Je, inawezekana kila kitu ni mpango wa Mungu?

Je, inawezekana kila kitu ni mpango wa Mungu?

haha hahha aiseee ...kuna watu wanavichwa vigumu sana ""... mkuu huwa unatirilika vyema mnooo"".. ajabu ni kwamba "" maswali ambayo huwa unaulizwa Humu ""ulishawahi kuyapatia majibu yake mara 8000" lakini hawakomi bado wanarudia kuuliza tu "" ilhali majibu Yke " walishapatiwaga""...
Kuna wakati huwa nafikiri ama wanajifanya hawaelewi makusudi kwa kile wanasaikolojia wanachokiita "cognitive dissonance", ama watu tuko na tofauti za msingi katika ubongo kiasikwamba unaweza kuwaonesha watu wawili rangi ile ile (metaphorically speaking0 mmoja akasema nyekundu na mwingine akasema bluu, kwa sababu zile zile.

We angalia.

Unamuuliza mtu kwanini anasemaMungu yupo?

Anakujibu kifo. Kifoni sababu tosha kusema Mungu yupo.Watu wameshindwa kuzuia kifo, kwahiyo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Wakati, ukiangalia, kifo ni sababu ya kusema Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo. Angekuwepo,kwa nini aruhusu kifo kiwatenganishe viumbe wake wanaopendana sana? Baba na mtoto, mama na mtoto, baba na mama, marafiki etc.. Huyu Mungu ana ukatili gani mpaka aruhusu kifo?

Mwingine anakwambia complexity ya duniainaonesha lazima kuna muumba, complexity haiwezi kutokea bila muumba.

Wakati, ukishasema complexity haiwezi kutokea bila muumba, maana yake muumba naye ni complex na yeye hawezi kuwepo bila muumba. Ukisema complexity haiwezikutokea bila muumba ushakubali Mungu hayupo, kwa sababu Mungu naye kamakaumba vitu complex, na yeye ni complex na hivyo atahitaji muumba, na muumba wake atahitaji muumba, ad infinitum, ad absurdium.

Sasa hapo utaona watu tulivyo tofauti na sababu zile zile zinavyomfanya mmoja aseme Mungu hayupo, na mwingine aseme Mungu yupo.
 
Sijadili imani, najadili fact.

Ukisema unaamini Mungu yupo, sina mjadala nawe.

Nimesema mara nyingi sana hapa kwamba.

1. Natetea haki za watu tofauti kuamini imani tofauti, hata zile ambazo sikubaliani nazo.
2. Misingi ya haki ya kuamini unachotaka ipo kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.Naikubalina kuithamini.
3. Misingi hiyo ilikuwapohata kablaTanzania haijakuwapokamanchi, iliwekwakatika Azimio linaloheshimika kabisa duniani "Universal Declaration of Human Rights" la December 10 1948. Azimiohili nalipenda sana na kulithamini sana.

Hivyo, sina nia ya kumuingilia mtu katikaimani yake.

As long as anakubali hiyoniimani.

Abudu chura, mti, kichaka cha kwenu, kivyako. Mradi usije anga zangu kusema unachoamini ndiyo ukweli wenyewe (fact).

Ukishanihubiria ama hapa JF ama popote, au kusema unachoamini ni kweli (fact) ushatoka kwenye uwanja wa imani, umekuja kwenye uwanja wa uthibitisho.

Umeshajianika kuulizwa maswali na kutakiwa kutoa uthibitisho.

Hapa sijadili imani, najadili fact.
Hahaha...kama kawaida unarudi kule kule tulipotoka na kuanza upya.


Kwanini nikisema nachokiamini ni kweli nakuwa natoka kwenye imani? je,nilitakiwa kusema nachokiamini si kweli?
 
hahaha sasa huoni kama ni contradiction "" huo ni uwezo au mapungufu "" umejenga nyumba halafu "" ina nyufa kibao "" utajinasibu kuwa ni uwezo "" maana inapobomoka huwa inahatarisha maisha ya watu "".... kama ni muweza wa yote na upndo kwa wote "" kwanini asingeumba dunia ambayo haina maafa "" ili kuonyesha uwezo wake na huo upendo wake upate kuwa wenye mantiki "" haiwezekani " "baba uwe na uwezo wa kiuchumi kisha uwalaze wanaonjaa"" halafu kesho pakikukucha uanze kuwaambia kuwa unaupendo kwa wote "" bila shaka watakuona mwehu "" au katili type ya nduli idd amini "" kama sio savimbi
Mkuu unazunguka tu mbuyu bila kuelewa! utaamka lini!!?? Hivi kama kusinge kuwa chuki upendo ungeujulia wapi, pasinge kwepo giza mwanga usinge kuwa na thamani, kungekuwa hakuna njaa shibe unge ijulia wapi?? Ukweli mchungu mambo mengi ambayo unayaona ni mabaya nilazima yawepo ili utambue tofauti ya baya na zuri.
 
Hahaha...kama kawaida unarudi kule kule tulipotoka na kuanza upya.


Kwanini nikisema nachokiamini ni kweli nakuwa natoka kwenye imani? je,nilitakiwa kusema nachokiamini si kweli?
Imani maana yake si hakika, ndiyo maana ikawa imani.

Ukishasema kitu ni kweli, umetoka kwenye kauli ya imani, umeingia kwenye kauli ya ujuzi.

Kamakauli yako ya ujuzi kwamba imani yako nikweli ina contradiction au inaonekana wazi si kweli au haieleweki, umealikawatu kukuhoji nakutakauthibitisho kwa fact.

Ukisema unachoamini si kweli, wakati mimi sikubali kwamba ni kweli, hujapingana nami na sina sababu ya kukupinga.
 
Mkuu unazunguka tu mbuyu bila kuelewa! utaamka lini!!?? Hivi kama kusinge kuwa chuki upendo ungeujulia wapi, pasinge kwepo giza mwanga usinge kuwa na thamani, kungekuwa hakuna njaa shibe unge ijulia wapi?? Ukweli mchungu mambo mengi ambayo unayaona ni mabaya nilazima yawepo ili utambue tofauti ya baya na zuri.
Mungu wako muweza yote alishindwa kuumba ulimwengu ambao chuki haijulikani, bali una upendo tu?

CC hearly
 
Nataka uthibitisho ulio logically consistent.

Hata kama nikishindwa kushika upepo kwa mkono, hilo halithibitishi Mungu yupo. Linathibitisha siwezi kushika upepo kwa mkono.

Unawezakuthibitisha Mungu yupo?
Hewa unayo vuta imetoka wapi? Mwili wako umejaa maajabu tosha kabisa! unataka uthibitisho gani ?
 
Hewa unayo vuta imetoka wapi? Mwili wako umejaa maajabu tosha kabisa! unataka uthibitisho gani ?
Hata nikisema sijui hewa inatokawapi, hilo litathoibitisha sijui hewa inatoka wapi, halithibitishi Mungu yupo.

Mwili wangu unaumwa na kufa, huu ni uthibitishokwamba Mungu muweza yote, mwenye ujuzi wote na upendo wote hayupo, angekuwepo, asingeumba mwiliunaoweza kuugua na unaokufa.
 
Imani maana yake si hakika, ndiyo maana ikawa imani.

Ukishasema kitu ni kweli, umetoka kwenye kauli ya imani, umeingia kwenye kauli ya ujuzi.

Kamakauli yako ya ujuzi kwamba imani yako nikweli ina contradiction au inaonekana wazi si kweli au haieleweki, umealikawatu kukuhoji nakutakauthibitisho kwa fact.

Ukisema unachoamini si kweli, wakati mimi sikubali kwamba ni kweli, hujapingana nami na sina sababu ya kukupinga.
Neno "si hakika" lina maana ya uongo kwamba si kweli? au lina maana ipi?
 
Hata nikisema sijui hewa inatokawapi, hilo litathoibitisha sijui hewa inatoka wapi, halithibitishi Mungu yupo.

Mwili wangu unaumwa na kufa, huu ni uthibitishokwamba Mungu muweza yote, mwenye ujuzi wote na upendo wote hayupo, angekuwepo, asingeumba mwiliunaoweza kuugua na unaokufa.
Hahaah dah! Hujui hewa inapotoka na unataka uthibitisho kama Mungu yupo!!? Kweli bado unahitaji chakula laini laini, vigumu bado huwezi kumeza. Umejuaje kama utakufa na kwa nini ufe na ukifa unaenda wapi?
 
Mungu wako muweza yote alishindwa kuumba ulimwengu ambao chuki haijulikani, bali una upendo tu?

CC hearly
hahaha anshindwa kujiuliza mswali madogo kama hayo "" ama hakika sijui ana matatizo gani ""!?
 
Asili ya vyote uvionavyo ni wapi?
Nikikwambia sijui,hilohalithibitishi Mungu yupo,linathibitisha sijui asili ya vote nivionavyo.

Na ukishikilia sana kwamba kila kilichopo kina asiliyake,utajifunga mwenyewe kwa sheria yakohiyo, kwa maana kwamba sheria yakohiyo itatuambia huyo unayemuita Mungu naye ana asili yake tofauti na yeye mwenyewe, na kwa sababu hiyo, siMungu.

Kwa kifupi, maswali ya "kitu fulani asili yake nini?" yakiwa na kusudi la kuonesha Mungu yupo, bila kuelewa, yanaonesha Mungu hayupo.
 
unaweza kumzuia "" mwanao asikue "".. kama nikweli tumepewa free will "".inakuwaje " ushindwe " kufanya jambo kama hilo "". ??
Kuna matendo ya mazingirà ambayo huwezi kuzuia hill Ni mojawapo
 
Hahaah dah! Hujui hewa inapotoka na unataka uthibitisho kama Mungu yupo!!? Kweli bado unahitaji chakula laini laini, vigumu bado huwezi kumeza. Umejuaje kama utakufa na kwa nini ufe na ukifa unaenda wapi?
Maswaliyako yote uliyoniuliza na ambayo badohujaniuliza,nikisemakwa mpigo sijuimajibu yake, kutokujuakwangu majibu hayohakuthibitishi Mungu yupo.

Kutathibitisha sijui majibu ya maswali hayo.

Sijawahi kusemanajua majibu ya maswali yako.

Kwa hiyo, nikiwa sijuimajibu ya swali lakololote, hilo halitapingana na nilichosema hapo nyuma.

Ila wewe unayesema Mungu yupo, unahitaji kufanya jambo moja tu, ambalo hujalifanya.

Thibitisha kwamba Mungu yupo.

Ukiniuliza swali lolote, nikasema sijui jibu lake, hilohalithibitishi Mungu yupo, zaidi, litathibitisha Mungu hayupo.

Kwa sababu, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezowote na upendo wote angekuwepo, kungekuwa hamna swali analoweza kulifikiria kiumbe wake ambalo hana jibu lake.

Mimi naweza kukwambia kwamba kushindwa kujibu swali lako lolote ni ushahidi kwamba Mungu hayupo,angekuwepo angenipa majibu.

Wewe unaweza kuthibitisha Mungu yupo?
 
Back
Top Bottom