Je, ipo siku Taifa la Tanganyika litafufuka? Je, itakuwaje? Je, Zanzibar itakuwepo ama?

Je, ipo siku Taifa la Tanganyika litafufuka? Je, itakuwaje? Je, Zanzibar itakuwepo ama?

Maamuzi yanayofanywa na wanasiasa ni nadra sana kuyahoji hasa ukiwa mwananchi usiyekuwa na nafasi yoyote kwenye siasa. Hivyo hivyo haikuwa rahisi wakati huo kuhoji maamuzi ya Nyerere na Karume kufikia uamuzi wa kuunganisha nchi mbili zilizokuwa zimepata uhuru wake muda mfupi. Tanganyika ilikuwa mali ya watanganyika wakati Zanzibar na Pemba zilikuwa mali ya Sultan wa Oman, Muungano ulioundwa baada ya uhuru ulikuwa na hila ndani yake ikiwa ni kumuondoa mwarabu katika umiliki wa visiwa na kuunda muungano wenye kuzingatia uafrika zaidi, kwa kumpora mwarabu haki yake kwenye visiwa vile. Umeuliza, kwa nini watanganyika hawaidai nchi yao? .... Jibu ni kwamba muda ulikuwa haujafika na kwa kuwa ni mchakato wa kisiasa, huenda hivi tunavyozungumza utashika kasi kwa kutegemea siasa na wanasiasa wa sasa wanavyonyumbulika.

Tanganyika ikirudi utaliunganishaje kama taifa? Nyerere aliyeweza kuyaunganisha makabila ya Tanganyika ameshakufa. Tena enzi zile makabila yalikuwa madogo, leo makabila yana mamilioni ya watu. Tanganyika lazima isambaratike. Zanzibar pekee ndiyo taifa la kihistoria litabaki.
 
Tanganyika ikirudi utaliunganishaje kama taifa? Nyerere aliyeweza kuyaunganisha makabila ya Tanganyika ameshakufa. Tena enzi zile makabila yalikuwa madogo, leo makabila yana mamilioni ya watu. Tanganyika lazima isambaratike. Zanzibar pekee ndiyo taifa la kihistoria litabaki.
Tanganyika ni jina tu linalowakilisha eneo linalopakana na nchi nane bara na ukanda wa bahari mashariki. Hiyo ndio Tanganyika. Kisiwa cha Mafia hakitajwi kwenye tafsiri hiyo na Unguja na Pemba hivyo hivyo!. Wakazi wa Tanganyika ni mchanganyiko wa makabila 120 ambayo yana ardhi na maeneo yao ya asili ambayo yalichangia kuunda nchi iliyoitwa Tanganyika. Alichokifanya Nyerere ni kujenga utaifa kwa kuyaunganisha makabila haya na kupata nchi ya Tanganyika, lakini alizidisha chumvi zaidi kwa kutamani kuiunganisha Afrika nzima huku akianza na Zanzibar. Sababu ya kuichagua Zanzibar nimeishaitaja na ni wazi kuwa ina hila, vinginevyo kama nia yake ingekuwa safi, bila kuficha madhambi ya Zanzibar, angeanza kuiunganisha Burundi na Rwanda kwanza, zilizounda pamoja na Tanganyika, Germany East Afrika. Jibu la swali lako ni kuwa, ikirudi Tanganyika sasa hata bila kuwepo Nyerere, hakutakuwa na mgogoro kwani hakuna makabila yanayotaka kutambulika kama nchi, zaidi ya kutambika na tambo za kimila.
 
Tanganyika ikirudi utaliunganishaje kama taifa? Nyerere aliyeweza kuyaunganisha makabila ya Tanganyika ameshakufa. Tena enzi zile makabila yalikuwa madogo, leo makabila yana mamilioni ya watu. Tanganyika lazima isambaratike. Zanzibar pekee ndiyo taifa la kihistoria litabaki.
Kwa hiyo zanzibar ndo inalinda makabila ya bara yasitengane? 😁😁
 
Dola la Tanzania lilishaundwa Aprili 26. 1964, na waasisi wetu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Mzee Karume. Kuthubutu kuvunja Muungano ni uhaini. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania si suala la sera ya chama chochote. Jadilini mengine.
Suala la kuundwa enzi hzo si maagano ya kutokuvunja. Ile ni km ndoa, inapokuwa na dosari hakuna budi kuiangalia upya. Hatumaanishi kuivunja bali kuirekebisha ili wanandoa hao waendelee kuishi kulingana na matakwa yao. Nyerere na karume enzi hizo ukifuatilia huenda hadi wake zao walitafutiwa na wazee wao na haikuwa noma lakini kwa sasa mtu unakuwa huru kusaka mwenyewe. Ndo tunataka marekebisho kama hayo, mfumo ule ulifit enzi hizo na sasa tunahitaji mfumo mpya wenye kuitambua tanzania tu ama kutambua tanganyika km ilivyo kwa zanzibar.
 
Hiyo ni hela ya mboga kwa Oman. Usichukulie Zanzibar poa namna hiyo, nyuma yake kuna mataifa makubwa tajiri ya kiarabu. Zanzibar ikiachiwa huru tuu, soon inakuwa extended arm ya Oman na kujenga jeshi imara ni sekunde tu.
Sasa uhuru gani ambao mnautaka kama bado mtatakimbilia kulamba mataakle ya waarabu ili muendelee ku survive.


#MaendeleoHayanaChama
 
Nchi huru kuungana na kufanya mambo yao kwa umoja kama vile EAC, ECOWAS, SADC, EU, nk ni jambo jema na hakuna anayepinga..
Tatizo ni nchi moja kugeuka koloni la nchi nyingine🙄
Nahisi kwamba hizi kelele za kuidai Tanganyika zinatoka kwa wabaguzi wachache wa huku bara wanaodhani kuwa Samia kuwa rais ni makosa yalifanyika, pengine hawakuwepo duniani wakati Mwinyi alipokuwa rais wa JMT.

Ni roho zile zile za chuki, kuona mzenji halafu mwanamama anakuwa rais wetu inawauma sana, kuna ubaguzi umejificha nyuma ya hizi hisia za kuidai Tanganyika.

Na ubaguzi siku zote haumuachi mtu salama unapouanza unaendelea kukutafuna mpaka mwisho wako ufike.
 
Nahisi kwamba hizi kelele za kuidai Tanganyika zinatoka kwa wabaguzi wachache wa huku bara wanaodhani kuwa Samia kuwa rais ni makosa yalifanyika, pengine hawakuwepo duniani wakati Mwinyi alipokuwa rais wa JMT.

Ni roho zile zile za chuki, kuona mzenji halafu mwanamama anakuwa rais wetu inawauma sana, kuna ubaguzi umejificha nyuma ya hizi hisia za kuidai Tanganyika.

Na ubaguzi siku zote haumuachi mtu salama unapouanza unaendelea kukutafuna mpaka mwisho wako ufike.
Fuatilia katiba pendekezwa ya warioba, tanganyika ilidaiwa hata kabla hajawa makamu wa rais. Acha fikra finyu watu wanapodai uhalsia wa muungano.
 
Fuatilia katiba pendekezwa ya warioba, tanganyika ilidaiwa hata kabla hajawa makamu wa rais. Acha fikra finyu watu wanapodai uhalsia wa muungano.
Vyovyote utakavyoamua kuziita hizi hisia, bado siamini kama ni halisia. Zina ubaguzi ndani yake.
 
Taifa la watu wa Tanganyika. Taifa alilopewa baba wa Taifa hili hayati Mwl Julius Nyerere. Ilakutokana na vita baridi moja ya mashirika ya kijasusi yakaipa taarifa tanganyika kile siku za mbele kitatokea na kwa nn kile kisiwa lazima kiwe kama Taifa moja. Well nisiandike zaidi yahiki nimepata kukisikia.

Ila mission hii bado ni mbichi japo maana kuwepo kwa Znz nikufufuka kwa Tanganyika nakufa kwa znz nikuwepo kwa Taifa moja Tanzania.

End
Unapopuuza jina la ukoo la baba mzazi ukang,ang,ania jina la ukoo la baba wa kufikia Basi ujue wewe Ni sawa na popo anayejisaidia kichwa chini miguu juu.....
 
Nahisi kwamba hizi kelele za kuidai Tanganyika zinatoka kwa wabaguzi wachache wa huku bara wanaodhani kuwa Samia kuwa rais ni makosa yalifanyika, pengine hawakuwepo duniani wakati Mwinyi alipokuwa rais wa JMT.

Ni roho zile zile za chuki, kuona mzenji halafu mwanamama anakuwa rais wetu inawauma sana, kuna ubaguzi umejificha nyuma ya hizi hisia za kuidai Tanganyika.

Na ubaguzi siku zote haumuachi mtu salama unapouanza unaendelea kukutafuna mpaka mwisho wako ufike.
Dogo,
Kwani madai ya Tanganyika huru yameanza leo?
Hujui Watanganyika waliidai nchi yao hata kipindi Nyerere alipokuwa bado yupo?
Uliwahi kusikia juu ya G55 ya hayati Makweta (Rip), na kama ulisikia, SSH alikuwepo kipindi hicho?!!!
 
Dogo,
Kwani madai ya Tanganyika huru yameanza leo?
Hujui Watanganyika waliidai nchi yao hata kipindi Nyerere alipokuwa bado yupo?
Uliwahi kusikia juu ya G55 ya hayati Makweta (Rip), na kama ulisikia, SSH alikuwepo kipindi hicho?!!!
Dogo Nyerere alizijibu hoja zao na akaua umoja wao miaka ile Ulimwengu akiwa bungeni, pale Karimjee.

Wakati wa JPM hoja hizi kutojadiliwa na zikaanza kuongelewa awamu hii ya SSH something is wrong.

Dogo tunasoma katikati ya mistari siku zote.
 
Unad
Zanzibar haina uwezo wa kuendesha wizara zilizoko kwenye muungano.

Mf ili Zbar iwe na jeshi lake, itahitaji ndege angalau 5 za kivita. Hii ni zaidi ya bil 500. Itahitaji meli angalau mbili za kivita, hii ni zaidi ya bil 200.

Itahitaji rada za kijeshi, hii ni zaidi ya bil 50.

Hadi hapo tu, Zbar itahitaji zaidi ya trilioni 1, kujenga jeshi lake. Kwa uchumi wa Zbar, watahitaji miaka 100 kujenga jeshi lake lenye uwezo angalau wa kukabiliana na wanamgambo kama Alshababu.

Kimsingi, nje ya muungano Zbar is a failed state.

Hawa wazee wanaokaribia kurudi kwa Maulana wasithubutu kuharibu future ya watoto wao na wajukuu wao kwa kuvunja muungano
Hivi unadhani umekaa na watoto wako ukumbini,unahadithia tu unavyotaka, Muungano ukivnjika tutamudu kil kitu
 
Unad

Hivi unadhani umekaa na watoto wako ukumbini,unahadithia tu unavyotaka, Muungano ukivnjika tutamudu kil kitu
Mkuu, nataka ujue jambo moja, 'nawapenda wazanzibar kuliko watu wote'!
Wakati nasoma chuo, IFM, nilipata mchumba wa kizanzibari, akanipenda 😍😍😍😍 ila alinipa sharti moja tu. Nibadili dini ili nimuoe 🤔🙄😏😥😫😪 Hiki kikawa ni kipengere🤗!
So, am trying to protect my would be inlaws in the 'best way I can'...

Kwa hyo ukiwa nchi ndogo utashindwa kuyamudu maisha yako? Sir lanka we unaizid kiuchumi?
 
Back
Top Bottom