Je, naweza kutumia fungu la kumi kwa kununua mahitaji ya watoto yatima?

Je, fungu la kumi linaweza tolewa kwa wajane, yatima na wenye shida au ni lazima nikatoe kanisani?

Naomba hekima zenu juu ya hili.
Peleka Kanisani......ila hakikisha umeiweka madhabahun ww mwenyewe na Mungu ataipokea na kuyanyosha mapito yako....!!! Watu wamekushaur upeleke kwa yatima lakin nakushaur tenga fedha nyngne ndio uende ukawape wahitaji
 
Peleka Kanisani......ila hakikisha umeiweka madhabahun ww mwenyewe na Mungu ataipokea na kuyanyosha mapito yako....!!! Watu wamekushaur upeleke kwa yatima lakin nakushaur tenga fedha nyngne ndio uende ukawape wahitaji
Ni wapi Mungu amekuagiza upeleke fungu la kumi kanisani?

Na amekuambia ukilipeleka kanisani ni nani anatakiwa alipokee?
 
Kwa mjibu wa Biblia nyakati zile za Torati Wajane na Yatima, walikuwa na sehemu ya Fungu la 10 siyo Walawi tu,
(Kumbu14:28-29)
(Kumbu.26:12-13)
Lakini Nyakati hizi kwa sababu Wachungaji wanachuja maandiko ili kujinufaisha, huwa hawawakumbuki Wajane na Yatima kama maandiko yanavyosema!
 
Wachungaji wajanja sana, wanajua sisi hatupendi kujisomea wanatumia nafasi hiyo kujinufaisha.
 
Kwenye agano la kale fungu la kumi maelekezo yake linapaswa lipelekwe hekaluni hakuna maelekezo tofauti na hayo kama unayo leta kifungu cha andiko.
Mkuu yalikuwepo Maelekezo! Soma maandiko haya,
Kumbu.26:12-13
Kumbu.14:28-29
Sema Wachungaji wa Nyakati hizi wanachuja maandiko kwa ajili ya Maslahi yao Binafsi.
Kwa maandiko hayo Mjane, Yatima ana sehemu katika Fungu la 10.
 
Fungu la kumi ni fungu la Mungu, peleka madhabahuni unapoabudia.
Kitabu cha Yoeli Mungu anasema mnaniibia kwa kutotoa zaka, leteni zaka kamili ghalani Ili kiwepo chakula nyumbani mwangu.

Misaada kwa yatima hiyo ni sadaka.
Hicho chakula hemani mwake anakula nani....!? Dini iliyosafi.....!!
 
Ha
Hao huku kwetu tunawapata wapi na tunawajuaje!?
 
Nyie mnaotoa zaka mmebarikiwa hata isiwepo nafasi?au mnaganga njaa?kongwa kitu kibaya sana
 
Sio kila kitu mpaka muhusianishe na ukoloni ili ndo watu wawaone mnaongea vya maana sana jamani. Sasa wewe mwafrika unatoa hela gani kanisani kusema unawafaidisha wazungu. Hivi unajua ni kiasi gani wazungu wamechangia kwenye hayo makanisa mpaka kufika hapo yalipo. Labda useme waafrica baadhi wanajinufaisha na sadaka ntakuelewa ila sio eti ela za sadaka africa nd zimefaidisha wazungu. Wazungu wameiba madini ni kweli na vitu vingine vya thamani ila usisema sadaka sijui kwanza mwafrica hela alitoa wapi kipindi cha ukoloni.

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Sasa mbona taasisi za kizungu ndo zinaendesha makanisa ya africa aisee hii story umetoa wapi? Kwahiyo unadhani hii misaada ya kikanisa inaletwa africa hela zinakuwa zimetoka wapi?

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Hamtaki kutoa hela kwa Mungu kuwa mtafirisika ila kuhonga, kulewa na starehe nyingine hazifirisi basi sawa. Mkristo wa kweli huwezi sita mtolea Mungu neno liende maana wewe huna kwa kupeleka hela kwa kijinga. Kwanza huna mikosi ya kupoteza hela kijinga, hutoi hela kwa waganga, hufanyi mastarehe yasio lazima( maan sio mlevi na huezi kuwa na michepuko) na unajisikia faraja sababu watu wengi wamebarikiwa kupitia wewe( wale uliowasaidia) . Kuna raha sana kumtolea bwana kwanza utoaji unakupa nguvu ya kutafuta ili uwabariki na wengine kama vile kutolea injili ya bwana isambae. Labda mngesema tu jina la zaka na tafsiri yake mjadili ila kuna wengine ni wapagani na wachoyo ndo hao hawataki kusikia kabisa kuhusu utoaji. Halafu makanisa yana msaada sana na zile hela maana watu wanakopeshwa bila riba kama wakipatwa na shida( kuna jmaa yangu alisaidiwa ada na mchungaji) yanatoa kwa wahitaji( bila camera maana kuwadhalilisha uliowasaidia sio msaada wa kiMungu)

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 

Je, fungu la kumi linaweza tolewa kwa wajane, yatima na wenye shida au ni lazima nikatoe kanisani?

Naomba hekima zenu juu ya hili.
Uzi kama huu watu aina ya mama D lazima wakuparure.

Kumbukumbu la Torati 12:5-6​

"Lakini mahali atakapochagua Bwana, Mungu wenu, katika kabila zenu zote, apaweke jina lake, maana, ni makao yake, elekezeni nyuso zenu hapo, nawe wende huko;​

pelekeni huko sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu zenu, na zaka zenu, na sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu, na sadaka zenu za hiari, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ng'ombe na ya kondoo;"​




Ukipeleka kwa yatima au wajane umepeleka msaada sio sadaka
 
Halafu kuna huu upuuzi sijui hawa wachungaji/walimu wanatupotosha au laa

Issue ya kusema agano la kale/sheria za kale limepitwa/zimepitwa na wakati hii issue sijui imekaaje, maana hata hizi amri 10 za Mungu zimetoka huko agano la kale na bado tunazitumia

Sasa inakuwaje baadhi ya sheria za agano la kale tuzikatae/tuziache halafu zingine tuzichukue?? Yaani tunadonoadonoa. Hasa zile zilizongumu zote tumeziacha e.g mtu akitenda dhambi apigwe hadi kufa, Kitimoto kimepigwa ban agano la kale lakini sasa kizazi hiki ni mwendo wa kushushia tu si mchungaji wala muumini

Utasikia tumekombolewa kwa neema, na hatuhesabiwi haki kwasababu ya sheria.
HIKI KIZAZI KIMEPOTOKA SANA NDIO MAANA WENGI WETU TUNAISHI TU, NGUVU ZA MUNGU HAMNA KABISA. TUMEKAIDI SHERIA ZAKE.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…