Heaven Seeker
JF-Expert Member
- May 12, 2017
- 479
- 1,071
Kwa taarifa tu ni kwamba, Wakufunzi ( Wahadhiri) wa Vyuo mbalimbali hasahasa vyuo vikuu, mojawapo ya majukumu yao ya msingi ni kufanya Tafiti mbalimbali. Ukiangalia kwenye google scholar kisha ukaanza kutafuta research zilizofanyika hapa nchini na wahadhiri wetu, utakutana na utitiri wa tafiti nyingi sana kwenye journals mbalimbali. Hata tu ukitembelea kwenye websites zao za vyuo wanavyofundisha utakutana na tafiti nyingi sana ambazo zimefanyika.
Kikubwa zaidi, ukisoma hizo tafiti utakuta zimetoa recommendations mbalimbali kutokana na tafiti husika kuwa ni kipi kifanyike.
Hakika kama kweli sisi kama nchi, tungeamua kufanya mambo yetu kwa kuzingatia tafiti zilizofanyika, tungekuwa mbali sana, maana mambo mengi yangefanyika kitaalamu na tungekuwa tumepiga hatua kubwa.
Chakushangaza, ni nadra sana kumsikia kiongozi wa Serikali, awe wa kisiasa au wa Taasisi flani akitoa maelezo au amelekezo kwa kuanzia na maneno kama ''kwa mujibu wa utafiti uliofanyika mwaka flani kuhusu kitu flani, ilibainika kuwa changamoto kubwa ya jambo flani ni kutokana na sababu kadha wa kadha na hivyo tumeamua kuanza utekelezaji wa mapendekezo kulingana na utafiti huo kwa kufanya jambo moja mbili tatu''. Yaani unakuta kiongozi anaongea mambo muhimu sana kuhusu sera au utekelezaji wa mambo muhimu yanayowagusa wananchi kwa maoni yake binafsi tu.
Hata watunga sheria huko Bungeni ni nadra sana kuwasikia wakizungumza kuhusiana na utafiti wowote uliofanyika. Hii kwa maoni yangu ni kuamua kufanya mambo kienyeji sana. Huenda Serikali ikawa inatekeleza baadhi ya mapendekezo ya Tafiti hizi, ila nina mashaka makubwa kama huwa wanafanya hivyo kwa kiwango kikubwa.
Nchi za wenzetu, unakuta wana Taasisi maalumu ya kufanya analysis ya research zinazofanyika, na baadhi ya lecturers wanafanya kazi Vyuoni na pia kwenye Taasisi nyingine za Serikali za kuchakata sera za nchi kulingana na Tafiti zinazofanyika, kisha wanaishauri Serikali nini kifanyike.
Sisi tunafeli wapi? Shida haswa ni nini kwani? Kwanini tusitekeleze mipango yetu kwa kuzingatia tafiti za wasomi wetu zinazofanyika kwa gharama kubwa hapa nchini? Nini umuhimu wa hizo tafiti kuendelea kufanyika?
karibuni kwa mjadala.
Kikubwa zaidi, ukisoma hizo tafiti utakuta zimetoa recommendations mbalimbali kutokana na tafiti husika kuwa ni kipi kifanyike.
Hakika kama kweli sisi kama nchi, tungeamua kufanya mambo yetu kwa kuzingatia tafiti zilizofanyika, tungekuwa mbali sana, maana mambo mengi yangefanyika kitaalamu na tungekuwa tumepiga hatua kubwa.
Chakushangaza, ni nadra sana kumsikia kiongozi wa Serikali, awe wa kisiasa au wa Taasisi flani akitoa maelezo au amelekezo kwa kuanzia na maneno kama ''kwa mujibu wa utafiti uliofanyika mwaka flani kuhusu kitu flani, ilibainika kuwa changamoto kubwa ya jambo flani ni kutokana na sababu kadha wa kadha na hivyo tumeamua kuanza utekelezaji wa mapendekezo kulingana na utafiti huo kwa kufanya jambo moja mbili tatu''. Yaani unakuta kiongozi anaongea mambo muhimu sana kuhusu sera au utekelezaji wa mambo muhimu yanayowagusa wananchi kwa maoni yake binafsi tu.
Hata watunga sheria huko Bungeni ni nadra sana kuwasikia wakizungumza kuhusiana na utafiti wowote uliofanyika. Hii kwa maoni yangu ni kuamua kufanya mambo kienyeji sana. Huenda Serikali ikawa inatekeleza baadhi ya mapendekezo ya Tafiti hizi, ila nina mashaka makubwa kama huwa wanafanya hivyo kwa kiwango kikubwa.
Nchi za wenzetu, unakuta wana Taasisi maalumu ya kufanya analysis ya research zinazofanyika, na baadhi ya lecturers wanafanya kazi Vyuoni na pia kwenye Taasisi nyingine za Serikali za kuchakata sera za nchi kulingana na Tafiti zinazofanyika, kisha wanaishauri Serikali nini kifanyike.
Sisi tunafeli wapi? Shida haswa ni nini kwani? Kwanini tusitekeleze mipango yetu kwa kuzingatia tafiti za wasomi wetu zinazofanyika kwa gharama kubwa hapa nchini? Nini umuhimu wa hizo tafiti kuendelea kufanyika?
karibuni kwa mjadala.