Je, jehanamu ziwa la moto na adhabu za huko ni za milele au sio za milele?

Je, jehanamu ziwa la moto na adhabu za huko ni za milele au sio za milele?

milele kwa maana kwamba mtu anachomwa tu moto anaungu halafu hafi au?
Iko hivi,kwanza binadamu mwenyewe ni roho inayoishi ndani ya mwili wa nyama,kwa hiyo binadamu mwenyewe ambaye ni roho huwa hafi,bali roho inatoka kwenye mwili huu wa duniani ambao unaoza na kuvalishwa mwili mpya ambao hauteketei kwa moto na haufi kwa mtu yule ambaye atakwenda motoni.

Hivyohivyo na kwa mtu anayekwenda peponi naye anavalishwa mwili mwingine unaofanana na mazingira ya peponi kwa kuwa ni mwili mpya na ambao haujawahi kugusa dhambi.

Kwa ufupi ni kwamba kufa kwa binadamu ndio mwanzo wa maisha mapya ya milele na milele motoni au peponi,na hakuna kufa tena kwa kuwa hakuna kufa mara mbili na miili mipya haifi inafanana na malaika wa mbinguni.
 
Kwa wale ambao wamemshirikisha Mungu kwa kusema Mungu ni watatu hao watachomwa moto milele, na wale wenye dhambi ila waliamini Mungu ni mmoja hajazaa wala hajazaliwa wao wataadhibiwa kutokana na dhambi zao lakin baadae utapita msamaha na watatolewa katika adhabu.

Na kwa wale waliofanya mema wakatubu dhambi zao na wakamuabudu Mungu mmoja ambae hajazaa wala hajazaliwa na wala hakuna anaefanana nae hao malipo yao yatakua ni kuingia peponi
Hakuna anayesema kuna Mungu watatu ila kuna Mungu mmoja katika nafsi tatu.
 
Maisha ya Watanzania tayari wapo motoni, sasa kuna moto zaidi ya huu?

Sijawahi kuona Baba anayeweza kumchoma mwanaye moto, halafu Yesu si alishabeba dhambi za binadamu? mbona tunaleteana ngonjera nyingine?
Kutudanganya tu kama watoto wadogo wanaoanza chekechea!
Yaani kwamba eti Mungu anayetupenda siku ya mwisho atuchome moto milele kisa tumevunja amri zake!
Kama ni hivyo hakika tutarostiwa binadamu wote
 
Ziwa la moto ,limepewa baraka zote za show za kibabe,


Ukisikia mtokoto wa 🔥🔥🔥 ndotoni hivi,
Huenda ukawa teari,duniani hatuko nawe,
 
Ziwa la moto ,limepewa baraka zote za show za kibabe,


Ukisikia mtokoto wa 🔥🔥🔥 ndotoni hivi,
Huenda ukawa teari,duniani hatuko nawe,
 
Man Jau ,
DR Mambo Jambo
Rabbon

NAOMBA muje ,na mnisaidie kuwa tag watu wote ,wa mada za mambo ya kiroho ,

Waje kutowa mchango wao,

Naitaji huu uzi ,umalize ule utata ,tutoke na nibu Moja,

Je,Ziwa la moto ni la Milele au sio la Milele?

NaAdhabu zake humo ,kwenye Ziwa la Moto, ni za Milele au si za Milele?
Hapo ujue kuwa kuna mambo 2,kuna kuzimu na jehanam na kote huko kuna moto,kuzimu ndio sehemu ya kwanza wanakopelekwa binadamu waliotenda dhambi,wakati wanangojea hukumu yao ya kupelekwa jehanamu ambako ndiko liliko ziwa la moto,huko kuzimu hawatakaa milele na milele,kuzimu ni kama vile lock up ya polisi ambako wanatunzwa watuhumiwa wanaosubiri kuhukumiwa kupelekwa kufungwa magereza.

Jehanamu ambako ndiko kunaziwa la moto huko ndiko watenda dhambi watakaa milele na milele tofauti na kuzimu ambako watenda dhambi watakaa kwa muda kadhaa wakati wanasubiri hukumu yao ya kutupwa jehanamu kwenye ziwa la moto.

Japo kuwa kote kuna moto lakini moto wa kuzimu siyo wa milele na milele ni sehemu ya mangojeo ya wale walioko kuzimu wakati wanasubiri hukumu ya mwisho itakayofanya wapelekwe jehanamu kwenye ziwa la moto pamoja na shetani ambako wataungua milele na milele na hakuna kufa.

Jehanamu kwenye ziwa la moto hakuna mtu yeyote anayeungua huko kwa sasa,bado wapo kuzimu kusubiri hukumu ya mwisho ya kuwatupa jehanamu,japo kuwa maumivu wanayoyapata wakati wako kuzimu ni maumivu kama yaleyale watakayoyapata jehanamu kwa kuwa wote ni moto uleule.

Ni kama vile mbinguni,mbinguni hakuna watu,wote waliokufa katika Bwana wako paradiso ambako ndiko kwenye mangojeo yao ya kwenda mbinguni baada ya hukumu ya mwisho,na kote huko paradiso(peponi)na mbinguni maisha ya huko yanafanana,tofauti yake ni kwamba maisha ya paradiso ni ya muda tofauti na mbinguni ambako maisha yake ni ya milele na milele.
 
Hapo ujue kuwa kuna mambo 2,kuna kuzimu na jehanam na kote huko kuna moto,kuzimu ndio sehemu ya kwanza wanakopelekwa binadamu waliotenda dhambi,wakati wanangojea hukumu yao ya kupelekwa jehanamu ambako ndiko liliko ziwa la moto,huko kuzimu hawatakaa milele na milele,kuzimu ni kama vile lock up ya polisi ambako wanatunzwa watuhumiwa wanaosubiri kuhukumiwa kupelekwa kufungwa magereza.

Jehanamu ambako ndiko kunaziwa la moto huko ndiko watenda dhambi watakaa milele na milele tofauti na kuzimu ambako watenda dhambi watakaa kwa muda kadhaa wakati wanasubiri hukumu yao ya kutupwa jehanamu kwenye ziwa la moto.

Japo kuwa kote kuna moto lakini moto wa kuzimu siyo wa milele na milele ni sehemu ya mangojeo ya wale walioko kuzimu wakati wanasubiri hukumu ya mwisho itakayofanya wapelekwe jehanamu kwenye ziwa la moto pamoja na shetani ambako wataungua milele na milele na hakuna kufa.

Jehanamu kwenye ziwa la moto hakuna mtu yeyote anayeungua huko kwa sasa,bado wapo kuzimu kusubiri hukumu ya mwisho ya kuwatupa jehanamu,japo kuwa maumivu wanayoyapata wakati wako kuzimu ni maumivu kama yaleyale watakayoyapata jehanamu kwa kuwa wote ni moto uleule.

Ni kama vile mbinguni,mbinguni hakuna watu,wote waliokufa katika Bwana wako paradiso ambako ndiko kwenye mangojeo yao ya kwenda mbinguni baada ya hukumu ya mwisho,na kote huko paradiso(peponi)na mbinguni maisha ya huko yanafanana,tofauti yake ni kwamba maisha ya paradiso ni ya muda tofauti na mbinguni ambako maisha yake ni ya milele na milele.
Ulishawahi kufika huko mkuu?😳
 
Kuzimu nauwakika ipo, lakin jehanam nikesoma kisa cha yona ni sehemu ya mateso roho chafu, lakin hapa kwenye umilele ukii ichambua utapata jipu zuri tu.
Ujue watu wanapo sikia milele wanajua wana tafsiri miaka mingi isiyo na mwisho au unlimited time, sasa picha linaanza time does not exist sasa huo umilele umeutoa wapi?? Ukisema unlimited time maana yake still time is there but unlimited kitu ambacho siio sahihi,
Nitoe mfano, Mtu alie kufa leo na alie kufa miaka 200 ilii pita kwa hesabu zetu huku duniani lakin kuzimu hawawote hamna record nan aliwa anza kufika nan kachelewa, ukifika utahisi kama kilakitu kimesimama
 
Inaonekana hili Dubwana JEHANAM SIO ZA LEVEL ZAKO,

MAANA ,CODE ZAKE ZINAFUNGULIWA KIIMANI,

ILO DUBWANA LINATAKA MAELEZO YA KIIMANI ZAIDI, NA WALIO NA IMANI WATALIPOKEA,

MAANA HATA CODE ZAKE ZIMEKAA KIIMANI NA ZIKIFUNGULIWA CODE HUMU, WATAO ELEWA NA KIPOKEA NI UZAO WA IMANI,

EBWANA HILO DUBWANA ZIWA LA MOTO LIPO ,


NACHO TAKA KUJUA ZAIDI ,NI JE LA MILELE AU SIO LA MILELE
Kukaa milele inategemea na makosa ulio Fanya wapo watakao kaa milele na wapo hawatokaa milele
 
Ulishawahi kufika huko mkuu?😳
Bado niko hai ninaishi kwa hiyo sijafika na sitegemei kwenda kuzimu,ila hayo ni mambo ya kiroho ni mpaka uwe wa kiroho ndio utaelewa mambo kama hayo,kama we we unaamini katika ukristo soma kitabu cha Luka sura ya 16 kuanzia mstari wa 23 utakuta kuna kisa cha Ibrahimu,masikini Razalo na tajiri ambao wote walikutana kuzimu baada ya kufa,ila walikuwa sehemu tofauti pamoja na kwamba wote walikuwa kuzimu.
 
Iko hivi,kwanza binadamu mwenyewe ni roho inayoishi ndani ya mwili wa nyama,kwa hiyo binadamu mwenyewe ambaye ni roho huwa hafi,bali roho inatoka kwenye mwili huu wa duniani ambao unaoza na kuvalishwa mwili mpya ambao hauteketei kwa moto na haufi kwa mtu yule ambaye atakwenda motoni.

Hivyohivyo na kwa mtu anayekwenda peponi naye anavalishwa mwili mwingine unaofanana na mazingira ya peponi kwa kuwa ni mwili mpya na ambao haujawahi kugusa dhambi.

Kwa ufupi ni kwamba kufa kwa binadamu ndio mwanzo wa maisha mapya ya milele na milele motoni au peponi,na hakuna kufa tena kwa kuwa hakuna kufa mara mbili na miili mipya haifi inafanana na malaika wa mbinguni.
Duh mbona hatari sasa hii
 
Jehanam si ya milele
Itafutwa
Kila kitu kilichoanzishwa chenye mwanzo kina mwisho
Ila vya milele hukaa milele
Jehanam hata ikikaa miaka milion kumi lakin itafutwa na watu wake
Maana wenye haki ya uzima wa milele ni wana wa Mungu tuu
Waovu hawatabahatika kupata uzima wa milele hata kwenye shida za jehanam
 
Sasa why mungu atese watoto wake wew unaweza tesa watot wako kisa wamenyoa kiduku au model
Hizo UNAZO zitafuta ni sababu za kimwili kibinadamu,mitazamo ya kibinadamu.

Ila kirohoni ,Mungu Yuko sahihi siku zote,

Ziwa la Moto lipo ,na SHOW YAKE SIO YA KITOTO NDIO MAANA KAWEKWA KAMA FUNGA KAZI WA KURASA ZOTE ZA UOVU NA UASI,
 
ENYI WATU NAOMBENI MCHANGO WA MAWAZO YENU ,

TAZAMA HII,

Mwilini = Start-End format
Rohoni=n.start-n.End format

Mwilini= Time
Rohoni= No Time

Mwilini= Kuna mwanzo na mwisho
Rohoni= Hakuna mwanzo Wala mwisho.

Mwilini = Kuna Muda
Rohoni= hakuna Muda

Hivyo ,jehanamu Haina muda, Haina mwisho ?

Na
Vipi kuhusu mateso ,tunaweza sema hayana muda, no end,

VIPI KUHUSU UZIMA WA MILELE,

HAPO NDIO KIINI CHA MADA ILIPO,

UZIMA WA MILELE JUU
UZIMA WA MILELE CHINI

UZIMA WA MILELE WA NURUNI
UZIMA WA MILELE WA GIZANI

UZIMA WA MILELE WA UHAI
UZIMA WA MILELE WA MAUTI,

UZIMA WA MILELE NA MUNGU
UZIMA WA MILELE NA SHETANI

UZIMA WA MILELE WA UTUKUFU
UZIMA WA MILELE WA DHAMBI


LABDA TUSEME, TUJIKITE KUCHAMBUA HUO UZIMA WA MILELE WA KIROHO ,NA WATU WA CHINI JEHANAM WATAKUWA NA UZIMA USIO NA MWISHO WA MILELE AU WATA KUFA MARA YA PILI KWA KUKOSA UZIMA WA MILELE,

TAGETI NI HUU UZIMA WA MILELE ,

JE, KUTOKUWA NAO HUO UZIMA NI KAMA HUKU DUNIANI MTU ANAKUFA MARA YA KWANZA ,

KULE JE MTU ATAKUFA MARA YA PILI AU KUWA KWENYE LILE ZIWA LA MOTO MILELE NDIO INAYOHESABIWA KUWA MULE ZIWANI NDIO KIFO CHENYEWE LAKINI ROHO YA MTU HAIFI ,

JE ZIWA NDIO MAUTI YA PILI , AU MAUTI HIO YA PILI NI WATU KUFA KABISA ZIWANI PA MOTO ,

KIMWILI MTU ALIEKOSA UZIMA TUNASEMA
ROHO IMETENGANA NA MWILI HIO KATIKA MWILI
NA

VIPI ROHONI TUTASEMA NAFSI IMETENGANA NA ROHO WA UZIMA (MUNGU) HIO NDIO KATIKA ROHO,NA HIO NDIO AWAMU YA PILI,

LAKINI KITU KINGINE TUNAONA KABLA HAWAJATUPWA JEHANAM WALE WATU WALIOPEWA MIILI YA DHAMBI ISIO NA UTUKUFU ILE MIILI YA KIFINYO CHA JEHANAM
 
Hizo UNAZO zitafuta ni sababu za kimwili kibinadamu,mitazamo ya kibinadamu.

Ila kirohoni ,Mungu Yuko sahihi siku zote,

Ziwa la Moto lipo ,na SHOW YAKE SIO YA KITOTO NDIO MAANA KAWEKWA KAMA FUNGA KAZI WA KURASA ZOTE ZA UOVU NA UASI,
Me naamini mungu yupo ila hakuna ziwa la moto maan mungu ni mwenye huruma hawez kubal ufe kwa maumivu makali
 
Back
Top Bottom