Je, kweli ni bora kuamini Mungu yupo halafu siku ya mwisho usimkute, kuliko kutoamini halafu ukamkuta?

Je, kweli ni bora kuamini Mungu yupo halafu siku ya mwisho usimkute, kuliko kutoamini halafu ukamkuta?

Scars

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2017
Posts
48,055
Reaction score
116,512
Makala hii nitaiweka kwa vipande kuepusha kero ya usomaji.

Moja ya hoja maarufu kutoka kwa watu wanaoamini Mungu (Theists).

Ni hoja ambayo imelenga kuweka matumaini ya mwelekeo katika maisha ili kuwafanya watu waone kuamini Mungu yupo ndio uchaguzi bora zaidi (rational) kwasababu haitakupa matokeo mabaya mwishoni.

Hii ni Analogy iliyopata sana umaarufu miaka ya 1640s na muazilishi aitwaye Pascal Wager.

Huyu jamaa alihoji kuwa ni vyema ukaamini kuwa Mungu yupo ukafa na usimkute kuliko kutokuamini halafu ukafa ukamkuta.

Pascal analaani kuwa kuamini kuwepo kwa Mungu ni tendo la busara zaidi kuliko kutokuamini kuwepo kwake, hata kama hatuna uhakika kuhusu kuwepo kwake. Hii ni kwasababu zifuatazo.

  1. Kama Mungu yupo na tutamwabudu, tutapata thawabu ya milele (kama ushindi mkubwa).
  2. Lakini kama Mungu hayupo na hatumwamini, hatutapata chochote (kama hasara ndogo).
  3. Kwa upande mwingine, kama Mungu yupo na hatumwamini, tutapata adhabu ya milele (hasara kubwa).
  4. Lakini kama Mungu hayupo na hatumwamini, hatutapata chochote (ushindi mdogo).

Hivyo, Pascal anasema kwamba kuamini kuwepo kwa Mungu ni tendo la busara zaidi, kwasababu unaweza kupata thawabu ya milele na kuepuka adhabu ya milele, hata kama hatuna uhakika kuhusu kuwepo kwake.

Swali: Je Atheists hawatuogopi siku ya mwisho kukutana na hukumu ya Mungu na kutupwa kwenye moto wa milele?

Hatuogopi kubaini kuwa hadithi za mitume zinazosimuliwa kuhusu Yesu na Muhammad kuwa ni za kweli na kwamba tumepoteza nafasi ya kuishi maisha ya milele peponi kwa kutoamini?

Je isingekuwa vyema Atheists kuwa upande salama wa kumuamini Yesu, Muhammad na Mungu kama backup just in case?
 
Haijalishi kuna njia ngapi za ku-make hiyo analogy ila bado haibadilishi maana kuwa ni swali la kijinga.

Ni swali la kijinga ambalo limekuwa likiulizwa na watu wa dini kwa zaidi ya miaka 300

Unajua kwanini?

Let's say kwamba ni kweli Atheists tumekosea kuhusu kila kitu na tukifa tutakutana na Mungu mwenye hasira ambaye ameahidi kuwapeleka motoni wateseke milele wale wote wasiomuamini.

Of course, hilo ni jambo linaloweza kutegemewa kuliona likifanywa na baba mwenye upendo wote kwa watoto wake ambao wamemkosea adabu?

So kwa mafikirio hayo ni kweli tunapaswa kubadili mitizamo kwa kugeuka kuwa waumini??

Kwanini woga wa adhabu ya kufikirika au woga wa kukosa zawadi (pepo) ya kufikirika itufanye sisi tuamini hivyo vitu?

Haya nanyie Theists jaribuni hii...

Wamisri wakale waliamini kwamba ukifa nafsi yako itahukumiwa na Anubis ambaye ni Mungu wa kifo.
1734357215309.png


Utaulizwa maswali kwa kutaja majina 42 ya Assessors of Maat kwa ufasaha huku ukitaja madhambi yao ambayo hawakuwahi kuyafanya katika kipindi cha uhai wao

Baada ya kutoka hapo utapimwa uzito wa moyo wako kwa kuwekwa kwenye mzani ambao itabidi uwe balanced na unyoya.
1734357400349.png


Ikiwa moyo wako utaonekana kuwa mzito kuliko unyoya basi moyo wako utasambaratishwa na kuliwa na Mungu aitwaye Ammit.
1734357444068.png

Sasa ushajua hatima inayokusubiri ikiwa hautaamini hizi habari. Je tayari ushaanza kuwa muumini wa Anubis?
 
Lakini pia kumbukeni na hii.

Mamilioni ya waamini Mormon (members of the Church of Jesus Christ of Latter-day Saints) wanashawishi watu kuwa Kanisa lao pekee ndio la kweli.
1734357891021.png


Na ndio kanisa pekee ambalo linaishi katika uso huu wa dunia.

Kwa njia ya kubatizwa ndani ya hilo kanisa pamoja na kufuata miongozo ya kanisa pekee ndio kunaweza kukufanya uungane na familia yako milele.

Sasa je mafikirio ya kutoweza kuungana na familia yako baada ya kifo ndio yanayofanya uanze kuamini kuwa Joseph Smith alimuona Mungu na Yesu??

Kama wewe ni Mkristo, unatambua kuwa katika ulimwengu wa kiroho kwenye uislamu wanaamini kwamba Muhammed ndio nabii wa mwisho wa Mungu?

Na kwa hilo unapaswa kufuata mafundisho yote yaliyoandikwa katika Quran tukufu, kwa kufanya hivyo utakuwa umeepuka moto na kuzawadiwa bikra 72 peponi.

Ukipuuza au kubagua mafundisho ya Quran utajikuta kwenye adhabu ya kaburi huku ukisubiriwa kumaliziwa kwenye jehanam yenyewe.

Niambie ushakuwa convinced kuwa muumini wa Kiislamu kwasababu tayari umejua hatima yako iwapo utakaidi kuwa muislamu?

Na kama wewe ni Muislam, kwa namna nyingine unatambua kuwa wakristo wanaamini wokovu unawezekana kupitia upatanisho wa sadaka ya kifo cha Yesu aliyefia msalabani?

Na wote wasioamini kuhusu uungu wa Yesu watachomwa moto wa milele. Sasa kwa kuyajua hayo, kuna namna yeyote inayoweza kukufanya uwe mkristo??

Vipi kama tukiwaambia kuwa miaka 20 ijayo jua linaenda kulipuka unless utoe 30% ya pesa zako zote kuanzia sasa?

Hupendi jua lilipuke sindio? je hiyo inafanya uamini?

Serious unauliza Atheists vipi kama wapo wrong as if ni kama wewe upo kwenye mstari sahihi, vipi kama na wewe upo wrong?

Fact inayofanya uone haupo sahihi, inaweza kukufanya ukaamini kitu kingine?
 
Kujua ni bora zaidi kuliko kuamini.

Kwa nini huyo Mungu ajifiche na aachie watu wakisie uwepo wake ilhali angeweza tu kujitokeza na wote tukamjua?
Wanasema Mungu ni roho yupo kila sehemu ila haonekani kwasababu hana mwili.

Ila ukumbuke huyo huyo Mungu anayetajwa kuwa hana mwili ana jinsia ya kiume na ukifanya mocking kwa kumuita mwanamke utakumbana na ghadhabu za waumini kuwa umemdhalilisha Mungu wao.

Huyo huyo Mungu ambaye hana material body ana makazi yake huko juu yanaitwa Mbinguni, and just in case ukumbuke kuwa huko juu sio kama amesimama wima hapana maandiko yanasema ameketi kwenye kiti cha enzi kwa ajili ya kutu-monitor sisi. That means he's got a butt too.

But when it comes to evidence he disappears like poof.
 
Wanasema Mungu ni roho yupo kila sehemu ila haonekani kwasababu hana mwili.

Ila ukumbuke huyo huyo Mungu anayetajwa kuwa hana mwili ana jinsia ya kiume na ukifanya mocking kwa kumuita mwanamke utakumbana na ghadhabu za waumini kuwa umemdhalilisha Mungu wao.

Huyo huyo Mungu ambaye hana material body ana makazi yake huko juu yanaitwa Mbinguni, and just in case ukumbuke kuwa huko juu sio kama amesimama wima hapana maandiko yanasema ameketi kwenye kiti cha enzi kwa ajili ya kutu-monitor sisi. That means he's got a butt too.

But when it comes to evidence he disappears like poof.
Kama yupo kila sehemu kwa nini anaachia watoto wa kule Gaza wauliwe na wengine kupewa vilema vya maisha?
 
Lakini pia kumbukeni na hii.

Mamilioni ya waamini Mormon (members of the Church of Jesus Christ of Latter-day Saints) wanashawishi watu kuwa Kanisa lao pekee ndio la kweli.
View attachment 3178079

Na ndio kanisa pekee ambalo linaishi katika uso huu wa dunia.

Kwa njia ya kubatizwa ndani ya hilo kanisa pamoja na kufuata miongozo ya kanisa pekee ndio kunaweza kukufanya uungane na familia yako milele.

Sasa je mafikirio ya kutoweza kuungana na familia yako baada ya kifo ndio yanayofanya uanze kuamini kuwa Joseph Smith alimuona Mungu na Yesu??

Kama wewe ni Mkristo, unatambua kuwa katika ulimwengu wa kiroho kwenye uislamu wanaamini kwamba Muhammed ndio nabii wa mwisho wa Mungu?

Na kwa hilo unapaswa kufuata mafundisho yote yaliyoandikwa katika Quran tukufu, kwa kufanya hivyo utakuwa umeepuka moto na kuzawadiwa bikra 72 peponi.

Ukipuuza au kubagua mafundisho ya Quran utajikuta kwenye adhabu ya kaburi huku ukisubiriwa kumaliziwa kwenye jehanam yenyewe.

Niambie ushakuwa convinced kuwa muumini wa Kiislamu kwasababu tayari umejua hatima yako iwapo utakaidi kuwa muislamu?

Na kama wewe ni Muislam, kwa namna nyingine unatambua kuwa wakristo wanaamini wokovu unawezekana kupitia upatanisho wa sadaka ya kifo cha Yesu aliyefia msalabani?

Na wote wasioamini kuhusu uungu wa Yesu watachomwa moto wa milele. Sasa kwa kuyajua hayo, kuna namna yeyote inayoweza kukufanya uwe mkristo??

Vipi kama tukiwaambia kuwa miaka 20 ijayo jua linaenda kulipuka unless utoe 30% ya pesa zako zote kuanzia sasa?

Hupendi jua lilipuke sindio? je hiyo inafanya uamini?

Serious unauliza Atheists vipi kama wapo wrong as if ni kama wewe upo kwenye mstari sahihi, vipi kama na wewe upo wrong?

Fact inayofanya uone haupo sahihi, inaweza kukufanya ukaamini kitu kingine?
Kwa andiko hili inamaana itakuwa sawa kama kila mtu atabaki kwenye anachokiamini.
 
Haya maneno ya Marcus Aurelius ni mazuri sana;

"Live a good life. If there are gods and they are just, then they will not care how devout you have been, but will welcome you based on the virtues you have lived by. If there are gods, but unjust, then you should not want to worship them. If there are no gods, then you will be gone, but will have lived a noble life that will live on in the memories of your loved ones.”
 
Kujua ni bora zaidi kuliko kuamini.

Kwa nini huyo Mungu ajifiche na aachie watu wakisie uwepo wake ilhali angeweza tu kujitokeza na wote tukamjua?
...Hata wapumbavu huzeeka , usitegemee hekima kuikuta humo . Ndo wewe sasa umri mkubwa lakini unajizima Wi-Fi.

Kuhusu uwepo wa Mungu , Ni sawa na kumwaminisha mtu duni Sana anayeishi kijijini ndani ndani Huko kwamba Kuna watu hapa nchini Ni matajiri wakutupwa.

Kutokana na fikra zake na mazingira magumu ya kijijini ataamini Ni story tu za kusadikika , lakini haimanishi Hakuna matajiri , isipokuwa Ni yeye hawajui au hajashuhudia.

Ndo kwako wewe , miaka yote umekuwa namba moja kukosoa kumuhusu Mungu lakini kwa bahati nzuri Mungu anawapenda hata wamchukiao Kama wewe.

Uamini au usiamini haifanyi Mungu kutokuwepo. Mpumbavu husema moyoni mwake Hakuna MUNGU.
 
Makala hii nitaiweka kwa vipande kuepusha kero ya usomaji.

Moja ya hoja maarufu kutoka kwa watu wanaoamini Mungu (Theists).

Ni hoja ambayo imelenga kuweka matumaini ya mwelekeo katika maisha ili kuwafanya watu waone kuamini Mungu yupo ndio uchaguzi bora zaidi (rational) kwasababu haitakupa matokeo mabaya mwishoni.

Hii ni Analogy iliyopata sana umaarufu miaka ya 1640s na muazilishi aitwaye Pascal Wager.

Huyu jamaa alihoji kuwa ni vyema ukaamini kuwa Mungu yupo ukafa na usimkute kuliko kutokuamini halafu ukafa ukamkuta.

Pascal analaani kuwa kuamini kuwepo kwa Mungu ni tendo la busara zaidi kuliko kutokuamini kuwepo kwake, hata kama hatuna uhakika kuhusu kuwepo kwake. Hii ni kwasababu zifuatazo.

  1. Kama Mungu yupo na tutamwabudu, tutapata thawabu ya milele (kama ushindi mkubwa).
  2. Lakini kama Mungu hayupo na hatumwamini, hatutapata chochote (kama hasara ndogo).
  3. Kwa upande mwingine, kama Mungu yupo na hatumwamini, tutapata adhabu ya milele (hasara kubwa).
  4. Lakini kama Mungu hayupo na hatumwamini, hatutapata chochote (ushindi mdogo).

Hivyo, Pascal anasema kwamba kuamini kuwepo kwa Mungu ni tendo la busara zaidi, kwasababu unaweza kupata thawabu ya milele na kuepuka adhabu ya milele, hata kama hatuna uhakika kuhusu kuwepo kwake.

Swali: Je Atheists hawatuogopi siku ya mwisho kukutana na hukumu ya Mungu na kutupwa kwenye moto wa milele?

Hatuogopi kubaini kuwa hadithi za mitume zinazosimuliwa kuhusu Yesu na Muhammad kuwa ni za kweli na kwamba tumepoteza nafasi ya kuishi maisha ya milele peponi kwa kutoamini?

Je isingekuwa vyema Atheists kuwa upande salama wa kumuamini Yesu, Muhammad na Mungu kama backup just in case?
Kwa nini uhitaji kuamini Mungu yupo Badala ya kujua yupo?

Huyo Mungu kama yupo kwa nini anataka aaminiwe yupo, Badala ya kujulikana yupo kwa uhakika na uthibitisho?

Kama huyo Mungu yupo kwa nini anajificha ili aaminike yupo?

Kwa nini asijitokeze hadharani akajulikana yupo na kila mtu akajua yupo kwa uhakika kabisa, Bila utata na utofauti wa kiimani?

Huyo Mungu kama yupo anastahili bakora kabisa maana inaonekana hajielewi kabisa.

Yani anajificha halafu anataka sisi tuhangaike kumwamini na kumtafuta!!

Kwani sisi binadamu tukisha mwamini huyo Mungu, Yeye anafaidika nini?

Kama huyo Mungu yupo na alitaka aaminiwe yupo, Alishindwaje kuumba binadamu wenye imani ya kumwamini yupo siku zote?

Kama Mungu yupo na alitaka aaminiwe yupo na kila mtu, Na ni Mungu mwenye kujua yote tangu mwanzo na hata milele, Je HAKUJUA kwamba kuna watu watakuja kutokumwamini, Awadhibiti na kuwa angamiza mapema?
 
Aiseee!!

Kwanza natamani nikutane na huyo Mungu tufanye mjadala mkali.

Maana nina maswali mengi sana ya kumhoji na kujua uwezo wake wa kufikiri kama uko sawasawa kweli?

Na kama kweli yupo nitahitaji anipe majibu ya kueleweka.

Maana haiwezekani aumbe viumbe vije viteseke duniani, Halafu yeye anakula bata huko mbinguni halafu akiombwa aje atoe msaada japo kidogo hapa duniani haonekani kwenye jambo lolote kusaidia.

Watu wanazidi kuteseka na kuumia tu.

Sasa kama kweli Mungu yupo, Alituumba kwa nini?

Aje atutese duniani, Halafu baadae ndio tuje kui enjoy mbinguni!!!

Hivi hii ni akili ya namna gani kama sio makusudi haya?

Yani unaumba kiumbe ukitese kwanza, Halafu baadae ndio uje ukipe raha!!

Hivi hii ni akili au matope
Yani kama huyo Mungu yupo,

Anastahili kufurushwa kabisa maana hajielewi kabisa.
 
Back
Top Bottom