Je, jina la Yesu ni kweli lina nguvu na uwezo mkubwa katika kutenda miujiza hadi leo? Wewe limekutendea makubwa gani? Karibu ushuhudie

Je, jina la Yesu ni kweli lina nguvu na uwezo mkubwa katika kutenda miujiza hadi leo? Wewe limekutendea makubwa gani? Karibu ushuhudie

Inabidi mtu kulitumia ukiwa na imani ya hali ya juu sana mimi nilikuwa na tatizo la kukabwa usiku nikawa naliita kimazoea mazoea sikuwa napata majibu stahiki mpaka hiyo hali ya kukabwa inaondoka yenyewe.

Kuna siku moja nilikabwa (hii kukabwa inakuwa ni kama mtu anakugandamiza kichwa kwa nguvu huku mikono yako imeshikwa) nikaona hapa sasa naondoka maana ilikuwa nimeshafika point ya mwisho nilijikuta napata nguvu na imani nikaliita kwa nguvu mara tatu ile hali ikaisha hadi leo haijajirudia.

Muhimu imani tu.

MIZANI YA IMANI YA WAKRISTO

Bwana Yesu Kristo alieleza mizani na alama za imani kama ifuatavyo:

1. Mkiwa na imani ya punje ya haridali, mtauambia mlima huu, ondoka hapa nenda kule, nao utaondoka; wala halitakuwapo neno lisilowezekana kwenu. (Mathayo17:20; 21:21; Marko 11:22-23, 9:23, Luka 17:6, 12, 13).

2. Bwana akasema: “Kama mngekua na imani kiasi cha chembe ya haridali mngeuambia mkuyu huu, ng'oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.” (Luka 17:7).

3. Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia mkiwa na imani , msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, ngo'ka ukatupwe baharini, litatendeka. na yoyote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea. (Mathayo 21:21-22)

4. Amin, Amin, nawaambieni, yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwani mimi naenda kwa Baba. (Yohana 14:12-13).

5. Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lolote nanyi mtatendewa. (Yohana 15:7).

6. Tena nawaambia, wawili wenu mtakapopatana duniani katika jambo lolote watakalo liomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. (Mathayo 7:3-12).

7. Ombeni nanyi mtapewa.... (Mathayo 7:3-12).


Katika mizani hii ya imani ya Wakristo, tumejua kwamba Mkristo atatambulika kwa alama zilizotajwa hapo juu.

Tena hizi ni alama za imani ndogo sana ya chembe ya haridali. Lakini kama Mkristo atakuwa na imani kubwa ataweza kuonesha miujiza mikubwa zaidi.

Vilevile Mkristo mwenye imani ni yule ambaye ataweza kuonesha miujiza na hasa sawa na ya Bwana Yesu bali mikubwa zaidi kuliko yake.

Sasa kwanza tutafute miujiza ya Bwana Yesu katika Biblia, tumeona baadhi yao kama ifuatavyo:

1. Kuponya wagonjwa (Mathayo 8:16, 9:22, na 15:21).

2. Kuponya walemavu (Mathayo 8:1-3).

3. Kuponya mabubu. (Mathayo 9:3-7; 12-22).

4. Kuponya mwenye kupooza upande mmoja (kiarusi) (Mathayo 8:5-13. 9:1-7, 12:22).

5. Kumponya mwenye kifafa. (Mathayo 17:14-19).

6. Kuponya mkono wenye ukoma. (Mathayo 12:15).

7. Kuponya mgongo uliopinda (Kibyongo) (Luka 13:10).

8. Kuwafufua wafu. (Mathayo 9:24).

9. Kugeuza maji kuwa pombe. (Yohana 2:1-9).

10. Chakula kidogo kitoshe watu elfu tano.(Mathayo 14:13-21).

11. Kutembea juu ya maji. (Mathayo 14:22-23).

12. Kuzuia tufani . ( Mathayo 8:23-33).

Hapa nimetoa baadhi ya mifano tu ya miujiza ya Bwana Yesu.

Kama Wakristo hamuwezi kuonesha miujiza ya aina hii au alama ya imani yao sawa na Biblia, basi
mambo mawili yanathibitika.

A. Bwana Yesu pia hakuonesha mujiza wowote bali ni hadithi za kutungwa tu zisizo na ukweli ndani yake.

B. Siku hizi Mkristo yeyote hana imani sawa na chembe ya haridali, bali wote mumeshapotea tayari na hamna alama au dalili yoyote ya imani.

Hali hizi zote mbili ni mbaya sana na za kutisha.

Na dawa yake ni moja tu kwamba muingie katika dini ya Mwenyezi Mungu, ISLAM, baada ya kutambua umoja wa Mungu na Mtume Muhammad s.a.w. bila hivyo mtaendelea kufedheheka siku hadi siku.


TAMBIO:

Ninawapa Wakristo tambio (challenge) kwamba kama wanayo imani sawa na chembe ya haridali, watuoneshe miujiza iliyotajwa hapo juu. Mkristo mmoja au wawili au wajumuike wote, tunataka kuona miujiza tu ya imani yao, hata Pope au wachungaji wenu wajitokeze.
 
🤣🤣
Eti kiti anataka maji, dhahabu
Sie hatuna muda, tunayafukuza Ili kae Roho Mtakatifu ndani ya mtu sio majini

Mathew 24


Jesus answered: “Watch out that no one deceives you.

5 For many will come in my name, claiming, ‘I am the Messiah,’ and will deceive many.
 
Wewe bado hujamjua Yesu Kristo.

Ngoja nikupe Homework.

Mama wa Nabii Musa alimtupa mtoto wake Musa mtoni kwa kuogopa atachinjwa na Herode.
Binti Farao akamwokota mtoto Musa na kuamua kumlea.

Mama wa Musa alifuatilia tukio lote la mtoto wake Musa kuchukuliwa na Binti Farao.

Kwa mapenzi makubwa ya Mama ya Musa kwa mtoto wake Musa ilibidi Mama wa Musa aende kwa Farao kuomba kazi ya Kijakazi au Housegirl ili amlee mtoto wake Musa.

Naomba unijibu hapa.

1.Familia ya Farao ilimjua Housegirl wao kuwa ni mama yake Musa?

2. Kwanini Mama wa Musa hakujitambulisha kama Mama wa Musa kwa Farao?

3. Je huyo Housegirl wa Farao alipo ongea kwenye familia ya Farao aliongea kama Mama wa Musa au kama Housegirl wa Farao?

4. Tufanye siku ya kwanza ya mama wa Musa kufika kwa Farao na kuomba kazi ya ujakazi, hivi angesema yeye ndiye mama mzazi wa Musa unafikiri nini kingetokea?

5. Kuna mtu kwenye familia ya Farao aligundua kuwa huyo hakuwa mjakazi bali ni mama mzazi wa Musa na hakumwambia mtu yeyote, unafikiri ni kwanini alinyamaza?

6. Ungekuwa wewe kwenye familia ya Farao. Ungeweza kumtambua yule mjakazi kuwa ni mama mzazi wa Musa?

7. Kama wewe ulivyo, ungehitaji nini ili umtambue mama mzazi wa Musa kuwa amejifanya tu kuwa ni Housegirl ili awe karibu na mtoto wake?

Tafakari haya maswali kwa muda kadhaa.
Halafu unijibu kadiri ya uelewa wako.

Nakusikiliza.

Mbona unatuletea ya Musa , lete ya Yesu
 
Yesu alihubiri upendo, ndiyo tofauti yake na Eliya, Eliya aliua manabii wa Baali lakini Yesu akiwa msalabani alisema "Baba uwasamehe kwa maana hawajui wanalolitenda... "

Usimdhihaki FaizaFoxy mfundishe kwa upendo. Hata Paulo kaandika muwaonye wazee kwa heshima

Yesu alihubiri kwa upendo ??

Hivi ndivyo watu wanavyohubiri kwa upendo ??



LUGHA YA YESU

Kila mti hutambulika kwa matunda yake (Luka 6:44) na vile vile mtu anatambulika kwa ulimi na lugha yake kwamba anazo tabia za aina gani?

Maana lugha ya mtu inaonesha masomo yake, tabia na vitendo vyake.

Hapa tunampima Bwana Yesu Kristo sawa na maandiko ya Biblia.

Bila ya kupoteza muda , ningependa kukuletea baadhi ya maneno na lugha ya Bwana Yesu aliyotumia katika uhai wake.

1. Wasioamini (wasio Waisraeli) wameitwa mbwa na nguruwe. (Mathayo 7:6).

2. Aliwaita watu wabaya: ”Enyi wazao wa nyoka” (Mathayo 12:34).

3. Mayahudi waliitwa: “Kizazi cha zinaa.” (Mathayo 12:40,, 16:4).

4. Mayahudi waliitwa “Wazinifu na wakosefu.” (Marko 8:38).

5. “Ole wenu waandishi na wafarisayo, wanafiki,” (Mathayo 23:16).

6. “Ole wenu viongozi vipofu.” (Mathayo 23:16).

7. “Enyi nyoka, wana wa majoka” (Mathayo 23:33).

8. “Watu wengine waliitwa mbwa.” (Mathayo 15:27).

9. Aliwaita manabii wenzake: “wote walionitangulia ni wevi na wanyang'anyi.” (Yohana 10:8).

10. Aliwaita wanafunzi wake: ”Enyi kizazi kisicho amini, kilichopotoka.” (Mathayo 17:17).

11. Akamwambia Petro “Nenda nyuma yangu Shetani.” (Mathayo 16:23).

12. Akamwambia mama yake: “Ewe mwanamke nina nini nawe? (Yohana 2:4).

13. Akasema mama yangu ni nani na ndugu zangu ni akina nani? (Mathayo 12:48).

14. Siku ya Kiyama atawaita wahubiri Wakristo: “Nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi mtendao maovu.”

(Mathayo 7:23).
 
Na dawa yake ni moja tu kwamba muingie katika dini ya Mwenyezi Mungu, ISLAM, baada ya kutambua umoja wa Mungu na Mtume Muhammad s.a.w. bila hivyo mtaendelea kufedheheka siku hadi siku.
Hahahaha,umenichekesha sana kwa hiyo line hapo kwenye bold

First of all sidhani kama nipo tayari kupokea wanawake bikra 70 na kunywa pombe peponi sijui ahera,also duniani sipo tayari kusimama kupigana vita kwa ajili ya Mungu ninaemini anaweza kila kitu nyie mliofanikiwa kuyaelewa hayo mnatosha
 
Hili ni swali tu katika kujua uweza na uwezo wa nguvu za Jina la Yesu katika kutenda miujiza.

Yesu alipata kuishi yapata miaka 2019 iliyopita. Je inakuwaje jina lake leo lisemwe kwamba lina nguvu sana katika kutenda miujiza?

Kuna manabii wengi sana na mitume wengi wamepita, kina Krishna, Elisha , Elizabeth Mtishbi nk mbona hatusikii visa vya majina yao katika kutenda miujiza? Sanasana Wlisha ametajwa mara moja kwamba jamaaa walibeba maiti wakienda kuzika, walipofika katika kaburi la Elisha ikatokea vita, katika kujinusuru wakaibwaga maiti chini, maiti ikaangukia kaburi la Elisha, maiti ikafufuka, ikatoka nduki kichizi.

Ndugu mnaoelezea uweza wa jina la Yesu njooni hapa mshuhudie
Katika uumbaji wote wa Mungu kwa uzao wa Adamu hakuna hata mmoja aliyewahi kufa na kufufuka na kupaa mbinguni bila kuuacha mwili wa nyama na damu ila Yesu peke yake.
Ndio maana anatajwa kuwa aliye hai milele.
Huu ndio muujiza uliozidi miujiza yote wa Yesu mfufuka.
Wengine wote wapo makaburini wakisubiri kiama ya wafu wafufuliwe na wachache sana wawili au watatu walitwaliwa bila kifo hivyo hawana sifa ya kukishinda kifo na mauti bali walipewa neema ya kutokugusa huo mfupa mgumu uliowashinda wengine wote.
 
Hahahaha,umenichekesha sana kwa hiyo line hapo kwenye bold

First of all sidhani kama nipo tayari kupokea wanawake bikra 70 na kunywa pombe peponi sijui ahera,also duniani sipo tayari kusimama kupigana vita kwa ajili ya Mungu ninaemini anaweza kila kitu nyie mliofanikiwa kuyaelewa hayo mnatosha

Kama unaendelea na ukristo utakuwa hata imani ndogo ya chembe ya hardali huna maana hata kuiambia kalamu ianguke kutoka kwenye meza huwezi

Mbona biblia inasema vyengine kuhusu huyo mungu unayemuabudu wewe ??


Kuna vifungu vingi katika Agano Jipya vinavyokana uungu wa Yesu.

Kwa mfano, katika Mathayo 19:17, Yesu alimjibu yule aliyemtambulisha yeye kama ni “Mwalimu mwema” kwa kusema “Akawaambia, Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja…”

Kama Yesu amekataa kuitwa “mwema”, na ameeleza kuwa ni mungu pekee ndiye aliyemwema wa kweli, naye kwa uwazi kabisa ameashiria kuwa yeye si Mungu.

Katika Yohana 14:28, yesu alikuwa anasema:

“Mlisikia ya kwamba mimi niliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahia kwa sababu naenda kwa Baba; kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.” Kwa kusema “Baba” ni mkuu kuliko yeye, Yesu amejitenganisha na Mungu.

Pia katika Yohana 20:17, Yesu alimwambia Mariam Magdalene awaambie wafuasi zake:

"Yesu akawaambia, Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu.

” Yesu amemwashiria Mungu kuwa ni “Baba yangu na Baba yenu” amesisitiza zaidi, tofauti yake na Mungu.

Zaidi ya hayo, Yesu amemwashiria Mungu kuwa ni “Mungu wake”, hakutoa nafasi kwa yoyote kudai kiujanja ujanja kuwa Yeye Yesu ndiye Mungu.

Ingawa katika baadhi ya maandiko ya Paulo, yaliyochukuliwa na kanisa kuwa ni matakatifu,

Yesu anaonyeshwa kuwa ni “mtu” ametofautiana na kutengana na Mungu.

Katika 1 Timotheo 2:5, Paulo anaandika

“Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu.”
 
Katika uumbaji wote wa Mungu kwa uzao wa Adamu hakuna hata mmoja aliyewahi kufa na kufufuka na kupaa mbinguni bila kuuacha mwili wa nyama na damu ila Yesu peke yake.
Ndio maana anatajwa kuwa aliye hai milele.
Huu ndio muujiza uliozidi miujiza yote wa Yesu mfufuka.
Wengine wote wapo makaburini wakisubiri kiama ya wafu wafufuliwe na wachache sana wawili au watatu walitwaliwa bila kifo hivyo hawana sifa ya kukishinda kifo na mauti bali walipewa neema ya kutokugusa huo mfupa mgumu uliowashinda wengine wote.
Msingi wa Ukristo siku hizi ni kifo cha msalaba cha bwana Yesu a.s. Mayahudi na Wakristo wanadhani kwamba Bwana Yesu alifariki juu ya msalaba, kifo cha laana.

A. Mayahudi walidhani hivi kwa sababu ya kupata nafasi ya kumkataa Bwana Yesu, kuwa wa kweli, maana Torati inasema kwamba “Aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu, (Kumbukumbu la Torati 21:23).

Kwahiyo Mayahudi walitaka sana kumfisha Yesu msalabani ili athibitike kuwa mlaaniwa na mlaaniwa hawezi kuwa Nabii wa Mungu.

B. Wakristo walikubali kwamba Yesu alikufa msalabani kwa sababu waliambiwa kwamba Yesu amebeba dhambi za watu kwa kufa msalabani.
Hivi wavivu wote ambao hawataki kufuata sheria ya Mungu, mara moja walikubali kwamba damu ya Yesu imetuokoa. (Wagalatia 3:13).
 
Katika uumbaji wote wa Mungu kwa uzao wa Adamu hakuna hata mmoja aliyewahi kufa na kufufuka na kupaa mbinguni bila kuuacha mwili wa nyama na damu ila Yesu peke yake.
Ndio maana anatajwa kuwa aliye hai milele.
Huu ndio muujiza uliozidi miujiza yote wa Yesu mfufuka.
Yesu alipofufuka, makaburi yakapasuka, wafu wakafufuka. Baada ya kukufuka wakafa tena au waliyeyuka hamna ajuaye walienda wapi?
 
Mathew 24


Jesus answered: “Watch out that no one deceives you.

5 For many will come in my name, claiming, ‘I am the Messiah,’ and will deceive many.
Hapo uliponi quote inahusiana nn na huu mstari?

Hao fake wako wengi tu na biblia imesema
 
Domo ni nyumba ya maneno ,

Uhuru wa kusema utakalo unao lakini ushahidi huna


Was there a Jesus? Of course there was a Jesus – many!



The archetypal Jewish hero was Joshua (the successor of Moses) otherwise known as Yehoshua (Yeshua) bin Nun (‘Jesus of the fish’). Since the name Jesus (Yeshua or Yeshu in Hebrew, Iesous in Greek, source of the English spelling) originally was a title (meaning ‘saviour’, derived from ‘Yahweh Saves’) probably every band in the Jewish resistance had its own hero figure sporting this moniker, among others.


Josephus, the first century Jewish historian mentions no fewer than nineteen different Yeshuas/Jesii, about half of them contemporaries of the supposed Christ! In his Antiquities, of the twenty-eight high priests who held office from the reign of Herod the Great to the fall of the Temple, no fewer than four bore the name Jesus: Jesus ben Phiabi, Jesus ben Sec, Jesus ben Damneus and Jesus ben Gamaliel. Even Saint Paul makes reference to a rival magician, preaching ‘another Jesus’ (2 Corinthians 11,4). The surfeit of early Jesuses includes:


Jesus ben Sirach. This Jesus was reputedly the author of the Book of Sirach (aka 'Ecclesiasticus, or the Wisdom of Jesus the Son of Sirach'), part of Old Testament Apocrypha. Ben Sirach, writing in Greek about 180 BC, brought together Jewish 'wisdom' and Homeric-style heroes.


Jesus ben Pandira. A wonder-worker during the reign of Alexander Jannaeus (106-79 BC), one of the most ruthless of the Maccabean kings. Imprudently, this Jesus launched into a career of end-time prophecy and agitation which upset the king. He met his own premature end-time by being hung on a tree – and on the eve of a Passover. Scholars have speculated this Jesus founded the Essene sect.


Jesus ben Ananias. Beginning in 62AD, this Jesus had caused disquiet in Jerusalem with a non-stop doom-laden mantra of ‘Woe to the city’. He prophesied rather vaguely:





Arrested and flogged by the Romans, Jesus ben Ananias was released as nothing more dangerous than a mad man. He died during the siege of Jerusalem from a rock hurled by a Roman catapult.


Jesus ben Saphat. In the insurrection of 68AD that wrought havoc in Galilee, this Jesus had led the rebels in Tiberias ("the leader of a seditious tumult of mariners and poor people" – Josephus, Life 12.66). When the city was about to fall to Vespasian’s legionaries he fled north to Tarichea on the Sea of Galilee.


Jesus ben Gamala. During 68/69 AD this Jesus was a leader of the ‘peace party’ in the civil war wrecking Judaea. From the walls of Jerusalem he had remonstrated with the besieging Idumeans (led by ‘James and John, sons of Susa’). It did him no good. When the Idumeans breached the walls he was put to death and his body thrown to the dogs and carrion birds.


Jesus ben Thebuth. A priest who, in the final capitulation of the upper city in 69AD, saved his own skin by surrendering the treasures of the Temple, which included two holy candlesticks, goblets of pure gold, sacred curtains and robes of the high priests. The booty figured prominently in the Triumph held for Vespasian and his son Titus.
Naona umetoka nje ya mada
Ulichojibu na nilichosrema vitu viwili tofauti
Sina muda wa kupoteza
 
YESU MWENYEWE ANASEMA hawezi kufanya chochote


John 5:30


By myself I can do nothing; I judge only as I hear, and my judgment is just, for I seek not to please myself but him who sent me.
Whatever you ask in my name........John 16:23
 
Whatever you ask in my name........John 16:23

Sasa unaamini yapi maneno ya kweli ?? John 16 :23 au John 5:30 ??

halafu imeanzia John 16 : 19 imeandikwa

Jesus saw that they wanted to ask him about this, so he said to them ....

Hapo anayetupa habari za Yesu ni nani ??
 
Sasa unaamini yapi maneno ya kweli ?? John 16 :23 au John 5:30 ??

halafu imeanzia John 16 : 19 imeandikwa

Jesus saw that they wanted to ask him about this, so he said to them ....

Hapo anayetupa habari za Yesu ni nani ??
Mie nakupa POLE
 
Warumi 10:17
Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.
 
Mie nakupa POLE
Nimeipokea pole yako sasa jibu hoja

Sasa unaamini yapi maneno ya kweli ?? John 16 :23 au John 5:30 ??

halafu imeanzia John 16 : 19 imeandikwa

Jesus saw that they wanted to ask him about this, so he said to them ....

Hapo anayetupa habari za Yesu ni nani ??
 
Warumi 10:17
Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.

Anayesema maneno hayo anaendelea kusema

Warumi 7

14. Tunafahamu kwamba sheria ni ya kiroho. Lakini mimi si wa kiroho; mimi nimeuzwa utumwani, ni mtumwa wa dhambi.

15 Sielewi nitendalo: kwa maana lile ninalotaka kulifanya, sifanyi; badala yake, ninafanya lile ambalo nachukia kulifanya.
 
Back
Top Bottom