI HAWAINGII NCHINI NA, WAKIINGIA NA KUIBA WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE??? Nina hakika wawakingiao VIFUA NI WATANZANIA WENZETU!!!!!
 
JB ni janga kwa taifa hili....mpeni muda kidogo tu you will prove this..... mbali na hayo mambo ya down to earth ni mzinzi sana na anaharibu sana mabinti pale Quality Centre

Mkuu Kigogo
Anawabaka au wanajipeleka wenyewe????
 
Paradise Hotel inamilikiwa na msomali Kwa jina Mohamed ingawa yeye ni mrithi, hawa ndio wanamiliki wa Paradise Hotel ya Bagamoyo ile iliyoungua moto mwaka 2009 na ndio wanamiliki mgahawa wa city garden pale ppf tower pembeni ya imalaseko na atc, na pia mgahawa wa city garden wa pale gerezani, na hotel za arusha zijulikanazo kama east africa, kwa faida ya wengine baba wa Mohamed ni moja ya mawaziri kipindi cha UTAWALA WA SIAD BALEH

Barre.
 
Ni kweli sijwawahi kufika chuo cha Dodoma, nakiona kwa mbali. Je mwenzagu umewahi kutembelea KIU hivi karibuni - na mimi nilikuwa nafikili ni kidogo lakini nilipo fika pale nilichoka.

Udom ujenzi unaisha 2015. KIU NI KAMA BAFU TU.
 
Kwa kiasi kikubwa inaonekana watu wanamjua kile kilichowekwa mbele yao. Kitu pekee ambacho naona kimekosekana sana ni kushindwa kuhusisha influx pia ya baadhi ya waganda ambao wameamua kubadilisha majina... ili kufanya biashara fulani fulani.

Unamengi ya kutujuza ila naamini unasubiri catch up ya watu flani flani
 
Nadhani kuna mambo nyuma ya pazia kuhusu huyu jb. Mwanakijiji na baadhi ya wadau tufungueni macho mapema hii nchi imeshindikana.
 
Back
Top Bottom