Je, ni halali kwa askari wa usalama barabarani kuwatoza wananchi faini ya 30,000/= kwa kutokuwa na sticker za nenda kwa usalama?

Je, ni halali kwa askari wa usalama barabarani kuwatoza wananchi faini ya 30,000/= kwa kutokuwa na sticker za nenda kwa usalama?

Tate Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2019
Posts
33,092
Reaction score
96,127
Habari ndugu Wanajamii Forums. Nimeona nije kupata ufafanuzi kutoka kwa wataalam wa mambo ya usalama barabarani.

Kwa ufupi nilikuwa na safari kutoka Mkoa mmoja kwenda mwingine huku nikitumia usafiri wangu binafsi. Kiukweli njia nzima changamoto zilikuwa ni nyingi kutoka kwa hawa askari wetu wa usalama barabarani. Changamoto mojawapo ilikuwa ni ile ya kuviziana na tochi kwenye yale naeneo ya 50/KPH! Hapa niliwashinda.

Changamoto nyingine ilikuwa ni ile ya kusimamishwa na kuulizwa leseni yako, kukaguliwa bima kupitia mashine, kukaguliwa kama gari inadaiwa, nk. Na hapa pia nilikuwa mshindi.

Jambo lililonifanya kuanzisha huu uzi sasa ni hili suala la askari mmoja wa eneo fulani katika hiyo safari yangu, kunisimamisha na baada ya kukagua gari na kukosa makoda mengine; akanitia hatiani kwa kosa la kutokuwa na sticker ya nenda kwa usalama barabarani. Huyu askari nilibishana naye kwa muda mrefu pasipo na mafanikio! Na mwisho wa siku akalazimisha kuniandikia hiyo faini ya elfu 30.

Kwenye maelezo yake wakati tunabishana, aliniambia eti hizo sticker zinatolewa kituo cha polisi na mtu anayeitwa VECO! Na kwa hiyo kila dereva/mmiliki wa gari anatakiwa kwenda kituo cha polisi na gari lake ili likaguliwe, ndipo apewe hiyo sticker ya nenda kwa usalama!!

Sasa maswali yangu kwenu wanajukwaa ni haya hapa;

1.) Je, huyo VECO ana uwezo wa kukagua magari yote nchini na hivyo kuyapatia hizo sticker za nenda kwa usalama?

2.) Je, ni halali askari wa usalama barabarani kunitoza faini ya elfu 30 kwa kukosa hiyo sticker? Au na hii ni njia mojawapo ya kukusanya mapato ya serikali kupitia mifumo kandamizi na ya hovyo?

3.) Na kama hizo sticker zina ulazima kwa kila gari, ni kwa nini zoezi lisifanyike barabarani ambako magari ndiyo hutembea, badala ya kuwataka madereva/wamiliki wa magari kwenda kwenye vituo vya polisi (tena ni kuanzia vile vya Wilaya) kuwaona hao VECO! (Na mbaya zaidi siyo mara zote utawakuta huko vituoni) Ili tu kununua hizo sticker! Halafu ukimkosa, unaishia kuandikiwa faini? Kwa nini jeshi ka polisi linatengeneza mazingira ya aina hii kwa wamiliki wa magari?

4. Huu mradi wa sticker za nenda kwa usalama ni wa nani? Maana miaka nenda tunalazimishwa tu kuwa na hizo sticker, huku magari yenyewe yakiwa hayakaguliwi! Na badala yake watu wamekuwa wakiuziwa hizo sticker kwa bei ya ulanguzi na hao polisi?

5.) Je, serikali ya CCM hamuwezi kutuondolea huu uonevu tunaofanyiwa wamiliki wa vyombo vya moto, hususani wamiliki wa magari? Maana tumekuwa sasa kama ng'ombe wa maziwa kutoka kwenu na pia kutoka kwa hawa askari wenu wa barabarani!!

Kwa uonevu wa aina hii nikiichukia serikali na pia hawa askari wapenda rushwa, mtanilaumu kweli!!

NB:- kuna kijana wa mwaka 2000 anaweza kuja kuniponda kwa kulalamikia faini ya elfu 30!! Hajui hiyo hela ni bora mara mia ningeenda kunywea pombe, au kwenda kununulia nyama ya swala! Kuliko kuitoa kwa watu wasio na faida.
 
Kuna siku nilienda kununua hio sticker aisee VECO anajivuuuta mixer kusema hizo sticker hazipo ZIMEISHA ikabidi NIJIONGEZE kama mTanzania mzalendo mkono wangu ukazama mfukoni ndani kdg ndo akanipatia kumbuka hapo nishaliwaga vi buku 5 5 nyingi tu na mapoti mbalimbali pale road😀😀😀😀😀
 
Hapa umenikumbusha machungu niliyopitia wiki iliyopita. Nimetoka umbali wa takribani km 40 kwenda kituo cha Polisi kwa ajili ya kupewa hiyo sticker. Nilipofika nikaambiwa huyo Vehicle Inspector yupo na wanafunzi wa udereva. Nikamfuata kumuomba anisaidie niweze kupata hiyo sticker kwani nina safari ya kwenda kumuona mgonjwa. Nilijibiwa kuwa yupo na wanafunzi kuwa hawezi kunitolea control number kwa wakati huo hivyo nimsubirie hadi saa sita akimaliza. Kwa kuwa nilikuwa nasubiriwa nikasema hapa nikiendelea kusubiri itakuwa siyo sawa. Nikaondoka kwenda kwenye hiyo safari. Wakati narudi nikasimamishwa na askari wa usalama barabafani. Nikamueleaza vizuri tu kuwa sikuvunja sheria bali Vehicle alikuwa na majukumu mengine akashindwa kunihudumia. Basi nikaona hataki kunielewa baada ya mabishano ya muda mrefu akaniandikia faini. Nilipofika kwa Vehicle hata sikutaka kuongelea hilo suala kwa sababu nimeshaandikiwa na pengine ni dhumuni lilitakiwa kutimia. Namshukuru Mungu nimeshalipa hiyo faini japo iliniumiza kwa kweli naona nimeonewa kwa sababu nilifuata taratibu zote za kufikisha gari kukaguliwa kabla ya safari.
 
Kuna siku nilienda kununua hio sticker aisee VECO anajivuuuta mixer kusema hizo sticker hazipo ZIMEISHA ikabidi NIJIONGEZE kama mTanzania mzalendo mkono wangu ukazama mfukoni ndani kdg ndo akanipatia kumbuka hapo nishaliwaga vi buku 5 5 nyingi tu na mapoti mbalimbali pale road😀😀😀😀😀
Ukienda kulipia hiyo sticker wape Tsh 5000 badala ya Tsh 3000 iliyopo kwenye sticker
 
Mimi nilikutana na mkasa kama wako mkoani LINDI maana kila idara nilikuwa nimekamilika wakaja kunidaka kwenye sticker lkn mwisho wa picha nillipa Tu tena haikuwa na shida yeyote kwasababu nilitoa Tsh 5000 badala ya 3000.

Huyo jamaa amekuonea Tu Kwa kuandika kosa la faini, sometimes ukikutana nao hao jamaa jitahid kujishusha Tu mbele yake ili maisha yaende
 
Kuna siku nilienda kununua hio sticker aisee VECO anajivuuuta mixer kusema hizo sticker hazipo ZIMEISHA ikabidi NIJIONGEZE kama mTanzania mzalendo mkono wangu ukazama mfukoni ndani kdg ndo akanipatia kumbuka hapo nishaliwaga vi buku 5 5 nyingi tu na mapoti mbalimbali pale road😀😀😀😀😀
Sticker za nenda kwa usalama ni mradi wa wakubwa kupiga pesa ndefu sana.
Kuna msela Arusha huwa hakosi sticker kama 30,000 kwa mwaka mzima zipo tu na hukusanya 5,000 kwa kila sticker.
Anakwambia huo ni mradi wa namba wani wao nk.

Tate Mkuu umeanza kumiliki gari mwaka huu mkulungwa?
Mbona huu mradi ni wa miaka na miaka?

Kibaya zaidi hawakagui magari wanauza sticker kiholela tu.
 
Pole.
Utaratibu ni huu, ukiwa na safari pamoja na ile pesa ya mafuta kuwa na pesa ya kubrash viatu.
Nimeachaga huu ujinga, siku hizi bora nipigwe faini kuliko kutoa hongo.
Wengi wao hasa maeneo ninapopita mara kwa mara wamenielewa kuwa sitakagi ujinga.
Huwa navutana nao hadi inatisha.

Hawa mafala ukiwaogopa wanakufilisi.
Jana tu nimevutana na mmoja kiasi cha kumtolea lugha kali sana
 
Habari ndugu Wanajamii Forums. Nimeona nije kupata ufafanuzi kutoka kwa wataalam wa mambo ya usalama barabarani.

Kwa ufupi nilikuwa na safari kutoka Mkoa mmoja kwenda mwingine huku nikitumia usafiri wangu binafsi. Kiukweli njia nzima changamoto zilikuwa ni nyingi kutoka kwa hawa askari wetu wa usalama barabarani. Changamoto mojawapo ilikuwa ni ile ya kuviziana na tochi kwenye yale naeneo ya 50/KPH! Hapa niliwashinda.

Changamoto nyingine ilikuwa ni ile ya kusimamishwa na kuulizwa leseni yako, kukaguliwa bima kupitia mashine, kukaguliwa kama gari inadaiwa, nk. Na hapa pia nilikuwa mshindi.

Jambo lililonifanya kuanzisha huu uzi sasa ni hili suala la askari mmoja wa eneo fulani katika hiyo safari yangu, kunisimamisha na baada ya kukagua gari na kukosa makoda mengine; akanitia hatiani kwa kosa la kutokuwa na sticker ya nenda kwa usalama barabarani. Huyu askari nilibishana naye kwa muda mrefu pasipo na mafanikio! Na mwisho wa siku akalazimisha kuniandikia hiyo faini ya elfu 30.

Kwenye maelezo yake wakati tunabishana, aliniambia eti hizo sticker zinatolewa kituo cha polisi na mtu anayeitwa VECO! Na kwa hiyo kila dereva/mmiliki wa gari anatakiwa kwenda kituo cha polisi na gari lake ili likaguliwe, ndipo apewe hiyo sticker ya nenda kwa usalama!!

Sasa maswali yangu kwenu wanajukwaa ni haya hapa;

1.) Je, huyo VECO ana uwezo wa kukagua magari yote nchini na hivyo kuyapatia hizo sticker za nenda kwa usalama?

2.) Je, ni halali askari wa usalama barabarani kunitoza faini ya elfu 30 kwa kukosa hiyo sticker? Au na hii ni njia mojawapo ya kukusanya mapato ya serikali kupitia mifumo kandamizi na ya hovyo?

3.) Na kama hizo sticker zina ulazima kwa kila gari, ni kwa nini zoezi lisifanyike barabarani ambako magari ndiyo hutembea, badala ya kuwataka madereva/wamiliki wa magari kwenda kwenye vituo vya polisi (tena ni kuanzia vile vya Wilaya) kuwaona hao VECO! (Na mbaya zaidi siyo mara zote utawakuta huko vituoni) Ili tu kununua hizo sticker! Halafu ukimkosa, unaishia kuandikiwa faini? Kwa nini jeshi ka polisi linatengeneza mazingira ya aina hii kwa wamiliki wa magari?

4. Huu mradi wa sticker za nenda kwa usalama ni wa nani? Maana miaka nenda tunalazimishwa tu kuwa na hizo sticker, huku magari yenyewe yakiwa hayakaguliwi! Na badala yake watu wamekuwa wakiuziwa hizo sticker kwa bei ya ulanguzi na hao polisi?

5.) Je, serikali ya CCM hamuwezi kutuondolea huu uonevu tunaofanyiwa wamiliki wa vyombo vya moto, hususani wamiliki wa magari? Maana tumekuwa sasa kama ng'ombe wa maziwa kutoka kwenu na pia kutoka kwa hawa askari wenu wa barabarani!!

Kwa uonevu wa aina hii nikiichukia serikali na pia hawa askari wapenda rushwa, mtanilaumu kweli!!

NB:- kuna kijana wa mwaka 2000 anaweza kuja kuniponda kwa kulalamikia faini ya elfu 30!! Hajui hiyo hela ni bora mara mia ningeenda kunywea pombe, au kwenda kununulia nyama ya swala! Kuliko kuitoa kwa watu wasio na faida.
Haya mambo ya sticker hayana tija,nani anataka kuendesha gari bovu?Wafute kabisa.
 
Nimeachaga huu ujinga, siku hizi bora nipigwe faini kuliko kutoa hongo.
Wengi wao hasa maeneo ninapopita mara kwa mara wamenielewa kuwa sitakagi ujinga.
Huwa navutana nao hadi inatisha.

Hawa mafala ukiwaogopa wanakufilisi.
Jana tu nimevutana na mmoja kiasi cha kumtolea lugha kali sana
Hata kama nina kila kitu bora nitoe elf tano kwa sababu kuu 3.

1. Siwezi ingia kwenye rariba yao ya kazi nitumie dk 10/15 tunajadiliana ilihali wao wapo kazini kwao hawana cha kupoteza na anayepoteza muda ni mimi.

2. Sheria inamruhusu kukukagua sio hapo tu, anaruhusiwa pia kupeleka gari kituoni iwapo anaona kuna tatizo, huwezi mshinda askari akiwa kwenye majukumu yake na ukifanikiwa siku utaimaliza kwenye hiyo shughuli.

3. Mwisho wa kubishana na askari huishia na faini tu, mara chache sana utatoka bila faini. Sasa kwanini nipoteze muda kupewa elfu thelathini? Si nampa chap elf tano tu mtanganyika mwenzangu huyu mwenye viatu vinavyotakiwa kubrashiwa tunatabasamu mambo yanaendelea.
 
Hata kama nina kila kitu huwa nawapaga elf tano sababu kuu 3.

1. Siwezi ingia kwenye rariba yao ya kazi nitumie dk 10/15 tunajadiliana ilihali wao wapo kazini kwao hawana cha kupoteza na anayepoteza muda ni mimi.

2. Sheria inamruhusu kukukagua sio hapo tu, anaruhusiwa pia kupeleka gari kituoni iwapo anaona kuna tatizo, huwezi mshinda askari akiwa kwenye majukumu yake.

3. Mwisho wa kubishana na askari huishia na faini tu, mara chache sana utatoka bila faini. Sasa kwanini nipoteze muda kupewa elfu thelathini? Si nampa chap elf tano tu mtanganyika mwenzangu huyu mwenye viatu vinavyotakiwa kubrashiwa?
Hua unapita sana barabara ya wapi boss?
 
Hua unapita sana barabara ya wapi boss?
Kwanini mkuu, walinzi wa usalama barabarani si wapo nchi nzima? Au unataka kunipa kesi ya kutoa rushwa nikae ndani bila dhamana? Ile si rushwa mkuu ni ya kubrashia viatu tu, huwa natii sheria bila shuruti.
 
Back
Top Bottom