zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 20,537
- 31,729
Habari za jioni wana JF intelligence, natumaini wote wazima humu. Na kama kawaida nitoe angalizo kuwa mada ni sensitive sababu linagusa pia imani za wengine hivyo ningeomba tusome kwa makini tujiridhishe kwa tafiti binafsi kabla hatujachangia hii mada hivyo sitegemei watu waje na kejeli za kidini wala kukashifiana imani zetu maana uzi huu ni wa kuelimishana zaidi kuliko kukosoana. Kwa kusema hayo twende moja kwa moja kwenye mada. Na nitaigawa mara mbili ili tusome kwa urahisi.
UTANGULIZI
Kwa miaka mingi sasa kumekuwepo na imani kwamba kitabu cha mwanzo kimeandikwa na Nabii Musa na hata vile vitabu 5 vya kwanza kwenye biblia kwa ujumla wake vinavyoitwa pentateuch pia wengi tunaamini viliandikwa na Nabii Musa na watu wengi wanajikita kwenye mistari hii kuprove hilo
Yohana 5:46
46 Kwa maana kama mngalimwamini Musa, mngeniamini mimi; kwa sababu yeye aliandika habari zangu.
Kutoka 17:14
14 BWANA akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua.
Mistari hii na mingine kama 20 kwa wengi inaonyesha kuwa kwa namna moja au nyingine vitabu 5 vya kwanza (pentateuch) ikiwemo Mwanzo iliandikwa na Musa. Imani hiyo ilivuka mpaka karne ya 20 ambapo baada ya elimu ya theolojia kusambaa dunia nzima,teknolojia na Elimu kwa ujumla kukua hivyo reasoning ya watu ikaongezeka ndio wakaanza kuhoji.
Waliibuka wasomi wa theolojia na dini mbalimbali kama Professor Julius wellhausen wa Ujerumani ambaye alikuja na nadharia ya Documentary hypothesis ambayo ilikuja kuzaa mjadala mkubwa kiasi kufikia karne hii ya 21 wanatheolojia wengi wanakiri kuwa Musa hakuandika kitabu cha mwanzo na pentateuch nzima kwa hoja tutakazoona hapo chini.
NB: Naomba ieleweke kwamba hakuna mahala kwenye maandiko ya biblia inaposema Musa aliandika kitabu cha mwanzo bali wote wanaongelea maandiko ya Musa ila sio vitabu kma vilivyopangwa kwenye Bible. Hivyo msimamo wa wanaopinga uandishi wa Musa ni kwamba, Musa aliandika mambo mengi ya wakati wake kwenye nyaraka kadhaa alafu wakaja waandishi wengine ambao walisoma nyaraka za Musa ndio wakajengea hoja zao ambazo zikazaa kitabu cha mwanzo na pentateuch nzima. Ni kama useme katiba pendekezwa draft yake iliandikwa na warioba ila sitta akaja kuifanyia editing, kuongeza maoni yake na maboresho hivyo ikatoka kuitwa rasimu mpaka kuitwa katiba pendekezwa. Hivyo kwa msimamo huu ni kwamba kitabu cha mwanzo kiliandikwa miaka 600 kabla ya Yesu ilihali Musa aliishi miaka takriban 1400 kabla ya Yesu ikimaanisha HAKUWA MUANDISHI WA KITABU CHA MWANZO.
DOCUMENTARY HYPOTHESIS
Nadharia hii inaamini kwamba kitabu cha mwanzo kiliandikwa na waandishi zaidi ya 4 ambao baadae wakaunganisha kazi zao na kutengeneza kitabu cha mwanzo. Wanawatenganisha watu hawa kwa kuangalia lugha iliyotumika, majina anayotumia, matamshi ya maneno ili kuprove walikuwa watu wanne walioishi vipindi tofauti kabisa. Mfano kitabu cha mwanzo kuna mistari inaongelea Musa kupewa sheria Mlima Horeb na kwingine inasema Mlima Sinai ikimaanisha mmoja wa waandishi aliishi baada ya kuwa jina mlima Horeb lilikwisha badilishwa na kuitwa Sinai and vice versa hivyo muandishi hawezi kuwa mmoja.
Kuna tofauti nyingi sana zimeorodheshwa kwa mifano na mwanatheolojia maarufu Mr Richard Friedman aliyeunga mkono nadharia hii unaweza soma hapa kwa upana wake tofauti zote.... Ningeomba msome hii document kabla hujachangia hii mada.
The Documentary Hypothesis Evidence
USHAHIDI WA KIMAANDIKO
Mwanzo 11:31
31 Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko.
Hapa Mwandishi anamzungumzia Abraham kuwa anaishi kwenye mji wa Uru na akauhusianisha mji huo na kabila la wakaldayo. Lakini kwa ushahidi wa kiacholojia wakaldayo wameanza kuishi hapo Uru 1000 BC ilihali Musa aliishi miaka 1400 BC ikimaanisha kuwa mwandishi wa sura hii aliishi miaka mingi baada ya Musa ndipo akashuhudia wakaldayo wakiishi Uru hivyo akaandika habari za Abraham kuwa aliishi Uru ya wakaldayo kitu ambacho wakati wa Musa kabila hilo halikuwepo.
UTANGULIZI
Kwa miaka mingi sasa kumekuwepo na imani kwamba kitabu cha mwanzo kimeandikwa na Nabii Musa na hata vile vitabu 5 vya kwanza kwenye biblia kwa ujumla wake vinavyoitwa pentateuch pia wengi tunaamini viliandikwa na Nabii Musa na watu wengi wanajikita kwenye mistari hii kuprove hilo
Yohana 5:46
46 Kwa maana kama mngalimwamini Musa, mngeniamini mimi; kwa sababu yeye aliandika habari zangu.
Kutoka 17:14
14 BWANA akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua.
Mistari hii na mingine kama 20 kwa wengi inaonyesha kuwa kwa namna moja au nyingine vitabu 5 vya kwanza (pentateuch) ikiwemo Mwanzo iliandikwa na Musa. Imani hiyo ilivuka mpaka karne ya 20 ambapo baada ya elimu ya theolojia kusambaa dunia nzima,teknolojia na Elimu kwa ujumla kukua hivyo reasoning ya watu ikaongezeka ndio wakaanza kuhoji.
Waliibuka wasomi wa theolojia na dini mbalimbali kama Professor Julius wellhausen wa Ujerumani ambaye alikuja na nadharia ya Documentary hypothesis ambayo ilikuja kuzaa mjadala mkubwa kiasi kufikia karne hii ya 21 wanatheolojia wengi wanakiri kuwa Musa hakuandika kitabu cha mwanzo na pentateuch nzima kwa hoja tutakazoona hapo chini.
NB: Naomba ieleweke kwamba hakuna mahala kwenye maandiko ya biblia inaposema Musa aliandika kitabu cha mwanzo bali wote wanaongelea maandiko ya Musa ila sio vitabu kma vilivyopangwa kwenye Bible. Hivyo msimamo wa wanaopinga uandishi wa Musa ni kwamba, Musa aliandika mambo mengi ya wakati wake kwenye nyaraka kadhaa alafu wakaja waandishi wengine ambao walisoma nyaraka za Musa ndio wakajengea hoja zao ambazo zikazaa kitabu cha mwanzo na pentateuch nzima. Ni kama useme katiba pendekezwa draft yake iliandikwa na warioba ila sitta akaja kuifanyia editing, kuongeza maoni yake na maboresho hivyo ikatoka kuitwa rasimu mpaka kuitwa katiba pendekezwa. Hivyo kwa msimamo huu ni kwamba kitabu cha mwanzo kiliandikwa miaka 600 kabla ya Yesu ilihali Musa aliishi miaka takriban 1400 kabla ya Yesu ikimaanisha HAKUWA MUANDISHI WA KITABU CHA MWANZO.
DOCUMENTARY HYPOTHESIS
Nadharia hii inaamini kwamba kitabu cha mwanzo kiliandikwa na waandishi zaidi ya 4 ambao baadae wakaunganisha kazi zao na kutengeneza kitabu cha mwanzo. Wanawatenganisha watu hawa kwa kuangalia lugha iliyotumika, majina anayotumia, matamshi ya maneno ili kuprove walikuwa watu wanne walioishi vipindi tofauti kabisa. Mfano kitabu cha mwanzo kuna mistari inaongelea Musa kupewa sheria Mlima Horeb na kwingine inasema Mlima Sinai ikimaanisha mmoja wa waandishi aliishi baada ya kuwa jina mlima Horeb lilikwisha badilishwa na kuitwa Sinai and vice versa hivyo muandishi hawezi kuwa mmoja.
Kuna tofauti nyingi sana zimeorodheshwa kwa mifano na mwanatheolojia maarufu Mr Richard Friedman aliyeunga mkono nadharia hii unaweza soma hapa kwa upana wake tofauti zote.... Ningeomba msome hii document kabla hujachangia hii mada.
The Documentary Hypothesis Evidence
USHAHIDI WA KIMAANDIKO
Mwanzo 11:31
31 Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko.
Hapa Mwandishi anamzungumzia Abraham kuwa anaishi kwenye mji wa Uru na akauhusianisha mji huo na kabila la wakaldayo. Lakini kwa ushahidi wa kiacholojia wakaldayo wameanza kuishi hapo Uru 1000 BC ilihali Musa aliishi miaka 1400 BC ikimaanisha kuwa mwandishi wa sura hii aliishi miaka mingi baada ya Musa ndipo akashuhudia wakaldayo wakiishi Uru hivyo akaandika habari za Abraham kuwa aliishi Uru ya wakaldayo kitu ambacho wakati wa Musa kabila hilo halikuwepo.