Je, ipo siku Taifa la Tanganyika litafufuka? Je, itakuwaje? Je, Zanzibar itakuwepo ama?

Je, ipo siku Taifa la Tanganyika litafufuka? Je, itakuwaje? Je, Zanzibar itakuwepo ama?

Taifa la watu wa Tanganyika. Taifa alilopewa baba wa Taifa hili hayati Mwl Julius Nyerere. Ilakutokana na vita baridi moja ya mashirika ya kijasusi yakaipa taarifa tanganyika kile siku za mbele kitatokea na kwa nn kile kisiwa lazima kiwe kama Taifa moja. Well nisiandike zaidi yahiki nimepata kukisikia.

Ila mission hii bado ni mbichi japo maana kuwepo kwa Znz nikufufuka kwa Tanganyika nakufa kwa znz nikuwepo kwa Taifa moja Tanzania.

End
mkuu ukiongelea habari nzito kama hizi ujue kuna watu flani unawaumiza moyoni vibaya mno hii kitu yaani wanatamani waweke sheria asisikike mtu yoyote akiongelea hii habari ya muungano huu FEKI. na wanahisi kwamba kuna siku hii kitu itakuwa hakuna ubishi itakuja tu.. je wataikubali vipiii,,, ndo wanalotakiwa wawaze vinginevyo waanze mapemaaa kutafuta pa kuelekea kuhifadhiwa
 
Taifa la watu wa Tanganyika. Taifa alilopewa baba wa Taifa hili hayati Mwl Julius Nyerere. Ilakutokana na vita baridi moja ya mashirika ya kijasusi yakaipa taarifa tanganyika kile siku za mbele kitatokea na kwa nn kile kisiwa lazima kiwe kama Taifa moja. Well nisiandike zaidi yahiki nimepata kukisikia.

Ila mission hii bado ni mbichi japo maana kuwepo kwa Znz nikufufuka kwa Tanganyika nakufa kwa znz nikuwepo kwa Taifa moja Tanzania.

End
... Ni kukosekana kwa viongozi wenye maono ya mbele na mipango, ila wangekuwepo kuna siku Unguja na Pemba zingekuwa Mikoa kama ilivyo Mafia kuwa wilaya ya Pwani. sababu vizazi vya sasa havijui kuilinda historia vinahadahika kiwepesi mno.
 
Tanganyika ni jina tu linalowakilisha eneo linalopakana na nchi nane bara na ukanda wa bahari mashariki. Hiyo ndio Tanganyika. Kisiwa cha Mafia hakitajwi kwenye tafsiri hiyo na Unguja na Pemba hivyo hivyo!. Wakazi wa Tanganyika ni mchanganyiko wa makabila 120 ambayo yana ardhi na maeneo yao ya asili ambayo yalichangia kuunda nchi iliyoitwa Tanganyika. Alichokifanya Nyerere ni kujenga utaifa kwa kuyaunganisha makabila haya na kupata nchi ya Tanganyika, lakini alizidisha chumvi zaidi kwa kutamani kuiunganisha Afrika nzima huku akianza na Zanzibar. Sababu ya kuichagua Zanzibar nimeishaitaja na ni wazi kuwa ina hila, vinginevyo kama nia yake ingekuwa safi, bila kuficha madhambi ya Zanzibar, angeanza kuiunganisha Burundi na Rwanda kwanza, zilizounda pamoja na Tanganyika, Germany East Afrika. Jibu la swali lako ni kuwa, ikirudi Tanganyika sasa hata bila kuwepo Nyerere, hakutakuwa na mgogoro kwani hakuna makabila yanayotaka kutambulika kama nchi, zaidi ya kutambika na tambo za kimila.

Makabila hayakuchangia kuiunda Tanganyika, ni wazungu ndiyo walichora mistari kwenye ramani wakaita Tanganyika. Ilikuwa ni nchi bandia tuu. Ndiyo maana husikii mtu anajiita mtanganyika. Unasikia wanajiita watanzania au wasukuma au wahaya lakini hakuna anayejitambulisha kama Mtanganyika. Hakuna hilo taifa.
 
Makabila hayakuchangia kuiunda Tanganyika, ni wazungu ndiyo walichora mistari kwenye ramani wakaita Tanganyika. Ilikuwa ni nchi bandia tuu. Ndiyo maana husikii mtu anajiita mtanganyika. Unasikia wanajiita watanzania au wasukuma au wahaya lakini hakuna anayejitambulisha kama Mtanganyika. Hakuna hilo taifa.
Wazungu walikuja wakakuta mipaka ya makabila, walichofanya ni kuliita eneo walilotawala kwa jina la Tanganyika. Kwa nini wabara hawajiiti watanganyika hivi sasa? ... Sababu ni mchakato wa muungano ulioasisiwa kinyemela na watu wawili kwanza, Karume na Nyerere kisha kutangaza kwa wananchi kuwa sasa tumeungana kuwa nchi moja Tanzania. Kabla ya muungano nimeshuhudia nchi ikiitwa hivyo, radio zikitangaza hivyo, nimeshuhudia bendera ya Tanganyika na wimbo wa Taifa wa Tanganyika. Wananchi wa bara waliukubali huu muungano, ingawa mimi nikiwa mtoto sikulielewa lengo la kuibadilisha Tanganyika kuwa Tanzania. Nina wasiwasi na wazanzibari, kama wote waliukubali huu muungano hivyo ni wazi wale walioporwa mamlaka na umiliki wa visiwa, kwa vyovyote watakuja kudai uhuru wa visiwa vya Zanzibar na Pemba. Swali linakuja, Zanzibar nje ya muungano inarudi kwa mwenye himaya yake ... Oman? Je mapinduzi yaliyofanywa matakatifu yataendelea kuwa hivyo au walioporwa mamlaka watadai chao. Kwangu mimi naitaka Tanganyika irudi na Zanzibar na Pemba pia zirudi kama zilvyokuwa kabla ya muungano ili tuulizane kama huu muungano tunautaka kweli na kama tunautaka basi tuamue kuupanga uwe na manufaa kwa wote na hapa suruhisho ni kuwa na Serikali moja tu.
 
"kila mtu abaki kwao akubaliane na faida na hasara za kuvunjika muungano"
lakini pia akubaliane na maisha baada ya Muungano.

Kila mtu atalinda mipaka yake, na kila mtu atalipia cha mwenzie atakachotumia, Wazanzibar wanatumia umeme kutoka bara ambao sasa watachagua waulipie au wawe na umeme wao, Wazanzibar wanafanya biashara bara sasa watachagua waje watafute vibali vya kuishi na kufanya biashara bara. Hizo ndio athari za kuvunjika muungano kwao na wakishindwa kulinda mipaka yao shauri yao, sisi tutalinda mipaka yetu.
Hakuna kitu chochote wazanzibari wanachopewa bure kutoka bara. Wanalipia kila kitu na vya ziada pia
 
Wazungu walikuja wakakuta mipaka ya makabila, walichofanya ni kuliita eneo walilotawala kwa jina la Tanganyika. Kwa nini wabara hawajiiti watanganyika hivi sasa? ... Sababu ni mchakato wa muungano ulioasisiwa kinyemela na watu wawili kwanza, Karume na Nyerere kisha kutangaza kwa wananchi kuwa sasa tumeungana kuwa nchi moja Tanzania. Kabla ya muungano nimeshuhudia nchi ikiitwa hivyo, radio zikitangaza hivyo, nimeshuhudia bendera ya Tanganyika na wimbo wa Taifa wa Tanganyika. Wananchi wa bara waliukubali huu muungano, ingawa mimi nikiwa mtoto sikulielewa lengo la kuibadilisha Tanganyika kuwa Tanzania. Nina wasiwasi na wazanzibari, kama wote waliukubali huu muungano hivyo ni wazi wale walioporwa mamlaka na umiliki wa visiwa, kwa vyovyote watakuja kudai uhuru wa visiwa vya Zanzibar na Pemba. Swali linakuja, Zanzibar nje ya muungano inarudi kwa mwenye himaya yake ... Oman? Je mapinduzi yaliyofanywa matakatifu yataendelea kuwa hivyo au walioporwa mamlaka watadai chao. Kwangu mimi naitaka Tanganyika irudi na Zanzibar na Pemba pia zirudi kama zilvyokuwa kabla ya muungano ili tuulizane kama huu muungano tunautaka kweli na kama tunautaka basi tuamue kuupanga uwe na manufaa kwa wote na hapa suruhisho ni kuwa na Serikali moja tu.

Hayo makabila yaliishi kama nchi moja kabla ya wazungu?
 
Suala la kuundwa enzi hzo si maagano ya kutokuvunja. Ile ni km ndoa, inapokuwa na dosari hakuna budi kuiangalia upya. Hatumaanishi kuivunja bali kuirekebisha ili wanandoa hao waendelee kuishi kulingana na matakwa yao. Nyerere na karume enzi hizo ukifuatilia huenda hadi wake zao walitafutiwa na wazee wao na haikuwa noma lakini kwa sasa mtu unakuwa huru kusaka mwenyewe. Ndo tunataka marekebisho kama hayo, mfumo ule ulifit enzi hizo na sasa tunahitaji mfumo mpya wenye kuitambua tanzania tu ama kutambua tanganyika km ilivyo kwa zanzibar.
Wewe unapoteza nini kwa dola ya Tanzania iliyopo?
 
Hayo makabila yaliishi kama nchi moja kabla ya wazungu?
Hapana, kulikuwa na tawala za kimakabila (Kimila)ambazo msingi wake ulijengwa kutokana na ukoo uliosimikwa toka enzi za mababu na mabibi ndizo zilizotoa viongozi kwa kuzingatia vigezo walivyojiwekea. Viongozi hawa walioulikana kama machifu,watemi, mangi, mwami, wafalme na malkia walitawanyika katika eneo lote la Tanganyika na mifano ipo.
Huko Iringa kwa wahehe, kulikuwa na chifu Mkwawa na ukichimba sana utakuta kuwa wahehe walikuwa na eneo lao la utawala. Wanyamwezi walikuwa na chifu wao wa unyanyembe Milambo, waha walikuwa na mwami wao,akina Mtare, Ruhinda, Ruhaga, Ruyangwa nk. Huko Moshi kulikuwa na Mangi, akina Shangali, .... Tanga akina Kimweri, Kusini kule akina Mputa.
Hawa wote walikuwepo hata kabla ya wakoloni kuingia Afrika na wakati huo utaratibu wa Utaifa na maeneo yake kutengwa kama nchi ulikuwa bado haujaingia.
 
Hapana, kulikuwa na tawala za kimakabila ambazo msingi wake ulijengwa kutokana na ukoo uliosimikwa toka enzi za mababu na mabibi ndizo zilizotoa viongozi kwa kuzingatia vigezo walivyojiwekea. Viongozi hawa walioulikana kama machifu,watemi, mangi, mwami, wafalme na malkia walitawanyika katika eneo lote la Tanganyika na mifano ipo.
Huko Iringa kwa wahehe, kulikwa na chifu Mkwawa na ukichimba sana utakuta kuwa wahehe walikuwa na eneo lao la utawala. Wanyamwezi walikuwa na chifu wao wa unyanyembe Milambo, waha walikuwa na mwami wao,akina Mtare, Ruhinda, Ruhaga, Ruyangwa nk. Huko Moshi kulikuwa na Mangi, akina Shangali, .... Tanga akina Kimweri, Kusini kule akina Mputa.
Hawa wote walikuwepo hata kabla ya wakoloni kuingia Afrika na wakati huo utaratibu wa Utaifa na maeneo yake kutengwa kama nchi ulikuwa bado haujaingia.

Na ndiyo maana Tanganyika ni nchi bandia. Kabla ya mkoloni kuileta haikuwepo, watu walikuwa wanaishi kikabila kwa mila na desturi zao. Ukisema Tanganyika irudi unazungumzia hiyo Tanganyika aliyoleta mkoloni, hakuna nchi ya Tanganyika kihistoria. Hakuna taifa lilioitwa Tanganyika kihistoria. Taifa ni Zanzibar na ndiyo maana Wanzanzibari wanajitambua kama Wazanzibari hata ukiwakuta popote pale duniani.
 
Na ndiyo maana Tanganyika ni nchi bandia. Kabla ya mkoloni kuileta haikuwepo, watu walikuwa wanaishi kikabila kwa mila na desturi zao. Ukisema Tanganyika irudi unazungumzia hiyo Tanganyika aliyoleta mkoloni, hakuna nchi ya Tanganyika kihistoria. Hakuna taifa lilioitwa Tanganyika kihistoria. Taifa ni Zanzibar na ndiyo maana Wanzanzibari wanajitambua kama Wazanzibari hata ukiwakuta popote pale duniani.
Najaribu kuelewa mantiki ya hoja yako, sipati picha unalenga nini. Unaposema wazungu ndio walioileta Tanganyika, waliileta kutoka wapi? Hao watu waliokuwa wanaishi kikabila walikuwa wanaishi wapi? Tarehe 9 December ya kila mwaka huwa tunasherehekea uhuru wa nchi gani kama siyo Tanganyika?

Hiyo Zanzibar yenyewe unayoinadi kama taifa ilipata uhuru wake December 10, 1963 ingawa huwa haisherehekewi!. Watu wa Zanzibar ni mkusanyiko wa watu waliotoka bara, na kundi la waarabu kutoka Ghuba ya Oman, wana tofauti gani kama taifa na mchangnyiko wa makabila yaliyoko bara?

Unachonadi ni mwendelezo wa ghiriba na mazingaombwe ya kisiasa kwenye utata unaoghubika muungano, ambapo wanasiasa wachache ndio wanaofaidika na hawako tayari kuona mtego huu ukiteguliwa.
 
Najaribu kuelewa mantiki ya hoja yako, sipati picha unalenga nini. Unaposema wazungu ndio walioileta Tanganyika, waliileta kutoka wapi? Hao watu waliokuwa wanaishi kikabila walikuwa wanaishi wapi? Tarehe 9 December ya kila mwaka huwa tunasherehekea uhuru wa nchi gani kama siyo Tanganyika?

Hiyo Zanzibar yenyewe unayoinadi kama taifa ilipata uhuru wake December 10, 1963 ingawa huwa haisherehekewi!. Watu wa Zanzibar ni mkusanyiko wa watu waliotoka bara, na kundi la waarabu kutoka Ghuba ya Oman, wana tofauti gani kama taifa na mchangnyiko wa makabila yaliyoko bara?

Unachonadi ni mwendelezo wa ghiriba na mazingaombwe ya kisiasa kwenye utata unaoghubita muungano, ambapo wanasiasa wachache ndio wanaofaidika na hawako tayari kuona mtego huu ukiteguliwa.

Tanganyika ililetwa na Waingereza. Kabla hawajaja hakuna aliyeongelea Tanganyika kama nchi au sehemu. Watu walikuwa wanaishi Busukuma, Uhehe, Buhaya n.k. siyo Tanganyika. Makabila tofauti yaliishi kwa mila na desturi zao, hayakuishi kama taifa moja. Na Tanganyika aliouwa Nyerere ikifufuka itasambaratika tuu.

Wazanzibari wa asili wameshajinganya na kuishi pamoja kama Wazanzibari tangu ya karne ya 1. Ni Wazanzibari kama taifa moja. Na ndiyo maana ukitembea dunia yote ukikutana na Mzanzibari anajijua kama Mzanzibari. Mie katika mazunguko yangu duniani hii sijawahi kukutana na Mtanganyika. Nimekutana na watanzania tele, wachaga, wazaramo, wasukuma n.k. Lakini Mtanganyika bado.

 
Tanganyika ililetwa na Waingereza. Kabla hawajaja hakuna aliyeongelea Tanganyika kama nchi au sehemu. Watu walikuwa wanaishi Busukuma, Uhehe, Buhaya n.k. siyo Tanganyika. Makabila tofauti yaliishi kwa mila na desturi zao, hayakuishi kama taifa moja. Na Tanganyika aliouwa Nyerere ikifufuka itasambaratika tuu.

Wazanzibari wa asili wameshajinganya na kuishi pamoja kama Wazanzibari tangu ya karne ya 1. Ni Wazanzibari kama taifa moja. Na ndiyo maana ukitembea dunia yote ukikutana na Mzanzibari anajijua kama Mzanzibari. Mie katika mazunguko yangu duniani hii sijawahi kukutana na Mtanganyika. Nimekutana na watanzania tele, wachaga, wazaramo, wasukuma n.k. Lakini Mtanganyika bado.


Kwa maana hiyo ni heri huu muungano uvunjwe,tena haraka sana ili Zanzibar ibakie kama taifa huru na sisi bara tubaki na Tanganyika yetu tuliyoletewa na wazungu. Tatizo kubwa ni kundi dogo la wanasiasa wanaonufaika na muungano hivi ilivyo sasa.
 
Mnajivunia kujiita watanganyika kwa lipi hasa ambalo hilo jina linamaanisha? Kama sio ukoloni au Kuna lingine la kujivunia kwa hilo jina???

Wazanzibar wanajivunia kuitwa wazanzibar sababu wao bado wanahisi wanavina Saba na watu wa Oman ambao usultan ulitawala

Zanzibar walifanya mapinduzi kutoa uongozi wa usultan ila walikataa kufanya mapinduzi la jina la taifa lao wakabaki na wasalia ya jina la kisultan na hadi leo wanahisi ndugu zao ni waoman waarabu kuliko watu wa bara.

Watanganyika ndio hawa wanaojiita watanzania

Wazanzibar wanaojiita wazanzibar wala hawajiiti watanzania

Tanzania lipo badala la jina la Tanganyika kwa hiyo hakuna Cha Tanganyika hatuwezi kurudia matapishi ya miaka 60 mapitio ya wakoloni
 
Wewe unapoteza nini kwa dola ya Tanzania iliyopo?
Napoteza utanganyika huku uzanzibar ukiwepo. Zanzibar ndo ilifanya neno tanganyika lipotee why yenyewe haipotei ili wote tuwe watanzania tu?
 
Back
Top Bottom