Je, Israel ya sasa ni Taifa teule la Mungu au ni propaganda tu za kanisa?

Je, Israel ya sasa ni Taifa teule la Mungu au ni propaganda tu za kanisa?

Mkuu huu mstari wa Roman 11: nilioutumia hapo juu umetoa majibu yote,,kwamba ndio wayahudi walimkataa Yesu..Ila kwa ule ufalme kuondoka kwao sio moja kwa moja....hebu upitie tena mwenyewe utaona point yangu.
Ila kwa Sasa unakubaliana umeondolewa kwa mda Hadi pale watakapo tubu na kutambua Yesu kristo waliomkataa ndiye Masihi waliyekuwa wanasubiri? Na ukiona ilo limetokea basi ujue Mwisho wa ulimwengu umefikia.
 
Israel ni taifa lililoko pale mashariki ya kati,,wakristo waliomwamini Yesu wote ni kanisa/mwili wa Kristo na sio waisrael.
Shida yangu sio waitwe waisrael point yangu ni kwamba warithi halali wa hizo ahadi za waisrael ni nani je ni kina netanyahu au wakristo??? Hio Israel ya mashariki ya kati ni ya kimwili tu haina impact yeyote kwa ufalme wa Mungu.

Jikite kwenye hiyo mistari ya petro nilioweka je petro alimaanisha nini kuwaita wakristo taifa teule
 
Habari za jioni wana JF mada ya leo ni sensitive kidogo maana inagusa moja ya topic zenye utata katika ulimwengu wa imani ila ningependa tusome kwa utulivu uzi wote alafu tujadiliane kwa hoja ili tuweze kusolve hili swali la karne nyingi sasa.
View attachment 929882
UTANGULIZI
Mwanzoni kulikuwa na agano kati ya wanadamu na Mungu kupitia Adam ila tunaona Adam analivunja agano hili

(Hosea 6:7)
Lakini wao wamelivunja hilo agano kama Adamu;

Hivyo Mungu alitaka kurudisha uhusiano tena na mwanadamu tunaona akapatikana Nuhu ambaye alimcha Mungu sana na akachaguliwa kuianza dunia upya baada ya gharika. Sasa baada ya gharika dhambi ilirudi tena kupitia Ham ambaye alipelekea Nuhu kumlaani mwana wake Ham yaani canaan kuwa atakuwa mtumwa wa kaka zake Ham yaani Shem na Yapheth (Hili la muhimu sana huko mbeleni) hivyo uzao wa Ham ukawa na watu waovu sana mfano Nimrod wa Babylon aliyeleta ibada za sanamu na dini za kipagani hadi kuleta machafuko kwenye ukoo wa Nuhu na kusababisha dunia nzima kumuacha Mungu wa Nuhu.

Katika sintofahamu hii aliyesimama imara alikuwa Shem/Melchizedek ndie aliendelea kushika wokovu na hata Abraham alipozaliwa aliendelea kumsimamia kiimani na hivyo hata alipokufa Abraham kati ya wanadamu wengi ndio aliendeleza imani ya kumuabudu Mungu wa babu zake (YAHWEH) hivyo baada ya Mungu kuona Abraham ana msimamo thabiti kwake akampa ahadi ya kuwa na uzao wa watu wengi kama nyota za angani lakini pia alimpa ahadi ya kumpa nchi hii ya canaan.

Mwanzo 15
18 Siku ile BWANA akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,

Hivyo ni kupitia ahadi hii ndipo taifa la Israel lilipotabiriwa rasmi kuwepo. Na ahadi hiyo itakuja kutekelezwa na mjukuu wake yaani Yakobo ambaye aliiba urithi wa mtoto wa kwanza hivyo hii baraka ya Abraham akairithi yeye na tunaona uzao wake kupitia Joshua na Caleb ndio wanaingia kwenye nchi hii ya canaan rasmi na kuasisi taifa la Israel.

Je Mungu aliichagua Israel??

Kumb. La torati 7:6
6 Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako; BWANA Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.

Kupitia mstari huu tunaona Israel ilichaguliwa na Mungu lakini je kwanini aliichagua??

Kumb. Torati 7:7-8
7 BWANA hakuwapenda ninyi, wala hakuwachagua ninyi, kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote, maana mlikuwa wachache kuliko watu wote;
8 bali kwa sababu BWANA anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza uapo wake aliowaapia baba zenu.

Hivyo Mungu aliwachagua Israel sababu hiyo ya kutimiza uapo kwa mababu ikiwemo Nuhu + Abraham. Na hili ndio lilisababisha Israel wapewe nchi ya Canaan sababu ilikuwa inahitimisha unabii wa Nuhu kuwa Canaan atakuwa mtumwa wa shem (Babu wa Abraham) na sio kwa sababu nyingine yeyote.

Mwanzo 9
26 Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake

View attachment 929883
Ramani ya canaan


Hivyo baada ya Agano hili na Israel ambalo kupitia wao ndio Mungu alipanga kuwaletea Messiah yaani Yesu ili aweze kurejesha uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu kama wa kipindi cha Adamu lakini wayahudi walimkataa Yesu kwa sababu hawakujua kutafsiri unabii ulioandikwa kuhusu maisha ya Yesu kwenye agano la kale. Kwa kifupi maisha yote ya Yesu kuanzia kuzaliwa mpaka kufa yalikuwa yanaendana na unabii wa agano la kale 1 korinto 15:1-4 Mfano wa nabii zilizotimizwa kupitia maisha ya Yesu ni hizi. Kuanza mahubiri yake galilaya ulitabiriwa na Isaya 9:1-2 na ukatimia Mathayo 4:13, Pia Yesu kupanda Punda kuingia jerusalem ulitabiriwa na Zakaria 9:9 na kutimia Mathayo 21:1-9 n.k yaani kuna mistari zaidi ya 100 iliyotabiriwa kuonyesha Huyo Messiah ataishije.

Lakini wao wayahudi hawakuliona hili sababu walidhani Yesu atakuwa handsome boy, Damu ya kifalme,Mwanajeshi kama alexander the great n.k hivyo kwa jinsi alivyokuja "kimasikini" wakaona kama anakufuru mwisho wa siku wakamuua na yote ni kutokana na kushindwa kutafsiri maandiko ya unabii.

Matendo 13:26-27
27 Kwa maana wakaao Yerusalemu, na wakuu wao, kwa kuwa hawakumjua yeye, wala maneno ya manabii yanayosomwa kila sabato, wameyatimiza kwa kumhukumu.

'Israeli', kama 'taifa teule la Mungu' haina maana ya nchi ya Israeli, bali wale ambao kwa mafundisho ya Yesu na mitume wake wamekuja kuamini na kuishi maneno ya habari njema. Hawa ndio kanisa huwa linasema, familia ya Mungu, taifa la Mungu etc.
 
Hakuna cha propaganda. Unapaswa kuelewa kuwa ule uteule Wa Israeli kwa Mungu umebakia Wa kihistoria. Sasa Taifa teule ni Kanisa lake Kristu. Kwa njia ya Kanisa watu wake tunakombolewa kutoka dhambini kwa ubatizo kuondoa dhambi ya asili na sakramenti ya upatanisho kutuondolea dhambi zingine tunazozitenda baada ya ubatizo.


Kanisa la kristo , Hivi kristo gani mwenye kanisa ??
 
Hivi Taifa teule la Mungu ndo ili la Benjamin Netanyahu au kwakuwa Biblia ina mafumbo mengi labda Taifa Teule la Mungu ni watenda mema wote haijalishi ni Mtanzania, Mpakistan, Mnyarwanda au Mkenya,

Je Taifa teule la Mungu ni lipi? Ndo Israel hii??
 
Hivi Taifa teule la Mungu ndo ili la Benjamin Netanyahu au kwakuwa Biblia ina mafumbo mengi labda Taifa Teule la Mungu ni watenda mema wote haijalishi ni Mtanzania, Mpakistan, Mnyarwanda au Mkenya,

Je Taifa teule la Mungu ni lipi? Ndo Israel hii??
Israel walijiita hivyo kwa vile waliwahi kustaarabika, na kwa uzalendo waliokuwa nayo kwa nchi ya na miji yao eg Jerusalem wakayaita maeneo matakatifu. Lakini ukiniuliza mimi hakuna bustani nzuri ya Eden kama Serengeti & Ngorongoro ambako viumbe wote wa Mungu wanapatikana, na Tanganyika yangu ikiwa ndiyo taifa teule. Sema sisi technology duni, umasikini, uongozi mbovu usiothamini raia wake nk
 
mkuu, talk about land not people...............


ardhi ya lile taifa ndio imebarikiwa na Mungu, so automatically linakua taifa teule/barikiwa la Jehovah Mungu!!!!.......

kuhusu zile kabila 12 za Israel, who knows? wengi hatuna uhakika kama ndio hao kina Netanyahu au wenyewe wapo mahali kwingine...........


ila ukifika wkt wa Bwana, hao watarudi (kama kweli hawapo Israel hivi leo), si unajua MASHAURI YA BWANA mwanadamu hawezi kuyazuia!
 
Hivi Taifa teule la Mungu ndo ili la Benjamin Netanyahu au kwakuwa Biblia ina mafumbo mengi labda Taifa Teule la Mungu ni watenda mema wote haijalishi ni Mtanzania, Mpakistan, Mnyarwanda au Mkenya,

Je Taifa teule la Mungu ni lipi? Ndo Israel hii??
kuna tofauti pia kati ya KANISA, na taifa la Israeli.........


KANISA ni wale wote wamwaminio KRISTO kama BWANA, MASIHI, MKOMBOZI NA MFALME.............


ISRAELI ni ile ardhi ambayo BABA MUNGU alimwapia IBRAHIMU, ISAKA NA YAKOBO kuwapa wazao wao!.............


N.B/ kitabu cha Danieli ndio kimeongelea kwa mapana na marefu destiny ya Israeli
 
Wayahudi walitumia maandiko ya Mwenyezi Mungu vibaya sana kujipa "superiority"...hata hivyo hali ya sasa inawaumbua mbele ya macho ya Watu duniani kote kwani hawana tofauti na Congo (DR), Syria au Afghanistan. Kwanza kisheria na kiutaratibu ni Wadhulumat wa ardhi ya Wapalestina japo wanatumia hayohayo maandiko kujisafishia njia ya kuwanyanyasa Wapalestina. Kwa kiburi walimkataa hata Yesu (Nabii Issa A.S).
 
Wayahudi walitumia maandiko ya Mwenyezi Mungu vibaya sana kujipa "superiority"...hata hivyo hali ya sasa inawaumbua mbele ya macho ya Watu duniani kote kwani hawana tofauti na Congo (DR), Syria au Afghanistan. Kwanza kisheria na kiutaratibu ni Wadhulumat wa ardhi ya Wapalestina japo wanatumia hayohayo maandiko kujisafishia njia ya kuwanyanyasa Wapalestina. Kwa kiburi walimkataa hata Yesu (Nabii Issa A.S).
Hivi ndio ambavyo mimi huwa natambua pia.. Kongole mkuu
 
Taifa la Israel liliundwa na watoto 12 wa Yakobo ambaye baadaye allitwa Israel. Na hao watoto walitengeneza kabila 12 za waisrael. Hii familia katika mazingira Fulani walijikuta wako Misri kama watumwa ,baadaye wakaondolewa kwa nguvu za Mungu akimtumia Musa hadi katika nchi alyowaahidi.Inaamini ndio hao hao akina Natanyahu kwa kuwa kuna baadhi ya tamaduni na mila za waisrael wale wailoelezwa kwenye biblia na akina Natanyahu wanazifuata.Kimsingi Mungu aliyokuwa akiwaeleza Waisrael ilitakiwa wayaeneze kwa mataifa mengine yote ulimwenguni. Hata hivyo baada ya Yesu kuja ,wale wote wanaomwamini nao ni waisrael wa Kiroho.Hata milango ambayo ipo kwenye mji wa mbinguni kuna milango kumi na mbili na kila mlango umeandikwa jina la kabila la Israel.
Ufunuo 21:9-15
Akaja mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na vile vitasa saba vilivyojaa yale mapigo saba ya mwisho, naye akanena nami, akisema, Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo.
10 Akanichukua katika Roho mpaka mlima mkubwa, mrefu, akanionyesha ule mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mwenyezi Mungu;

11 wenye utukufu wa Mungu, na mwangaza wake ulikuwa mfano wa kito chenye thamani nyingi kama kito cha yaspi, safi kama bilauri;

12 ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu, wenye milango kumi na miwili, na katika ile milango malaika kumi na wawili; na majina yameandikwa ambayo ni majina ya kabila kumi na mbili za Waisraeli.

13 Upande wa mashariki milango mitatu; na upande wa kaskazini milango mitatu; na upande wa kusini milango mitatu; na upande wa magharibi milango mitatu.

14 Na ukuta wa mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na katika ile misingi majina kumi na mawili ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.

15 Na yeye aliyesema nami alikuwa na mwanzi wa dhahabu, apate kuupima huo mji, na milango yake, na ukuta wake.
 
Wayahudi walitumia maandiko ya Mwenyezi Mungu vibaya sana kujipa "superiority"...hata hivyo hali ya sasa inawaumbua mbele ya macho ya Watu duniani kote kwani hawana tofauti na Congo (DR), Syria au Afghanistan. Kwanza kisheria na kiutaratibu ni Wadhulumat wa ardhi ya Wapalestina japo wanatumia hayohayo maandiko kujisafishia njia ya kuwanyanyasa Wapalestina. Kwa kiburi walimkataa hata Yesu (Nabii Issa A.S).
Waislam wachache wahovyo kweli wakiongozwa na media zinazojiita zina misingi ya kiislam.
.
Nenda kawakomboe sasa hao wapalestina wanaodhurumiwa anzisheni jihad dhidi ya Israel mwasubiri mini miongo yote hiyo?
 
Waislam wachache wahovyo kweli wakiongozwa na media zinazojiita zina misingi ya kiislam.
.
Nenda kawakomboe sasa hao wapalestina wanaodhurumiwa anzisheni jihad dhidi ya Israel mwasubiri mini miongo yote hiyo?
Uislamu umetokea wapi wewe pimbi? Kwanza unajua kuwa wayahudi siyo Wakristu na walishamkataa Yesu? Acheni kudanganyana huko vijiweni mkahisi hao wayahudi ni ndugu zenu...you are a very poor minded creature i ever met here. Soma vitabu vya kihistoria utaujua ukweli.
 
Wayahudi walitumia maandiko ya Mwenyezi Mungu vibaya sana kujipa "superiority"...hata hivyo hali ya sasa inawaumbua mbele ya macho ya Watu duniani kote kwani hawana tofauti na Congo (DR), Syria au Afghanistan. Kwanza kisheria na kiutaratibu ni Wadhulumat wa ardhi ya Wapalestina japo wanatumia hayohayo maandiko kujisafishia njia ya kuwanyanyasa Wapalestina. Kwa kiburi walimkataa hata Yesu (Nabii Issa A.S).
Hakuna taifa ambalo halina ardhi yake, wanatumia maandiko kuunda upya lile taifa lao, baada ya kuzaliwa kwa red haife, muda si mrefu ule msikiti watabomoa ili wajenge hekalu na hivyo kukamilisha unabii wa nabii Ezekiel!
 
Uislamu umetokea wapi wewe pimbi? Kwanza unajua kuwa wayahudi siyo Wakristu na walishamkataa Yesu? Acheni kudanganyana huko vijiweni mkahisi hao wayahudi ni ndugu zenu...you are a very poor minded creature i ever met here. Soma vitabu vya kihistoria utaujua ukweli.
Tofautisha kati ya waisrael na wayahudi, uyahudi ni dini ambayo wanavikubali vitabu vya torati ila bado wanamsubiria masihi, waisrael ni taifa kwa ujumla, ndani yake kukiwa na wayahudi, wakristu, waislam, na hata ambao hawana dini. Mada inazungumzia Waisrael na siyo wayahudi.
 
Uislamu umetokea wapi wewe pimbi? Kwanza unajua kuwa wayahudi siyo Wakristu na walishamkataa Yesu? Acheni kudanganyana huko vijiweni mkahisi hao wayahudi ni ndugu zenu...you are a very poor minded creature i ever met here. Soma vitabu vya kihistoria utaujua ukweli.
Ahsante mimi pimbi wewe nyumbu.
.
Wayahudi au Judaism sio dini ni dhehebu haiko kama unavyopotoshwa au ulivyopotoshwa na mama yako.
.
Wayahudi wanatumia biblia kuabudu japo wana baadhi ya taratibu ambazo madhehebu mengine hayazifuati, wasabato nao ni wakristo japo nao kuna baadhi ya mambo yanayofanywa na madhehebu mengine hawayafuati, PENTECOSTAL n.k nao wanataratibu zao.
.
Kwa jinsi ulivyo tahira wewe mtoto haujui hata mabohora nao ni waislam Ila wana namna zao za kuabudu.
.
Pumbavu sana ujielewe
 
Back
Top Bottom