Je, jina la Yesu ni kweli lina nguvu na uwezo mkubwa katika kutenda miujiza hadi leo? Wewe limekutendea makubwa gani? Karibu ushuhudie

Nimemtolea mfano, mchungaji Mwamposa, jinsi anavyotumia Shuhuda za uongo kuibia wakristo wenzake.

Wewe umejibu wewe siyo Muumini wake.
Ndiyo nimekuuliza wewe ni muuni wa mtu.
Unachotakiwa kujua hizi ni nyakati za mwisho na Neno la Mungu lazima litimie,itakuwa katika nyakati za mwisho watainuka watumishi.................Jihadharini na mbwa mwitu waliovaa ngozi ya kondoo.......msiziamini kila roho bali zijaribuni kuona kama zinatoka kwa Bwana...Watu wangu wanaangamizwa kwa kusoma maarifa.Acha watapeliwe,Yesu akasema Neno la Mungu na lijae kwa wingi mioyoni mwenu,ukilijua Neno la Mungu huwezi kutapeliwa kirahisi.
 
Reactions: _ly
Una Quote, ni vizuri kuanza mwanzo, mwanza ujue mpaka naandi hivyo tulianzis wapi.
Maana unadhani umejibu hoja yangu, kumbe jujanijibu bado.
 
Ndivyo älivyokuambia mchungaji wako?

Akipotea mmoja ,mnapotezana wote hakuna jipya msome na ndugu yako mwingine huyu mko na desa moja
 
Una Quote, ni vizuri kuanza mwanzo, mwanza ujue mpaka naandi hivyo tulianzis wapi.
Maana unadhani umejibu hoja yangu, kumbe jujanijibu bado.
Kama hoja yako nikiona kuna umuhimu wa kuijibu nitakujibu sijibu kila hoja ndugu yangu,hapo nimekujibu juu ya huyo uliyemtaja au hujaelewa nilichokiandika.Ungekuwa msomaji wa Biblia ungeelewa kwani mengin nimeandika ni kwa mujibu wa biblia.
 
Wewe leta jibu huku usiwahamishe watu,umekamata mwizi hapa mshugurikie hapa hapa wewe unaenda kumshughurikia kwingine🤣🤣
Tulia basi kama hutaweza kwenda kusoma mwenyewe basi acha wengine watasoma
 
🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Kama hoja yako nikiona kuna umuhimu wa kuijibu nitakujibu sijibu kila hoja ndugu yangu,hapo nimekujibu juu ya huyo uliyemtaja au hujaelewa nilichokiandika.Ungekuwa msomaji wa Biblia ungeelewa kwani mengin nimeandika ni kwa mujibu wa biblia.
Huu upumbavu wa kudhani imani yako ni bora kuliko kuliko ya mwingine, iliniganya ninunue bibilia nisome ili niwe najibu kwa mstari, humu tulikua na akina mgeni na wakristo wengine wenye majina fulani ya kishoga.

Lakini mwisho wa Siku tulikubaliana, Uwe Muislam uwe mkristo maisha ni yale yale Shida raha tunaziishi wote, bila kujali imani yako.

Hivyo kubisha hapa ni upumbavu tu, imani yako kama ndiyo bora kwanini ulalamikie kupanda kwa mafuta, kwanini Mungu wako asikurahishie eneo hilo, ili tabu muachie wasiamini kwenu.

Mtu anafunga Ramadhini yake kwa imani yake, alafu anatokea mjinga mmoja, anakosoa kupitia bibilia, huu si ujinga, yeye hafungi kupitia bibilia yako.

Kitabu chenu nimempa rafiki yangu John Ndongo, Ujinga uishie Mbali, Mungu hawezi kukuacha Salama ikiwa huheshimu wengine, Maana kwa mkosaji nini yeye mwenye uwezo wa kumuonyesha njia sahihi nae ndiye mwenye Kuhukumu.

Ila mkilianzisha sikai kimya.
 

Yesu ni Mungu

Kama ilivyotabiriwa na manabii. Na jina lake ndilo jina lipitalo majina yote

Isaya 9: 6-7
"Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepata mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.
Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo."

Luka 2: 10 - 11 ~ Aliyezaliwa ni Kristo, Jina Yesu lilishushwa na malaika. Yesu ni Mungu
"Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana."

Mathayo 1: 20 -21
"Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu"


Yohana 10: 17 - 18
"Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. "
 
Reactions: _ly


Yesu alionya, lakini Paulo hakusikia:

"Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie. Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na wakawararua."


Yaliyosemwa yamekuwa. Kwa kitendo cha Paulo kuwaingiza mapagani wa Kizungu katika dini ya Yesu sharia ya Mwenyezi Mungu ikaambiwa ni laana, ikatolewa ruhusa kula nyamafu, nguruwe na damu, na kila kiuzwacho sokoni bila ya kutia wasiwasi wo wote katika dhamiri.

Tohara aliyoamrishwa Ibrahimu na Mwenyezi Mungu na Manabii wote wakaifuata mpaka mwenyewe Yesu na wanafunzi wake, Paulo aliipuuza kuwaridhi makafiri. Imani za kipagani za mungu mwana na utatu zilizoenea katika mila za Mithra, Osiris, Attis n.k. zikaingizwa katika dini ya Kikristo.

Katika ufalme wa mbinguni Yesu ana yakini kuwa hatokuwa nao ila wana wa Israili tu. Injili ya Mathayo inasema:

Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.
Mathayo 19.28

Hata katika maombi yake inaonyesha kuwa Yesu alikuwa anajua mipaka yake na uwezo wake.

Madai ya kuwa yeye ni mwombezi, mbali kuwa ni mwokozi, wa ulimwengu mzima ni kumsingizia jambo ambalo mwenyewe hakulidhania.

Kumpa mtu cheo asichokuwa nacho ni kumtukana, ni kumvika kilemba cha ukoka, kama Mayahudi walivyotaka kumkejeli kwa kumvika taji la miba.

Cheo alicho nacho kwa hakika si kidogo. Kuwa ni Mtume wa Mwenyezi Mungu miongoni mwa Mitume na Manabii watukufu ni jambo kuu kweli kweli.

Kuwa mtumishi wa Mwenyezi Mungu mwenye kupendeza si utukufu mdogo.

Na Yesu alitafakhari nao, na alitafakhari kuwa yeye hakutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa Ki-Israili.

Na hayo si kwa upungufu wo wote kwa upande wake, ila ni kuutumikia ujumbe wa Mwenyezi Mungu kwa kuulinda usiharibiwe na washirikina mpaka ufike wakati wa kuja huyo atayekuwa kazi yake ni kuitangazia risala ya Mungu kwa ulimwengu mzima.
Katika Injili ya Yohana ananukuliwa Yesu kusema:

Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa.
Yohana 17.9

Ni jambo linalojuulikana katika historia - na hata ukisoma katika Biblia kitabu cha Matendo ya Mitume utaona - ya kuwa Ukristo kwanza haukuhubiriwa kwa mataifa mengine mpaka alipoingia Paulo.

Na yeye alipingwa vikali sana kwa kutoa shauri hiyo na wanafunzi wake Yesu waliomwona na wakawa naye siku zote na wakajifunza vilivyo mafunzo yake na makatazo yake ya kwenda kuwahubiria watu ambao bado ni makafiri.


Ukristo tuuonao na ulioenea ulimwenguni sio Ukristo aliofundisha Yesu. Wa Yesu ulitoweka na mwenyewe na wafuasi wake wa mwanzo wa kabila la Kiyahudi. Paulo kaufuja Ukristo.

Kauli zinazonukuliwa kwa kudai kuwa ni ushahidi kuwa Yesu mwenyewe alitaka mafunzo yake yakafundishwe kwa ulimwengu wote yamo katika Injili ya Mathayo 28.19-20, Injili ya Luka 24.46-49 na Marko 16.15. Mathayo inasema:

Basi, enendeni, mkwafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Mathayo 28.19-20

Luka anatwambia:

(Yesu) akwaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya. Na tazama, naweletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kueni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.
Luka 24.46-49

Na Injili ya Marko inasema:

(Yesu) akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
Marko 16.15

Je, imekuwaje?

Yesu ni kigeugeu?

Mbona huku anawakataza wanafunzi wake wasende kuwahubiria ila kabila kumi na mbili za Israili, na huku anawaambia nendeni kuwahubiria Injili ulimwengu mzima.

La, Yesu si mbabaishi, wala si kigeugeu.

Hebu natuziangalie vilivyo hizo amri mbili, moja ya kuwa mafunzo yake wasifunzwe ila wana wa Israili tu, na ya pili ni hii ya kuwa watu wote wafunzwe dini.

Vipande vyote vitatu tulivyonukulu mwishoni havitaji mambo ya Yesu alipokuwa na maisha yake ya uhai wa kidunia, lakini vyaeleza mambo yaliyotukia baada ya "kufufuka kutoka wafu" kama inavyosimuliwa na Injili zote tatu.

Yajuulikana kuwa Injili ya mwanzo kuandikwa ni Injili ya Marko. Hizo nyingine ziliandikwa baadae, na labda ujuzi wao ulitegemea hiyo hiyo Injili ya Marko.

Yajuulikana vile vile kuwa maneno yote yaliyohusu kufufuka Yesu kutokana na wafu, pamoja na hayo maamrisho ya kwenda kuihubiri Injili "kwa kila kiumbe", kinyume na maamrisho yake yote ya kuwa asihubiriwe ila Muisraeli tu - maneno hayo yote hayakuwamo katik Marko ya asli, bali yaliongezwa baadae.

Encyclopaedia Brittanica, nakla ya 11, jalada 17, sahifa 730, yasema ya kuwa kipande chote hicho kiliongezwa baadae, yamkini mwanzo mwanzo wa karne ya pili, kuchukua maneno yaliyopotea, au yaliyoonekana kuwa ni mapungufu.
 


Yesu anasemaje katika Injili yake:

Yohana 17:3 imeandikwa hivi –

uzima wa milele ndiyo huu wakujue Mungu wa pekee na Yesu uliyemtuma.

Katika Aya hii Yesu anasema kwamba ili kupata uzima lazima tumjue kwanza Mungu wa pekee na umjue Yesu Kristo aliyetumwa na Mungu, hapa Yesu hasemi lolote kuhusu yeye kuwa nafasi ya pili ya Mungu ila anakiri wazi yeye ametumwa na Mungu mmoja wa pekee.

Luka 2:40 imeandikwa hivi: -

Yule mtoto akakua akaongezeka nguvu amejaa hekima na neema ya Mungu ilikua juu yake.

Katika Aya hii tunaambiwa kwamba Yesu alijaa hekima na neema ya Mungu.

Tahadhari ufikirie vizuri kwa makini sababu hapa inayonyesha kwamba bila ya Mungu kumpa neema Yesu asingelikuwa na hekima hii inaonyesha wazi Yesu ni kiumbe aliyeteuliwa na Mungu na hii ni kawaida yake Mwenyezi Mungu kwa Mitume na Manabii wake kuwapa neema na hekima.

Yohana 13:13 imeandikwa hivi: -

Nanyi mwaniita Mwalimu na Bwana nanyi mwasema vema maana ndivyo nilivyo. Maneno hayo yatueleza wazi kwamba alikuwa anajua wazi kwamba yeye ni Mwalimu na Bwana ndiyo maana anawasifu wanafunzi wake, NANYI MWASEMA VEMA.

Mathayo 23:9 imeandikwa: -

Wala msimwite mtu Baba maana Baba yenu ni mmoja wa Mbinguni wala msiitwe Kiongozi maana Kiongozi wenu ni mmoja naye ndiye Yesu Kristo. Hapa Yesu anaendelea kutuonyesha jinsi alivyo tofauti na Mungu, na yeye hayuko sawa na Mungu daima Mungu ni Baba lakini Yesu ni Kiongozi tu.

Ufunuo: 1:1-2 imeandikwa hivi: -

Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu awaonyeshe watu wake…Naye akatuma Malaika akamuonyeshe Mtumwa wake Yohana… Wakati ufunuo unatolewa na Mungu na kupewa Yesu wakati huo Yesu ameshatoka Duniani yuko Mbinguni (kwa mujibu wa bible), lakini bado inaonyesha Mungu ndiye mkubwa Yesu bado ni wakutumwa ili awaonyeshe watumwa kuhusu mambo yao yatakayokuja kama tulivyosoma. Zipo Aya nyingi sana zinazoonyesha wazi kuwa Yesu alikuwa halijui kabisa fundisho la tatu na wala kuhusu kuwa yeye ni Mungu.

Wanafunzi wa kwanza walimuelewaje Yesu?

Matendo ya Mitume 3:13 imeandikwa hivi… Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa Baba zetu amemtukuza Mtumishi wake Yesu ambaye nyinyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake ili afunguliwe.

Maneno ya wanafunzi yalikuwa wazi kuwa Yesu ni Mtumishi wa Mungu tu yaani Mtume pia ni Nabii.

Matendo ya Mitume 4:27 imeandikwa hivi…

maana ni kweli Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israel walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako Mtakatifu Yesu uliyemtia mafuta. Wanafunzi wanaendelea na msimamo wao kwamba Yesu ni Mtumishi wa Mungu aliyetumwa (Mtume) tu.

Luka 24:19 imeandikwa: -

Akawauliza mambo gani? Wakamwambia mambo ya Yesu Wanazareti aliyekuwa mtu nabii mwenye uwezo wa kutenda na kusema mbele za Mungu na Wanadamu.


Marko 6:2 imeandikwa: -

Na ilipokuwa Sabato aliingia katika Sinagogi, wengi waliposikia walishangaa wakasema huyu ameyapata wapi haya! Hekima gani hii? Aliyopewa huyu? Nini miujiza hii mikubwa inayotendeka kwa mikono yake? Huyu si ni yule Selemala mwana wa Mariamu na nduguyao Yakobo na Yosef na Yuda na Simoni na Maumbu wake hawapo hapa? (Maana ya Umbu ni dada)

Maneno haya yanathibitisha kwamba watu waliomfahamu Yesu walishangaa matendo makubwa anayoyatenda hata hivyo walijua kwamba yeye ni Selemala wa Mwana wa Mariamu tu. Na ni kiumbe mwenye ndugu zake na dada zake, kama watu wengine.

Marko 13:31 tunasoma hivi –

Mbingu na Nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe. Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna anaye ijua hata malaika wala Mwana (Yesu) ila Baba tu Mungu…

Hapa Yesu alikua anazungumza habari ya siku ya mwisho alikiri wazi kwamba yeye siku haijui hata Malaika hawajui ila Mungu peke yake.
 
Sema amina kubwa kubwa
 


Ukiweza kutofautisha Kristo na Yesu utapata majibu ya ulichoandika

Yohana 14: 8-9
"Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha. Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?"

Yesu ni Mungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…