Je, baba alitutesa au alitufundisha maisha?

Je, baba alitutesa au alitufundisha maisha?

Aliwafundisha kuthamini na kutambua fursa. Mfano kwenye tofali na mchanga sidhani kama atatokea yoyote kati yenu atakayetaka hata kuiona nyumba inaharibika au kuuzwa. Pia aliwaandaa vyema kuyakabili na kiyatekeleza majukumu ya kimaisha. Kwa mfano kwenye kumwagilia miti na bustani; na dunia ya sasa ndivyo ilivyo huwezi pata pale ambapo hujapaandaa/kuwekeza. Na pia dunia haina huruma ndio maana akawa anahakikisha anakula na nyinyi sahani moja kwenye maagizo yake. Aliwandaa vyema na dunia yetu hii. Kongole nyingi kwake. Hata sisi kwetu tulipitia hayo; mwanzoni na kwa fikra za kitoto tuliona manyanyaso lakini baadae tuliona faida kubwa sana haswa tulipoanza kujitegemea au kwenda kuishi ugenini; wanashangaa vijana rika lakini sisi malezi tofauti na utekelezaji wa majukumu upo vizuri tofauti na wenyeji
Mkuu sikupingi Yale malezi yamenisaidia Sana kupambana na maisha na kuwa makini na nidhamu kwa kila jambo
 
Alifanya hivyo ili siku nyingine umakini na uwajibikaji uongezeke; sipati picha angekuwa amepotea au kuliwa na wanyama usiku huo ; nadhani mngepewa zamu ya kuwika kama jogoo alfajiri
Mkuu kweri kabisa
Kuku asingeonekana sijui Ile siku ingekuwaje
 
Kongole kwake, hayo maisha kawaida sana kwa watoto wa kota
 
Hilo la kwako dogo... mimi nikiwa std 1 nilikua nafuga nguruwe wa mzee.

Ole wako aje ucku saa 6 angurume... uatenda tafuta magimbi na majani ucku huo huo

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Huyu sasa ndio aliwafundisha Kwa vitendo bila kukutesa,aliwaonyesha umuhimu wa kuyachukulia mambo serious.

Nakumbuka na Sisi tulifundishwa Kwa vitendo Jambo Fulani,ilikuwa mwaka Mpya,baada ya shamra shamra za kuingia mwaka Mpya,hatukuingia ndani kulala badala yake tulikesha Kwa disco,kufika asubuhi mshua akatumbia hakuna kulala tuchukue majembe na kulima bustani,daah sio poa,hivi umeshawi ona mtu analala huku amesimama na jembe mkononi?

Basi hakika alitufundisha kitu ambacho hatukukisahau
Ukiishi na mtu anaedhaniwa kuwa ni katili kuna vingi sana unajifunza na hutoshindwa kuishi mazingira yoyote
 
Baba yangu alikuwa kanali wa jeshi la wananchi (jwtz)huko kusini mwa Tanzania mkoa unaozalisha mahindi kwa wingi hapa nchini mzee wetu alikuwa mkali Sana

Nakumbuka mwaka 2008 wakati Mimi nko darasa la sita ,kaka yangu mkubwa first born yupo form one na mdogo angu marehemu kwa Sasa (r.i.p) tulipewa kazi ya kubeba tofali 100 Mimi na Kaka, mdogo wetu abebe tofali 50 na sehemu zilipokuwa tofali ni mbali Sana hakuna gari unabeba kichwani unavuka Kama mitaa 3 mikubwa nakumbuka siku Ile tulibeba tofali mpaka unalia njia nzima unapumzika ukikutana mtu mnaye fahamiana anakupiga tafu kidogo,nakumbuka bimkubwa alikuwa ana toa machozi kutuhurumia na sauti kwa mzee hana ilibidi tupambane tu

Tukio lingine home tulikuwa na eneo kubwa mzee alipanda miti ya matunda na migomba kila mtu alipewa miti yake ole wake mti wako unyauke utachezea fimbo na adhabu zakutosha
Ukirud shuleni baada ya kula unachukua ndoo zako unaenda mtoni kuchota maji tulikuwa tunaisha karibu na mto na usiku ata arudi saa 6 anachukua tochi anapita kugagua kila mti Kama umepata maji ya kutosha ole wako usimwagilie utaenda mtoni usiku kuchota maji umwagilie

Nakumbuka nilikuwa mchezaji mzuri Sana wa mpira nishachaguliwa Sana umintashuta na umisenta kwenda kuwakilisha shule kwenye soka Ila tatizo mzee alikuwa hataki kusikia habari za mpira alichotaka yeye ni kusoma tu na saa 12 jioni uwe ndani kipaji kikapotea...

Tukio lingine nyumbani tulikuwa tunafuga kuku Kuna siku moja kuku mmoja jogoo kumbe hakulala ndani na sisi hatukukagua na tulikuwana na jogoo mmoja tu kwa wakati huo usiku kumbe mzee ajalala anasikilizia saa 9 jogoo awike kimya saa 11 alfrajiri Tena kimya jogoo ajawika akatoka kwenda chumba Cha kuku kuangalia kumbe yule jogoo hayupo nakumbuka tuliamsha wote nyumba nzima tukatafute kuku Hadi tumpate ilikuwa kasheshe kila pori tunatafuta hatuna ata tochi tulifanikiwa kumpata asubuhi kesi ikaisha

Ni matukio mengi Sana yalitokea home mzee alikuwa mafia afu acheki ovyo majirani walikuwa wanamuogopa Sana
Nw kastaafu yupo nyumbani tu Japo ukali umepungua wajukuu na ndugu wanaoishi pale wananienjoy tu

Hongereni sana

Mwamba aliwajenga
 
Natumai ushakuwa mtu mzima sasa. We unaonaje, mliteswa ama mlifundishwa maisha?
 
Kuna kaumri washua wakifika huwa na ukali ukali sometimes hata usio na maana ila wakizeeka wajukuu wanawachezea sana
 
Mdingi hawezi kukutesa ulimtafsiri vibaya shukuru Mungu umebahatika kuishi na mshua mpaka anazeeka
Miss you Dad
 
Kama malezi uliyopitia yalikuwa sahihi basi ungejua jibu la hili swali lako bila kuja kuuliza hapa ila inaonekana malezi aliyowalea baba yenu hayajaleta matokeo chanya au aliyoyadhania kwa asilimia 100%. Maana yake kuna sehemu mzee wako alikosea. Mfano unatumia jibu alilotoa member numbisa kujibu members wengine.

Malezi kama haya mara nyingi yanafanya baba na mtoto wasipatane ukubwani kitu ambacho sio kizuri kwa mzazi lakini hasa mtoto. Mimi sitaki hata kufikiria malezi yangu lakini ndio yamenifanya niwe jasiri na katili, real fighter lakini sio hapo tu bali kwenye akili pia. Tatizo mahusiano ya baba na mtoto ndio hayapo, kitu muhimu zaidi kwenye maisha.

Malezi kama haya yana uzuri na ubaya wake, ukipatia mtoto atakuwa jasiri, fighter na anayetumia akili kufanya maamuzi binafsi na ukikosea sehemu mtoto atakuwa muoga, asiyejiamini na asiyetumia akili yake kufanya maamuzi binafsi bali ataendeshwa kwa hisia na mitazamo ya watu.
Bila shaka umepata jibu lako hapo.

NB: Mzee alikuwa mjeshi vilevile.
 
Chief

Kwa upande wangu naona Mzee wenu ingawa alikuwa na Nia ya kuwafundisha lakini hakuwa na namna nzuri ya kufanya hivyo,Bali aliwapelekesha kijeshi jeshi Tu.

Mfano muamshwe usiku WA manane kumtafuta jogoo,je mngepata madhara ya kuumwa na viumbe kama nyoka ingekuwaje Kwa usiku huo?

Ila kuhusu kumwagilia mimea hakika nakubaliana nae,ingawa Napo kuna changamoto moja,je kama mimea ingenyauka Kwa ugonjwa,nyie kosa lenu ni lipo?

Anyways ndio changamoto za kuwa na wazazi wajeda,mambo ya kazini wanayaleta home.
Kunyauka kisa ugonjwa au cio
 
Back
Top Bottom