Je, Kiusalama na Kiulinzi hiki ninachokiona sasa huku nchini Puerto Rico si hatari kwa Rais wetu?

Je, Kiusalama na Kiulinzi hiki ninachokiona sasa huku nchini Puerto Rico si hatari kwa Rais wetu?

Huyo Rais wa Puerta Rica labda ana maadui wengi ila sijui technolojia za huko Puerta Rica maana watunguaji huwa si watu wa mchezo...... Ulinzi huo kidogo ufanane wa huku niliko.......
 
Je Kiusalama na Kiulinzi ni ' afya ' kwa Kiongozi yoyote yule wa nchi kulindwa na askari waliobeba silaha kali na nzito popote pale anapokuwa au hasa akiwa katika halaiki ya Watu? Na kama ni sahihi je hawa Walinzi wanaoonekana wamebeba hizi ' silaha ' nzito wanaaminika vipi na Wenzao waliopo kuwa labda hawawezi ' kugeuka ' nyuma au wale waliopo nyuma hawawezi ' kumshambulia ' Kiongozi wetu?

Nitafurahi sana endapo nitajibiwa haya maswali yangu kwani kwa siku za hivi karibuni namuona sana Rais wa huku nilipo nchini Puerto Rico ' akilindwa ' namna hiyo hivyo nikaona si vibaya nikiwauliza ' Wabobezi ' wa masuala ya Kiulinzi na Kiusalama mliopo huko Tanzania mnisaidie kunifafanulia Kitaaluma na Kiueledi kabisa.

Nawasilisha na karibuni mno nchini Puerto Rico wana JF.


Mahali Rais anapokuwa Usalama umeimarishwa...usione wale tuu waliobeba silaha...bali wapo waliovaa kiraia na hawajulikani.

Pia kwa nyie ambao si watu wa usalama ni vigumu sana kuyafahamu haya hivyo waachieni wenyewe...Ya kaisare muachie kaisare ...wewe fanya la taaluma yako...
 
Kweli bongo vilaza wengi , yani wanashindwa kuielewa nch ya "Puerto Rico" mtoa mada aliyoimaanisha.

Mkuu hata mimi naish Puerto Rico , nilijiuliza swali hili nikakosa jibu, labda ni maagizo ya mwenyew kiongoz wetu Puerto Rico.
Hao ndio watu wanashiriki kuchagua viongozi, fumbo dogo tu wameshindwa kuelewa, tuna safari ndefu sana.
 
akina Netanyahu wakilindwa na masilaha waziwazi mnapongeza kuwa ni ulinzi makini, kisa tanzania mnahoji? ushamba unawaponza mlikariri zamani saivi full security makanjanja nyie!!
 
Thread zinazohusu mambo nyeti ya taifa ndizo zinazosababisha viongozi wa jf kusumbuliwa mara kwa mara, endeleeeni tu!!!
 
Mimi nilielewa anawapa Kiki jamaa wa kibiti,watajiona wako imara mpaka presida anajipanga
 
GENTAMYCINE. Mkuu ni hatari tena kubwa sana usalama wa Taifa ndio wanatakiwa kwa wingi maana wao ndio wamepata mafunzo ya kiuweredi kumlinda kiongozi wa inch Rais.
Sijui usalama wa Taifa hawaoni tatizo hususani kipindi hiki kigumu cha walio wengi wameathirika na wapendwa wao ndgg kufukuzwa kazi, ama wao kubomolewa nyumba.
Usalama wa Taifa watatumia uweredi wao kuliona tatizo hili kubwa.
 
GENTAMYCINE. Mkuu ni hatari tena kubwa sana usalama wa Taifa ndio wanatakiwa kwa wingi maana wao ndio wamepata mafunzo ya kiuweredi kumlinda kiongozi wa inch Rais.
Sijui usalama wa Taifa hawaoni tatizo hususani kipindi hiki kigumu cha walio wengi wameathirika na wapendwa wao ndgg kufukuzwa kazi, ama wao kubomolewa nyumba.
Usalama wa Taifa watatumia uweredi wao kuliona tatizo hili kubwa.
 
Mpeni jibu kama mnajua acheni ushamba, kwani Poerto Rico si Nchi tu kama Nchi nyingine kipi cha ajabu yeye kuwa huko? That's childish.
 
akina Netanyahu wakilindwa na masilaha waziwazi mnapongeza kuwa ni ulinzi makini, kisa tanzania mnahoji? ushamba unawaponza mlikariri zamani saivi full security makanjanja nyie!!

Katika ' uzi ' wangu kuna mahala popote nimeitaja Tanzania au hata kumuhusisha Rais wa huko Kwenu Tanzania? Pumbavu.
 
GENTAMYCINE. Mkuu ni hatari tena kubwa sana usalama wa Taifa ndio wanatakiwa kwa wingi maana wao ndio wamepata mafunzo ya kiuweredi kumlinda kiongozi wa inch Rais.
Sijui usalama wa Taifa hawaoni tatizo hususani kipindi hiki kigumu cha walio wengi wameathirika na wapendwa wao ndgg kufukuzwa kazi, ama wao kubomolewa nyumba.
Usalama wa Taifa watatumia uweredi wao kuliona tatizo hili kubwa.

Ni wapi katika ' uzi ' wangu nimewahusisha Usalama wa Taifa wa huko Kwenu Tanzania? Mimi nipo huku Kwetu nchini Puerto Rico na nimeanzisha huu ' uzi ' baada ya kila mara kumuona Rais wetu huku akiwa na ' Ulinzi ' mkali sana hadi sisi ' Raia ' sasa tunaogopa.
 
Poerto Rico si ndiko juzi wamepiga kura za maoni ili kuwa jimbo la 51 la Marekani?

Huyo Raisi atakuwa Gavana wa kawaida kama walivyokuwa akina Arnold Schwarzenegger hivi karibuni.

Ila Poerto Rico ina sifa za kutukuka kwenye ndonga au masumbwi, mabondia kama akina Felix Tridad "Tito", Hector Camacho na huyu nguli kabisa mtaalamu Miguel Cotto alipigana mapambano ya kutukuka na akina Floyd Maywether, Man Pac, Shane Mosley 'Sugar', bila kusahau kisasi cha karne kwa Margarito wa Mexico.
 
Back
Top Bottom