Je, jina la Yesu ni kweli lina nguvu na uwezo mkubwa katika kutenda miujiza hadi leo? Wewe limekutendea makubwa gani? Karibu ushuhudie

Lakini wakimaanisha jina moja
Jina moja lipi sasa ambalo wanalimaanisha? Nachojua ni kwamba huyo ambaye unamtambua kama Yesu ndio ambaye kwa kiingereza humwita Jesus, sasa hapo wanamaanisha jina moja au wanamkusudia mtu mmoja?
 
Yesu hakuwa nabiii bali akuwa Mesiya!! tuanzia hapo kwanza ili tuendelee na mengine.

Ujio wa Yesu kristo kama Mesiya ulitabiliwa na manabii wengi tu akiwemo Zakaria, Isaya na wengine kuonyesha ukuu wake.

Isaya 7:14: "Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli”

Isaya 9:6: "Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume, na uweza wa kifalme utakuwa juu ya mabegani mwake. Naye ataitwa jina lake Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani."

Mika 5:2: "Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katiaka Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.”

Utabiri kuhusu kifo chake pia kilishuhudiwa na manabii wa kale

Zakaria 9:9: " Furahi sana, Ee binti Sayuni; piga kelele, Ee binti Yerusalemu; Tazam, mflame wako anakuja kwako; Ni mwenye haki, naye ana wokovu; Ni mnyenyekevu, amepanda punda, Naam, mwana-punda, motto wa Punda” ( Neno hili lilitimia wakati Yesu akiingia Yerusalem huku akiwa amempanda wanapunda)


Zaburi 22:16-18: "Kwa maana mbwa wamenizunguka; kusanyiko la waovu wamenisonga; wamenizua mikono na miguu. Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; wao wannitazama na kunikodolea macho. Wanagawanya nguo zangu, na vazi langu wanlipigia kura.” ( Hapa neno hili lilitimia akiwa msalabani na wakati walipoipigia kura Kanzu ya Yesu)
 
Malaika wa ovu awajabadilika wamebakia kwenye uovu,pili wao walishahukumiwa tayari, mwanadamu ndo anaesubiria hukumu
Namaanisha hao malaika waovu wana sifa za kimalaika kama walivyo malaika ambao si waovu au walibadilika na kutokuwa malaika tena?
 
Namaanisha hao malaika waovu wana sifa za kimalaika kama walivyo malaika ambao si waovu au walibadilika na kutokuwa malaika tena?
Kwa tasfiri ya wengine malaika wapo wa aina mbili wema na waovu,yaani wa Mungu na wa shetani.
 
Jina moja lipi sasa ambalo wanalimaanisha? Nachojua ni kwamba huyo ambaye unamtambua kama Yesu ndio ambaye kwa kiingereza humwita Jesus, sasa hapo wanamaanisha jina moja au wanamkusudia mtu mmoja?
Matamko tu lakini maana moja tu
 
Kwahiyo Mungu aliumba kiumbe kinaitwa shetani?
 
Lingekua linaponya wangeenda hospital wakawaponye wagonjwa na siyo kusubiri sadaka kanisan.
Usanii mwingi hiyo ni biashara
 
Kwa tasfiri ya wengine malaika wapo wa aina mbili wema na waovu,yaani wa Mungu na wa shetani.
Nakuuliza hivyo kwa sababu hao unaosema ni malaika waovu huwa mnasema kuwa ndio hawa viumbe wanaoitwa majini, na ukiangalia sifa za hao viumbe majini haziendani na malaika.

Majini sifa zao nyingi hufanana na binaadamu, ndio maana nauliza hao malaika waovu bado ni malaika au walibadilika na sio malaika tena?
 
Matamko tu lakini maana moja tu
Ndio maana nikakwambia kuwa hayo majina yanamkusudia mtu mmoja ila ni majina tofauti, hakuna jina ambalo utasema kuwa ndio linakusudiwa bali kuna mtu mmoja ambaye ndio anakusudiwa kutoka kwenye majina tofauti tofauti.
 
Waliofurushwa na shetani still bado ni waouvu, wengine uwaita majini
 
Tuthibitishie Kama kweli hayo maneno alisema au hakusema
Maandiko ni yenu mmeandika wenyewe Muhammad kasema , sasa Mimi nije nipinge au ? Shetani wa muhammad alikuwa muislamu

"I looked for the Messenger of Allah and I put my hand on his hair." He said: "Your Shaitan has come to you." I said: "Don't you have a Shaitan?" He said: "Yes, but Allah helped me with him, so he submitted." Sunan an-Nasa'i 3960
[/QUOTE]
Your browser is not able to display this video.
 
Wapi nimesema mimi ni muumini wa mtu.
Nimemtolea mfano, mchungaji Mwamposa, jinsi anavyotumia Shuhuda za uongo kuibia wakristo wenzake.

Wewe umejibu wewe siyo Muumini wake.
Ndiyo nimekuuliza wewe ni muuni wa mtu.
 
Labda nikuulize majini ni viumbe gani au ni akina nani?
Majini viumbe vilivyomuasi Mwenyezi Mungu.Majini roho ni viumbe katika ulimwengu wa roho.
Ni vitendea Kazi vya shetani,utumika na wachawi na waganga wa kienyeji.
 
Nimemtolea mfano, mchungaji Mwamposa, jinsi anavyotumia Shuhuda za uongo kuibia wakristo wenzake.

Wewe umejibu wewe siyo Muumini wake.
Ndiyo nimekuuliza wewe ni muuni wa mtu.
Kuthibitisha kama ni uongo au ukweli ni hadi uingie kwenye ulimwengu wa roho sio wa nyama
 
Hakuna jina jingine tunalopaswa kuokolewa nalo isipokuwa jina la Yesu Kristo pekee. Jina kuu kupita majina yote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…