Je, Mungu wa Wakatoliki amebadilika au Wakatoliki wamepata Mungu mwingine?

Je, Mungu wa Wakatoliki amebadilika au Wakatoliki wamepata Mungu mwingine?

Kwanini Yesu aliwafundisha mitume wake sala ya kusalimia ambayo ni BABA YETU au na yeye alitaka wanafunzi wake wakariri?
Ile ni sample ukiisoma vizuri imebeba kila kipengele muhim kwenye maombi,
Inaanza kwa kumpa mungu utukufu wake, kuomba msamaha, kuwaombea wengine kujiombea mwenyewe mahitaji yako na kuwasilisha kupitia kwa yesu kristo. Haina maana uicopy na kupaste kama Newton's laws of motion watu tunapishana mahitaji siyo mkate kila siku.
 
Mathayo 16:18
"Nami ninakuambia: Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, wala milango ya kuzimu haitalishinda."

Kristu amejenga Kanisa Katoliki juu ya mwamba. Hakuna nguvu za kuzimu zinazoweza kulishinda.

Kamwe halitaruhusu dhambi ya ushoga wala kuruhusu manyanyaso ya mashoga na wadhambi wengine.

Mungu huchukia dhambi, si wadhambi.

Vp kuhusu kashfa ya mapadiri kuwanyanyasa kingono watoto wadogo?’
Huo sio ushoga
 
Hakuina mahali nimeona wakatoliki wanamuamini papa .
Basi itakuwa ama hujui maana ya kuamini au hujui kinachozungumziwa.

Halafu, siyo tu kwamba wanamwabudu; papa ni mmoja tu kati ya miungu wao wasio na idadi.

Ndiyo maana wanawaabudu hata wafu, akiwemo ^Bikira^ Maria.
 
Pope hana uwezo wala mamlaka ya kubadili mafundisho ya kanisa. Kazi yake ni kusimamia mafundisho ambayo kanisa linayo kwa enzi na enzi.
Kama anataka ndoa ya jinsia moja, akaanzishe kanisa lake. Ndani ya ukatoliki ameshashindwa na hatakuja kuweza

It’s a matter of time ushoga na usagaji utaruhusiwa huko ukatoliki.
Wameshaanza kujadili na sasa hivi wameruhusu transgender kuwa baba wa ubatizo
 
Catholicism is not Christianity basing on the history of the church.

Huwa nikiisoma historia ya Ukristo na machungu ambayo Jesuits waliwapa wakristo wa kweli, pamoja na nguvu kubwa iliyotumika kuharibu na kupoteza maandiko ya Biblia ya kale badi sichelei kusema Catholic church is a pagaic church not a Christian Church.
Ukatoliki siyo kanisa, per se. Hiyo ni religio-political entity iliyojivika vazi la dini na kujinasibia baadhi ya mafundisho ya Ukristo ili kutimiza malengo yake ya kuzimu.
 
Siyo hivyo tu ...ukimwona mtu yoyote awe wa dini yoyote ukamuuliza yeye ni dhehebu gani akakutajia dhehebu lake basi ujue huyo ni mpumbavu kama wapumbavu wote ....maana mtu wa dini ya kweli hawezi kuwa na dhehebu .....mkristo wa kweli awezi kuwa na dhehebu kwa sababu ukristo wa kweli ni kinyume na mambo ya madhehebu ...na muislamu wa kweli awezi kuwa na dhebebu kwa sababu uislamu wa kweli ni kinyume na madhehebu .....Yesu siyo mkatoliki wala msabato wala mpentekosti nk ..Muhamadi siyo msuni wala mshia wala musarni ..nk
Madhehebu ni upotevu na ujinga kabisa...Ukiona tu anashabikia dhehebu basi tambua hana elimu .
 
INASIKITISHA SANA KUONA WAKRISTU WENZETU WAKITUCHUKIA KWA KIASI KIKUBWA NA NAMNA HII
HAKIKA INASIKITISHA MNO

ILIBIDI TUJENGE NYUMBA MOJA ILA HII CHUKI MLIYO NAYO WAKRISTU WENZETU SIO TU INAONDOA IMANI, MATUMAINI NA MAPENDO BALI INAKARIBISHA ROHO YA UMAUTI KUPITIA MAPANDIKIZI YA CHUKI JUU YETU WAKATOLIKI


INAUMA SANA

Tokeni huko kwa waabudu sanamu na upagani. Wala sio chuki
 
Nawao kwanini wamuulize swali hilohilo kila mwaka?
Kwa sababu lina umuhimu sana kwa mustakabali wa Ukristo.

Kama anadai RC ni Ukristo, vipi habari za ushoga? Jibu lake ni affirmative.

Maana yake ni kwamba hilo si kanisa la Kristo, bali ni taasisi inayojinufaisha kupitia mgongo wa dini.
 
Wakatoliki wanamhubiri Kristo nanyi mnamhubiri Kristo nadhani hili liwe msingi mkuu wa amani na umoja kati yenu.
^Bikra Maria, Mama wa Mungu, tuombee sasa na saa ya hukumu.^

Je, huko ni kumhubiri Kristu?
Wasio mtangaza na kumuhubiri Kristo hao ndio wapinga Kristo.
Hasa! Huu ujumbe uwafikie wote wanaowaombea marehemu ama wafu, huku wakiacha kumhubiri Kristu aliye hai.
 
Kuna nyuzi nyingi za kushambulia kanisa katoliki, hata hivyo mti wenye matunda ndio unaotupiwa mawe. Kanisa katoliki Lina sakramenti Saba ikiwamo ndoa na ndoa inayotambulika ni ya mke na mme. Wanaosema papa kabadilisha ni wale wanaorukia Mambo kijuujuu na ambao siku zote wanalifikiria mabaya kanisa katoriki . Ili kanisa katoliki libadilishe msimamo wakeninabidi kwanza wabadilishe kanuni na taratibu za kanisa.
 
Kwanini Yesu aliwafundisha mitume wake sala ya kusalimia ambayo ni BABA YETU au na yeye alitaka wanafunzi wake wakariri?
kuna sala za kukariri sikatai!!,lakini kuna sala za mishale ya moto!!!hauwezi kushambuliwa na mapepo alaf ukategea usali sala ya baba ye2 eti ndo yatakimbia,,,no way,,,,kukimbiza mapepo unahitaji "roho mtakatifu"..okay!!!,YESU alifundisha sala za kukariri!!,,lakini ROHO MTAKATIFU alipowashukia mitume siku ya pentekoste walinena kwa lugha,,,walirap kama 2PAC SHAKUR!!,,,unaona bhana!!!!!,,,,,,,,,,,,,,,,,ROHO MTAKATIFU akikushukia,,unapoteza ufaham wa kibinadamu,,na unanena lugha ya mbinguni!!!...lakini ata YESU kristu alipoondoka alisema"naondoka ila ninamwacha msaidizi ambae ndio ROHO MTAKATIFU"kimsingingi huu ni wakati wa ROHO MTAKATIFU...ata biblia inasema"dhambi zoooooooooooooote zinasehemeka,ila dhambi ya kumkashif ROHO MTAKATIFU haisameheki kamwe!!!,,,,,,naaa,kwenye Q'RAN tukufu,ROHOMTAKATIFU anajulikana kama malaika GIBRIL,,ila kwenye BIBLIA TAKATIFU ROHO MTAKATIFU anajulikana kama MUNGU katika utatu mtakatifu!!
 
Amka ndotoni usije ukajikojolea. Walishasema hivyo miaka 2000 iliyopita tena kanisa lilipigwa vita na kina hitler na badala yake kanisa linazidi kuimarika 😀
jana papa katangaza kwamba mashoga wana haki ya kubatizwa na kusimamia ndoa,,,kimsingi ushoga ni ruksa kwa katoliki
 
Mkuu ni vyema na inapendeza kama dunia tukiwa na dini moja itapendeza sana kuliko huu upuuzi na takataka za dini zinznzoendlea duniani kwa sasa.
Ni ngumu sana kuwa na dini moja katika ulimwengu ambao, wale wanaodai eti walipewa ufunguo wa kanisa la Petro, wanaabudu sanamu na kufuata mapokeo kinyume na mafundisho ya Kristu.

😭😭😭👇👇👇
TUACHENI WAKATOLIKI TUABUDU SANAMU ZETU, Nyingi siyo Mungu hamuwezi kutuhukumu.
 
Biblia inasema Mungu ni yeye yule jana na leo na hata milele, yaani Mungu habadiliki wala habadilishi misimamo yake. Mwaka juzi papa alipoulizwa kama kanisa Katoliki linaweza kubariki ndoa ya jinsia moja, alijibu haiwezekani KWA SABABU MUNGU HAWEZI KUBARIKI DHAMBI:

ROME (AP) — The Vatican declared Monday that the Catholic Church won’t bless same-sex unions since God “cannot bless sin.”

The Vatican’s orthodoxy office, the Congregation for the Doctrine of the Faith, issued a formal response to a question about whether Catholic clergy have the authority to bless gay unions. The answer, contained in a two-page explanation published in seven languages and approved by Pope Francis, was “negative.”

Lakini mwaka huu alipoulizwa swali lile lile papa amesema ndoa za jinsia moja zinaweza kubarikiwa, na watu hao wanaruhusiwa kuwa baba na mama wa ubatizo!:

Catholic Church relaxes rules for transgenders​

Pope Francis recently suggested priests could bless same-sex unions on an individual basis.
The Vatican’s doctrinal office has clarified its stance on transgender believers, saying they may get baptized and play various roles within the Catholic faith so long as it does not risk “public scandal.”

In a letter responding to questions posed by a Brazilian bishop, the church’s Dicastery for the Doctrine of the Faith outlined its position toward transgender and other LGBT worshipers, affirming that they may receive the sacrament of baptism, serve as witnesses in wedding ceremonies and act as godparents to Catholic children.

Je, Mungu kabadili msimamo kuhusu dhambi ya ushoga maana papa alisema awali kuwa MUNGU HAWEZI KUBARIKI DHAMBI, au kanisa katoliki chini ya papa Fransis limepata mungu mwingine wa kichina ambaye yeye kwake kubariki dhambi ya ushoga siyo tatizo?

Kwa maoni yangu binafsi, kwa kuwa ninaamini kuwa Mungu hawezi kubadilika kwa mujibu wa Biblia (Ebr 13:8), basi italkuwa kanisa katoliki limeachana na Mungu wa Biblia na limejipatia mungu wa kichina anayekwenda na wakati hasa akizingatia haki za kidemokrasia kam,a zinavyosimamiwa na mataifa ya magharibi hasa Marekani (Democratic). Wadau mnasemaje? karibuni tudadavue!!
Heri wenye moyo safi maana watamuona Mungu. Dini ni uhuni
 
Asiye na dhambi apinge hayo ya Catholic kwa Nguvu zake zote
Hiki kichaka ni kidogo sana, huwezi kujifichamo. Toka humo haraka usije ukafa ewe mfuasi wa kadinali.

Ninyi mnapojidai kuwahubiria wengine ^injili ya papa,^ huwa mmegeuka malaika, siyo?
 
Huko ulaya na marekani kuna makanisa yanafungisha ndoa za jinsia moja ni ya katoliki?
Mbona huongelei Anglican au Lutheran? Kwa wasabato nako kuna fujo na makelele kama walokole?
 
Mpinga Kristo ni wale wasio mtambua Kristo katika imani zao na wanaosema Kristo sio Mwana wa Mungu.
Watu wasiomtambua Kristu (wapinga-Kristu) ni wale wanaofuata mapokeo yao ya dini, huku wakiyaacha mafundisho ya Kristu. Soma Mathayo 15:9.

👉Yesu alibatizwa kwa kuzamishwa. Ukatoliki ukasema No. Wao wananyunyiza tumaji kichwani.

👉Yesu alisema niaminini Mimi -- Roho, Kweli na Uzima. Ukatoliki ukasema No. Sisi tunamtambua ^Bikra^ Maria.
 
Ila hizi kauli za huyu papa sa hivi zinaweka kanisa njia panda wewe kama ni kukataa ukata au kama ni kukubali ukubali tatizo hyu kiongozi amekuwa Neutral mno kiasi cha kuwaacha waumini njia panda kuhusu suala la LGBTQ yani inaboa sana hta tu kumwona😏😏
Hivyo ndivyo Ukatoliki ulivyo, na wala haujawahi kubadilika.

Ngoja waendelee kukunjua makucha yao halisi ndipo mtajua hilo siyo kanisa, bali taasisi tu yenye mchanganyiko wa dini na siasa.

Ukatoliki unaangalia zaidi ushawishi na maslahi kuliko ukweli wa Kristu.

Matajiri (mfano, LGBTQ) watu maarufu, wanasayansi nk. watakubalika humo kwa kigezo tu cha ushawishi wao.

Ukatoliki umekaa kisiasa zaidi ili kujinufaisha na kila fursa inayojitokea, bila kujali athari husika kwenye misingi ya Neno.

Catholicism is an opportunitic religio-political entity.
 
Back
Top Bottom