Hivi ndivyo nilivyo mimi. Nimekupa stahiki yako na hii ni saizi yako, nachelea kukudhulumu. Fanya kama nilivyo kuagiza ili nichuje sasa.We nae unachuja sasa! Tushakuzoea na hako ka kauli kako ka kutaka wanaokataa kuthibitisha.
Huu ni uhalisia mzee, sababu kama kusema mtu akitaka kusema atasema anachokitaka na muda anao utaka, lakini ithibati ndiyo inachuja. Hutakiwi utumie akili kubwa kuona ya kuwa wewe unae kanusha ndiyo unapaswa kuthibitisha, maana lazima ujibu swali ambalo haliepukiki la kwanini umesema hivyo au umejuaje hilo ? Lakini sisi tulianza kuwajua wakubwa zenu kwa kujificha kwao kwenye kivuli na kukimbia jukumu lao la kuthibitisha na kwa ujinga wao wakaona ya kuwa wanao kiri ndio wanapaswa kuthibitisha, uoga ulioje huu. Huku wakisahau ya kuwa wao wanayo yaandika ni madai tu ambayo ili yasimame lazima yawe na ithibati. Swali hili hamlikimbii.Sijui ni shule gani hiyo uliyosoma inayomtaka mtu anayesema kitu hakipo athibitishe.
Hili litarudi kwangu endapo ungenihoji na si kukanusha kile nilichokiandika. Vijana shida yenu huwa mnaingia kwenye mijadala wakati hamjui mijadala ni nini na adabu za kujadiliana ni zipi.Wewe unayesema yalikuwepo kweli na yalitokea ndo unatakiwa kuthibitisha.
Ningewajibika kukuthibitishia wewe, endapo ungeni hoji ya kuwa bwana Zurri kwanini unasema Qur'aan ni maneno ya Mungu, lakini siyo wewe unae kanusha na kukimbia jukumu la kuthibitisha, huwa nacheka sana.
Nacheka sana, hakuna kulea ujinga katika dini ndiyo maana viatu vyetu nyinyi vina wapwaya.Alafu kama hauna cha kuthibitisha naomba uwe unakaa kimya uache kabisa kuzoea kuni quote. Mfia dini usiyejielewa![]()
![]()
![]()
Mwenye akili haandiki handiki tu utumbo ambao hawezi kuuthibitisha, hapa unaonyesha wazi kwa namna gani unafikiria kitoto.
Mimi nimeshatangaza vita na mabazazi kama wewe na wa mfano wake, popote nitakapo waona nawajeruhi tu, kwahiyo huna haki ya kunikataza kukuquote pale napo ona unaandika ujinga.
Naona swali limekushinda, ukija tena hakikisha umepima size ya mguu wako, viatu vyetu wafia dini ni vikubwa nyinyi vinawapwaya.