Je! ni kweli dunia inazunguka jua?

Je! ni kweli dunia inazunguka jua?

1. Dunia sio duara bali ni bapa isipokuwa ni bapa yenye milima na mabonde.

2. Dunia hsizunguki jua. Tumia akili ya kawaida, chukua mpira au chubgwa kisha igundike zile toothpick kueneza pande zote alafu zungusha. Utaona kuna point fulani ukifika toothpick zinadondoka.

Kama dunia duara why sisi hatudondoki? Nilikubali dunia duara ili nifaulu mitihani lakini moyoni nasema NO.

Duh! Mmasai kaingia Disco na sime.
 
Ahaa!! Kwa hiyo unataka kuniambia mjadala hapa ni kuhusu foundation (msingi) ni nani kati ya jua na dunia (Geocentrism vs Heliocentrism) na si habari ya dunia kuzunguka jua? Maana title ya thread naona inasema "Je ni kweli dunia inazunguka jua?" Kwa hiyo hizo nukuu za Biblia ulizoweka ni kusisitiza hoja ya Geocentrism na si kuwa Biblia inasema dunia haimove?

Kama nilivyosema Misahafu haijakusudiwa kuwa marejeo/reference ya hoja za kisayansi. Huwa naona Waislam fulani wanavyohangaika "kuipa nguvu" Qur'an kwa kuonesha wapi hoja zake zinathibitishwa na sayansi! Hili ni tatizo.

Kuhusu Biblia ama Qur'an hasa Bible kwa nukuu ulizoweka hapo juu kusudio lake ni kuzungumzia juu ya uumbaji na ukuu wa Mungu na kwamba ndiye aliyeanzisha yote.

Usahihi wa kisayansi hauna maana kama hoja ya nani kaanzisha existence.. kuna mambo kibao si Biblia wala Qur'an zinazoweza kuyaeleza kwa mantiki (na hakuna haja) kama kwanini Mungu aliumba Shetani!!

Si kazi ya hivi vitabu kujibu hayo na wala havijajibu ila watu wanalazimisha kuwa vimejibu!!! Hivyo idea hapo ya Biblia si Geocentrism bali "Eeeh nyie Binadamu Mungu ndiyo kaanzisha haya yote."

Poteza muda na Geocentrism ya Biblia usahau kutenda mema kisha uende motoni!! Hivyo Qur'an ama Biblia ikitofautiana na sayansi juu ya facts fulani binafsi huwa naangalia muktadha na makusudio ya vitabu hivyo kueleza hayo kwa namna hiyo na si kuishambulia sayansi ama kulazimisha eti Biblia iko sahihi!!

Excellento!!
 
Hivi ndivyo jf inatakiwa itumike hata sisi wanafunzi tunafaidika kwa ufahamu wenu mlioupata kabla yetu na tukienda darasani tunatoa changamoto hizi

mkuu ukijibu tofaut na makubaliano ya syllabus itakula upande wako tu
 
NAOMBA NIJIBU KWA URAHISI JILI SWALI:

Baada ya kusoma post zote nimegundua maswali mawili makuu ni haya

1) kwanini hatuanguki
2) je dunia inazunguka au la
3) kwanini setelite na viombo vingine havituachi mfano settelites zipo pale pale siku zote.
4) kutua kwa ndege za space eneo lilelile

jibu langu:

1> Hatuanguki sababu ya gravitationa force ina tu fanya tuwe tunavutwa kwenda kati ya dunia ndio maana ukirusha jiwe juu lazima lirudi chini hata ukizamisha jiwe baharini litazidi shuka chini.

na hio gravitational force haiishii kwenye mawingu. na unavyosema angani bado upo ndani ya hio force hata usimame mwaka mzima na helcopta bado utakuwa upo pale pale na unavutwa kushuka chini kama jiwe na lazima utumie nguvu kuwa hapo ulipo

hata watu walio pembeni kushoto kulia au chini ya dunia bado wanavutwa kwenda kati ya dunia.


2> Dunia inazunguka

huwezi feel au ona spidi hio sababu na wewe unazunguka kwa speed hio hio,,, ndio maana unaweza kunywa maji kwenye basi na maji hayarudi nyuma sababu kila kitu kilichipo kina kimbia spidi hio hio, haya ubebe samaki ndani ya chupa kwenye gari huwezi ona samaki anarudi nyuma sababu maji na samaki mwenyewe yapo kwenye spidi hio hio.

proof ndogo... juwa linazama magharibi na kuchomoza mashariki , tofauri ya masaa hapa kwetu na nchi nyingine ni huo mduara na mzunguko, nyota na mwezi huvioni muda wote sababu ya mzunguko hadi tuzunguke kwenye ile point tulipoa onea mwanzo ndio utaiona tena. easy

3)kwanini setelite hazituachi

setelite bado zipo kwenye gravitationa force ya dunia ila ni nje ya orbit zipo kati kati ya kuvutwa na space na kati kati ya kuvutwa na dunia. ndio maana ya orbit. ikisogea nje kidogo tunaiacha ikizidi kido duniani inaanguka, ni balance tu ndio maana pakaitwa orbit.

kwann hatuiach ni sababu bado ipo na spidi ile ile ya dunia haipo nje ya dunia tofauti ya setelite na ndege ni kwamba yenyewe imewekwa kwenye poin t maarumu kiasi kwamba gravity hainauwezo wa kuishusha wala spacehainanguvu ya kuivuta.ila na yenyewe inazunguka na spidi ile ile. na pia inaweza kuhama sababu ina engena au plopera ya kuiamisha point a to b ndani ya orbit hio hio. easy

4) space craft kutua pale pale

easy ukijua zinavyo paa utajua zinavyoshuka..... huwa haziend angani kama ukipiga bastola juu. huwa zinaenda kimlalo kama sinazunguka dunia kwenda ile point watakayo ili ku kuwepa gravitational force ni sawa na kudive kwenye maji ili usupige kichwa chini, na kurudi ni hivyo hivyo wanafanya mahesabu na kutua pale pale watakapo.

ni hayo nimerahisisha na kutumia lugha rahisi sana.


cheers!!
 
Ukiwa ndani ya bus linaloenda, halafu ukaruka juu unadhani utatua wapi? You will land at same spot you launched from as long as the bus is moving with un accelerated velocity, its Newton's first law of motion or inertia

Usitumie bas mkuu tumia kichanja scania maana kwa mujibu wa dunia tupo nje sio ndani.
 
Usitumie bas mkuu tumia kichanja scania maana kwa mujibu wa dunia tupo nje sio ndani.

Hata ukiwa kwenye pickup, kama utaweza kuhakikisha upepo haukuzuii pia utatua pale pale uliporukia, nimetumia mfano wa basi kwa sababu ndani ya basi effect ya wind ni ndogo, soma Newton's first law of motion.(Tumeshaielezea sana kwenye hii thread)
 
dunia inazunguka jua mf sisi ni sisimizi tupo ndani ya scania ambayo ipo sana kasi we feel nothing going tukiangalia nje kama kuna mlima tutaona unatuzunguka sisi ilhali upo stationery
 
Pole sana.Ungeuliza



Pole sana,acha kutuzingua,umesema ulikimbia umande,mbona unajiuliza kati ya hayo masomo mawili?
 
1. Dunia sio duara bali ni bapa isipokuwa ni bapa yenye milima na mabonde.

2. Dunia hsizunguki jua. Tumia akili ya kawaida, chukua mpira au chubgwa kisha igundike zile toothpick kueneza pande zote alafu zungusha. Utaona kuna point fulani ukifika toothpick zinadondoka.

Kama dunia duara why sisi hatudondoki? Nilikubali dunia duara ili nifaulu mitihani lakini moyoni nasema NO.

Kumbe moyoni, hapo sawa
 
Dunia inazunguka ikiwa pamoja na anga lake, ikiwa ina maana inaenda na kila kitu chake hivyo hakuwezi kuwa na ukinzani kati ya dunia na upepo kwakuwa inazunguka nao.

Gari linapokimbia haliendi sawa na huo upepo.

Asipoelewa na hapa, ndio basi tena, tatizo sisi huwa tunachukua habari za vijiweni na kuanza kubisha bila fact, mtu unakuta hapotezi ata dakika 1 kujisomea juu ya kitu anachotaka kubisha ila atabisha tu kwa mazoea, km mtu alisoma na hakumuuliza mwalimu wake ili ajue ss huyo unazani alikuwa mwanafunzi au mjasiriamali
 
Mazee unafahamu tofauti ya elimu ya madarasa?

Tatizo unachanganya elimu na madarasa, nikikuuliza elimu yako imeishia wapi kwenye mada hii naweza kumaanisha kuna kitabu gani kizuri umesoma, wewe unaona nakuuliza una degree ngapi.

Mpaka hapo ushajionyesha si critical thinker, na siwezi kushangaa unavyopinga kwamba dunia inazunguka jua, kwa sababu unafikiri very shallow.

Uko sawa mkuu unachosema ata mm nina wasi wasi na uwezo wake
 
Unfahamu theory ni nini na fact ni nini?

Ukitaka ku discredit kitu kwa sababu kinaitwa "theory", unafahamu kwamba hizo namba unazohesabia kila kitu, mpaka jedwali ulilotupa lilizotumia, nazo bado ni theory na si fact strictly speaking?

Unaposikia "anti-west" unaelewa nini? A geographical location?

Akili yako finyu inarudi mulemule, kufikiri elimu ni madarasa na "anti-west" ni some geographical location.

Mbona mm nakuelewa? Nilichohisi ni kwamba hawa wanaobisha ni wale watu ambao waliwekwa kiti moto na kuanza kumezeshwa haya mambo, either na waumini wa dini au watu wanao waamini ndio maana utagundua hawana mifano mingi na yenye uhai km ulivyo ww, siku zote mtu aliemeza kitu huwa hatoki nje ya kile alichomeza ila mtu aliejua/kuelewa waga anaenda mbali zaidi
 
tumesoma kwenye jografia kua dunia inazunguka jua hivyo tunapata majira ya mwaka kama kiangazi na masika je ni kweli? galileo alikuwa sahihi?

Fikra ya kawaida
chukulia umepanda ndege au hellcopter halafu unaenda marekani then ile hellcopter ikasimama juu angani kwa muda mrefu lets say mwezi mmoja, je dunia itakuacha? kama haikuachi hio dunia inazungukaje kwenye orbit? na zile satelite ambazo zipo angani kama dunia inazunguka kwenye orbit mbona hatuzigongi? tunaambiwa dunia inazunguka kwa speed kubwa sana ina maana satelite zinamatch speed ya dunia?


Theory ya taycho brahe
Jamaa huyu mdanish (denmark) alitoa theory yake ambayo inamashiko tu

-sayari nyengine kama mercury na venus zinazunguka jua
-then jua na mwezi vinazunguka dunia

Tychonian_system.svg


Kama theory ya juu ipo sahihi inamaana hata dunia haizunguki bali jua ndio linatuzunguka.

Mnaonaje hii ipoje? kuna mtu ana point za kuprove kuwa galileo yupo sahihi?
Kaka Chief-Mkwawa Jua

na mwezi Vinazunguka dunia vitu hivyo vimekwisha tajwa kwenye Kitabu cha Waislam Quran Miaka 1500

iliyopita. Ushahidi Soma hapa Quran Sura 36 AYA YA 39-40.

36. Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua

37. Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani

38. Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua

39. Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe

40. Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao

chanzo. Qur'an 36. SURAT YA-SIN
 
Wakuu hebu nitoeni tongotongo leo humu,hiv hiyo orbit nikitugani?najua mgano tyre za gari zina bering pale kwenye kiungio na diff hivyo kuifanya izunguke kwa ulaini bala friction so kwa dunia ni vip je kwenye kiungo cha orbit na dunia kunanini au ni mamiamba tu ambayo baada ya muda kwakuwa hakuna grees pata bomoka au inakuaje wakubwa,na satelit inazunguka kwa speed gani hiyo ya masaa 24 je ni tofauti na speed ya dunia kulizunguka jua?
 
Back
Top Bottom