Ila kwa Sasa unakubaliana umeondolewa kwa mda Hadi pale watakapo tubu na kutambua Yesu kristo waliomkataa ndiye Masihi waliyekuwa wanasubiri? Na ukiona ilo limetokea basi ujue Mwisho wa ulimwengu umefikia.Mkuu huu mstari wa Roman 11: nilioutumia hapo juu umetoa majibu yote,,kwamba ndio wayahudi walimkataa Yesu..Ila kwa ule ufalme kuondoka kwao sio moja kwa moja....hebu upitie tena mwenyewe utaona point yangu.
Shida yangu sio waitwe waisrael point yangu ni kwamba warithi halali wa hizo ahadi za waisrael ni nani je ni kina netanyahu au wakristo??? Hio Israel ya mashariki ya kati ni ya kimwili tu haina impact yeyote kwa ufalme wa Mungu.Israel ni taifa lililoko pale mashariki ya kati,,wakristo waliomwamini Yesu wote ni kanisa/mwili wa Kristo na sio waisrael.
Habari za jioni wana JF mada ya leo ni sensitive kidogo maana inagusa moja ya topic zenye utata katika ulimwengu wa imani ila ningependa tusome kwa utulivu uzi wote alafu tujadiliane kwa hoja ili tuweze kusolve hili swali la karne nyingi sasa.
View attachment 929882
UTANGULIZI
Mwanzoni kulikuwa na agano kati ya wanadamu na Mungu kupitia Adam ila tunaona Adam analivunja agano hili
(Hosea 6:7)
Lakini wao wamelivunja hilo agano kama Adamu;
Hivyo Mungu alitaka kurudisha uhusiano tena na mwanadamu tunaona akapatikana Nuhu ambaye alimcha Mungu sana na akachaguliwa kuianza dunia upya baada ya gharika. Sasa baada ya gharika dhambi ilirudi tena kupitia Ham ambaye alipelekea Nuhu kumlaani mwana wake Ham yaani canaan kuwa atakuwa mtumwa wa kaka zake Ham yaani Shem na Yapheth (Hili la muhimu sana huko mbeleni) hivyo uzao wa Ham ukawa na watu waovu sana mfano Nimrod wa Babylon aliyeleta ibada za sanamu na dini za kipagani hadi kuleta machafuko kwenye ukoo wa Nuhu na kusababisha dunia nzima kumuacha Mungu wa Nuhu.
Katika sintofahamu hii aliyesimama imara alikuwa Shem/Melchizedek ndie aliendelea kushika wokovu na hata Abraham alipozaliwa aliendelea kumsimamia kiimani na hivyo hata alipokufa Abraham kati ya wanadamu wengi ndio aliendeleza imani ya kumuabudu Mungu wa babu zake (YAHWEH) hivyo baada ya Mungu kuona Abraham ana msimamo thabiti kwake akampa ahadi ya kuwa na uzao wa watu wengi kama nyota za angani lakini pia alimpa ahadi ya kumpa nchi hii ya canaan.
Mwanzo 15
18 Siku ile BWANA akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,
Hivyo ni kupitia ahadi hii ndipo taifa la Israel lilipotabiriwa rasmi kuwepo. Na ahadi hiyo itakuja kutekelezwa na mjukuu wake yaani Yakobo ambaye aliiba urithi wa mtoto wa kwanza hivyo hii baraka ya Abraham akairithi yeye na tunaona uzao wake kupitia Joshua na Caleb ndio wanaingia kwenye nchi hii ya canaan rasmi na kuasisi taifa la Israel.
Je Mungu aliichagua Israel??
Kumb. La torati 7:6
6 Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako; BWANA Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.
Kupitia mstari huu tunaona Israel ilichaguliwa na Mungu lakini je kwanini aliichagua??
Kumb. Torati 7:7-8
7 BWANA hakuwapenda ninyi, wala hakuwachagua ninyi, kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote, maana mlikuwa wachache kuliko watu wote;
8 bali kwa sababu BWANA anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza uapo wake aliowaapia baba zenu.
Hivyo Mungu aliwachagua Israel sababu hiyo ya kutimiza uapo kwa mababu ikiwemo Nuhu + Abraham. Na hili ndio lilisababisha Israel wapewe nchi ya Canaan sababu ilikuwa inahitimisha unabii wa Nuhu kuwa Canaan atakuwa mtumwa wa shem (Babu wa Abraham) na sio kwa sababu nyingine yeyote.
Mwanzo 9
26 Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake
View attachment 929883
Ramani ya canaan
Hivyo baada ya Agano hili na Israel ambalo kupitia wao ndio Mungu alipanga kuwaletea Messiah yaani Yesu ili aweze kurejesha uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu kama wa kipindi cha Adamu lakini wayahudi walimkataa Yesu kwa sababu hawakujua kutafsiri unabii ulioandikwa kuhusu maisha ya Yesu kwenye agano la kale. Kwa kifupi maisha yote ya Yesu kuanzia kuzaliwa mpaka kufa yalikuwa yanaendana na unabii wa agano la kale 1 korinto 15:1-4 Mfano wa nabii zilizotimizwa kupitia maisha ya Yesu ni hizi. Kuanza mahubiri yake galilaya ulitabiriwa na Isaya 9:1-2 na ukatimia Mathayo 4:13, Pia Yesu kupanda Punda kuingia jerusalem ulitabiriwa na Zakaria 9:9 na kutimia Mathayo 21:1-9 n.k yaani kuna mistari zaidi ya 100 iliyotabiriwa kuonyesha Huyo Messiah ataishije.
Lakini wao wayahudi hawakuliona hili sababu walidhani Yesu atakuwa handsome boy, Damu ya kifalme,Mwanajeshi kama alexander the great n.k hivyo kwa jinsi alivyokuja "kimasikini" wakaona kama anakufuru mwisho wa siku wakamuua na yote ni kutokana na kushindwa kutafsiri maandiko ya unabii.
Matendo 13:26-27
27 Kwa maana wakaao Yerusalemu, na wakuu wao, kwa kuwa hawakumjua yeye, wala maneno ya manabii yanayosomwa kila sabato, wameyatimiza kwa kumhukumu.
Hakuna cha propaganda. Unapaswa kuelewa kuwa ule uteule Wa Israeli kwa Mungu umebakia Wa kihistoria. Sasa Taifa teule ni Kanisa lake Kristu. Kwa njia ya Kanisa watu wake tunakombolewa kutoka dhambini kwa ubatizo kuondoa dhambi ya asili na sakramenti ya upatanisho kutuondolea dhambi zingine tunazozitenda baada ya ubatizo.
Israel walijiita hivyo kwa vile waliwahi kustaarabika, na kwa uzalendo waliokuwa nayo kwa nchi ya na miji yao eg Jerusalem wakayaita maeneo matakatifu. Lakini ukiniuliza mimi hakuna bustani nzuri ya Eden kama Serengeti & Ngorongoro ambako viumbe wote wa Mungu wanapatikana, na Tanganyika yangu ikiwa ndiyo taifa teule. Sema sisi technology duni, umasikini, uongozi mbovu usiothamini raia wake nkHivi Taifa teule la Mungu ndo ili la Benjamin Netanyahu au kwakuwa Biblia ina mafumbo mengi labda Taifa Teule la Mungu ni watenda mema wote haijalishi ni Mtanzania, Mpakistan, Mnyarwanda au Mkenya,
Je Taifa teule la Mungu ni lipi? Ndo Israel hii??
kuna tofauti pia kati ya KANISA, na taifa la Israeli.........Hivi Taifa teule la Mungu ndo ili la Benjamin Netanyahu au kwakuwa Biblia ina mafumbo mengi labda Taifa Teule la Mungu ni watenda mema wote haijalishi ni Mtanzania, Mpakistan, Mnyarwanda au Mkenya,
Je Taifa teule la Mungu ni lipi? Ndo Israel hii??
Hivi ndio ambavyo mimi huwa natambua pia.. Kongole mkuuWayahudi walitumia maandiko ya Mwenyezi Mungu vibaya sana kujipa "superiority"...hata hivyo hali ya sasa inawaumbua mbele ya macho ya Watu duniani kote kwani hawana tofauti na Congo (DR), Syria au Afghanistan. Kwanza kisheria na kiutaratibu ni Wadhulumat wa ardhi ya Wapalestina japo wanatumia hayohayo maandiko kujisafishia njia ya kuwanyanyasa Wapalestina. Kwa kiburi walimkataa hata Yesu (Nabii Issa A.S).
Tuko pamoja mkuu ahsante.Hivi ndio ambavyo mimi huwa natambua pia.. Kongole mkuu
Waislam wachache wahovyo kweli wakiongozwa na media zinazojiita zina misingi ya kiislam.Wayahudi walitumia maandiko ya Mwenyezi Mungu vibaya sana kujipa "superiority"...hata hivyo hali ya sasa inawaumbua mbele ya macho ya Watu duniani kote kwani hawana tofauti na Congo (DR), Syria au Afghanistan. Kwanza kisheria na kiutaratibu ni Wadhulumat wa ardhi ya Wapalestina japo wanatumia hayohayo maandiko kujisafishia njia ya kuwanyanyasa Wapalestina. Kwa kiburi walimkataa hata Yesu (Nabii Issa A.S).
Uislamu umetokea wapi wewe pimbi? Kwanza unajua kuwa wayahudi siyo Wakristu na walishamkataa Yesu? Acheni kudanganyana huko vijiweni mkahisi hao wayahudi ni ndugu zenu...you are a very poor minded creature i ever met here. Soma vitabu vya kihistoria utaujua ukweli.Waislam wachache wahovyo kweli wakiongozwa na media zinazojiita zina misingi ya kiislam.
.
Nenda kawakomboe sasa hao wapalestina wanaodhurumiwa anzisheni jihad dhidi ya Israel mwasubiri mini miongo yote hiyo?
Hakuna taifa ambalo halina ardhi yake, wanatumia maandiko kuunda upya lile taifa lao, baada ya kuzaliwa kwa red haife, muda si mrefu ule msikiti watabomoa ili wajenge hekalu na hivyo kukamilisha unabii wa nabii Ezekiel!Wayahudi walitumia maandiko ya Mwenyezi Mungu vibaya sana kujipa "superiority"...hata hivyo hali ya sasa inawaumbua mbele ya macho ya Watu duniani kote kwani hawana tofauti na Congo (DR), Syria au Afghanistan. Kwanza kisheria na kiutaratibu ni Wadhulumat wa ardhi ya Wapalestina japo wanatumia hayohayo maandiko kujisafishia njia ya kuwanyanyasa Wapalestina. Kwa kiburi walimkataa hata Yesu (Nabii Issa A.S).
Tofautisha kati ya waisrael na wayahudi, uyahudi ni dini ambayo wanavikubali vitabu vya torati ila bado wanamsubiria masihi, waisrael ni taifa kwa ujumla, ndani yake kukiwa na wayahudi, wakristu, waislam, na hata ambao hawana dini. Mada inazungumzia Waisrael na siyo wayahudi.Uislamu umetokea wapi wewe pimbi? Kwanza unajua kuwa wayahudi siyo Wakristu na walishamkataa Yesu? Acheni kudanganyana huko vijiweni mkahisi hao wayahudi ni ndugu zenu...you are a very poor minded creature i ever met here. Soma vitabu vya kihistoria utaujua ukweli.
Ahsante mimi pimbi wewe nyumbu.Uislamu umetokea wapi wewe pimbi? Kwanza unajua kuwa wayahudi siyo Wakristu na walishamkataa Yesu? Acheni kudanganyana huko vijiweni mkahisi hao wayahudi ni ndugu zenu...you are a very poor minded creature i ever met here. Soma vitabu vya kihistoria utaujua ukweli.