Je, harusi ya Adam na Hawa ilifanyikia wapi, nani aliwafungisha ndoa?

Je, harusi ya Adam na Hawa ilifanyikia wapi, nani aliwafungisha ndoa?

Ila mkuu kitabu hakijasema walifunga ndoa hakijatuambia Hawa alivaa shela na Adamu suti tuliambiwa akawabariki akawaambia zaeni mkaongezeke muijaze Dunia
Kauli hiyo ya kubarikiwa tukazaliane, iliwahusu Adam na Hawa pekee au ilihusu vizazi vyote vya binadamu hadi leo hii?
 
Iliwahusu binadamu wote, nashangaa tunabaniana na kuwekeana mipaka
Kwahiyo duniani hakuna dhambi ya kuzini sivyo? Maana binadamu wote tumeshafungishwa ndoa kwa kauli hiyo, tena tumefungishwa ndoa hadi na dada zetu, sivyo?
 
Waafrika bado tumelala usingizi fofofo! Hadi leo hatujajua kuwa hizi hadithi ,a kwenye vitabu vya dini ni simulizi za kutunga tu kwa ajili ya kufundishia?? Hizi ni ngano na visasili sawa na vile vya Nani atamfunga paka kengele, Jogoo aliyesema, Kisa cha mbuzi kiwa na mkia mfupi, n.k. Sema waliotuletea sisi walitwambia ni vya kweli tukazama mazima.

Kama papa mwenyewe anasema kisa cha Adam na Eva pale Eden kilikosewa kinapaswa kufanyiwa marekehisho, wewe ni nani unataka kushupaa??
Tell dem
 
Usijali mijadala kama hii kuelewana ni ngumu sana ndio maana na mimi naendelea kujadiliana na wewe kwa sababu naamini point yangu hujaifahamu pia.

Sawa na mimi baadae nitaenda unavyotaka wewe ili tunogeshe mazungumzo yetu.

Sasa hivi nitajibu kwa kifupi ili iwe rahisi kwako kusoma na kuelewa point ya moja kwa moja.



Ndio Mungu kamuumba binadamu katika asili ya kutokuwa mkamilifu.

Na hapa maana ya ukamilifu ninayoikusudia ni ; kutokukosea kabisa ama kutokutenda dhambi yeyote iwe hafifu ama kubwa.
Hii ndio maana ya ukamilifu.

Sasa Mungu hajawahi kusema kuwa kamuumba binadamu aliyekamilika kwamba hakosei wala hatendi dhambi,yeye mwenyewe anasema kuwa binadamu wote tunakosea na tunatenda dhambi.

Ndio maana

Kuna toba : ili aliyetenda dhambi ajirudi kwa amungu.

Kuna pepo : aliyeacha madhambi aingie huko

Kuna motoni : mfanyaji wa madhambi aende huko.

Laiti kama Mungu angekuwa kwa hakika ameumba mtu mkamilifu asiyekosea basi bila shaka asingesamehe kwa sababu wewe kwa nini ukosee na ni mkamilifu ?

Na kama ingekuwa kamuumba mtu mkamilifu hakosei basi kusingekuwa na haja ya kuwepo kwa moto na pepo kwa sababu watu wote wamekamilika hawakosei,jee motoni angeingia nani wakati watu wote ni wasafi....



Kwa maana hiyo Mungu tokea asili na asili alimuumba binadamu ambaye sio mkamilifu,sio msafi kabisa.



Mungu alikusudia kumuumba mtu ambaye hajakamilika yaani hakosei kwa sababu huko kukusudia kumuumba mtu ambae hajakamilika ndio maana akampa nafsi ambayo inaweza kufanya baya na kuacha,inaweza kufanya mema na kuacha.

Kwa hiyo tafsiri ya Mungu kumuumba mtu ambaye hajakamilika ni kule Mungu kumpa mtu nafsi ambayo inaweza kufanya mema kwa kuamua,na kufanya mabaya kwa kuamua kwa maana nafsi imeumbwa na uhuru wa kufanya ilitakalo.

Na tunaposrma uhuru,kufanya jambo bila kulazimishwa tunapima ama tunajua kwa kuangalia tu matendo yetu ya kila siku.

Ukitaka kufanya jambo huoni kama kuna nguvu yeyote inayokukataza.

Yaani mfano ukitaka kula huoni kama kuna nguvu inazuia mkono wako usile,kutokuwepo kwa nguvu hiyo maana yake ndio uhuru wa kufanya unalotaka.



Kukamika kwa maana ya kutokumpa nafsi yenye maamuzi ya kuchagua mema na mabaya uwezo huu alikuwa nao,

Lakini kumbuka kuwa ili iwe mtihani lazima kuwe na jaribio na ili iwe jaribio kwetu basi tuwe na uhuru wa nafsi,tuwe na nafsi ambayo haijakamilika.

Mungu anaweza kupenda jambo na asilifanye.
Na anaweza kufanya jambo ambalo halipendi.

Kupenda kwa Mungu hajakufungamanisha na kufanya,kwamba akipenda jambo lazima afanye.

Na kufanya kwa Mungu hajafungamanisha na kupenda kwamba akifanya jambo basi lazima iwe amelipenda.

Kwa hiyo unaposema kapenda kufanya hivyo sio sahihi sema kataka kufanya hivyo.

Kama ambavyo mtu huamka mapema na kwenda kupigwa na jua shambani sio kwamba anapenda jua limpige bali kataka kufanya hivyo ili atimize malengo yake.

Kwa hiyo sio sahihi kufungamanisha baina ya kufanya na kupenda.
Sio kila lifanywalo na wahusika basi linapendwa hapanaa.

Kama tulivyoelezana kuwa usiseme mapenzi,sema ametaka.

Kwa hiyo Mungu ametaka kumuumba binadamu ambaye hajakamilika kwa maana ya kuwa nafsi yake ina uhuru wakuacha zuri na kufanya baya,kufanya hiki na kuacha kile.

Huku kuwa na uwezo wa kufanya hili na kuacha lile basi ndio uhuru wenyewe huu.

Na huu uhuru wa nafsi maana yake ndio watu wanautumia kufanya mabaya,na mazuri pia.

Na ndio maanaukamilifu wa kufanya mema tu,kutokukosea akawapa malaika kwa sababu wao sasa hawapo katika miitihani ya dunia,hawapo katika kujaribiwa kabisa.
Kwahiyo Mungu kaumba binadamu mtenda makosa kwa makusudi, sivyo? Haikuwa bahati mbaya?
 
Na watoto wa huo uzinzi walifunga ndoa wapi na lini, na walifunga ndoa na nani wakati hapakuwa na watu duniani? Incest? Na aliwapa ruhusa ya kufanya incest?
Unachoita Incest ni asili ya mwanadamu au Sheria za Kiingereza?
 
Kwahiyo duniani hakuna dhambi ya kuzini sivyo? Maana binadamu wote tumeshafungishwa ndoa kwa kauli hiyo, tena tumefungishwa ndoa hadi na dada zetu, sivyo?
Amri ya 6 ya Mungu inasema usizini.
 
Sura uliyo iweka kweli inaelezea kisa cha nabii Adamu, ila haionyeshi hilo agizo kwa Malaika kwenda kuwaua majini wote kisha wakakaidi wakambakiza mmoja. Nachotaka mimi ni hilo agizo na utuonyeshe wapi walipo kaidi.

Kisa kimesimuliwa kuanzia aya ya 30 mpaka 38 katika surat al Baqarah.

Soma hapa :

30. Na pale Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Mimi nitamweka katika ardhi Khalifa (mfwatizi), wakasema: Utaweka humo atakaye fanya uharibifu humo na kumwaga damu, hali sisi tunakutakasa kwa sifa zako na tunakutaja kwa utakatifu wako? Akasema: Hakika Mimi nayajua msiyo yajua.

31. Na akamfundisha Adam majina ya vitu vyote, kisha akaviweka mbele ya Malaika, na akasema: Niambieni majina ya hivi ikiwa mnasema kweli.

32. Wakasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hatuna ujuzi isipokuwa kwa uliyo tufunza Wewe. Hakika Wewe ndiye Mjuzi Mwenye hikima.

33. Akasema: Ewe Adam! Waambie majina yake. Basi alipo waambia majina yake alisema: Sikukwambieni kwamba Mimi ninajua siri za mbinguni na za duniani, na ninayajua mnayo yadhihirisha na mliyo kuwa mnayaficha?

34. Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam, wakamsujudia wote isipo kuwa Iblis, alikataa na akajivuna na akawa katika makafiri.

35. Na tulisema: Ewe Adam! Kaa wewe na mkeo katika Bustani, na kuleni humo maridhawa popote mpendapo, lakini msiukaribie mti huu tu; mkawa katika wale walio dhulumu.

36. Lakini Shet'ani aliwatelezesha hao wawili na akawatoa katika waliyo kuwamo, na tukasema: Shukeni, nanyi ni maadui nyinyi kwa nyinyi. Katika ardhi yatakuwa makaazi yenu na starehe kwa muda.

37. Kisha Adam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na Mola wake Mlezi alimkubalia toba yake; hakika Yeye ndiye Mwingi wa kukubali toba na Mwenye kurehemu.

38. Tukasema: Shukeni nyote; na kama ukikufikieni uwongofu utokao kwangu, basi watakao fuata uwongofu wangu huo haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika. (al Baqarah : 30 - 38)
Brother, Allah akulipe kheri kwa jinsi unavyojitahidi kuwaelewesha hawa makafiri wa humu. Yaani mimi kwa jinsi walivyo wajinga hawa sijui hata ningeanzaje kuwaelekeza. Maana hawajui chochote kuhusu Uislam lakini wanakaza shingo wanajifanya wajuaji.
 
Sheria nyingi zilizo katika kitabu Cha biblia zmeendelea kutumiwa na wakristo Hadi leo
Kwahiyo binadamu wote tumeshafungishwa ndoa na jinsia wote wa tofauti wanaokatisha mbele, hivyo dhambi ya zinaa duniani haipo, maana ile kauli ilitufungisha ndoa hadi sisi binadamu sasa
 
Unaulizia Harusi au Ndoa, maana ndoa alifunga Mungu Mwenyewe. I harusi ingefanyikaje bila kuwa na watu wengine maana Sherehe ni watu
Ndoa hiyo umeisoma au kuiona au kuisikia katika kitabu kipi?
 
Brother, Allah akulipe kheri kwa jinsi unavyojitahidi kuwaelewesha hawa makafiri wa humu. Yaani mimi kwa jinsi walivyo wajinga hawa sijui hata ningeanzaje kuwaelekeza. Maana hawajui chochote kuhusu Uislam lakini wanakaza shingo wanajifanya wajuaji.
Kafiri babaaako mbwa wewe
 
Waafrika bado tumelala usingizi fofofo! Hadi leo hatujajua kuwa hizi hadithi ,a kwenye vitabu vya dini ni simulizi za kutunga tu kwa ajili ya kufundishia?? Hizi ni ngano na visasili sawa na vile vya Nani atamfunga paka kengele, Jogoo aliyesema, Kisa cha mbuzi kiwa na mkia mfupi, n.k. Sema waliotuletea sisi walitwambia ni vya kweli tukazama mazima.

Kama papa mwenyewe anasema kisa cha Adam na Eva pale Eden kilikosewa kinapaswa kufanyiwa marekehisho, wewe ni nani unataka kushupaa??
Mimi ukinithibitishia ya kuwa hizi ni hadithi za kutunga, naacha kutumia hii ID rasmi, na wewe utakuwa shahidi.

Acheni kuandika mambo kwa lengo la kufurahisha nafsi zenu, hali ya kuwa mnajua kabisa hamna ithibati juu ya haya mnayo yaandika.
 
Kafiri babaaako mbwa wewe
Kafiri siyo tusi mzee. Ukipewa haki yako ichukue kwani ulichokiandika hakibadilishi ukweli wa kuwa wewe ni KAFIRI.

Kafiri kilugha ni mficha ukweli na kudhihirisha uovu na uongo.

Jifunze kuwa mvumilivu na uwe na moyo wa kiume.
 
Mimi ukinithibitishia ya kuwa hizi ni hadithi za kutunga, naacha kutumia hii ID rasmi, na wewe utakuwa shahidi.

Acheni kuandika mambo kwa lengo la kufurahisha nafsi zenu, hali ya kuwa mnajua kabisa hamna ithibati juu ya haya mnayo yaandika.
Wewe ndio unatakiwa udhibitishe kwamba hizo sio hadithi za kutunga, na sio the other way round we jamaa vipi? Mfano mi nakuja halafu nakuambia hapo mbele yako kuna Simba ila humuoni na hakuna namna ya kumuona kamwe, halafu ukinimbia huo ni uongo, mimi nakwambia dhibitisha kwamba ni uongo badala ya mimi nidhibitishe kwamba huyo Simba yupo kweli
 
Mimi ukinithibitishia ya kuwa hizi ni hadithi za kutunga, naacha kutumia hii ID rasmi, na wewe utakuwa shahidi.

Acheni kuandika mambo kwa lengo la kufurahisha nafsi zenu, hali ya kuwa mnajua kabisa hamna ithibati juu ya haya mnayo yaandika.
Ingekuwa ni vyema kama ungeweza kuthibitisha hadithi ni za kweli na sio za kutunga. Chochote kinawezekana..
 
Back
Top Bottom