Je, Mungu wa Wakatoliki amebadilika au Wakatoliki wamepata Mungu mwingine?

Je, Mungu wa Wakatoliki amebadilika au Wakatoliki wamepata Mungu mwingine?

Ila hizi kauli za huyu papa sa hivi zinaweka kanisa njia panda wewe kama ni kukataa ukata au kama ni kukubali ukubali tatizo hyu kiongozi amekuwa Neutral mno kiasi cha kuwaacha waumini njia panda kuhusu suala la LGBTQ yani inaboa sana hta tu kumwona[emoji57][emoji57]

Mkuu hakuna mahali kahalalisha,ila kasema kanisa lisiwakunjie mikono manake kanisa lowapokee liwafunze waishi maisha ya utakatifu.

Kumbuka Yesu alikula na makahaba,wezi nk.
 
Kuambiwa ukweli siyo kuchukiwa, bali kupendwa. Mtu mnafiki ndiye atakwambia kile unachotamani kusikia tu.

Ukatoliki uko mbali sana na Ukristo. Na kwa kweli unapingana kabisa na imani ya Kristu na mitume. Sasa hilo ni kanisa la Mungu kweli?

Ukatoliki ni taasisi inayojificha kwenye vazi la dini na Ukristo.

Wakatoliki wanajua wanachoambiwa na Wakristu ni ukweli 100% na wao wako kinyume na Yesu, ndiyo sababu wanapaniki na kujaa jazba kirahisi.

Unauhakika mkuu,halafu pamoja na maneno yote mbona kanisa linakuwa kila siku na ndio kanisa lenye nguvu ulimwenguni?
 
Maria hawezi kuwaokoa nafsi zao
Wala hawezi kuwaombea wasamehewe
Mariamu ilimbidi afunge na kuomba kwa machozi ili aiokoe nafsi yake mpaka siku ya pentekost
Hakina wwakukuombea wewe madhabi yako usamehewe ila wewe mwenyewe ukatubu kwa mungu.

Alafu wanasahau kuwa mariamu hakutoa chembe ya yai kwenye utengenezaji wa mimba ya yesu
Ila alitumika kuikuza mimba kama chombo
Hakukuwa na damu yake kwenye mwil wa kristo
Na ndomana yesu hajawah kumuita mariamu mama.
 
Unauhakika mkuu,halafu pamoja na maneno yote mbona kanisa linakuwa kila siku na ndio kanisa lenye nguvu ulimwenguni?
Kukua kwa kanisa sio idadi brooo
Amkaa
Yesu alikuwa na wafuasi wengi mnoo wakafika wafuasi 70 anaotembea nao kila sehem
Ila kanisa lake lilipozidi kukua akawa na watu 12
Soma biblia mungu hajawai kufanya kazi na kundi kubwa
Sikuzote nikikundi kidogo tu cha watu.
Akiwa na watu wengu anaongea kwa amafumbo
Akiwa na kikundu chake anawaeleza wazi wazi
Alafu anakaa nao anawapa mambo ya kimbinguni

Kukua sio wingi wa sadaka wala watu
 
Kuna nyuzi nyingi za kushambulia kanisa katoliki, hata hivyo mti wenye matunda ndio unaotupiwa mawe.
Labda kweli mti wenu wa Ukatoliki unaweza kuwa na matunda, tena mengi sana.

Ila swali la msingi, ni matunda ya namna gani hayo?

👉^mti mwovu huzaa matunda mabaya^ - Mathayo 7:17.
 
.
 

Attachments

  • Screenshot_20231110-125847_Gallery.jpg
    Screenshot_20231110-125847_Gallery.jpg
    94.7 KB · Views: 1
Thank you Lord Jesus kwa kufumbua watu macho sasa wanaona, ila ubishi tu wa kibinadam. Ila ukweli sasa uko wazi.
Amina
Inabidi wajue kila kitu ili siku ya hukumu tukose chakujitetea
Humu tumeeleza kila kitu waze
Japo sio vyote
Ni mtu akaze shingo yake ili aelekee shimoni mwenyewe
Ukwel upo wazi
 
Mkuu ungechukua muda ukajifunza falsafa za RC usingeandika hiki ulichokiandika

1. Kanisa haliamini kuwa biblia ndo muongozo pekee wa kusimamia hilo kanisa, wana vyanzo vingine vya mambo mambo yao

2. Wanaamini pope ni mungu, yupo daraja la juu kuliko binadamu, ni muakilishi wa Mungu hapa duniani

3. Kanisa linaweza kufuta amri yoyote unayoijua kwenye biblia wakaweka ya kwao. mfano walifuta ile inayokataza kuchonga sanamu na wakagawanya ile ya kutamani ikawa mbili ili mradi kuzuga kuwa ni kumi
Umetoa wapi hii
 
LICHA YA YOTE MUNGU ANGALI ANANAFASI YA KUOKOA . AYA ULIYOYASOMA YATAFAKARI MUOMBE NA MUNGU AKUONYESHE PICHA HALISI. PAULO ALIPINGA SANA NENO HALISI NAKUSHIKILIA MAFUNDISHO YA KANISA LAKE MPAKA ALIPOKUTANA NA BWANA YESU MWENYWE. MAADAM YALIYOZUNGUMZWA NI NENO LA BIBLIA WW YATAFAKARI KWA MAKINI. BIBLIA INASEMA KAMA VILE MUNGU ALIVYOWAFUMBA MACHO WAYAHUDI WAKAMKATAA YESU WALIEMSUBIRI MIAKA YOTE ,,,ILI TU NEEMA IWAACHE NA SISI TUPATE NAFASI YA KUOKOLEWA... BASI HIVYO HIVYO NA SISI TUTAMKATAA TENA YESU TUNAEMWAMINI KWA KUBISHA NENO LAKE ILI NEEMA IWARUDIE WAYAHUDI WAPATE KUOKOLOWA NA KUMTAMBUA YESU WALIEMSULUBISHA...... WAKAT HUO MAKANISA YATAKUWEPOKUWEPO TUU KAMA VILE WAYAHUDI WALIVYOSASA BILA MUNGU.... TAFAKARI
 
Jomba Acha janja janja unapotosha jamii kwa waminisha vitu Huna hata ushaidi
 
Vp kuhusu kashfa ya mapadiri kuwanyanyasa kingono watoto wadogo?’
Huo sio ushoga
Ninafikiri unapaswa utueleze na au kututhibitishia msimamo rasmi wa Kanisa Katoliki kama linaunga mkono unyanyasaji wa kingono kwa yeyote, siyo watoto pekee.
 
Kwani uwezi kumcha Mungu wako bila ya kuwa na dhehebu tumia akili ....
👇👇👇
Dhana ya madhehebu haiwezi kukwepeka hata kidogo kwenye suala la dini au imani, kwa sababu ya uwepo wa mbegu ovu aliyoipanda Ibilisi.

Ni kama tu ambavyo dini na mfumo wa dini haviwezi kukwepeka. Huwezi kuacha jina zuri, kisa tu linatumiwa na mtu mwingine (mathalani aliye mbaya).

Kwa mfano, Ukatoliki unaamini ubatizo wa kunyunyiza maji, wakati Ukristu wa kweli unafundisha kuhusu ubatizo wa kuzamisha majini kabisa.

Tayari mpaka hapo ni madhehebu mawili kwenye kundi linalodai linafuata dini moja ya Ukristu.

Thibitisha. Nangoja jibu.

Yohana Mbatizaji alikuwa mfuasi wa dini ya Kiyahudi, dhehebu lake lilikuwa Mnazorayo.

Huyu ndiye alimbatiza Kristu, na wala Kristu hakuukemea Unazorayo wake maadamu hakupingana na dini ya Kiyahudi (ambayo ndiyo msingi wa Ukristu).
nitajie mtume au mtakatifu yoyote wa kweli aliye kwenye maandiko aliyekuwa na dhehebu au aliye anzisha dhehebu
Nimekupa mfano hapo wa Yohana Mbatizaji. Huyu, kama hujui, alikuwa nabii. Tena Kristu alimwita kuwa ni nabii wa juu kabisa. Luka 7:28.

Mfano mwingine ni Mafarisayo Yusufu wa Arimathaya (mjumbe wa Sanhedrini, Mathayo 27:57; Marko 15:43) na Nikodemo (Yohana 3:1, 2).
 
Ninafikiri unapaswa utueleze na au kututhibitishia msimamo rasmi wa Kanisa Katoliki kama linaunga mkono unyanyasaji wa kingono kwa yeyote, siyo watoto pekee.
Hao mapadri wamechukuliwa hatua gani?!
 
Hawasomi kabisaaa
Wanasubiri padri awasomee mstari mmoja
Watoe sadaka waende zao
Ni wavibu mnooo sijapata kuona
Wanataka mpaka zambi zao padri awaombee wasemehewe
Wakaona haitoshi
Wanamuomba maria amshawishi mwanae awasamehe dhambi zao

Yani ni upagani
Yesu alikufa na pazia likapasuka la hekalu iliiweje
Ili mtu aingie madhahahuni na aombe kwa mungu yeye mwenyew na sio kuhani awapelekee maombi yao

Ila ni wavivu mnoo
Ni wapagani waabudu sanamu waliojificha kwenye kivuli cha ukristo.
 
Yohana hakuwa na dhehebu
Soma Mathayo 2:23.

Dhehebu ni kikundi cha watu wenye mfumo wao mahususi wa imani na mienendo, hasa ndani ya au tofauti na jamii kubwa ya kidini.

Na hakuwa na kanisa
Bila kuwa na kanisa, hivi alikuwa akiwahubiri akina nani?

Wakati wa kuanza kwa Ukristo, makanisa yalikuwa majumba ya watu. Filemoni 1:2; 1 Wakorintho 16:19; Warumi 16:4.

Kanisa ni mwili wa Kristu; uko kila mahali penye watu wampendao, hata kama hakuna jengo, kunaweza kuwepo kanisa la Kristu.

Alikuwa anahubiri nakuwapinga viongozi wa dini na madhehebu
Yohana alikuwa akiwapinga viongozi wa dini na viongozi wa madhehebu, waliokuwa hawafuati misingi sahihi ya dini.

Dini ni mfumo wa imani. Madhehebu yapo kwa sababu mfumo huo wa imani unatofautiana baina ya waumini wa dini moja.

Kwenye dini ya Ukristo, kwa mfano, kuna madhehebu ya Ukatoliki, Anglikana, Walokole, nk.

Uislamu una madhebu kama Washia na Wasuni.

Huwezi kupinga dini au dhehebu, then ukasema huna dhehebu au dini. Kwa sababu mtazamo au imani inayokuongoza kuzipinga zingine, hiyo ndiyo dini yako mwenyewe.
Hajawah kuingia kwenye makanisa yao
Alihubiri mitaani na mtoni
Siyo lazima uingie kanisani au kwenye sinagogi, ndipo uwe na dini au dhehebu. Tafadhali jielimishe kidogo kuhusu maana ya kanisa, dini, dhehebu, na imani.
 
Yesu alisema ibilisi anapanda magugu kwa siri
Alipanda zamani sana
Kanisa lilianza siku ya pentekoste
Ila dhehebu la kwanza lilianza rumi miaka 300 baadae

Kwa sasa ndio mavuno lazima ukweli uonekane wazi na rangi zao
Romanj haifichi tena kama zaman uasi wake
Ipo wazi mnoo

Sijui kwanini mtu anatetea ushetani

Hata malaika akiwahubiria na vifungo vya biblia wanayoibeba kila siku kanisan watapinga.
Na watamuua kabisa
Na sasa hivi wameshaanza kujadili maswala mapenzi ya jinsia moja?!
Does it make sense?
 
Ndo mana wanauziwa maji yaliyonunuliwa sh 250 kwa sh 2000 eti wakawe matajiri.yaani maji nusu Lita unauziwa 2000 bado unamjadili mkatoliki?siku nyingine mkitaka kutujadili mtuletee bajeti ili mtujadili huku mnapiga vyuku sio mnatujadili huku mnapiga miayo.
Ukatoliki ni tajiri duniani leo kwa sababu ya ulaghai kama huo huo wa makanisa mengi leo.

Kuna mataifa na falme zililazimika kupeleka kodi RC ili ziweze kudumu. Nchi na falme zilizokataa zilipinduliwa na viongozi wake kuuawa.

Utajiri wa Vatikani ni wizi na upokaji mtupu. Hapo hatujazungumzia uuzaji wa vyeti vya misamaha na vitubio na mbinu nyingi za kipagani ili kukomba na kuhodhi pesa zote kutoka kwa waumini wao.

Na ndicho kinachoendelea hadi leo kwenye mfumo Katoliki. Pesa za waumini zinapokwa kwa kila mbinu iwezekanayo.

Kwa hiyo, haya makanisa (madhehebu) mengine yalijifunza unyang'anyi kutoka Ukatoliki, kwa kutumia silaha ya uongo na ulaghai.
 
Kanisa lilianza siku ya pentekoste
Ila dhehebu la kwanza lilianza rumi miaka 300 baadae
Mfalme Daudi, anayetajwa kwenye Biblia kwamba aliupendeza moyo wa Mungu, alikuwa mpagani? Hakuwa na kanisa?

Wana wa Israeli? Manabii wa zamani?

Kanisa la kwanza duniani ni lile la kwenye Bustani ya Edeni.

Mahali popote penye watu wanaomwabudu Mungu katika Roho na Kweli, hilo ndilo kanisa la Mungu.

Musa aliambiwa na Mungu nyikani avue viatu vyake kwa sababu alikuwa mahali patakatifu.

Kila alipo Mungu na watu wanaomwabudu ni kanisa la Mungu hilo.
 
Back
Top Bottom