GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Kwa Posho au hili ulikuwa hulijui Mkuu?Inabidi achunguzwe na aondolewe madarakani. Anaishije?
Najua, ila tafsiri yake analipwa posho nyingi kuliko mshahara na huo ni ufisadi.Kwa Posho au hili ulikuwa hulijui Mkuu?
Kama hujui ukiwa raisi hadi chupi unanunuliwa we ni hatari kabisaInabidi achunguzwe na aondolewe madarakani. Anaishije?
Posho anazopata kwa mwezi unajua ni kiasi gani?Kwa Posho au hili ulikuwa hulijui Mkuu?
Ulipomtaja Rais wangu Kipenzi kwa sasa Afrika 'Genius' Paul Kagame umenifurahisha sana, ila ungenitajia Yule 'Goigoi' mwingine kutokea nchi niliyoisahau kwa sasa hakika ningekudharau mno.Hon. Hakainde Hichilema tungempata huku kwetu na hizi rasmali zote tulizo nazo tungekuwa mbali, achana na huyu anayewasogeza na kuwakumbatia mafisadi na kuwasahau wananchi wa hali ya chini.
Juzi naona Hon. Paul Kagame kaenda kumtembelea na watasaini mikataba zaidi ya nane kwa manufaa ya nchi zao.
Yaani mpaka Hon. Paul Kagame ameenda kumtembelea jua ya kwamba Hon. Hakainde ni level nyingine kwenye kutumia akili yake aliyojaliwa na Mungu, huyu wetu kutwa nzima kushinda kwenye vioo kupaka picco.
Swali dogo kwako uko radhi kutumwa mahali kikazi lets say unaenda mkoa tofouti na kituo chako cha kazi kwa sharti la kutumia mshahara wako binafsi pasipo posho??Posho anazopata kwa mwezi unajua ni kiasi gani?
Unaweza kuta ingekua heri apokee mshahara akatae posho.
Nahisi posho kwa maraisi ni pesa nyingi kwa mwezi kuliko mshahara.
Smtz mwanasiasa unatakiwa uwe na vijitekiniki kama hivi ili iwe rahisi kurudi madarakani.
Kulipwa Posho nyingi ni Ufisadi? Kwani hizo Posho anazolipwa hazipo Kisheria? Na je, amejitungia Yeye? Posho huwa zinazidi Mishahara?Najua, ila tafsiri yake analipwa posho nyingi kuliko mshahara na huo ni ufisadi.
Precisely Chief.Kama hujui ukiwa raisi hadi chupi unanunuliwa we ni hatari kabisa
Acha kuwauliza Maswali magumu Watu wenye Uvivu mkubwa wa Kufikiri tafadhali. Hili Swali lako kwa IQ yake 'Kiduchu' nina uhakika hawezi Kukujibu unavyotaka au inavyotakiwa na kama huamini subiri uone atakavyokujibu.Swali dogo kwako uko radhi kutumwa mahali kikazi lets say unaenda mkoa tofouti na kituo chako cha kazi kwa sharti la kutumia mshahara wako binafsi pasipo posho??
Hivi nchini Kwenu sasa hivi kuna Rais?Muda huo huo hapa nyumbani
Serikali yetu ipo busy kuhakikisha kuwa maisha ya Mtanzania yanakua magumu kila siku.
Kwanza walibadili bei ya kuunganishwa umeme toka elfu 27 mpaka laki tatu. Zanzibar imebakia ile ile.
Pili wakawafukuza kila mahali wamachinga. Zanzibar wameboreshewa vitambulisho vyao ili wakopesheke.
Tatu wakaondoa kiasi cha shs mia kwenye mafuta na kuirejesha tena kipindi ambacho bei ya mafuta imepanda. Hapa ukali wa bei umeongezeka mara mbili.
Nne hakuna mradi hata mmoja wa kimkakati uliokamilika wala hakuna jitihada za wazi na za dhati kuhakikisha inakamilika.
Tano ongezeko la mikopo isiyokuwa na tija inayopelekwa katika miradi ambayo haileti faida.
Sita kuanzishwa kwa tozo juu ya kodi jambo linalofanya mwananchi alipe kodi mara mbili kwa huduma moja.
Unabaki kujiuliza nia halisi ya serikali hii ni nini??
Je kuna jambo sisi wananchi tumeikosea serikali hii??
Sasa marupurupu ni mara bilioni ya mshahara, mshahara wa kazi gani sasa?Rais wa Zambia Mheshimiwa Hakainde Hichilema hajapokea Mshahara wake kutokana na hali Ngumu ya Kiuchumi kwa Miezi Nane iliyopita tokea aingie Madarakani.
Chanzo: Radio One Taarifa ya Habari Asubuhi hii.
Je, unadhani na Marais wengine unaowajua Weww hapa Barani Afrika wangekuwa na Uthubutu huu wa Kizalendo kabisa kama alionao huyu Rais wa Zambia?
Kuna Mmoja tu ninamjua asingekubali.
Kama ameweza kuacha mshahara akachukua posho kama ishara ya uzalendo,iweje iwe ajabu kuacha kuchukua posho akachukua mshahara?Swali dogo kwako uko radhi kutumwa mahali kikazi lets say unaenda mkoa tofouti na kituo chako cha kazi kwa sharti la kutumia mshahara wako binafsi pasipo posho??
Kiongozi mzuri ni yule ambaye anaongozwa na misingi ya haki na utawala bora. Sheria siyo msahafu au biblia, sheria inaweza kuwa mbaya au kandamizi. Issue ni kwamba kuwa na posho kubwa kuliko mshahara ni matakwa ya utawala bora? Kama siyo, kukiwa na sheria wezeshi wewe kama Raisi mzalendo unachukua hatua gani? Mkuu bado sijaanza kutumia akili zangu, embu tafakari hili.Kulipwa Posho nyingi ni Ufisadi? Kwani hizo Posho anazolipwa hazipo Kisheria? Na je, amejitungia Yeye? Posho huwa zinazidi Mishahara?
Jamani sometimes tujaribu kutumia vyema Akili zetu tulizopewa bure na Mwenyezi Mungu kwa Kufikiri vyema tuwapo hapa Jamiiforums sawa?