Je, maneno na watu wa kibiblia kwenye Qurani ni Copypaste za kwenye Biblia?

Nasoma biblia ya kiswahili( suv).
Ninasoma Msaafu wa kiswahili (Tafsiri ya barwan)

Tafsiri au matoleo mengine yote ya biblia na quran kwa lugha zozote zile huwa natumia kama reference ili kutanua ufahamu.

Ila tukirudi kwenye mada. Visa na majina yanayozungumziwa yanapatikana katika version na tafsiri zote za biblia na quran.

Karibu sana mkuu.
 
Hii ndio ninajua. Ila waislam wanaaminishwa Yesu aliandika kitabu ambacho wao wenyewe hawana wala hakipo. Hii ni njama yq kuvizunguka vitabu vinne vya injili ili wapate sababu ya kuvishusha hadi waseme vimekosewa.
Mkiambiwa yesu au Ibrahim alikuja na kitabu mnadhani ni kuandika mwenyewe!?..ni wahyi/ufunuo ambayo ni maagizo ya Mungu kumwambia aseme nini kwa watu
 
Hakuna taurat kwenye biblia,Kuna kumbukumbu la taurati
Kwani hujawahi kusikia torati ya Musa kwenye maandiko mengine ya Biblia?

Iko hivi, Kitabu kinachoitwa Kumbukumbu la torati kinaitwa hivyo kwa sababu sio kitabu original kilichoandikwa na Musa bali ni kumbukumbu ya walioisoma torati ya Musa. Na ndio maana ukisoma maandiko yake utaona yanasema Musa akasema, au Musa akafanya nk. Inasadikika vitabu vilivyoandikwa kwa mkono wa Musa vilipotea vyote, hivyo vitabu vyote vya Musa unavyovisoma kwenye Biblia ni kumbukumbu ya maandiko ya Musa na sio maandiko original ya Musa.
 
Kisa Cha daudi kumla mke wa askari wake kipo kote!?..kisa Cha Mungu kushuka usiku mzigo watu wamelala akapigana na yakobo kipo kote!?..Mungu wa kwenye biblia anayebondwa na viumbe wake ndiyo Mungu wa kwenye QUR'AN!?
 
Ndiyo maana nikakwambia hakuna taurati kwenye biblia,huwezi tegemea kumbukumbu za watu na useme haya ndiyo Yale maneno ya Mungu wa Musa
 
ebu nitajie ukoo wa yesu kwa baba yake.au taja jina la baba yake
ukoo wa YESU KRISTO UPO kitabu cha Mathayo unaweza kuendelea hapa mwenyewe
ebu nitajie ukoo wa yesu kwa baba yake.au taja jina la baba yake
ukoo wa issa uko wap usikimbie tafafhal nisaidie na huyo mariamu alizaa na nani aliyempa mimba
 

Attachments

  • Screenshot_20230911-193809_Biblia.jpg
    81.5 KB · Views: 1
Kisa Cha daudi kumla mke wa askari wake kipo kote!?..kisa Cha Mungu kushuka usiku mzigo watu wamelala akapigana na yakobo kipo kote!?..Mungu wa kwenye biblia anayebondwa na viumbe wake ndiyo Mungu wa kwenye QUR'AN!?
Hujui msingi au mindset ya uandishi wa quran na ile iliyotumiwa kuandika biblia.
Hii ni mada nyingine nitaileta kama nitaona inafaa.

Nazungumzia vyote vilivyomo kwenye Quran na majina yaliyomo yenye ufanano hata wa kupapasa wa maandishi yaliyokuwepo zaidi ya miaka 500 kqbla ya quran.
 
120 kati ya wayahudi wangapi!?..waliomfitini wakitaka asulibiwe na kuuawa walikua akina nani!?..ikiwa Pana maandishi kwamba alihutubia watu elfu tano(bila microphone),hiyo 120 siyo negligible kwa idadi ya wayahudi wote!?..kwa nini aliahidi atakuja mkweli mwaminifu kuja kuwafundisha ambaye hatonena kwa mapenzi yake Bali ya Baba ikiwa alikubalika na alimaliza ujumbe!?
 
Ndiyo maana nikakwambia hakuna taurati kwenye biblia,huwezi tegemea kumbukumbu za watu na useme haya ndiyo Yale maneno ya Mungu wa

Deuteronomy _ repetation of the law.
Au marudio ya ileile torati.

Upajipotosha wa uelewa uliopachikiwa kingo.
 
Biblia ilikuwepo kabla ya uwepo wa yesu,agano la kale ni wahuni wamechanganya maandiko ya kale ya wayahudi na yao,agano jipya Kuna wahuni waliamua kuunda Imani yao yesu akiwa ingredient kuu,Imani ya kihunihuni ambayo Wala yesu haijui
 
Deuteronomy _ repetation of the law.
Au marudio ya ileile torati.

Upajipotosha wa uelewa uliopachikiwa kingo.
Torah ni neno la kiebrania linalomaanisha sheria, kiarabu taurati,watafsiri wa biblia wakaamua Waite kumbukumbu la taurati kwa kuwa taurati wahuni walikusanya wakati moto
 
Tunaangalia ratio.
Nani aliyekataliwa na wengi ili tufute vitabu.
Musa waisrael wote sio wayahudi tu kasoro 2.
Yesu Waisrael tena wachache tu waliokuwa uyahudi maana wengi walikuwa wametawanyika sehemu mbalimbali.

Pia hujazungumzia uwezo wa Allah kushindwa kutunza injil ya issa isiichezewe na wayahudi lakini katunza injil ya Muhammad isiharibiwe na waarabu.
 
Injili ni ya issa a.s, Muhammad saw yake ni Qur'an,Dawood ni zaburi,huwezi sema injili ya Dawood...issa a.s na injili yake ilikua kwa ajili ya Wana wa Israel Kama Qur'an inavyosema na yesu mwenyewe 'sikutumwa Ila kwa kondoo waliopotea wa Israel'....'je waweza chukua chakula Cha watoto na kumpa mbwa'.... Allah sw hakuamua tu vitabu vyake vya nyuma vitiwe mikono Bali aliacha pia hata manabii wake wakauawa,anafanya atakavyo,hakuna wa kumpangia
 
Kabla ya kuanza kwa uislam dini ya ukatoliki ilikuwepo tayari Duniani miaka mia tano
Jibu swali Jesuit imeanzishwa lini na mtume kafariki lini!?..si mnadai Jesuit ndiyo wameunda uislam..msivyo na akili ya kutafakari hamjiulizi mbona katoliki wenyewe wanahaha kuua uislam,na huo uislam mbona kiitikadi unapinga kabisa ukiristo na kutoa kasoro!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…