Je, Mtoto aliyezaliwa nje ya Ndoa anafaa kuitwa Jina la ubini la Baba yake?

Je, Mtoto aliyezaliwa nje ya Ndoa anafaa kuitwa Jina la ubini la Baba yake?

Kwa mujibu wa imani ya kiislamu mtoto ambaye amezaliwa nje ya ndoa hatambuliki Kwa mujibu wa Sheria kama mtoto wa Baba husika.

Kwasababu kizazi au uzao WA familia unatakiwa upatikane ndani ya ndoa ya kisheria au ndoa iliyofungwa Kwa misingi ya Dini,na nje ya hapo huyo ni mtoto wa zinaa ambaye kisheria anatambulika kama mtoto wa mama aliye mzaa Tu.

Ingawa kikawaida atafahamika kama mtoto wa Baba Fulani lkn kidini huyo Baba hatambuliki na hivyo kuna haki Fulani ambazo Baba hawezi kumfanyia mtoto wake.

Moja wapo ni huyo mtoto hafai kuitwa Jina la ubini WA Baba yake,Hilo Jambo ni haramu Sana na Mungu ameshalikemea tayari, ingawa Kwa bahati mbaya Sana Kwa kutojua wengi wamewapa majina ya ubini wao hao watoto wa nje ya ndoa.

Na lingine ni kumuozesha kwenye ndoa, Baba Hana haki ya kumuozesha binti yake WA nje ya ndoa Kwa mumewe kwani ndoa hiyo ni batili na haifai kabisa.

Lingine huyo mtoto hawezi kumrithi Baba yake kwasababu kisheria huyo mtoto sio WA huyo Baba,Bali Baba anaweza kumpa sehemu ya Mali huyo mtoto,lkn mara Tu huyo Baba anapokufa basi huyo mtoto Hana haki ya Kurithi chochote.

Lakini sio vibaya huyo Baba kumhudumia huyo kijana Kwa malezi na mahitaji mbali mbali maadam Tu yeye ndiye sababu ya kuja Hicho kiumbe hapa duniani.

Na mtoto ambaye Hana Baba kisheria anaweza kuitwa Kwa jina la mama yake, Kwa mfano ETUGRUL BEY ASHA au Kwa jina la ubini Kwa upande wa mama yake.

Kubwa ni kutambua uzao mzuri ambao hata kizazi chako kinaweza pata haki stahiki ni kizazi ambacho kinatokana na ndoa takatifu ambayo IPO Kwa mujibu wa Sheria.

Na hata wale ambao wanafunga ndoa za kiserikali basi watambue kidini Hicho kizazi Chao hakitambuliki na Sheria za Dini Kwa maana Baba Hana watoto hapo Ila watoto ni WA mama.

Ni hayo Tu!

Kazakh destroyer
Msonjo
Nurain
adriz
professional Driver
baby zu
I only appeal to sense.

Je hayo uliyoandika kwako binafsi yanakujakuja kuwa ni sahihi.

Kimantiki, kibaiolojia huyo ni mtoto wa huyo baba na ndio ukweli. Sasa kikija chanzo kingine au mamlaka nyingine ikasema kinyume na hivyo kimantiki inakuwa inasema uongo(kinyume na ukweli).

Ukweli siku zote haupingani na ukweli bali unajaziaga nyama tu. Maana ukweli ni mmoja. Tafakari. Chukua hatua ...
 
Ushasema ujambazi,ni vitu viwili tofauti kabisa,ni jinai.

Mtoto wa nje ya ndoa kafanya ujambazi upi hadi umtenge,aliomba azaliwe nje ya ndoa,vitu vingine havitaji akili nyingi kuona waliovitunga hawakuwa na mantiki

Unampaje pia adhabu mama wa mtoto utafikiri kajitia ujauzito yeye mwenyewe bila hiyo dini kumuwajibisha na huyo mwanaume
Chief wewe ulisema hao watoto wa nje ya ndoa wamejaaliwa na Mungu ndio maana unaona sawa Tu,ndio nikakujibu je wote waliojaaliwa wapo sahihi?

Nikatoa mfano hapo majambazi na wauza unga.

Mwanaume anawajibishwa Kwa kuwekwa Mbali na mtoto Kwa maana ananyang'wa mtoto na haki zake ikiwemo kurithiwa na kuitwa Jina la ubini wake
 
Hili la kubagua watoto limeongeza ukatili katika jamii kwa asilimia nyingi mno.
Kuna wale wauaji wa,,, aaah sijui kiswahili chake, ma serial killer ndivyo wanavyotengenezwa mtoto akue anaambiwa wewe ni kidudumtu, asijaliwe na apate uonevu kama huu kutengwa. Akigeuka akawa myama unyamani si tumejisababishia wenyewe matatizo katika jamii?

Kama jambo halileti afya ni kheri kuachana nalo tu. Kama suala ni zinaa basi adhabu ielekezwe kwa walioitenda... huyo baba na huyo mama sio kumlabel mtoto majina mabovumabovu
 
Mmekaa kikandamizi sana,ona lawama zote mnamsukumizia mwanamke…Hata katika mahusiano ya mapenzi kawaida nani huwa initiator kama sio mwanaume? Sasa mwanamke anakujaje hapo?ok sawa na je waliobakwa? Wao ndo wamesababisha?
Hili li dini linakandamiza wanawake
 
Labda huko kwenu,yaani hata leo mmewangu akajichanganya akamzaa huko yaani atampa haki zake atake asitake,mfanye starehe zenu afu mje kumhusisha mtoto
Yaani haki zake nakwambia utampa tu,
 
Mkuu kuna mambo ya kureason lkn zinapokuja Sheria za Mola wako aliyekuumba wewe na Mimi huna haki ya kuleta maoni yako
Ingekuwa reason haihitajiki basi tusingepewa. Tena kutoitumia ndio litakuwa kosa.

Yaani upewe utashi halafu ukatae kuutumia na uone ni sawa.

Kwa kuwa sheria na aya na kila kitu vyote vimepitia kwa wanadamu kabla ya kutufikia sisi. Reason inahitajika kujua ipi mbivu ipi mbichi lazma tu reason bhana.

Uzuri ni kwamba ukweli TRUTH hauiogopi reason, kwa sababu unajisimamiaga imara wenyewe.
 
Ukitaka kujuwa dini ni Utapeli waulize pesa imeumbwa na Mungu au binadamu?

Wakikujibu ni binadamu Sasa wahoji ni kwa nini Mungu huyu huyu anataka pesa za binadamu atolewe sadaka?

Na kwenye Utapeli huo dini zote hazipingani wanataka sadaka na fungi la 10.

Yani Mungu eti naye anamuomba binadamu commission ya pesa. Vichekesho haviishi ujinga mtupu.
Chief kila kitu kimeumbwa na Mungu,binadamu baada ya uwepo hapa duniani hakujua lolote Bali alikuja kupewa elimu ya mambo mbali mbali na Mola wake.

Mungu ndio mmiliki WA kila kitu hapa duniani Sisi tumepewa kama wasimamizi WA mambo hapa duniani.

Kwahiyo Mungu si mahitaji WA hizo pesa kwasababu Hana matumizi nazo Ila anataka tuzitumie Kwa kuwasaidia waja wake wenye uhitaji hapa duniani,ndio maana sadaka inatakiwa wapewe watu maalumu na kuendesha mambo ya ibada mbali mbali yaende Sawa.

Kwakifupi utaratibu upo WA kuyaendea mambo vizuri vile Mungu anavyotaka Ila binadamu Sisi ndio mafisadi
 
Ingekuwa reason haihitajiki basi tusingepewa. Tena kutoitumia ndio litakuwa kosa.

Yaani upewe utashi halafu ukatae kuutumia na uone ni sawa.

Kwa kuwa sheria na aya na kila kitu vyote vimepitia kwa wanadamu kabla ya kutufikia sisi. Reason inahitajika kujua ipi mbivu ipi mbichi lazma tu reason bhana.

Uzuri ni kwamba ukweli TRUTH hauiogopi reason, kwa sababu unajisimamiaga imara wenyewe.
Kuna mambo ambayo yapo wazi kabisa hauhitaji kureason, je kwa mfano kumuabudu Mungu unahitaji kureason?

Kufuata sheria mathalani usizini,usiue au kuiba je unahitaji kureason?

Mungu kuuwawa na watu wake hapo utahitaji reason,Mungu kuwa na mtoto hapo utahitaji kureason
 
Hizi dini za kizushi ndio chanzo cha migogoro, umasikini, ujinga, ugaidi na ubaguzi.

Uislam ni ujinga, ukristo ndio hovyo kabisa.

Mungu wa kwel hayupo kwenye dini.

Uislam ni tawi la ukristo wa warumi wa kale, haya yote ni magenge ya wahuni wa kizungu yanayofanya kazi kuwagawa waafrika na mijinga ya kule nchi za uarabuni isiyopenda kufikili zaidi ya kuwaza udini.

Uislam haukuanzishwa na ishamail, maana ishmail hakuwa muarabu wala hakuwa mzungu, kama ibrahimu akilkuwa mzungu na akazaa na binti wa kimisri(waafrika weusi) mnazan kunawezekana kutokea mwarabu hapo? Zaid ya Afrocast ama chotara asili ya uzungu(israel).

Biblia na quran zimeleta uharibifu kwa fikra duniano, hivyo ni vitabu vinavyoongoza kwa ugaidi dunia nzima kwa kificho..
Chief tumesikia maoni yako
 
Kwahiyo wadiz unataka kusema kuna Mungu wa Africa na Ulaya?

Anyways linapokuja swala la Imani ni kubwa Sana na very complicated lakini naheshimu maoni yako brother
Namaanisha kuna version za mitazamo Africa ilikuwa Mungu yuleyule wa Jana Leo na kesho hata bila uwepo wa Biblia ya Leo, Wala ukristo na uislam
 
Mahitaji ya mtoto hayana uhusiano na uzinzi wetu. Nimeshazini nimezaa huyo mtoto ni halali yangu na atapata haki zote hata kama dini haitaki. Viongozi wa dini wanaruhusiwa kununa. Sitelekezi mtoto, ni vile haijanitokea tu nikazaa nje ya ndoa.
Mkuu mbona ww ni mtu muelewa sana inakuwaje unashindwa kunielewa ?

Nimesha kwambia kuwa hujakatazwa na wala si haramu kwa ww kumuhudumia mtoto uliye mzaa nje ya ndoa ila hautakuwa na nguvu ya maamuzi, mamlaka wala haki yeyote mbele ya huyo mtoto kama baba.

Mfano kama ni mtoto wa kike akihitaji ruhusa ya kuolewa kutoka kwa wazazi wake mwenye mamlaka ya kufanya maamuzi ni mama yake na sio ww.

Na hauna haki ya kudai hisani yeyote kutoka kwa huyo hata awe tajiri kama Mo haijalishi umemlea au hujamlea.

Nadhani ume nielewa hakuna sehemu ambayo unakatazwa kulea.
 
Ila Dini sometimes inaleta UPUMBAVU Sana... yaani inakufanya unakuwa mjinga

Yaani mtoto wako mwenyewe,Damu yako, unakataa asichukue jina lako (Kwa kifupi Unamkataa), eti kwa sababu unamuamini Alah... Huu ni Upumbavu wa dini.

Huyu Alah wenu kwenye Hili Alichemka vibaya sana.
Unajua jinsi mtu anavyosoma na kujiona ana elimu kubwa basi huona Dini hazina maana na upumbavu.

Na Baya zaidi humuona Mola wake sio chochote kwakuwa Tu ana afya njema,ana bando la kuingia Jf na familia yake inakula.

Sawa mtuache Sisi wapumbavu tumuamini Mungu wetu
 
Biblia haijanipa hayo masharti ya kipumbavu ya kumtenga mtoto wa damu yangu asiye na hatia.

Biblia inaniambia niende nikazae niijaze dunia, na pia inanifundisha nisizini na endapo nikizini inaniambia niombe toba na Mungu atanisamehe na kunifutia kosa langu....na mwisho kabisa Biblia inanifundisha mimi mzazi kwenye kulea NISIWACHOKOZE watoto wangu... Hapo Biblia imemaliza.

Bible haituagizi kuwatenga watoto wetu tuliozaa nje kama hicho kitabu chenu cha karne ya 6 kinavyowafundisha nyie.
Mtoto wote walio zaliwa nje ya ndoa ni haramu kwa mujibu wa dini zote kuanzia Ukristo, Uislamu, na hata uyahudi usitake kujifariji hapa.

Tena mayahudi linapo kuja suala la kuzaa nje ya ndoa ni wakali mno na wakigundua wanakutenga.
 
Ndoa ndio inakupa uhalali wa kumiliki zao linalopatikana .
Kwa mfano unaweza kwenda kujenga nyumba kwenye kiwanja ambayo ina hati ya jina la mtu mwingine ?
Swadakta chief umesema kweli
 
kwani wakati mnakatikiana hamkujua kama atapatikana mtoto? maaneenerr huu uzi umekaa kibaguzi sana sikubaliani na mashala ya majina sijui ubini wala nini mtu akizaliwa kazaliwa full stop haya mambo ya kulazimishana sijui ukoo sijui kabila sijui ubini ni uwendawazimu tu. kwani hata akiamua kujiiya mti ama jiwe si ni binadamu tu? tutumie akili sio kila kitu cha kushobokea by the way haya madini tumeletewa tu
Chief tumepokea maoni yako
 
Mkuu mbona ww ni mtu muelewa sana inakuwaje unashindwa kunielewa ?

Nimesha kwambia kuwa hujakatazwa na wala si haramu kwa ww kumuhudumia mtoto uliye mzaa nje ya ndoa ila hautakuwa na nguvu ya maamuzi, mamlaka wala haki yeyote mbele ya huyo mtoto kama baba.

Mfano kama ni mtoto wa kike akihitaji ruhusa ya kuolewa kutoka kwa wazazi wake mwenye mamlaka ya kufanya maamuzi ni mama yake na sio ww.

Na hauna haki ya kudai hisani yeyote kutoka kwa huyo hata awe tajiri kama Mo haijalishi umemlea au hujamlea.

Nadhani ume nielewa hakuna sehemu ambayo unakatazwa kulea.
Mkuu sio kwamba sijakuelewa, ni kwamba nimezikataa hizo sheria na taratibu na kuamua kuwa sio za kuzizingatia pale jambo kama hilo linapotokea.
 
Back
Top Bottom